Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,799
- 30,724
Wanajamvi leo asubuhi nilikuwa natazama TBC1,kulikuwa na tangazo kwamba Rais J Kikwete atazungumza na wazee wa jiji la Dar sijui kama ni leo au kesho.Mara nyingi wazee wa jiji la Dar wamekuwa wakitumiwa na viongozi wakuu wa kisiasa tangu enzi za Mwl J Nyerere kufikisha ujumbe kwa wananchi wote wa Tanzania.
Nahisi Muungwana safari hii atazungumzia kitisho cha mgomo wa wafanyakazi ambao unaratibiwa na vyama vya wafanyakazi.Mei mosi hakualikwa kama ilivyo desturi ya nchi yetu,Muungwana anakuwa rais wa pili kususiwa na wafanyakazi iliwahi kumtokea Mzee Ruksa kipindi cha urais wake vyama vya wafanyakazi vilimualiaka Baba wa taifa Mwl Nyerere badala ya Mzee Ruksa.
Vyama vya wafanyakazi kwa mara ya kwanza vimeistukia serekali ya Muungwana kwamba vinawakumbatia wawekezaji na mafisadi na kuwasahau wafanyakazi wa nchi hii ambao historia inadhihirisha walihusika kupigania uhuru wa Tanzania.Nilikuwa nasikiliza risala ya mgeni rasmi kwenye kilele mei mosi kwa kweli ilimtwanga nyundo ya uhakika Muungwana,serekali na chama chake kwa ujumla.Nategemea kusikia porojo za Muungwana leo/kesho katika mkutano wake na wazee wa Jiji la Dar.Wenye data zaidi tafadhali mtuhabarishe.
====================
UPDATES:
Rais amewashutumu viongozi wa wafanyakazi kuwa ni WANAFIKI na wao ndio wanaoshinikiza mgomo na kusema watakaogoma watakiona cha mtema kuni.
Kasisitiza hakuna mgomo, vinginevyo virungu vitatembea. Pia kasisitiza mgomo ni batili na kinyume cha sheria.
Watakaogoma kupoteza nafasi za kazi?
'Aruhusu' waajiri kuwafungia milango watakaogoma!
Nahisi Muungwana safari hii atazungumzia kitisho cha mgomo wa wafanyakazi ambao unaratibiwa na vyama vya wafanyakazi.Mei mosi hakualikwa kama ilivyo desturi ya nchi yetu,Muungwana anakuwa rais wa pili kususiwa na wafanyakazi iliwahi kumtokea Mzee Ruksa kipindi cha urais wake vyama vya wafanyakazi vilimualiaka Baba wa taifa Mwl Nyerere badala ya Mzee Ruksa.
Vyama vya wafanyakazi kwa mara ya kwanza vimeistukia serekali ya Muungwana kwamba vinawakumbatia wawekezaji na mafisadi na kuwasahau wafanyakazi wa nchi hii ambao historia inadhihirisha walihusika kupigania uhuru wa Tanzania.Nilikuwa nasikiliza risala ya mgeni rasmi kwenye kilele mei mosi kwa kweli ilimtwanga nyundo ya uhakika Muungwana,serekali na chama chake kwa ujumla.Nategemea kusikia porojo za Muungwana leo/kesho katika mkutano wake na wazee wa Jiji la Dar.Wenye data zaidi tafadhali mtuhabarishe.
====================
UPDATES:
Rais amewashutumu viongozi wa wafanyakazi kuwa ni WANAFIKI na wao ndio wanaoshinikiza mgomo na kusema watakaogoma watakiona cha mtema kuni.
Kasisitiza hakuna mgomo, vinginevyo virungu vitatembea. Pia kasisitiza mgomo ni batili na kinyume cha sheria.
Watakaogoma kupoteza nafasi za kazi?
'Aruhusu' waajiri kuwafungia milango watakaogoma!