Kikwete: Hata Nyerere alishindwa ingawa tunamsifu sana

what would you expect from check bobs, pedeshee type of ndama mtoto ya ngo,mbe? Wait six months to come. People will folen for unga wa yanga
 
Una ukweli ndani yako. Labda nikukumbushe kitu hiki,: mchambuzi yeyote anayeweza kutoa tathimini yenye hoja zilizosimama ni yule ambaye aghalabu unbiased!. Mimi binafsi namtaza mwl Nyere na uongozi wake,mapungufu yake na mafanikio yake ktk angle hii:-1. Wakati anaichukua tanganyika,wasomi ambao angekaa nao kuweka mikakati ya kimfumo na utawala miongoni mwa watanganyika walikuwa wakihesabika..Sina kumbukumbu vizuri iliwahi kusemwa alianza akiwa na mainjia wasiozidi watano(naweza kusahihishwa).
2..katika mazingira duni,wasomi wakuhesabika,miundombinu isiyopitika,uchumi mbovu, nk ,mwl alijitahidi kwakweli kwa asilimia 100% (KWA WACHAMBUZI WANAOANGALIA MAZINGIRA YA TANGANYIKA 1961 kama nilivyoanisha hapo juu) kujenga Nchi yenye kuheshimiana,usawa,na ustaarabu. Kumbuka misingi na fikra zake juu ya Arusha declaration.,kufanikiwa au kutofanikiwa ni jambo lingine but dhamira na uthubutu unapambanua Mwl ni kiongozi wa aina gani..
Anyway,ninayomengi mno kutetea misingi na utukufu wa mwl in leadership. Huwezi kulinginsha wanariadha tamati zao bila kugusia muda na startng point zao. Lets say,mmoja aanze saa moja asubuhi poitia A, na mwingine aanze zaa tatu asubuhi point B ahed of opint A,then useme wote at the same contant speed wafike point C at ttime, huo ni uwendawazimu.
Mkuu Waberoya,nakuheshim sana,but kwa wenye hekima,kumsema mwl mapungufu yake kwa misingi ya kujitetea,au kuhalalisha upuuzi wao, ni UPUNGUANI. SI KWASABABU HAKUKOSEA,HAPANA,BALI KWA AINA NA UWAJIBIKAJI WA SERIKALI YAKE,ALIYOIONGOZA KWA KUANZIA NA WASOMI WATAALAM KIDUCHU,NA UMASKIN WA NCHI,UCHUMI AT ZERO,MIUNDOMBINU ZORO, THEN ULINGANISHE KIKWETE NA WASOMI WASHAURI KIBAO,ANAAMUA KWA MAKUSUDI KUCHAGUA MATAPEL BADALA YA WAZALENDO WASOMI,THEN UTETEE, NOOO!!! n

Mkuu mbona tuko wote!!! nilikataa angalia nimeanza vipi na nimemaliza vipi.... rudia post yangu nimelenga kuwa si kweli kumsema Nyerere vibaya ni kupata laana , mimi nilisimamia hapo sina habari na Mkwere wala sijamtetea Kikwete kujitetea kwa style hiyo soma post zangu zingine duh!
 
Wareboya
nimefanya makusudi kabisa kutumia maneno makali juu ya hoja yako kwa sababu nina uhakika kabisa wewe ni mtu msomi na muelewa wa mambo lakini kwa sababu ya chuki binafsi au maslahi binafsi sometimes hutaka kuutumia usomi wako kupotosha mambo! Wewe uko kama wanasiasa wa Kenya!

Asante sana!!

Kaka umeniamulia sina beef na wewe

1. Post yangu no.41 nilikuwa napinga kuwa kumsema vibaya Nyerere unapata laana!!! rudia post introduction na conclusion!!
2. Post yangu no.43 nimejieleza kwa nini Kikwete kakosea kusema hivyo
3. Post yako number 69 mimi nina hoja finyu!!
4. Post yako no. 79 mimi ni mkenya na nina chuki binafsi!

Mkubwa ni busara sana ukikosea ukasema sorry na sio kutafuta excuse nyingi zenye maswali mengi, mimi msomi... , nina chuki binafsi....mimi mkenya Kumbuka hizo zote ni allegations za kufikirika na kama ukikosea unamuumiza mtu, epuka hii kwenye real life mkuu!!! rudia post zangu zote sijaona sehemu niliyomtetea ila mawazo yenu yalikuwa inclined huko!!! kwa kifupi hoja zenu huwa mnazima kabisa mtu asiseme na akisema..basi ..una hoja finyu!! sijawahi kumtukana mtu humu ndani na ninajivunia hii rekodi nyie wenzetu sijui hii audacity huwa mnapata wapi!!
 
Leo katika hotuba yake ya siku ya kuzaliwa CCM, kuna kauli nyingi za kikwete ambozo kama rais hakustahili kuzisema, mojawapo ya ,ni kauli yake ya kwamba pamoja na kumsifu sana Nyerere lakini alishindwa kutatua changamoto nyingi katika utawala wake na hivyo hivyo kwa marais wengine waliomtangulia, sembuse mimi (Kikwete). Alisema hayo akijitetea kwamba yeye sio wa kwanza kushindwa kuondoa matatizo ya watanzania.

Mimi nimeichukulia kauli hii kama simple/cheap excuse ya kikwete kwa jinsi alivyoshindwa kutatua matatizo ya watanzania. Sio tu kikwete ameshindwa kutatua matatizo bali ameyaongeza na kufanya maisha ya watanzania kuwa magumu zaidi. Anaweza kutuambia yeye kama rais am-achiave nini, wenzake wote wana vitu vya kujivunia.

Nyerere alijenga umoja wa kitaifa na kufanya watanzania kuwa wamoja na kuwepo kwa amani ambayo kikwete anajivunia leo, lakini pia mzee huyu alijenga uwajibikaji kwa watumishi wa umma kitu ambacho kikwete ameshindwa.

Mzee Ruksa aliruhusu uchumi wa soko ambao ulisaidi kufanya upatikanaji wa bidhaa muhimu ambazo mwanzo zilionekana kama anasa.

Mzee Mkapa akajitahidi kujenga uchumi imara bila kusahau miundo mbinu na kurudisha heshima ya wafanyakazi.

Pamoja na mapungufu yao viongozi waliopita wanayo ya kujivunia.

Akaja kikwete
1) akaharibu kabisa umoja wa kitaifa kwa kuanza na makundi ndani ya CCM (kwa kuanzisha mtandao wake uliowavuruga wengine) na baadae kuharibu umoja taifa zima kwa kuchochea ajenda zake za udini na ukabila.
2) Akabomoa kabisa uchumi alioujenga mzee Mkapa kwa kuendekeza anasa, matumizi makubwa serikalini, kusafiri kwenda kubembea na kuendekeza ununuaji wa magari ya kifahari yasiyo na tija, gharama za maisha zimepanda mno, thamani ya shilingi imeshuka sana, mfumuko wa bei hauelezeki.
3) Ametengeneza mitandao ya wizi kwa kuwatumia marafiki zake kama RA, ED kwa kutaja wachache.
4) Akaharibu kabisa mfumo wa elimu kwa kuanzisha kisiasa shule za kata zisizo na walimu wala vifaa, ukiangalia wanafunzi wanaofeli ni heri hata tungebaki na shule chache bora,maana waliofeli wanabaki kuwa darasa la saba hawawezi kusema wana elimu ya form IV.
Ni mengi jamani yanayoonyesha tofauti ya utendaji kazi wa kikwete na watangulizi wake, naomba niishie hapa.

Lakini Kikwete please dont look for cheap excuses, just admit that ur the most failure president we ever had.

When Nyerere realized that "ameshindwa" aliamua kung'atuka.....should JK do the same since he has in his own words admitted that kazi imemshinda?

I present to you
 
hivi hamna njia ya amani ya kumfanya rais anyekiri kushindwa kazi kumfanya atoke madarakani awapishe wanaoamini kuwa wanaweza?
 
Katika hotuba ya JK alitanabaisha kuwa hata Nyerere alishindwa kwa baadhi ya mambo. Nakubaliana nae ni kweli ila ni pia ni ukweli dhahiri Nyerere hajawahi kushindwa ku provide leadership.
 
What a shame, hata kama ni kweli Nyerere alishindwa, sio excuse ya yeye kushindwa. kama Nyerere alikosea yeye ilibidi ajifunze kutokana na makosa. Bila aibu anahalalisha uchovu wake kwa kumsingizia Nyerere??
 
Hakuna utetezi kama huo katika failure!
Kushindwa ni kushindwa in person,basi--huwezi kuprecede kuwa fulani mbona alishindwa pia!
Nyerer atasemewa mengi sana!
 
Jamani wana JF, Mimi si mtetei Kikwete, lakini ukweli ni bora ukasemwa.Ni kweli kabisa nchi yetu inamatatizo mengi ya kiuchumi yanayosababishwa na udhaifu wa viongozi wetu wa juu.Kuanzia Rais hadi wakuu wa wilaya. Lakikni msikimbilie kumshambulia Kikwete peke yake mkasahau kuwa hata hao waliomtangulia waliboronga katika mambo mengi ya kiuchumi.Kwa mtazamo wangu, Kikwete ni kama tawi tu, mashina ni Mwinyi, Mkapa na Nyerere. Uchumi ulianza kudorola wakati wa Nyerere pale alipoiingiza Tanzania kwenye vita na Uganda bila sababu za kimsingi.lengo la vita lilikuwa ni kumsaidia rafiki yake kipenzi Milton Obote arudi madarakani.Wachilia mbali vita tulivyopigana kuwasaidia wenztu wa kusini mwa Afrika(South Africa, Angola, Mozambique,Namibia na Zimbabwe) wapate uhuru wao. Vita hivyo vilikuwa vikiigharimu nchi USA $600 kila siku kwa muda wa miezi 18 ya vita. Kuhusu madai ati Nyerere ndiye aliyejenga ummoja wa kitaifa hilo si kweli.Umoja wa kitaifa ulikuwepo kabla ya hata yeye Nyerere mwenyewe hajazaliwa tumboni mwa mama yake. Wazaramo, wandengereko n.k, walikuwa na mahusiano mazuri na wenzao wa mikoani tangu enzi za biashara ya masafa marefu(long distance trade in 8th century) hapakuwepo na ubaguzi wa rangi dini wala kabilra. Hata kudorola kwa elimu kumeanza wakati wa Nyerere pale alipofuta Kiiengerza kama lugha ya kufundishia na hatimaye kuanzisha elimu ya UPE. Kuhusu udini ulanza kujitokeza wakati wa Nyerere huyohuoy pale alipowajaza viongozi wengi ndani ya serkali yake kutoka katika madhehebu ya dini yake.Vipindi vya Mwinyi na Mkapa watanzaia wameshuhudi kuibuka kwa wimbi la wizi, ufisadi wamali za umma nk. Sasa kwa mtazamo wako ulitaka Kikwete ageuke malaika? Lakuvunda halina ubani ndugu zangu. Dawa ni kuiondo CCM na kuingiza utawala mpya utakaoanza na mikakati ya maendeleo kuanzia ngazi ya chini kabisa kwa kuwashirikisha raia zake bila kujali dini rangi wala makabila.
 
Kama kikwete anaona kazi hawezi aandike barua ya kuacha kazi mara moja. Ikulu anafanya nini sasa. Kuna wengine wanaweza wataifanya.
 
Ni kweli kuna mambo Nyerere yalimshinda ila Nyerere hakuwahi kushindwa ku provide leadership kama JK
 
NIMEISOMA HOTUBA JK -sikubaliani kabisa kabisa na kikwete anapodai kuwa Mwalimu aliacha nchi hii si TAJIRI, naomba nimkumbushe kikwete na CCM kwamba Baba wa TAIFA aliacha Tanzania na utajiri wa kutupwa na ni baabda ya kifo chake mafisadi wakaibuka, wawekezaji wanyonyaji wakaingia na kuididimisha nchi hii kwenye umaskani ukashika kasi kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya.

Kikwete na CCM wakumbuke kuwa Mwalimu alifanya haya wakati wake

1. Madini yote alitaka Watanzania wayachimbe ni kikwete kama waziri wa madini alishiriki uibaji wa mali yetu hiyo
2. Mali asili na utalii tunayojidai leo ni kwakuwa mwalimu hakuruhusu wizi wakati wake
3. Mwalimu aliwasomesha bure akina kikwete na mafisadi wote wanaotunyonya kwa sasa
4. Mwalimu hakuwa na mgao wa umeme -miradi ya mwalimu ya umeme ndio hiyohiyo mpaka leo serikali ya kikwete inategemea
5. Wakati wa Mwalimu hapakuwepo mafisadi
6. Wakati wa mwalimu hapakuwepo na bodi ya mikopo why bodi?
7. wakati wa Mwalimu hapakuwepo mfumuko wa bei kama huu wa sasa

JK na CCM wanatakiwa wamwombe radhi mwalimu ameshalala wamwache apumuzike
 
JK hampendi mwalimu toka alivyomuumbua na ile barua dhidi ya bosi wake Sayore.
 
huyu jamaa na mie naamini kuwa kuwa hata yeye hapendi Mwalimu kwani mara kadhaa amekuwa akitaka kujicompare na mwl utafikiri anafikia hata asilimia 0.5 ya mwalimu Mungu awalaani wote wanaobeza juhudi zake .......
 
Kwakweli hata mimi Kikwete kanisikitisha mno ktk hotuba yake ile kumsema baba wa taifa hili hakuliacha tajiri. Pamoja na uliyoyaainisha nami naongeza machache,

1. Reli zetu wamekula.
2. Air Taznania leo limebaki jina
3. Vyama vya ushirika vyote taabani
4. viwanda vy nguo wamemaliza(mashirika ya umma kwa ujumla)

Haya yote kama leo mtu wa gazi ya juu ya uongozi(Rais) na aliyefanya kazi na mwalimu hayatambui je kizazi kijacho kitamkumbukaje baba wa taifa hili?

Mh. rais atuombe radhi watanzania tunaomsadiki mno Nyerere.
 
Huyu ndugu yetu keshachanganyikiwa,anachofanya sasa ni kujipaka kinyesi usoni.TUMUHURUMIE TU!
 
NIMEISOMA HOTUBA JK -sikubaliani kabisa kabisa na kikwete anapodai kuwa Mwalimu aliacha nchi hii si TAJIRI, naomba nimkumbushe kikwete na CCM kwamba Baba wa TAIFA aliacha Tanzania na utajiri wa kutupwa na ni baabda ya kifo chake mafisadi wakaibuka, wawekezaji wanyonyaji wakaingia na kuididimisha nchi hii kwenye umaskani ukashika kasi kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya. Kikwete na CCM wakumbuke kuwa Mwalimu alifanya haya wakati wake
1. Madini yote alitaka Watanzania wayachimbe ni kikwete kama waziri wa madini alishiriki uibaji wa mali yetu hiyo
2. Mali asili na utalii tunayojidai leo ni kwakuwa mwalimu hakuruhusu wizi wakati wake
3. Mwalimu aliwasomesha bure akina kikwete na mafisadi wote wanaotunyonya kwa sasa
4. Mwalimu hakuwa na mgao wa umeme -miradi ya mwalimu ya umeme ndio hiyohiyo mpaka leo serikali ya kikwete inategemea
5. Wakati wa Mwalimu hapakuwepo mafisadi
6. Wakati wa mwalimu hapakuwepo na bodi ya mikopo why bodi?
7. wakati wa Mwalimu hapakuwepo mfumuko wa bei kama huu wa sasa

JK na CCM wanatakiwa wamwombe radhi mwalimu ameshalala wamwache apumuzike

Ni bora Mkapa kwani nijuavo mimi miradi mingi iliyopo sasa ilianzia kwa mkapa na huyu babu janja sijaona mpya kwake

NI kweli akaombe radhi tena kwenye kaburi la Mwalimu na Kugalagala kwenye kaburi lake, Anasema hivo kwa kuwa Chadema walikutana na mama MARIA??

Anahitaji kufanyiwa Maombi kikwete.
 
Wakati Nyerere anamkabidhi Mwinyi madaraka, pale Moshi kulikuwa na viwanda vifuatavyo vikifanyakazi kwa zaidi 50% ya uwezo wake

  1. Moshi Tanneries
  2. Tanzania Bag Corporation - Mill 1 and Mill 2
  3. Kiltimbers
  4. Moshi Plywood
  5. TBL
  6. Moshi Textiles
  7. Coffee Curing
  8. Kibo Match Corporation
  9. Kibo Paper
  10. National Milling
  11. TWICO Imara Furniture
  12. Kilimanjaro Machine Tools
  13. Babu Mkate
Leo hii ni viwanda vingapi vinafanya kazi na vinaajiri watu wangapi ukilinganisha na 1985? Huu mfano ni kwa wilaya moja ya Moshi
 
Back
Top Bottom