EasyFit
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 1,269
- 1,082
Rais Jakaya Kikwete amewaachia huru askari polisi wawili Koplo Juma Mswa na Konstebo Mataba Matiku waliokuwa wamehukumiwa adhabu ya kifo mwaka 1998 baada ya kupatikana na hatia ya kumuua kwa makusudi Mkurugenzi wa zamani wa Usalama wa Taifa, Luteni Jenerali Imran Kombe. Wamekuwa gerezani takriban kwa miaka 16, wamechiwa huru kwa huruma ya Rais ambaye alipunguza adhabu hiyo ya kifo, kuwa kifungo cha miaka miwili jela.
Kombe aliuawa kwa kupigwa risasi nne kifuani Juni 30, 1996 baada ya polisi waliokuwa wakisaka gari aina ya Nissan Patrol mali ya W. Ladwa, kumfananisha na mtuhumiwa sugu wa wizi wa magari.
::Mwananchi::
Kombe aliuawa kwa kupigwa risasi nne kifuani Juni 30, 1996 baada ya polisi waliokuwa wakisaka gari aina ya Nissan Patrol mali ya W. Ladwa, kumfananisha na mtuhumiwa sugu wa wizi wa magari.
::Mwananchi::