mbunghe wa arusha mjini kupitia chadema godbless lema akiwahutubia wananchi wa arusha kwenye mkutano wa hadhara aliwatangazia kuwa WOGA NI DHAMBI KUBWA KULIKO ZOTE DUNIANI...KUPIGANA VITA SIO DHAMBI...NI HERI VITA INAYOTAFUTA USAWA KULIKO AMANI...HIVYO VIJANA, WAZEE NA AKINA MAMA watumie kila walichonacho kupigana, kutokubali kuonewa, kutokuogopa kufa, wajitokeze kupigana VITA.
Je, kwa kauli hizi, lema sio mhaini? lema hajatangaza vita? lema hajahamasisha vurugu na kauli hii sio hatari sana kwa umoja wa kitaifa wa nchi yetu???
Watanzania tusikubali hadaa hizi za wanasiasa, tusikubali laghai hizi za wanasiasa, tutafakari na kutumia akili zetu ipasavyo.
Lema: Hakuna dhambi mbaya duniani kama dhambi ya Woga - YouTube
Raisini Amiri Jesh Mkuu wa nchi hapaswi kutoa kauli ya namna hiyo, usimfananishe na Lema tafadhari, tambua rais alitoa kauli kama mwenyekiti lakin amri yake huwa inapokelewa kama imetoka kwa raisi.