Kikwete Atibiwa Muhimbili: Mfano mzuri, for a change!

Dilunga

JF-Expert Member
Apr 8, 2009
679
49
Rais Kikwete apima macho hospitali ya Muhimbili

Patricia Kimelemeta na Devotha John

RAIS Jakaya Kikwete jana alifanyiwa uchunguzi wa macho na kutibiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).

Mwananchi ilinasa habari hizo kwenye Hospitali ya Muhimbili na baadaye kuthibitishwa na afisa uhusiano wa hospitali hiyo, Aminiel Aligaisha kuwa Rais Kikwete alikwenda hapo kuchunguzwa macho.

Rais Kikwete alifika hospitalini hapo majira ya saa 5:30 asubuhi na kuingia vyumba namba 44 na 46 ambako alikutana na madaktari na kupatiwa huduma.

Kwenye chumba namba 44 ndiko mkuu huyo wa nchi alipimwa macho na baadaye kuingia chumba namba 46 ambako alipewa miwani na kupata ushauri.

Wakati Rais akiwa anahudumiwa, huduma kwa wagonjwa wengine wa macho katika vyumba hivyo, zilimama kwa muda.

Afisa habari wa Muhimbili, Aminiel Aligaisha alisema hiyo si mara ya kwanza kwa Rais Kikwete kupatiwa matibabu kwenye hospitali hiyo kubwa kuliko zote nchini.

Alisema mara kadhaa Rais Kikwete hufika hospitalini hapo kuchukua vipimo na kutibiwa na hivyo si jambo la ajabu kwa wale wanaofahamu utaratibu huo wa rais.

Baadhi ya wagonjwa waliozungumza na gazeti hili hospitalini hapo walieleza kufurahishwa na kitendo cha Rais Kikwete kutumia hospitali za hapa nchini kupata matibabu.

Walisema utaratibu wa baadhi ya viongozi kwenda kutibiwa nje ya nchi si mzuri hasa kwa nchi maskini kama Tanzania.

"Tunapomwona rais wetu anakuja kutibiwa kwenye hospitali ya hapa nchini, tuna imani kwamba anajali wananchi kwa sababu tunaamini kuwa viongozi wengi wanatumia hospitali za nje kupima afya na kupata matibabu," alisema Musa Abdalah.

Aliongeza kusema: "Hali hiyo imeonyesha uzalendo wa kweli ambao viongozi wengine wanapaswa kuiga kwa maendeleo ya nchi na watu wake."

Ujio wa rais kwenye hospitali hiyo jana ulikuwa wa kawaida ikilinganishwa na misafara yake mingine wakati anapokuwa anafanya ziara za kikazi.

http://mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=14209
Kwa hili Kikwete apongezwe na kuigwa...
 
Kwa kweli nimefurahishwa sana na kitendo hiki cha Rais kuoonyesha kuwa anathamini huduma za afya zitolewazo na taasisi zetu.

Imekuwa kawaida ya viongozi wetu na familia yao kwenda Ulaya kwa gharama za serikali kwa ajili ya huduma za afya nyingine zikiwa ndogo sana na nyingine zinazoweza kuepukika kwa kubadili life style zao.
 
Kwa hili Kikwete apongezwe na kuigwa...

Apongezwe kwa kipi?. Alitakiwa baada ya kutibiwa atoe tamko kuwa ni marufuku kwa hela ya serikali kutumika kutibia watu nje ya nchi. Serikali iboreshe huduma za afya zilizopo nchini ili kuvutia watu wa nchi nyingine kuja kutibiwa Tanzania.

Serikali ingepiga marufuku viongozi kutibiwa nje basi ni dhahiri inge invest kwenye huduma bora za afya nchini. Hiki kitendo alichofanya ni usanii wa kuelekea 2010 election, hawana nia ya kuboresha huduma nchini kwani wao haziwahusu wakiugua tu wanaenda nje ya nchi.
 
..hivi mnategemea JK anaweza kulazwa au kufanyiwa upasuaji Muhimbili, KCMC, Bugando, Ocean Road, au Bombo?

..mara alipochaguliwa alitembelea magereza na hospitali ya Muhimbili, sasa naomba mnieleze mabadiliko yaliyotokea.
 
..hivi mnategemea JK anaweza kulazwa au kufanyiwa upasuaji Muhimbili, KCMC, Bugando, Ocean Road, au Bombo?

..mara alipochaguliwa alitembelea magereza na hospitali ya Muhimbili, sasa naomba mnieleze mabadiliko yaliyotokea.
Mkuu JokaKuu umenikuna hapo!

Halafu hivi JK hajaenda Geneva kwenye mkutano wa Climate Change? Au kaona aibu safari hii katuma wawakilishi?
 
Labda alifanya usanii tu,kila siku yuko ulaya halafu kutibiwa atibiwe bongo??????????its called political stunts..........

Ni usanii tu wa kujiandaa na 2010, hakuna lolote! Akiwa mgonjwa hatathubutu kukanyaga Muhimbili.
 
Apongezwe kwa kipi?. Alitakiwa baada ya kutibiwa atoe tamko kuwa ni marufuku kwa hela ya serikali kutumika kutibia watu nje ya nchi. Serikali iboreshe huduma za afya zilizopo nchini ili kuvutia watu wa nchi nyingine kuja kutibiwa Tanzania.

Serikali ingepiga marufuku viongozi kutibiwa nje basi ni dhahiri inge invest kwenye huduma bora za afya nchini. Hiki kitendo alichofanya ni usanii wa kuelekea 2010 election, hawana nia ya kuboresha huduma nchini kwani wao haziwahusu wakiugua tu wanaenda nje ya nchi.

True, true, angeweze kusema anapiga marufuku viongozi kutibiwa nje. Lakini nadhani kuonyesha mfano pia ni njia nyingine tofauti, japo sio robust kama kutoa amri za marufuku. Kikwete hana ethics deep kiasi hicho, au principle za kupiga marufuku matibabu ya nje, lakini, Hostede, nadhani kwa upeo wake amejitahidi. Kwa kuanzia.

Wenzake labda wataona aibu.
 
Halafu nyie wadanganyika nani amewaloga?. Kama anatibiwa na huduma zinasimama kwa watanzania WOTE si afadhali aende nje ya nchi?????????? wanakufa wangapi kwa humduma kusimama ili atibiwe yeye pekee yake!!

Je maisha ya watanzania elfu ni sawa na Rais pekee yake jamani??, labda kwenye vita tu!
 

..hivi mnategemea JK anaweza kulazwa au kufanyiwa upasuaji Muhimbili, KCMC, Bugando, Ocean Road, au Bombo?

Sidhani, Joka Kuu, nadhani hawezi.

Lakini tulichonacho mbele yetu ndio hicho, ametibiwa Muhimbili. Hayo mengine yote ni imaginations nzuri, kwamba ikiwa hivi itakuwaje, "hivi mnategemea akihitaji upasuaji atatibiwa Bombo" hayo yote tunaweza kuyajibu kabla ya, lakini ni speculations tu. Kwa sasa, kwa alichoonyesha so far, nadhani ni chema.

..mara alipochaguliwa alitembelea magereza na hospitali ya Muhimbili, sasa naomba mnieleze mabadiliko yaliyotokea.
Well, hakuna mabadiliko makubwa ya hali za mahospitali, labda (maana anaweza kusema Muhimbili wamejenga vitengo vipya since, kikiwepo cha Moyo kama kimeshamalizika) lakini hiyo ni mada nyingine nadhani. Tunaongelea yeye kukubali kutibiwa katika hali hiyo mbaya, wanakotibiwa wananchi, ni mfano kwa wenzie.

Hivi high-lifers kama kina Lowassa wanaweza kuvaa miwani ya waganga wa KCMC? Naona JK hapo amejitahidi.
 
Invisible, Dilunga,

..wangetueleza aina ya uchunguzi wa macho aliofanyiwa.

..isije ikawa amekwenda kwa shughuli ndogo ya kupima miwani mipya halafu wananchi tunaona ni big deal.

..vilevile haijulikani alitumia muda gani hapo Muhimbili, na madaktari wangapi walimhudumia. hiyo inaweza kutusaidia kujua case yake ni serious kiasi gani.

NB:

..hivi ile zahanati ya Ikulu pale karibu na ofisi ya waziri mkuu imefungwa?

..vilevile hivi mnaona Muhimbili ni hospitali ndogo hiyo? je, kila mlalahoi[shangazi na mjomba kule kijijini] anaweza kufika hapo?

..siku JK akienda kuchomwa "shindano" kwenye zahanati ya Lugoba basi ndiyo nitaona yuko serious na kuondokana na dhana ya kutibiwa nje ya nchi.
 
..siku JK akienda kuchomwa "shindano" kwenye zahanati ya Lugoba basi ndiyo nitaona yuko serious na kuondokana na dhana ya kutibiwa nje ya nchi.

Tupo pamoja...hili la kwenda Muhimbili ni usanii tu 2010 ipo njiani...hizo ni pipi tu! Alikwenda magerezani hakuna kilichoboreshwa, alikwenda bandarini hali ni mbaya zaidi....
 
... Kama anatibiwa na huduma zinasimama kwa watanzania WOTE si afadhali aende nje ya nchi?????????? wanakufa wangapi kwa humduma kusimama ili atibiwe yeye pekee yake!!

Je maisha ya watanzania elfu ni sawa na Rais pekee yake jamani??, labda kwenye vita tu!

Rais angepanga foleni kumuona daktari ndugu? Rais anapanga foleni kwenye traffic barabarani?

Tusiongee mradi tumeongea tu, hizo hoja sasa hazina mwelekeo. Nchi gani Rais anapanga foleni kupata huduma in the public square? Kumuita mtu Rais, moja ya maana zake na uzito wake ni kwamba tunampa dhamana ya heshima na kumpisha kwenye foleni.

Halafu hujui, labda alikuwa na appointment na hao madaktari, ndio maana Wananchi wakasogea pembeni.
 
Apongezwe kwa kipi?. Alitakiwa baada ya kutibiwa atoe tamko kuwa ni marufuku kwa hela ya serikali kutumika kutibia watu nje ya nchi. .....

Hofstede; Hata mimi naona kwa hilo apongezwe kwani kama unafuatilia viongozi wetu hata mafua inabidi wapande ndege wakatibiwe ulaya au india. Kama Mkuu wa kaya JK ameonesha kuwa yeye anatibiwa Muhimbili nadhani wengine wote watafuata mkumbo hata kwa shingo upande- si unajua wanavyojua kujipendekeza?

Si lazima JK atoe tamko rasmi, yeye kuanza kutibiwa Muhimbili ni tamko tosha!- Na viongozi wengi walivyowaoga wa kumwaga unga watakuwa wanafoleni Muhimbili na kwingineko kama KCMC au Bugando!

Ila, binafsi nahisi watakuwa wanaenda majuu kutibiwa kinyemela, si waziwazi kama ilivyo sasa.

Once again, pokea tano JK kwa kuonesha mfano mzuri.
 
Tupo pamoja...hili la kwenda Muhimbili ni usanii tu 2010 ipo njiani...hizo ni pipi tu! Alikwenda magerezani hakuna kilichoboreshwa, alikwenda bandarini hali ni mbaya zaidi....


Mchanga wa macho tu huo matibabu mengine yatafanywa mkishamchagua mwakani, ndio atakwenda marekani hapo ni geresha tu politics is a dirty game wahenga eeeehhhh
 
..jamani amekwenda kupimwa miwani. sasa hiyo mnaona ni big deal?

..ninavyoelewa mimi Muhimbili ni hospitali ya Rufaa, sasa JK alipata hiyo referal toka hospitali ipi?

..isije ikawa hata hicho kitendo chake cha kudamkia Muhimbili kwa ajili ya matibabu ni ukiukwaji wa taratibu.

..je, kupima miwani ni matatizo ambayo yanalazimisha aende Muhimbili, badala ya Mzani Mmoja, Mwananyamala, au Temeke?
 
Labda alifanya usanii tu,kila siku yuko ulaya halafu kutibiwa atibiwe bongo??????????its called political stunts..........

Mijitu mingine bwana, sasa akiumwa wakati yupo kazini ulaya, arudi bongo kutibiwa? Mijitu ya Ulaya mingapi ikiumwa hapa kwetu ina tibiwa hapa hapa?

Mijitu mingine bwana kazi kuponda tu, hata haya haioni?

JMK kaumwa Tanzania katibiwa Tanzania na for your information anaposafiri kote anafatana na Daktari wake official ambae ni kijana wa ki Tanzania aliebobea kwa tiba tofauti. Na kama yupo nje na kuumwa kwake kutahitaji vipimo au kulazwa Hospitali au uchunguzi wa Daktari bingwa wa tatizo lake, kwa nini asiende hospitali? na ikiwa yupo hapa nchini tumeona mfano, anakwenda hapo hapo panapotibiwa wa Tanzania wengine, hiyo pekee tosha kuwa motisha kwa wanaotowa huduma hapo Muhimbili.

Hongera JMK kwa yote uyafanyayo, kuna mijitu yenye chuki binafsi hata ufanye nini kwao inakuwa si kitu, tena kila unapofanya zuri na jema wao ndio huzidi kukereka na kutafuta kila hila na mbinu ya kulifanya lionekane si jema, lakini mwisho wa siku, uyafanyayo kwa nchi na wananchi wako tunayaona na yote ni mema na yote yana nia njema kabisa, mwenye macho haambiwi tazama, mwenye masikio haambiwi sikia.
 
..jamani amekwenda kupimwa miwani. sasa hiyo mnaona ni big deal?

..ninavyoelewa mimi Muhimbili ni hospitali ya Rufaa, sasa JK alipata hiyo referal toka hospitali ipi?

..isije ikawa hata hicho kitendo chake cha kudamkia Muhimbili kwa ajili ya matibabu ni ukiukwaji wa taratibu.

..je, kupima miwani ni matatizo ambayo yanalazimisha aende Muhimbili, badala ya Mzani Mmoja, Mwananyamala, au Temeke?

Uelewe kuwa JMK katika moja ya privileges zake kama Mkuu wa nchi, ana Daktari wake, na huyu Daktari wa JMK ni mTanzania na ametokea hapo Muhimbili na yeye ndie anaeweza kumpa referal ya kutibiwa panapoonekana anastahili kutibiwa. Si lazima akaanzie Mnazi Mmoja kama utakavyo wewe, after all, he is THE PRESIDENT of The United Republic of Tanzania and he must have his privileges.

For your information, kitengo cha kupima miwani Muhimbili hakihitaji uwe na referal yoyote.
 
Dar Es Salaam,

..asante kwa taarifa kwamba kupimwa miwani Muhimbili hakuhitaji referal.

..swali langu liko palepale: kwanini hakwenda Hospitali ya Mnazi mmoja,Temeke, au Mwananyamala?

..labda JK kwenda hospitali hizo za walalahoi anahitaji referal.

..JK kuwa na daktari Mtanzania siyo big deal. hilo lipo kwa viongozi wote wakuu.
 
Back
Top Bottom