Albert Msando
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 1,019
- 171
Mheshimiwa JK,
Nakusalim!
Hii ni taarifa ambayo nategemea utaifanyia kazi haraka iwezekanavyo!
Nategemea utachukua hatua. Sitaki kuwa mnafiki na nafsi yangu imenisukuma kuwa mkweli. Nakulaumu kwa mengi lakini mengine mimi binafsi nimeyachangia. Wapo wengi humu jamvini wamechangia!
Usipochukua hatua utathibitishia wananchi kwamba wewe huna maamuzi, ni muoga na huwajali wananchi masikini. Utaonyesha wazi kwamba taabu na shida za wanavyuo hazikukoseshi usingizi!
Majina ya hawa wafuatao hawajarudisha mikopo yao na uwezo wa kurudisha wanao!! Kama wangerudisha UVCCM wasingepiga kelele kwamba bodi ya mikopo ivunjwe badala yake wangesimamia tuliokopa turudishe.
1. Mh. Jakaya Mrisho Kikwete - Raisi (sheria haikulazimishi kulipa ila kumbuka ulisomeshwa bure na hali ya maisha haikuwa ngumu kama sasa. Kuna watoto wa masikini wengi hawana uwezo wa kusomeshwa hata kwa kuchangia kidogo sio bure kama wewe. Kama kiongozi kuwa mfano uchangie au urudishe kile ulichosaidiwa ukasoma ili na wengine wasome. Hii itatoa changamoto kwa waliosoma bure na wasiolazimishwa na sheria warudishe hizo 'grants' mlizofaidika nazo! Huo ni uzalendo).
2. Mh. Zitto Kabwe - Mbunge
3. Mh. Halima Mdee - Mbunge
4. Mh. Benno Malisa - Kaimu M/Kiti UVCCM
5. Mh. Martin Shigela - Katibu UVCCM
6. Mh. Ridhiwani Kikwete - Mjumbe UVCCM
7. Mh. Cyril Chami - Waziri (fuata ushauri/mawazo yangu kwa Mh. Raisi wako).
8. Mh. Mhonga Ruhanya - Mbunge
9. Wah. WanaJF wengi tu - Wanaharakati.
10. Mh. Francis Kiwanga - Mkurugenzi LHRC
11. Mh. Mwigulu Nchemba - Mbunge.
12. Wah. Mawakili wote waliosajiliwa Tanzania.(Waliopewa mikopo)
13. Wah. Madaktari wote Tanzania (waliopewa mikopo)
14. Wah. Mahakimu wote waliopewa mikopo.
15. Wah. Majaji wote waliopewa mikopo
16. Wah. Watendaji wote wa serikali waliopewa mikopo
Mheshimiwa Jakaya Kikwete, mimi na wewe na watanzania wengine lazima tuwaambie wanavyuo ukweli! Tulikopa hatujarudisha! Hao UVCCM wote hakuna hata mmoja aliyerejesha mkopo wake!!
Bodi inatoa wapi hela za kukopesha sasa hivi? Au ndio nchi na yenyewe inaenda kukopa??
Fedha ambazo tungerudisha mikopo tunajengea nyumba za kifahari, magari mazuri na kuendea safari dubai etc!
Kwa watakaochukia wachukie, ila niliowataja wote wanaweza kulipa hata kesho! Haiwezekani wote tusingizie kukosa ajira!! Niliowataja wote wana ajira na wanaweza kulipa. Wale ambao hawajapata ajira basi itamkwe kwamba wamesamehewa au watalipa pindi wakipata ajira!!
Kama wanaharakati wameenda mahakamani Dowans isilipwe na mimi nitaenda mahakamani hela za wananchi zilizokusomesha wewe na wengine zirudi ili wengine wazitumie!
Kama mwanaJF tutaungana wote humu jamvini kufungua kesi mikopo irudishwe kwa wale wenye kazi na biashara zinazojulikana!
Huo ni uamuzi mgumu, uchukue na uikoe elimu ya juu na taifa kwa ujumla!
Usafi na uadilifu uwe wa vitendo!! Sio unafiki!
Nakusalim!
Hii ni taarifa ambayo nategemea utaifanyia kazi haraka iwezekanavyo!
Nategemea utachukua hatua. Sitaki kuwa mnafiki na nafsi yangu imenisukuma kuwa mkweli. Nakulaumu kwa mengi lakini mengine mimi binafsi nimeyachangia. Wapo wengi humu jamvini wamechangia!
Usipochukua hatua utathibitishia wananchi kwamba wewe huna maamuzi, ni muoga na huwajali wananchi masikini. Utaonyesha wazi kwamba taabu na shida za wanavyuo hazikukoseshi usingizi!
Majina ya hawa wafuatao hawajarudisha mikopo yao na uwezo wa kurudisha wanao!! Kama wangerudisha UVCCM wasingepiga kelele kwamba bodi ya mikopo ivunjwe badala yake wangesimamia tuliokopa turudishe.
1. Mh. Jakaya Mrisho Kikwete - Raisi (sheria haikulazimishi kulipa ila kumbuka ulisomeshwa bure na hali ya maisha haikuwa ngumu kama sasa. Kuna watoto wa masikini wengi hawana uwezo wa kusomeshwa hata kwa kuchangia kidogo sio bure kama wewe. Kama kiongozi kuwa mfano uchangie au urudishe kile ulichosaidiwa ukasoma ili na wengine wasome. Hii itatoa changamoto kwa waliosoma bure na wasiolazimishwa na sheria warudishe hizo 'grants' mlizofaidika nazo! Huo ni uzalendo).
2. Mh. Zitto Kabwe - Mbunge
3. Mh. Halima Mdee - Mbunge
4. Mh. Benno Malisa - Kaimu M/Kiti UVCCM
5. Mh. Martin Shigela - Katibu UVCCM
6. Mh. Ridhiwani Kikwete - Mjumbe UVCCM
7. Mh. Cyril Chami - Waziri (fuata ushauri/mawazo yangu kwa Mh. Raisi wako).
8. Mh. Mhonga Ruhanya - Mbunge
9. Wah. WanaJF wengi tu - Wanaharakati.
10. Mh. Francis Kiwanga - Mkurugenzi LHRC
11. Mh. Mwigulu Nchemba - Mbunge.
12. Wah. Mawakili wote waliosajiliwa Tanzania.(Waliopewa mikopo)
13. Wah. Madaktari wote Tanzania (waliopewa mikopo)
14. Wah. Mahakimu wote waliopewa mikopo.
15. Wah. Majaji wote waliopewa mikopo
16. Wah. Watendaji wote wa serikali waliopewa mikopo
Mheshimiwa Jakaya Kikwete, mimi na wewe na watanzania wengine lazima tuwaambie wanavyuo ukweli! Tulikopa hatujarudisha! Hao UVCCM wote hakuna hata mmoja aliyerejesha mkopo wake!!
Bodi inatoa wapi hela za kukopesha sasa hivi? Au ndio nchi na yenyewe inaenda kukopa??
Fedha ambazo tungerudisha mikopo tunajengea nyumba za kifahari, magari mazuri na kuendea safari dubai etc!
Kwa watakaochukia wachukie, ila niliowataja wote wanaweza kulipa hata kesho! Haiwezekani wote tusingizie kukosa ajira!! Niliowataja wote wana ajira na wanaweza kulipa. Wale ambao hawajapata ajira basi itamkwe kwamba wamesamehewa au watalipa pindi wakipata ajira!!
Kama wanaharakati wameenda mahakamani Dowans isilipwe na mimi nitaenda mahakamani hela za wananchi zilizokusomesha wewe na wengine zirudi ili wengine wazitumie!
Kama mwanaJF tutaungana wote humu jamvini kufungua kesi mikopo irudishwe kwa wale wenye kazi na biashara zinazojulikana!
Huo ni uamuzi mgumu, uchukue na uikoe elimu ya juu na taifa kwa ujumla!
Usafi na uadilifu uwe wa vitendo!! Sio unafiki!