Gosbertgoodluck
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 2,855
- 401
Wengi wetu tulisoma maandishi ukutani kuhusu hatma ya nchi hii ikiwa mikononi mwa kiongozi ambaye ushindi wake umeacha manung'uniko badala ya furaha kwa wananchi. Hali hii katika ulimwengu wa kiimani inamuacha kiongozi katika wakati mgumu kwani wananchi anawaongoza wanamheshimu kwa nje tu kwa sababu ya matakwa ya kikatiba lakini mioyoni mwao wanamtakia kila lililobaya.
Leo hii nchi yetu imefikia hali mbaya kiuchumi, kisiasa na kijamii. Umaarufu wa kikwete siyo umeshuka tu bali umeporomoka na kinachomfanya atabasamu hadharani ni unafiki tu au waswahili wanasema anajibaraguza. Vinginevyo, lazima nafsi yake inamsuta kutokana na hali ya wananchi inavyozidi kuwa mbaya siku hadi siku. Mgao wa umeme ni aibu kubwa kwa taifa. Pamoja mgao huo, bei ya umeme ipo juu, vyakula muhimu bei juu, nauli za usafiri wa barabara juu, huduma ya maji hovyo, n.k. Kwa mwenendo huu nataka nimhakikishie kikwete kwamba hakuna siku wanayoisubiri watanzania kwa hamu kama siku atakayoacha madaraka na hiyo ndiyo gharama ya ushindi wa mezani.
Leo hii nchi yetu imefikia hali mbaya kiuchumi, kisiasa na kijamii. Umaarufu wa kikwete siyo umeshuka tu bali umeporomoka na kinachomfanya atabasamu hadharani ni unafiki tu au waswahili wanasema anajibaraguza. Vinginevyo, lazima nafsi yake inamsuta kutokana na hali ya wananchi inavyozidi kuwa mbaya siku hadi siku. Mgao wa umeme ni aibu kubwa kwa taifa. Pamoja mgao huo, bei ya umeme ipo juu, vyakula muhimu bei juu, nauli za usafiri wa barabara juu, huduma ya maji hovyo, n.k. Kwa mwenendo huu nataka nimhakikishie kikwete kwamba hakuna siku wanayoisubiri watanzania kwa hamu kama siku atakayoacha madaraka na hiyo ndiyo gharama ya ushindi wa mezani.