Kikwete azidi kun'gara Duniani!

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
Kikwete, Tanzania wavutia nje

Habari Zinazoshabihiana
• Mwaka mmoja madarakani...Rais Kikwete kutoa tathmini leo 21.12.2006 [Soma]
• Kikwete, Salma wamkuna mke wa Rais Bush 30.07.2007 [Soma]
• Lumbanga awa Balozi Umoja wa Mataifa 02.02.2006 [Soma]

Na Godfrey Lutego, Paris

WAKATI nchini Tanzania baadhi ya watu na hasa wa vyama vya upinzani wakimdhihaki na kumpaka matope Rais Jakaya Kikwete, Wazungu na watu wa mataifa mengine wa Ulaya, Marekani, Afrika na nchi za Pasifiki na Karibeani, wamevutiwa naye na kumwona kama alama ya kiongozi wa Afrika kwa vitendo vyake, mwelekeo na anavyoendeleza heshima ya Tanzania tangu enzi za Mwalimu Julius Nyerere.

Hayo yalibainishwa hapa juzi usiku na watu mbalimbali walioshiriki hafla iliyoandaliwa na Tanzania baada ya mchana Rais Kikwete kuhutubia mkutano wa 36 wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kwenye makao makuu yake mjini hapa.

Mkurugenzi wa Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania (COSTECH), Bw. Theophilus Mlaki na Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu, Profesa Peter Msolla ambao taasisi zao ziliandaa hafla hiyo, walisema walikuwa na kazi ya ziada kuwatuliza watu wa nchi mbalimbali za Afrika na Ulaya waliofurika kwenye moja ya kumbi za UNESCO juzi usiku kwa hafla hiyo fupi, waliokuwa na shauku ya kumwona Rais Kikwete kwa karibu, baada ya kuvutiwa naye na hasa kwa hotuba nzuri aliyoitoa alipohutubia mkutano wa 34 wa UNESCO.

"Sasa tunaweza kupumua. Yaani ilikuwa kazi kuwatuliza watu. Ilibidi tuhangaike kuwauliza wasaidizi wake kama anakuja au la, kwani watu walikuwa na shauku ya kumwona," mmoja wa viongozi wa Wizara ya Elimu, Bw. Oliver Mhaiki aliwambia waandishi wa habari baada ya Rais Kikwete kuingia ukumbini na kufanya watu wachangamke, kila mmoja akisalimiana naye kwa kushikana mikono na kupiga naye picha kuonesha walivyovutiwa naye kutokana na uwezo mkubwa wa uongozi aliouonesha katika Afrika hadi sasa.

Naye Bw. Mlaki alisema Tanzania na Rais wake, imejizolea sifa kubwa zaidi kwa ilivyoandaa mambo yake katika mkutano wa mwaka huu wa UNESCO kiasi cha Wazungu kuona fahari na wengine kutangaza ukumbini pale kuwa nao ni Watanzania mmoja akiwa ni Bw. hubert Gijzen, raia wa Uholanzi ambaye sasa ni Mkurugenzi na Mwakilishi wa UNESCO Jakarta, Indonesia.
Mzungu huyo alisema aliwahi kuishi Tanzania miaka minne ya 90 akifundisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Idara ya Fizikia na rafiki zake, Waziri Kiongozi mstaafu wa Zanzibar, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Profesa Juma Kapuya.

"Nchi ni watu si miti. Tanzania ni nchi bwana. Watu wake wakarimu. Nimetembea nchi nyingi duniani lakini Tanzania ni ya pekee. Watu wake ni wakarimu sana. Niliwahi kuishi Mikocheni. Nitakuja tena Tanzania kesho, " Mzungu huyo aliwaambia waandishi wa habari waliokuwa kwenye ziara ya Rais Kikwete, akiungwa mkono na mwanamke mwingine wa kizungu ambaye ameolewa na Mtanzania.

Mwanamke huyo awali alihangaika kumtafuta Rais Kikwete apige naye picha alipoingia ukumbini na baadaye alisema alivutiwa sana naye mwaka juzi wakati wa kampeni na aliposhinda, alisema alitamani siku moja amwone kwa karibu, hivyo juzi alifurahi.

"Wakati wa kampeni nilikuwa naishi kisiwani Mayote na nilikuja Dar es Salaam. Nakumbuka kampeni zilisimama, kwa sababu ya msiba wa mgombea mwenza wa urais wa CHADEMA. Nilipata khanga ya 'Chagua CCM' yenye picha yake lakini sijui iko wapi ningependa nipate nyingine ya CCM. Naipenda CCM," aliwaambia waandishi na kusema ingewezekana, angekuwa mwanachama wa CCM.

Mbali ya Wazungu hao na wengine waliofurahishwa na hotuba ya Rais Kikwete iliyozungumzia mwelekeo wa Tanzania katika elimu na utamaduni na umuhimu na haja ya taasisi za kimataifa kama Umoja wa Mataifa (UN) na mashirika yake kama UNESCO kuzidi kusaidia jitihada za Serikali kuboresha elimu na huduma nyingine za jamii ukiwamo utamaduni, wengine walifurahishwa na jinsi Watanzania walivyokuwa wakicheza muziki wa taarab uliporomoshwa na kikundi cha Daruwesh Sound kinachomilikiwa na msanii wa zamani wa kundi la East Africa Melody, Bw. Mohammed Ahmed Daruwesh, Mzanzibari aliyeweka makazi yake Paris akisema anatafuta maisha huku.

Watu wa mataifa mengine ya Afrika ya Senegali, Mali, Uganda, Kenya, Afrika Kusini wengine wakiwa na bendera za nchi zao, waliujaza ukumbi ambako hafla ya Tanzania ilifanyikia na kuufanya uchangamke zaidi na wengi wakionekana kupiga picha na kuzungumza na Rais Kikwete kwa muda mrefu, kabla hajapiga picha na wasanii wa taarab na kuondoka.

Bw. Mlaki alisema wamekuwa katika mkutano wa UNESCO kama wataalamu wa mambo ya elimu na sayansi na teknolojia yeye na wenzake wa ujumbe wa Tanzania na wamekuwa wakiulizwa sana kuhusu habari za Rais Kikwete na anavyofuata nyayo za Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere na kuendelea kusikika na kusikilizwa na mataifa ya nje na kuwa msemaji wa mataifa mengi ya Afrika.

Awali Rais Kikwete aliwashangaa Watanzania wanaoitukana nchi yao kwa kuwaambia Watanzania wanaoishi Roma, Italia, kuwa wasidhani Wazungu huwa wanawaona wana akili nyingi wanapoikandia nchi yao, bali wakiwapa kisogo huwa wanawang'ong'a kwa kuisema vibaya nchi yao wakati wao, Wazungu wanaiona ni nzuri na wanalilia kuja kuiona.

Aliwaambia Watanzania kuwa wale wanaowaambia Wazungu nchi zao za Afrika ni mbaya wanajitukanisha, kwani Wazungu hao hao baadaye huja kuzungumza na viongozi wa Serikali zao na kuzipa misaada, jambo linaloonesha kuwa wanawaheshimu na kuwaona kuwa nchi yao na uongozi wake unafaa.

Rais Kikwete alisema, Watanzania walioko nje ya nchi hawana budi kuipenda nchi yao na kuisaidia ipige hatua zaidi za maendeleo kwa kuleta wawekezaji, kampuni na asasi kuwekezea katika miradi mbalimbali ambayo wao wanaweza kuwa wabia na Serikali itawasaidia

Rais Kikwete jana jioni alitarajiwa kuzungumza na watanzania wanaoishi Ufaransa na leo anatarajiwa kurejea nyumbani.

Wakati huo huo, Rais Jakaya Kikwete amemteua Bw. Michael Mwanda, kuwa Katibu Mkuu Ikulu.

Uteuzi huo kwa mujibu wa taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi, Bw. Phillemon Luhanjo kwa vyombo vya habari jana, unajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bibi Rose Lugembe, ambaye amestaafu kwa mujibu wa sheria.

Taarifa hiyo ilisema uteuzi huo wa Bw. Mwanda ambaye kabla alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu unaanza rasmi leo.

http://www.dailynews-tsn.com/habarileo/index.php
 
Yale yale ya Mkapa kusifiwa na WB na IMF! wakati Watanzania wanalalamika kila kona ya nchi. Hii sinema tumeshaiona Watanzania na mwisho wake hatukuupenda!
 
Ha ha ha waulize Watanzania kulikoni wakamchukia Mkapa kiasi hicho wakati WB na IMF walikuwa wakimsifia kila kukicha!? Waulize Watanzania nani amewabrain wash mpaka wamchumkie Mkapa kiasi hicho!?Believe me...we have seen that movie before of getting all accolades outside the country, but in reality Watanzania kila kona wanalia.
 
Kwa kawaida ukiwaandalia hafla watu wastaarabu, huwa hawakuambii mabaya yako wa wakati hafla hiyo ikiendelea; watatoa sifa tupu.
 
Nimeisoma hotuba ya Kikwete ktk gazeti la Ippmedia ni nzuri lakini haya tena yanayosemwa na viongozi wetu hawa wapambe yanavuka mpaka. Huyu mzungu aliyedai kuwa yeye ni Mtanzania ameishi Tanzania wakati JK sio kiongozi (rais)kwa hiyo sifa ya Utanzania wake imetoka mbali nyuma wakati wa Nyerere kwa kumbukumbu zake. Huyo mama kamsifia JK na kampeni yake na sio Uongozi wa JKkwani hakuwepo Tanznaia toka JK amekuwa rais. Lakini ajbu ni kwamba yote haya yamewekwa kama mazuri ya JK ktk Uongozi.
Kisha hili swala la wataalam wa elimu ya sayansi na technologia yametoka wapi jamani ikiwa rais wetu alisema malengo ya kukuza elimu nchini ni kujenga taifa lenye elimu ktk fani hii, leo tayari tumesha kuwa wataalam.
Swala la kuifanya elimu ya msingi kuwa ni lazima kwa kila mtoto ni marudio ya mfumo uliotangulia, ujenzi wa shule za secondary nchini bado umekumbwa na tatizo kubwa la walimu na vifaa vya kufundishia sasa hapa watuambie elimu iko wapi ikiwa majumba yapo lakini hakuna walimu wala vifaa vya kutendea kazi. I mean una kiwanja huna nyumba tayari unalinga kuwa na jumba la fahari wakati uwezo huna.
Mwisho ktk swala la kupiga picha hata Osama leo hii akitokea watu watapenda kupiga picha naye tena kwa wingi zaidi. JK is a leader, a President ni fahari ilyoje kwa mtwana kama mimi kupiga picha naye hasa nikiwa tayari ktk hafla ambayo ametokea. was it JK aliyewavuta watu kuhudhulia hiyo Hafla ama mwaliko ulio tayarishwa ndio umealika watu wengi wa mataifa mbali mbali.
Sii kweli sisi watanzania huiponda nchi yetu kwa wazungu, hata kidogo mheshimiwa rais hapo umedanganywa na hao watu wako. Hii ni hisia tu ya viongozi wetu kwani mara nyingi ugonvi wetu sisi na wazungu ni pale wanapojaribu kuiponda Afrika. Ni tamaduni ya mwafrika kuthamini nyumbani hata kama kumegeuka jangwa na kama wapo wanaoiponda Tanzania basi hao tayari wamekwisha kuwa wazungu weusi ktk tabia zao. Hawa pamoja na wazungu hutung'onga tunapowaacha hawana la kusema kuhusu Tanzania!
Kusema mabaya ya JK ama kiongozi yeyote wa Tanzania haina maana tunaitukana Tanzania, hatuna akili za kina Al qaeda wanaochukia Wamarekani na wote wanao support kwa sababu ya Bush na Utawala wake.
 
Mkandara,

Mnyonge mnyongeeni lakini haki yake mpeni. JK ana mazuri pia, na ndio hayo yanayozumziwa.
 
FD,
Hakuna anayekataa kupongeza mazuri lakini hadi sasa bado hayajawa mazuri. JK amefanya jitihada ktk elimu na bado kabisa hatujafikia hatua ya kuita mafanikio. Ni kweli tumpe sifa pale anapostahili lakini tusiongeze maneno kuharibu sifa hizo. yaliyosemwa hapo juu ni kuharibu mchuzi wapishi wamekuwa wakitumia hili neno wapinzani wakati sii kweli hawa watu ni wapinzani ila wale wanaotaka haki itendeke nchini.
Wapinzani wangekuwa msituni ama tungewaona/kuwasikia hao insurgents. Nadhani baadhi viongozi wetu ndio wanajaribu kupaka tope upande wa pili bila kutueleza ukweli wa madai ya hao wapinzani.
 
Usanii unaendelea, sasa wameuhamishia nje ya nchi kutaka kutuonesha JK ni lulu hata kwenye nchi za wazungu. Hao hao wazungu ndo0 wanakuja kumwingiza mkenge
 
Alaaa kumbe JK anaweza kuonana na watu wanaoishi ughaibuni, nilidhani ameiahirisha maana jamaa wa kutoka kwa George William Bush, walileta makasheshe hapa!!!
 
Mkandara,

Mnyonge mnyongeeni lakini haki yake mpeni. JK ana mazuri pia, na ndio hayo yanayozumziwa.

lakini watu hawataki kuoina hayo mazuri. kampeni sio ndogo mzee ! watu wanafumba wenzao vitambaa vyekundu na vyeusi wakati mmoja ili mradi kuficha mazuri ya muungwana kuanika yale mabaya yake !!
 
Wao wamsifie lakini hukumu yetu iko pale pale kwa kutumia njia chafu kufika ikulu, kulifanya bunge kuwa lege lege, kuunda genge ndani ya CCM, uchu, kulindana, uwoga, kupuuza wapinzani, matumizi yasiyo ya lazima ya fedha zetu, kutoa vyeo kwa kulipa fadhila, kukumbatia matajiri ndani ya serikali, kutokuwa na political ideology inayoeleweka, kutokuwa na mipangilio mizuri ya kiutendaji, kutaka kufanya vitu vingi kwa wakati mmoja na kusababisha gharama kubwa za kuendesha nchi, kutokusimamia kauli zake, rejea kauli ya kutokusaini mikataba ya madini mpaka sheria na sera zifanyiwe mabadiliko, kutumia muda mwingi nje kuelezea umaskini wa Tanzania na kusahau kuunganisha nguvu za wananchi kutumia resources zetu kuendeleza nchi, kutanga mbali na sera ya kujitegemea, kutumia vitu visivyo vya msingi kuwapumbaza watanzania rejea michezo, kupoteza mwelekeo wa kiuongozi, Kuibuka kwa jina la UFISADI katika nchi hii katika utawala wake, nieleza ni wakati gani liliwahi kutumika nchini kama siyo Kenya? Kuruhusu mambo yasiyo ya kimaadili kutawala serikali yake na chama chake rejea rushwa, kujenga tabaka la kiuongozi yeye na marafiki zake na familia yake. Haya ni machache tu, maana yale ya maendeleo kama ujenzi wa miundo mbinu ya nchi bado.
 
Wazungu lazima wamsifie kwa sababu anawatukuza wazungu na kuwadhalilisha waafrika wenzake. Kama wao wanampenda sana wamchukue akawe rais wao na sio sisi kwani hizo rasilimali anazoiba na mafisadi wenzake ni za kwetu sisi WTZ na wala sio za wazungu.
 
Chanzo cha habari yenyewe ni Daily News, waongeaji wote ni wapambe wa JK, unategemea nini zaidi ya misifa?
 
I think it easy kufanya analysis why Mataifa ya Ulaya na Marakani wanamsifia, this is not a rocket sience.
(1)Most of the ivestors in Tanzania today are from europe and America, and the enjoy free lunch(law tax, subsidization from government, non labor law), so you think European and American will hate JK?

2. Most of this countries zinazomshabikia ni wanafiki, and thats how politics is. Angalia US walivyokuwa wanaichukia pakistan, lakini walipo pewa anga kumpiga afrighan, they call Pakistan allie. Thats how politics is, when i benefit from you i will always talk good things about you, and when you against me your dictator, you dont care about your people, your corrupted and many other things. So lets get use to this ass kisser
 
Kama alivyosema Kichuguu hapo juu, watu wastaarabu ukiwaalika kwenye hafla yako hawatakusema kwa mabaya yako, watakusitiri, ndicho kilichofanyika.

Hiyo ya eti walikuwa wanaulizia sana anakuja saa ngapi huyo mwandishi anachukulia kwamba walikuwa na shauku sana ya kumwona, pengine walikuwa na wasiwasi kama ata-keep timeau ataleta uswahili wa kuwagandisha watu...you never know, inawezekana ilikuwa hivyo au la, najaribu tu kuangalia upande mwingine tu!

Kuhusu mazuri ya JK, inawezekana kweli anayo, binafsi sijawahi kuyasikia, labda tatizo ni kwamba madhaifu yake ni makubwa zaidi sana kuzidi hayo mazuri.

Aidha kama kuna kampeni ya kumchafua mheshimiwa raisi nadhani yeye mwenyewe anaiongoza vizuri huku baraza lake la mawaziri likimsaidia na wapambe wake wakihakikisha anafanikiwa.
 
Back
Top Bottom