Kikwete azungumza na Dirk Kempthorne

Masaka

JF-Expert Member
Oct 1, 2007
437
1
Daily News; Wednesday,June 04, 2008 @00:03

Rais Jakaya Kikwete jana alikutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Marekani, Dirk Kempthorne kwenye Ukumbi wa Mikutano ya Kimataifa wa Arusha (AICC) mjini Arusha.

Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu, katika mazungumzo hayo, Rais Kikwete alimweleza Waziri Kempthorne kuhusu juhudi ambazo Tanzania inafanya katika kuhifadhi na kulinda mbuga zake za taifa za wanyama.

Rais pia alimweleza waziri huyo juu ya mafanikio ambayo Tanzania imeanza kuyapata katika kupambana dhidi ya ujangili katika mbunga zake za wanyama. Waziri huyo anamwakilisha Rais George W. Bush na kuongoza ujumbe wa Marekani kwenye Mkutano wa Nane wa Sullivan uliofunguliwa juzi usiku na Rais Kikwete katika Ukumbi wa Simba wa AICC.

Baada ya kukutana na Waziri Kempthorne, Rais Kikwete alikutana na kufanya mazungumzo na mpigania Haki za Binadamu hodari na mwanasiasa wa Marekani, Mchungaji Jesse Jackson. Mkutano huo pia ulifanyika katika Ukumbi wa AICC.

....

http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?id=9435
 
wengine wanapigania vyama, kwi kwi kwi ! wengine wanarithishwa vyama na wakwe zao !
 
Daily News; Wednesday,June 04, 2008 @00:03

Rais Jakaya Kikwete jana alikutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Marekani, Dirk Kempthorne kwenye Ukumbi wa Mikutano ya Kimataifa wa Arusha (AICC) mjini Arusha.

Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu, katika mazungumzo hayo, Rais Kikwete alimweleza Waziri Kempthorne kuhusu juhudi ambazo Tanzania inafanya katika kuhifadhi na kulinda mbuga zake za taifa za wanyama.

Rais pia alimweleza waziri huyo juu ya mafanikio ambayo Tanzania imeanza kuyapata katika kupambana dhidi ya ujangili katika mbunga zake za wanyama. Waziri huyo anamwakilisha Rais George W. Bush na kuongoza ujumbe wa Marekani kwenye Mkutano wa Nane wa Sullivan uliofunguliwa juzi usiku na Rais Kikwete katika Ukumbi wa Simba wa AICC.

Baada ya kukutana na Waziri Kempthorne, Rais Kikwete alikutana na kufanya mazungumzo na mpigania Haki za Binadamu hodari na mwanasiasa wa Marekani, Mchungaji Jesse Jackson. Mkutano huo pia ulifanyika katika Ukumbi wa AICC.

....

http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?id=9435


Baada ya kusoma story hii mbona sioni kuipigania nchi kokote? Kukutana na Kemptone na Jesse ndio kupigania nchi? I don't think so...
 
Kweli kabisa. Si lazima ashike mkuki. Naona anapigania nchi katika mapambano dhidi ya ujangili katika mbuga zetu za wanyama:)
 
Nasapoti juhudi zozote za kuinasua nchi kutoka ktk lindi la ufukara na matata yanayiokabili...
Kama anaipigania kwa mema ni budi kumpongeza ila kama ndo ile kutaka kujulikana basi tumekwisha
 
ulitaka ashike mkuki ndio ujue anapigania nchi??

wewe nawe tumekuchoka na vioja vyako. Unajua tunaweza kukutoa duniani, au haujui ya kwamba sauti ya wengi ni sauti ya Mungu we endelea. Tutakukabizi rasm kwa mpenda haki siku moja akushungurikie
 
Hapo JK anachofanya ni kuitangaza nchi ili watalii waongezeke na pato la taifa likuwe!!!

But kama anapigania nchi as you say "masaka", angedili na hawa wezi(mafisadi) basi wanaopita na hizi fwedha pindi zinapoingia serikalini???mbona yuko kimya.?

Bado nna dought naye!!!
 
Daily News; Wednesday,June 04, 2008 @00:03

Rais Jakaya Kikwete jana alikutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Marekani, Dirk Kempthorne kwenye Ukumbi wa Mikutano ya Kimataifa wa Arusha (AICC) mjini Arusha.

Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu, katika mazungumzo hayo, Rais Kikwete alimweleza Waziri Kempthorne kuhusu juhudi ambazo Tanzania inafanya katika kuhifadhi na kulinda mbuga zake za taifa za wanyama.

Rais pia alimweleza waziri huyo juu ya mafanikio ambayo Tanzania imeanza kuyapata katika kupambana dhidi ya ujangili katika mbunga zake za wanyama. Waziri huyo anamwakilisha Rais George W. Bush na kuongoza ujumbe wa Marekani kwenye Mkutano wa Nane wa Sullivan uliofunguliwa juzi usiku na Rais Kikwete katika Ukumbi wa Simba wa AICC.

Baada ya kukutana na Waziri Kempthorne, Rais Kikwete alikutana na kufanya mazungumzo na mpigania Haki za Binadamu hodari na mwanasiasa wa Marekani, Mchungaji Jesse Jackson. Mkutano huo pia ulifanyika katika Ukumbi wa AICC.

....

http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?id=9435


Katika habari nzika sijaona ambapo inaonyesa JK anapigania Nchi .Naomba mwongozo wa mleta hoja tafadhali .
 
Kweli kabisa. Si lazima ashike mkuki. Naona anapigania nchi katika mapambano dhidi ya ujangili katika mbuga zetu za wanyama:)

Anapigania ujangili katika mbuga za wanyama?? ama anavutia watalii wakuja lala kwenye hoteli yake na shemejize ya kitalii aliyo ijenga kwenye mbuga zetu??

Ndo maana sitoshangaa marekebisho ya mikataba ya madini yanakuja na sera za kuwanufaisha watafiti zaidi kuliko wawekezaji! ( refer Sinclair)

Hakuna jambo analolifanya JK la kuipigania nchi, nyuma ya pazia daima katika move zake ni kuipiga nchi ama kwa kulinda fisadi wenziwe ama kujitengenezea mazingira ya faida zake binafsi!

Haipiganii nchi bali anaipiga kwa hakika, na tusipo simama kidete, makonzi yake yaweza idondosha milele.
Ee maulana tusaidie!
 
Hii naona tumuachie kadaMpinzani na Masaka wadiscuss

Kweli kila ngoma ina mchezaji wake, na jinsi tunavyoendelea kujadili tunapoteza muda wa kujadili EPA na mengineyo, na muda unaenda na wao wanapeta wanakua wametimiza matakwa yao
 
Sasa hivi kaamua pigana katika Sekta ya Wanyamapori kwa kueleza kuna pundamilia na swala na tembo wenye masikio makubwa wangapi sasa hapa Tanzania.

Mbona sioni kama anapigania nchi kwa kupambana na Mikataba Mibovu ya Madini ambatyo inaliingiza taifa gizani katika Bottomless Pit!

Mbona sioni kama anafanya lolote kupigana dhidi ya Mafisadi ambao kafanya juhudi zote kuhakikisha ya kwamba anawakumbatia na kuwalinda kwa uwezo wake Wote akiwa kama Rais wa Jamuhuri?

Tuongelee hao.
 
Anapigania ujangili katika mbuga za wanyama?? ama anavutia watalii wakuja lala kwenye hoteli yake na shemejize ya kitalii aliyo ijenga kwenye mbuga zetu??

Hakuna jambo analolifanya JK la kuipigania nchi, nyuma ya pazia daima katika move zake ni kuipiga nchi ama kwa kulinda fisadi wenziwe ama kujitengenezea mazingira ya faida zake binafsi!

Haipiganii nchi bali anaipiga kwa hakika, na tusipo simama kidete, makonzi yake yaweza idondosha milele.
Ee maulana tusaidie!

Nilitaka "kumuunga" mkono kada kuhusu kuwa hatuna haja ya kuona JK ameshika mkuki kujua kuwa anapigania nchi, isipokuwa ni katika masuala ya ujangili kutokana na mada yenyewe. Hapa ameona kuwa JK kweli anapigania nchi.
 
wewe nawe tumekuchoka na vioja vyako. Unajua tunaweza kukutoa duniani, au haujui ya kwamba sauti ya wengi ni sauti ya Mungu we endelea. Tutakukabizi rasm kwa mpenda haki siku moja akushungurikie

just deal with it !
 
Na sasa Kikwete amekwenda UK kutetea masilahi ya nchi na amewakoromea wazungu kwa matatizo ya uchumi. kiongozi gani afrika anayeweza kuwakoromea wazungu?

Hongera kikwete kwa kuleta maendeleo ya Tanzania!
 
Self serving submissives stupidly supporting a succiduous suicidal stagnant stupor succès de scandale styled staled state.
 
Self serving submissives stupidly supporting a succiduous suicidal stagnant stupor succès de scandale styled staled state.

Pls, layman language(plain English)....inakuwa unatupa kazi kila mara kuangalia dictionary hayo ma jargon yako ni mazito......leave it for crosswords puzzle
 
Back
Top Bottom