Kikwete: Hata Nyerere alishindwa ingawa tunamsifu sana

Siyo cheap excuses, bali ameshindwa kuongoza na hakuwa na hana dira kabisa. eti nyerere alishindwa hapo ndipo kajishushia heshima na kuonekana dhaifu kuliko mrenda
 
Katika sherehe za ccm, kutokana na hotuba ya jk kuwa hata baba wa taifa aliyependwa alishindwa kuongoza sembuse yeye kikwete, kweli nina amini sasa hii ni laana na radhi kwa ccm na kikwete waliyoipata kwa kupuuza ushauri mwingi wa ekima wa baba wa Taifa. Kikwete anasema baba wa taifa alishindwa lakini alikubali kushindwa kwake na aliweka wazi mei mosi 1995 mbeya, kwa kusema awamu yake ilifanya makosa na kilichotakiwa awamu iliyofuata ni kuchukua yale mema yote yaliyofanywa ktk awamu yake na kuyaacha yale mabaya yote yaliyofanywa ktk awamu yake. Lakini kutokana na radhi na laana ya kikwete kutosikia ushauri wa baba wa taifa wao wanafanya kinyume kabisa wanachukua yale mabaya yote ndiyo wanaendeleza na yale mazuri yote ya kuigwa mfano wanayacha matokeo yake nchi inarudi nyuma kwani kila kukicha bora jana. Baba wa taifa kumdisqualify kikwete 1995 si kwaajili ya umri bali ni mjukuu wake katika chama anamjua ndiyo maana tunasema usalama wa taifa wa enzi ya mwalimu walifanya kazi nzuri za kueleweka walikuwa wanaandaa viongozi wazuri hivyo tabia chafu za viongozi wote kama kila malechela na wengineo zilimfikia lakini hawa usalama wa sasa kazi yao haieleweki kabisa zaidi ya kumjaza majungu, na ujinga mheshimiwa.
Bado tutasikia kauli nyingi sana za ajabu ajabu toka kwa JK hii ni laana na Radhi toka baba wa taifa, wanaenda kinyume kabisa hakuna umoja wa taifa kikwete aliuwa umoja wa taifa 2005 alivyounda makundi ndani ya ccm, rushwa kila kukicha, ajira za upendeleo kama si mtoto wa kigogo fulani uwezi pata kazi TRA, BANK kuu na kadhalika kweli ktakuwa na umoja hapo endapo wachache ndiyo wanapata ajira wengine wakiangaika mitaani pamoja na kupata elimu nzuri, rushwa kila kona ya nchi wananchi wamechoka na kukata tamaa. Kweli tutasikia mengi laana/radhi ya baba wa taifa inaendelea kuwatafuna. Hakuna mchawi wa kumshika mchawi ni kikwete mwenyewe.
 
kinachofanyika sasa ni wizi wa mali ya umma basi.aache longolongo,wasubiri siku yao ifike tu.
 
Bora Nyerere, Mwinyi na mkapa walishindwa kuyatatua matatizo kwa kuyapunguza. Je, yeye aliyeyaongeza mpaka sasa anaturudisha huko tulikokuwa tumetoka? Hajui alitendalo, anahitaji atuachie nchi yetu!!!
 
kwa haya tunayoyaona tusitegemee mabadiliko yoyote katika miaka mitano ijayo.
 
vilaza mpo wengi! huna hata uwezo wa ku-argue

Mkuu sasa wewe una tofauti gani na asiyejua ku argue? Una argue kwa maneno nane? Tukikosa la kuandika tukae kimya, wakati mwingine tuwe wasomaji tu.
 
Cerebral malaria hatari sana, Tunaomba wataalam wa tiba wampatie kiongozi wetu tiba inayofaa
 
Laana kajipa mwenyewe Mwl akimpa laana kwa maneno aliyotamka kwenye hotuba yake basi hata miaka mitano inaweza asimalize mwenyewe ataachia atajiuzuru kama Thabo Mbeki ilivyokuwa Afrika Kusini
 
Kwa maneno hayo amejipa LAANA kubwa sana, yeye mwenyewe na CCM, sasa sijui nini kitatokea ngoja tusubiri
 
Leo katika hotuba yake ya siku ya kuzaliwa CCM, kuna kauli nyingi za kikwete ambozo kama rais hakustahili kuzisema, mojawapo ya ,ni kauli yake ya kwamba pamoja na kumsifu sana Nyerere lakini alishindwa kutatua changamoto nyingi katika utawala wake na hivyo hivyo kwa marais wengine waliomtangulia, sembuse mimi (Kikwete). Alisema hayo akijitetea kwamba yeye sio wa kwanza kushindwa kuondoa matatizo ya watanzania.

Mimi nimeichukulia kauli hii kama simple/cheap excuse ya kikwete kwa jinsi alivyoshindwa kutatua matatizo ya watanzania. Sio tu kikwete ameshindwa kutatua matatizo bali ameyaongeza na kufanya maisha ya watanzania kuwa magumu zaidi. Anaweza kutuambia yeye kama rais am-achiave nini, wenzake wote wana vitu vya kujivunia.

Nyerere alijenga umoja wa kitaifa na kufanya watanzania kuwa wamoja na kuwepo kwa amani ambayo kikwete anajivunia leo, lakini pia mzee huyu alijenga uwajibikaji kwa watumishi wa umma kitu ambacho kikwete ameshindwa.

Mzee Ruksa aliruhusu uchumi wa soko ambao ulisaidi kufanya upatikanaji wa bidhaa muhimu ambazo mwanzo zilionekana kama anasa.

Mzee Mkapa akajitahidi kujenga uchumi imara bila kusahau miundo mbinu na kurudisha heshima ya wafanyakazi.

Pamoja na mapungufu yao viongozi waliopita wanayo ya kujivunia.

Akaja kikwete
1) akaharibu kabisa umoja wa kitaifa kwa kuanza na makundi ndani ya CCM (kwa kuanzisha mtandao wake uliowavuruga wengine) na baadae kuharibu umoja taifa zima kwa kuchochea ajenda zake za udini na ukabila.
2) Akabomoa kabisa uchumi alioujenga mzee Mkapa kwa kuendekeza anasa, matumizi makubwa serikalini, kusafiri kwenda kubembea na kuendekeza ununuaji wa magari ya kifahari yasiyo na tija, gharama za maisha zimepanda mno, thamani ya shilingi imeshuka sana, mfumuko wa bei hauelezeki.
3) Ametengeneza mitandao ya wizi kwa kuwatumia marafiki zake kama RA, ED kwa kutaja wachache.
4) Akaharibu kabisa mfumo wa elimu kwa kuanzisha kisiasa shule za kata zisizo na walimu wala vifaa, ukiangalia wanafunzi wanaofeli ni heri hata tungebaki na shule chache bora,maana waliofeli wanabaki kuwa darasa la saba hawawezi kusema wana elimu ya form IV.
Ni mengi jamani yanayoonyesha tofauti ya utendaji kazi wa kikwete na watangulizi wake, naomba niishie hapa.

Lakini Kikwete please dont look for cheap excuses, just admit that ur the most failure president we ever had.

Kwa kweli huyu bwana, yaani Kikwete ni mtu wa ajabu sana.Nilitegemea kwamba ka-degree kake kamoja aliko nako kangemsaidia kuona mbali kidogo,lakini duh,hali imekuwa tofauti kabisa. Alipashwa kuona mbali kidogo.Kwa vile wengine wameshindwa sio lazima na yeye ushindwe.Huu ni mtazamo finyu sana.
 
najuta kuwa kwenye utawala wa jk!!!

kauli yako nh tata coz imenifanya niwe na majibu mawil,moja labda ww ni miongoni mwa watumishi wake(kisiasa) au au unajuta kuwepo ktk kipindi hiki(yaani angalau ungekuwa umeaga dunia) dadavu zaidi kauli yako!!
 
Mr president, are you out of your mind? Do u want 2 compare urself with Nyerere? Never try this and shame upon you! Nyerere achieved a lot of thing and most of his subordinators were efficient and accountable to their responsibilities, those who were against this were expelled and prosecuted for malpractice. Mr Kikwete what yo are doing is just cheating us! How dare are you, to accept and tolerate corrupt subordinators? And yet your telling the world that Mr Nyerere went wrong! So you want to tell us that, although you are wrong enough we are not supposed to blame on you! Guy could you think and feel guilty for rulling the world's top ten poorest country. Have you seen the extent to which inflation affects ordinary people in rural arear, and still you have never made any efforts to solve the problem. Mr Mkapa did a lot on this matter, what about you? To speak the truth, you have proved failure. No one is happy of phaving you!. You always say Mungu ibariki Tanzania, do you think God can bless the country where its leaders who working for themselves and neglecting the God's people who owns the country? Mr president please turn back and think of the faith we had on you and gave the country so that you could lead us towards prosperity and better life. we ask you to pay attention on your people who are living under extreme poverty with inadequate social services.
 
mwl nyerere hajawahi kushindwa ku provide leadership kama kikwete. yeye aliongoza kipindi kigumu cha vita na kupanda bei ya mafuta otherwise angekuwa dhaifu kama jk wangemwondoa kwa nguvu. hivi hujiulizi pamoja na matatizo ya uchumi wakati wa mwl watu walikuwa hawalalamiki? viongozi walikuwa karibu na wananchi na wanashare pinch ya shida
 
Hii hoja inashabihiana kabisa na ile inayotolewa na wadini kwamba tunamlaumu
Jk kwa kuwa ni muislam na kwamba eti Mkapa aliboronga ila hakutuhumiwa kwa sababu ni mkristo.
Hatutaki excuse za aina yoyote,tunataka delivery.Waliotaka kumpindua
Nyerere kutokana na hali ngumu ya maisha walikuwa ni wakristo na
Waislamu,waliomzomea Mkapa kwa ufisadi wa kuuza nyumba za umma,
kujigawia mashirika ya umma n.k walikuwa wakristo kwa waislam.
Hoja ya ku-lift immunity ya Mkapa ilitolewa lakini ikapingwa na JK mwenyewe.
Rais bado una miaka 5 mbele,anajilinganisha na wastaafu au tuseme anajiandaa
kung'atuka?
 
hakuna hoja ya maana,zaidi ya chuki ndo imewatawala. Nyinyi mkisema maneno ya hovyo ok,sisi no. Tatizo JF imeingia ushabiki wa dini na vyama. Nasi twaenda kwa style iliyopo. Kwahiyo tuvumiliane

Kama wote tungeweza kufikiri kama watanzania na sio waislam au wakristo, wakati wote tungeweza kuuadibisha utawala unaoshindwa kutimiza matarajio ya watanzania. Lakini tukiendelea na upuuzi huu wa kabla ya kufikiria hoja iliyotolewa, tunakimbilia kutaka kujua kama aliyesemwa ni wa dini yangu au la na anayestoa hoja ni wa dini yangu au hapana, tujue viongozi wetu watautumia sana udhaifu huu kwa manufaa yao, na hawawezi kuwajibika kwa lolote maana pale wanaposhindwa kutimiza wajibu watajificha nyuma ya watu wa imani yao.

Hivi kufeli kwa watoto mtihani wa kidato cha nne kunachagua kama huyu ni muislam au mkristo? Kama tunataka nchi hii iwe na jamii ya watu sawa ni lazima elimu itolewayo iwe bora maana hawa waliofeli hawawezi kushindana katika soko la ajira na wale waliosoma shule nzuri za binafsi ambazo watanzania wengi hawawezi kuwapeleka watoto wao. Anayetetea elimu mbovu ya Tanzania, hawasaidiii waislam, hawasaidii wakristo, hawasaidii wanavijiji, wala watanzania wanaotaka kuiona Tanzania inastawi.
 
Ebu jamani acheni ku-show up a very big level of ignorance kwenye leadership, hivi kuna watu mmemuona Nyerere mtume?? Nyerere alishindwa vitu VINGI SANA NCHI HII NA ALIFANIKIWA KWNYE VITU VINGI SANA PIA.... this is reality, japo asilimia 99 ya Kikwete ni mbovu bado ana asilimia yake moja ya mazuri.........

Swala la Nyerere kushindwa halijaanza na Kikwete, wasomi, papers, books, articles nyingi zinaandika hayo HUO NDIO UKUBWA NA DEMOKRASIA-VITU VINGI LEO HAVIENDI SOURCE NI NYERERE!!! katiba hii mnaoililia source ni Nyerere he failed!!!!. Cha kujiuliza ni Kikwete kasema kwa mazingira gani?? kasema kwa kebehi kame vile anafabya makusudi kutoongoza nchi vizuri?? kwa nini hasa kasema hivyo??

Lakini hawezi kupata laana kwa kusema hivyo cammon Nyerere ni mtu, siyo mtume, siyo jini, siyo ghost ni mtu, aliishi akafa!!!! haya ya laana is justa nother nonsense ...kwa hiyo tulivyosema Mkapa kaiba, Mwinyi karuhusu Rushwa tutapata laana??? ebu futa thread
 
Back
Top Bottom