Kikwete in Dubai: On Transit.. kukutana na Al-Adawi?

Mimi siku hizi ninashangaa sana ninaposikia watu wengi wakimuorodhesha Muungwana kama mpambanaji dhidi ya mafisadi!! Jakaya ni fisadi nambari wani kwahiyo kwake si rahisi kuwatosa wakina RA na EL akifanya hivyo atakuwa anacommit suicide; the most he does ni kujifanya akiwa jukwaani kuwa anapinga ufisadi kumbe nyuma yake anaukumbatia; kudhihilisha ninayosema nyie ngojeni maadam amepitia Dubai akirudi tu, utasikia serikali imeamua kununua mitambo ya Dowans!! Msijekushangaa huyo ndio mnamuita mpambanaji wenu!!

Naam huyo ni fisadi Nambari one nakubaliana na wewe katika hili. Sakata lote hili la Richmond/Dowans likiendelea yeye kaamua kukaa kimya kabisa bila kutoa kauli yoyote. Mkurugenzi wa TANESCO anatutisha Watanzania eti nchi ikiingia kizani basi TANESCO isiilaumiwe, bado tu Rais wa nchi yuko kimyaaaa halafu yule comical Salva anasema Rais hahusiki kabisa na swala la Richmond/Dowans. Halafu hii njemba inataka kugombea tena 2010!!!! Kazi kweli kweli!!!! I hope watatokea watu ndani ya CCM kumpinga maana kama tungekuwa na katiba yenye kuweka maslahi ya nchi mbele huyu asingemaliza hata awamu yake ya miaka mitano. Angekuwa ameshaondolewa madarakani siku nyingi sana.
 
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu unatisha!....isije kuwa na wewe una shirika la kufua umeme?...
 
Nimekuwa nikijiuliza sana hivi JK atakapo pata kipindi cha pili atakuwaje kama sasa hivi anaface challenge ya re election bado amekuwa wa aina hii! Hivi kweli Tanzania haina watu wa maana! Kwa nini hata ndani ya CCM watu wasijitokeze kumpinga! Tutabaki kuogopa mpaka lini? Yaani taifa zima tunaogopa tu! Ninachokiona huyu jamaa akichaguliwa 2010 anaweza kugeuka dictator na watu tutabaki kusema tulijua!
 
juzi nimesema kama hukubaliani na suala la Dowans nitakupa namba za viongozi uwapigie kuwapa habari yao guess what? Mtu mmoja tu hapa na huyo ni mtu ambaye nina uhakika anaweza kufanya hivyo. Wengine wote wamebakia "conflict of interests"! doomed we are!

Mzee Mwanakijiji,
Mbona sikuiona hiyo posting yako? Naomba sana na mimi unipatie hizo namba ili na mimi niendeleze mapambano kutokea kwenye handaki langu.
 
Nimekuwa nikijiuliza sana hivi JK atakapo pata kipindi cha pili atakuwaje kama sasa hivi anaface challenge ya re election bado amekuwa wa aina hii! Hivi kweli Tanzania haina watu wa maana! Kwa nini hata ndani ya CCM watu wasijitokeze kumpinga! Tutabaki kuogopa mpaka lini? Yaani taifa zima tunaogopa tu! Ninachokiona huyu jamaa akichaguliwa 2010 anaweza kugeuka dictator na watu tutabaki kusema tulijua!

Sio uongo, waTZ tunawoga wa kupindukia ndio maana hata kwenye mitandao ingawa wengi tuko nje bado tunatumia majina kama Haki tupu, Makaayamawe n.k. Tumeshindwa hata na yule DJ wa Madagasca.

Lakini JK atakapoamua kuwanunua DOWANS, nitakata ticket ya one way to Dar na kushiriki kwenye maandamano yoyote yale mpaka ang'atuke.
 
Naam huyo ni fisadi Nambari one nakubaliana na wewe katika hili. Sakata lote hili la Richmond/Dowans likiendelea yeye kaamua kukaa kimya kabisa bila kutoa kauli yoyote. Mkurugenzi wa TANESCO anatutisha Watanzania eti nchi ikiingia kizani basi TANESCO isiilaumiwe, bado tu Rais wa nchi yuko kimyaaaa halafu yule comical Salva anasema Rais hahusiki kabisa na swala la Richmond/Dowans. Halafu hii njemba inataka kugombea tena 2010!!!! Kazi kweli kweli!!!! I hope watatokea watu ndani ya CCM kumpinga maana kama tungekuwa na katiba yenye kuweka maslahi ya nchi mbele huyu asingemaliza hata awamu yake ya miaka mitano. Angekuwa ameshaondolewa madarakani siku nyingi sana.

Bubu mwanzoni nilikuwa sijui kwanini wewe siku zote unalia ja JK kuwa hafai kuongoza zaidi ya 2010. sasa hivi naanza kukuelewa kwani rangi zinazidi kuja na ole wenu watanzania mtakaoona maandalizi ya uchaguzi wa 2015 kwani itakuwa ni kumwaga radhi kuliko hivi sasa sembuse atakuwa anaondoka? huku akitaka amwekwe mtu atakayemlinda kama yeye anavyomlinda BWM hivi sasa?
 
Makaayamawe,
Nakubaliana na concerns zako pia ingawa naamini kutumia majina ya aina hii hakuna shida na si lazima iwe ni kwa sababu ya uoga (tunaogopa conflict of interest zisizo na kichwa wala mkia). Hii inapunguza subjectivity watu tunapojadiliana. Ukimjua mtu mara nyingi unaanza kuwa biased - the good thing is kwa style hii kila mtu anatoa mawazo (anafungua moyo) na ni mawazo zaidi si jina la mtu linajadiliwa. Hii ni sawa na unapopiga kura - inakuwa siri ili watu wasinuniane - eti kumbe hata wewe hukunichagua nk! Kwa mtindo wa kutumia majina haya watu wanaweza kuanika wawazayo yote bila kificho - I can assure you, wengi wa wanaotumia majina halisi wanakosa uhuru wa kuchangia si kwa sababu ya uoga tu bali kwa sababu ya kuogopa kuonekana wanawaza vitu vya ajabu! Kama tungekuwa na viongozi wazuri wangeifurahia sana JF na kuipromote.

Nami nitakuwepo kwenye hayo maandamano - lakini ni ya Dowans tu? Mambo ni mengi sana yanayotia kinyaa kabisa. JK akipewa term nyingine hata maaskofu na masheikh watakiri kuwa huyo siye waliyedhani ametoka kwa mungu!
 
Hatufanyi chochote kwa sababu tunasubiri shujaa wa ukoo wa mashujaa azaliwe ili atukomboe kutoka katika makucha ya wakoloni weusi walio ndugu wa damu moja.
Tulizaliwa katika ukoo wa mwewe damu yetu ni ya mwewe, sura zetu ni za mwewe, hata makucha na mbawa zetu ni za mwewe.

Lakini kwa vile maisha yetu yote tumeishi katika banda la kuku na kulelewa kama kuku. Wote tunaishi kwa hofu ya kuku ya kuogopa kisu kutoka kwa mlakuku au kunyakuliwa na mwewe na kufanywa kitoeo.
Baada ya uwezo wetu wa kimwewe kuukalia na kudumisha woga wa kuku, Mzee MM unategemea nini kutoka kwetu?

Laiti tungejua kwamba sisi si kuku ila ni mwewe halisi.....!!!

Mwanzo wa moto ni cheche, na sisi tumeanza kujitambua kuwa sisi si kuku bali ni mwewe na ndio maana tumeanza kwa kumzaba kibao Alhaj Mwinyi!! Kibao kile cha kelbu ni kielelezo tosha kwa wenye akili kuwa wananchi wameanza kuchoka na ujinga wa viongozi na wanaweza kuchukua hatua za kijasiri..
 
Katoto ka "nzi" kanakozunguka katika mitaa ya Dubai na Oman kanadokeza kuwa katika jitihada za kuhakikisha mitambo ya Dowans inanunuliwa na serikali ya Tanzania mmiliki wake Bw. Suleiman Yahya al-Adawi na washirika wake wanapanga kutoa "kitripu" ka waandishi wa habari wa Tanzania kwenda Muscat Oman au hata Dubai katika kujifunza shughuli za makampuni yake bla bla bla..

Waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari ambao wanaonekana "kueleweka" na ni wepesi kushawishika wameshaorodheshwa na safari hiyo yaweza kutokea muda si mrefu. Lengo kubwa ni kuendeleza kile nilichosema kwenye Tanzania Daima jana...

Ka nzi kanaendelea kufuatilia jinsi ziara hivyo itakvyouzwa kwa Watanzania. Kuna uwezekano wa hata serikali yenyewe kutake care ya safari hiyo aidha katika mojawapo ya ziara za viongozi huko au katika utaratibu waina fulani hivi. Haya ni baadhi ya mambo ambayo yamezungumzwa kati ya wahusika wa Dowans hasa baada ya sakata la Portek kuibuliwa...
 
Kinachonifurahisha hapa ni kwamba kila move inayofanyika na hawa jamaa tuko nayo sambamba, thanks mwkjj na ka inzi kako!
 
Katoto ka "nzi" kanakozunguka katika mitaa ya Dubai na Oman kanadokeza kuwa katika jitihada za kuhakikisha mitambo ya Dowans inanunuliwa na serikali ya Tanzania mmiliki wake Bw. Suleiman Yahya al-Adawi na washirika wake wanapanga kutoa "kitripu" ka waandishi wa habari wa Tanzania kwenda Muscat Oman au hata Dubai katika kujifunza shughuli za makampuni yake bla bla bla..

Waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari ambao wanaonekana "kueleweka" na ni wepesi kushawishika wameshaorodheshwa na safari hiyo yaweza kutokea muda si mrefu. Lengo kubwa ni kuendeleza kile nilichosema kwenye Tanzania Daima jana...

Ka nzi kanaendelea kufuatilia jinsi ziara hivyo itakvyouzwa kwa Watanzania. Kuna uwezekano wa hata serikali yenyewe kutake care ya safari hiyo aidha katika mojawapo ya ziara za viongozi huko au katika utaratibu waina fulani hivi. Haya ni baadhi ya mambo ambayo yamezungumzwa kati ya wahusika wa Dowans hasa baada ya sakata la Portek kuibuliwa...

Ulisema nini kwenye Tanzania Daima? Kwani hao wajamaa wamelala kwenye mtandao wakiamka na uporo wa wiki.
 
najiuliza watu wakishapata hizi habari wanafanya nini?

Mwanakijiji, nakuhakikishia mchango wako hapa JF na hasa katika kuvumbua mambo mengi ya kifisadi ni msumari wa moto kwa viongozi wa nchi hii. Matokeo yake yataonekana muda si mrefu ujao.

Mkuu vuta subira. Utaona tofauti kubwa katika maamuzi hasa katika uchaguzi ujao zaidi ya wakati mwingine wowote. WaTanzania wanakusoma Mkuu.

Mimi nikiwa mfano mmoja wa watu ambao nimefaidika sana na matokeo ya uchambuzi wako, na uhabarishaji mkubwa wa mambo yanayokera katika Taifa hili, ninaanza kufanya tathmini ya kubadilisha mwelekeo wa kura yangu 2010.

Tupe muda, matokeo utayaona.
 
Kweli JF chiboko I like JF kwa kweli...mapambano ya kifikra...mbele...MJJ,Invisible na wengineo hongereni. Kwa ujasiri na uzalendo....
 
attachment.php

Karudi kwenye hio laptop kajaza DVD mpya......subirini kama atagusia hili saga..
 

Attachments

  • president.bmp
    1.1 MB · Views: 103
Back
Top Bottom