Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,227
- 113,583
Baadhi ya Wabongo ndivyo walivyo.
Kuna yule binti, Esther Wassira, wakati alipojiunga humu alimwagiwa masifa kemkem.
Watu wakawa wanasema ni kichwa sana na kumpa kila aina ya sifa.
Binafsi sikuona lolote alilolisema (andika) humu ambalo lilikuwa geni au jipya sana.
Inavyoelekea kwa wabongo (baadhi) mtu akiongea common sense wanavutika sana na kuona kama miujiza vile.
Kwangu mimi hiyo ni dalili ya kuzoea na kukubali viwango vya chini sana katika mambo kiasi kwamba akijitokeza mtu na kuvuka kidogo tu hivyo viwango basi, anatunukiwa 'ukichwa'.