Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,463
- 39,929
Kati ya vitu ambavyo inawezekana vimewaponyoka wengi ni kuwa Rais Kikwete alipozungumzia suala la Zanzibar alijikuta ameirudisha "Nchi ya Tanganyika" kwa makusudi (haiwezekani kuwa bahati mbaya). Aliirudisha hivyo kwa kufuata reasoning yake ambayo kwa kweli naamini ina makosa na alishindwa kutaja tatizo la Katiba tu.
Kikwete alifafanua kuwa tarehe 26 Aprili nchi mbili huru ziliamua kuachilia sehemu ya mamlaka yake na kuunda nchi moja inayoitwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Akasema kwa kufanya hivyo "nchi ya Zanzibar" na "nchi ya Tanganyika" zikakoma kuwepo na nchi moja ya Tanzania ikazaliwa (hadi hapo hana makosa).
Akaendelea kuelezea kuwa hivyo katika mahusiano yetu ya nje na nchi nyingine sisi ni Tanzania. Hiyo ndiyo inatupa utambulisho wetu. Akasema katika "utambulisho wetu wa nje nchi ni Tanzania". Akaendelea kusema "lakini kati yetu sisi wenyewe, nchi ni Zanzibar na ya Muungano" (hapo nikahamaki.
Kama kwa sisi wenyewe "nchi ya Zanzibar" bado ipo ndani ya huu Muungano, sasa nchi ya Tanganyika iko wapi? Ndipo nikagundua kwa urahisi tu kuwa kwa mara ya kwanza Rais wa Muungano ameelezea Tanzania Bara kama ni Tanganyika. Kuwa ni nchi iliyo sambamba na Zanzibar.
Next question? Serikali ya Tanganyika iko wapi?
Kikwete alifafanua kuwa tarehe 26 Aprili nchi mbili huru ziliamua kuachilia sehemu ya mamlaka yake na kuunda nchi moja inayoitwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Akasema kwa kufanya hivyo "nchi ya Zanzibar" na "nchi ya Tanganyika" zikakoma kuwepo na nchi moja ya Tanzania ikazaliwa (hadi hapo hana makosa).
Akaendelea kuelezea kuwa hivyo katika mahusiano yetu ya nje na nchi nyingine sisi ni Tanzania. Hiyo ndiyo inatupa utambulisho wetu. Akasema katika "utambulisho wetu wa nje nchi ni Tanzania". Akaendelea kusema "lakini kati yetu sisi wenyewe, nchi ni Zanzibar na ya Muungano" (hapo nikahamaki.
Kama kwa sisi wenyewe "nchi ya Zanzibar" bado ipo ndani ya huu Muungano, sasa nchi ya Tanganyika iko wapi? Ndipo nikagundua kwa urahisi tu kuwa kwa mara ya kwanza Rais wa Muungano ameelezea Tanzania Bara kama ni Tanganyika. Kuwa ni nchi iliyo sambamba na Zanzibar.
Next question? Serikali ya Tanganyika iko wapi?