Zawadi Ngoda
JF-Expert Member
- Aug 13, 2009
- 3,792
- 1,836
Ukiziamini takwimu za CIA kupitia website yao (www.aneki.com), basi hutakuwa na ubavu wa kukipinga kichwa cha habari hapo juu. CIA ni shirika lnaloaminika sana duniani, na lipo up to date katika takwimu zao.
Miaka miwili iliyopita nilitembelea mtandao wao na nikapata aibu, pale nilipoiona Tanzania katika bora 10 masikini duniani. Kwa wasomaji wazuri wa mtandao wa wakati ule T/Daima wanaweza kukumbuka jinsi nilivyokuwa naleta takwimu hizi kwa masikitiko. Mara leo hii upepo umegeuka na naweza kuandika kwa majigambo jinsi uchumi ulivyopanda kama ndege, mig 21. Leo hii Tanzania ipo nafasi ya 28, ikipanda toka nafasi ya 8 mwaka 2007. Ifuatayo ni orodha ya nchi 33, ikianzia Zimbawe msikini sana ikiwa na GDP $200, na ya 33 ni Chad ikiwa na GDP $1600
Top 100 countries with the lowest GDP per capita
Samahani; nilijaribu kuziweka hapa hizo nchi lakini hazijatokea. Hivyo tembelea www.aneki.com. Na angalia katika Top 100 countries.........kama hapo juu.
Mwaka 2007 Tanzania ilikuwa na GDP kama Somalia leo hii, $600 (sh 780000) na tulishika nafasi ya 8. Ninafurahi kusema kuwa leo hii tuna GDP ya $1400 (sh 1820000). na kuzibwaga nchi kadhaa na kushika nafasi ya 28. Kiwango hicho cha pesa kinafanya tofauti ya sh 1040000 kwa kipindi cha miaka miwili. Kwa hesabu rahisi ukuaji wa GDP kwa kipindi cha miaka miwili ni wastani wa sh 520000 kwa mwaka.
Ikiwa kama Kikwete atachaguliwa tena, katika uchaguzi wa 2010 na kuwa madarakani mpaka 2015, na kwa mwendo kasi huu inamaanisha kuwa GDP ya Tanzania mwaka 2015 itakuwa sh 1820000 +(520000*6)= 4940000 = $3800. Hii inamaanisha kwamba kama ilivyo leo hii, basi Tanzania itakuwa katika nafasi ya 67, sawa na Djibouti yenye kiwango hicho leo hii.
Watanzania tutakuwa wendawazimu kama hatutaridhika na kufurahia maendeleo hayo kiuchumi. Kwa maendeleo hayo, tunaweza vile vile tukasema bye bye misaada, sasa wenyewe tutajiendesha, kama vile warusi walivyofanya mwaka 2004 kwa IMF na World Bank. Na hii ndio ndoto yangu kubwa na nafikiri ndio ndoto ya Serikali na watanzania wote kwa jumla.
Tabasam la Kikwete lina bahati, ngekewa na linazivuta nchi zote duniani kuiona Tanzania kama Tumaini la uwekezaji. Kusema kuwa Kikwete anaweza, sio tu propaganda bali Takwimu zinajionyesha.
Pamoja tutashinda, safari ni ndefu na uvumilivu ndio dawa.
Miaka miwili iliyopita nilitembelea mtandao wao na nikapata aibu, pale nilipoiona Tanzania katika bora 10 masikini duniani. Kwa wasomaji wazuri wa mtandao wa wakati ule T/Daima wanaweza kukumbuka jinsi nilivyokuwa naleta takwimu hizi kwa masikitiko. Mara leo hii upepo umegeuka na naweza kuandika kwa majigambo jinsi uchumi ulivyopanda kama ndege, mig 21. Leo hii Tanzania ipo nafasi ya 28, ikipanda toka nafasi ya 8 mwaka 2007. Ifuatayo ni orodha ya nchi 33, ikianzia Zimbawe msikini sana ikiwa na GDP $200, na ya 33 ni Chad ikiwa na GDP $1600
Top 100 countries with the lowest GDP per capita
Samahani; nilijaribu kuziweka hapa hizo nchi lakini hazijatokea. Hivyo tembelea www.aneki.com. Na angalia katika Top 100 countries.........kama hapo juu.
Mwaka 2007 Tanzania ilikuwa na GDP kama Somalia leo hii, $600 (sh 780000) na tulishika nafasi ya 8. Ninafurahi kusema kuwa leo hii tuna GDP ya $1400 (sh 1820000). na kuzibwaga nchi kadhaa na kushika nafasi ya 28. Kiwango hicho cha pesa kinafanya tofauti ya sh 1040000 kwa kipindi cha miaka miwili. Kwa hesabu rahisi ukuaji wa GDP kwa kipindi cha miaka miwili ni wastani wa sh 520000 kwa mwaka.
Ikiwa kama Kikwete atachaguliwa tena, katika uchaguzi wa 2010 na kuwa madarakani mpaka 2015, na kwa mwendo kasi huu inamaanisha kuwa GDP ya Tanzania mwaka 2015 itakuwa sh 1820000 +(520000*6)= 4940000 = $3800. Hii inamaanisha kwamba kama ilivyo leo hii, basi Tanzania itakuwa katika nafasi ya 67, sawa na Djibouti yenye kiwango hicho leo hii.
Watanzania tutakuwa wendawazimu kama hatutaridhika na kufurahia maendeleo hayo kiuchumi. Kwa maendeleo hayo, tunaweza vile vile tukasema bye bye misaada, sasa wenyewe tutajiendesha, kama vile warusi walivyofanya mwaka 2004 kwa IMF na World Bank. Na hii ndio ndoto yangu kubwa na nafikiri ndio ndoto ya Serikali na watanzania wote kwa jumla.
Tabasam la Kikwete lina bahati, ngekewa na linazivuta nchi zote duniani kuiona Tanzania kama Tumaini la uwekezaji. Kusema kuwa Kikwete anaweza, sio tu propaganda bali Takwimu zinajionyesha.
Pamoja tutashinda, safari ni ndefu na uvumilivu ndio dawa.
Last edited by a moderator: