Kikwete atunukiwa cheti!

Bangoo

JF-Expert Member
Nov 3, 2011
5,597
1,005
Chuo kikuu cha tiba na sayansi muhimbili kimemtunuku cheti Rais Jakaya Mrisho kikwete kwa kutambua mchango wake katika sekta ya afya!
Ni kweli anamejitahidi kiasi lakini siungi mkono kila mara kumrundikia kiongozi vyeti kila mara!

Huyo ni Raisi anayofanya ni wajibu wake, na anatumia kodi zetu kuboresha sekta ya afya sasa hivyo vyeti vya nini

nchii hii tunakoelekea ni kuja kuwa na Raisi profesa asiye na elimu hiyo!
 
Rais wetu ukimsifia tu tayari anakupa unachotaka na ndiyo maana wanafanya hivyo ili awaangalie ktk chochote
 
Dongee kimewaumaaa haloooo

sizani kama ni donge ila Watanzania hawa ambao ni ma-great thinkers wanajaribu kufikiria mbali zaidi ambapo wajinga na wasio na upeo kama wewe hawawezi kufikiri, ulijaribu kujiuliza kwa nini Mwl hakuitwa Dkt na alibakia kuitwa Mwl. Mpaka wakati huu waleo japo ni marehemu.
 
Ni nchi pekee duniani hospitali kuu ya taifa wagonjwa wanalala chini! Alafu leo wanampa cheti!
 
Wanajipendekeza ili waongezewe mishahara na posho.
Njaa mbaya sana! Yuda alimdalalia Yesu!! Madaktari wakamtoa kafara ULIMBOKA!! sasa wanamuona Dhaifu ni bora na mwema kwao. SHAME ON THEM.
 
Na atakapokuwa anaachia madaraka tutampa LEAVING CERTIFICATE akaonyeshe wajukuu na vitukuu vyake huko.
 
Mwalimu Nyerere alichelewesha uhuru wetu ili nchi nyingine zijikombolewe, alijenga chuo kikuu cha dar salaam, amejenga mashule mengi sana,hivi mbona hakupewa hata cheti!

Ilikuwa ni wajibu wake
haiwezekani kila kitu kumpongeza wakati ni wajibu wake aliokabidhiwa na wananchi.

Nelsoni mandela mbona siyo dkt,
Kwame Mkuruma,
Jomo Kenyata,
Gadaff, clintoni,
Tufike mahali tuache haya mambo ya kipuuzi.

Haijawahi kutokea wananchi kuwa na hali ngumu kama kipindi cha jk leo mnampa tuzo.
 
Mwalimu Nyerere alichelewesha uhuru wetu ili nchi nyingine zijikombolewe, alijenga chuo kikuu cha dar salaam, amejenga mashule mengi sana,hivi mbona hakupewa hata cheti!

Ilikuwa ni wajibu wake
haiwezekani kila kitu kumpongeza wakati ni wajibu wake aliokabidhiwa na wananchi.

Nelsoni mandela mbona siyo dkt,
Kwame Mkuruma,
Jomo Kenyata,
Gadaff, clintoni,
Tufike mahali tuache haya mambo ya kipuuzi.

Haijawahi kutokea wananchi kuwa na hali ngumu kama kipindi cha jk leo mnampa tuzo.

Point of correction:Mwalimu Nyerere alipokea udaktari wa heshima mara nyingi zaidi ya kiongozi yoyote hapa Tanzania,lakini hakutaka kuitwa Dr.
Kwa kweli alistahili.
 
waliompa hicho Chet ni Madaktari au hospital. Siamini masikio yangu. Watanzania tuwe makini na matendo yetu katika macho ya Ulimwengu. Haingii akilini mwezi April mnagombana na Serikali kwa Maslahi duni mwezi November mnatoa cheti kwa kiongozi kwa lipi alilofanya. mishahara imepanda? T scan imepona au imenunuliwa mpya? ? NYIE NI MADAKTARI AU WAGANGA WA KIENYEJI?
 
Hao walitoa hicho cheti waache kujikomba!hata miezi 6 bado tangu mgomo mkubwa vile leo mnamtuni cheti kwa lipi?kufanya anayofanya kwa mapungufu ni wajibu wake na alitakiwa afanye na zaidi.....
 
Raisi anajua siku moja ataulizwa alifanya nini akiwa rais. Sasa lazima awe na ushahidi wa vyeti/ Degrees etc. sijui ni kwa nini washauri wake wanaona kuwa hii ni njia nzuri ya kujenga trust/profile ya Rais. Au wanampa ile kitu ambayo roho yake inapendaa????????? Hawezi kataa?????? Au kama hamna zawadi nyingine anadai angalau chetiii??? Mr President, kweli???
 
Chuo kikuu cha tiba na sayansi muhimbili kimemtunuku cheti Rais Jakaya Mrisho kikwete kwa kutambua mchango wake katika sekta ya afya!
Ni kweli anamejitahidi kiasi lakini siungi mkono kila mara kumrundikia kiongozi vyeti kila mara!

Huyo ni Raisi anayofanya ni wajibu wake, na anatumia kodi zetu kuboresha sekta ya afya sasa hivyo vyeti vya nini

nchii hii tunakoelekea ni kuja kuwa na Raisi profesa asiye na elimu hiyo!

Si bora ya kuwa hivyo kuliko Maprofesa halisi ambao hatuoni hata uprofes wao unaisaidia vipi nchi hii

"Tumefika hapa tulipo kwa sababu tumeruhusu akili ndogo itawale akili kubwa" (Msigwa, 2012)
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom