Kikwete asema Profesa Benno Ndulu ndiye aliyeleta utaratibu wa malipo ya fedha kwa njia ya simu

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Mar 8, 2020
2,204
4,692
Dar es Salaam. Rais wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete amesema gavana wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu ndiye aliyetoa fursa kwa mitandao ya simu kuanza kutoa huduma za kifedha hapa nchini.

Kikwete aliyasema hayo Aprili 22 nchini Marekani wakati wa majadiliano maalumu ya kumbukizi ya Profesa Ndulu yaliyoandaliwa na Chuo Kikuu cha New York (NYU) kupitia jukwaa lake la Africa House.

Profesa Ndulu alikuwa Gavana wa BoT kuanzia mwaka 2008 hadi 2018 alipostaafu. Mtaalamu huyo wa uchumi alifariki Februari 21 mwaka huu jijini Dar es Salaam katika Hospitali ya Kairuki.

Katika hotuba yake aliyoitoa katika majadiliano hayo, Kikwete alisema wakati akiwa Rais, Profesa Ndulu alimpelekea wazo lake la kuanzisha huduma jumuishi za kifedha, akamruhusu, sasa wazo hilo limeleta matokeo makubwa.

Alisema uamuzi wake huo ulisababisha ongezeko la huduma jumuishi za kifedha kwa wananchi kutoka asilimia 16 zilizokuwapo mwaka 2009 hadi asilimia 65 mwaka 2018 alipostaafu kama Gavana wa Benki Kuu.
 
Mwaka 2009 nikiwa darasa la nne bibi yangu M-Pesa alikuwa anaiita Mapesa. Hata transactions za mitandao mingine zilizofuatia aliziita hivohivo mpaka badae akajua kuzitofautisha. Mwanzoni alikuwa anagoma wasitume hela uko akidai itaibiwa na wafanyakazi wa mitandao ya simu.
 
Nitamkumbuka Nduru kwa kuigeuza shiling yetu kuwa pesa ya madafu,mpaka ilifikia kupata chumba na sebule mitaa ya ostbah au massaki mpaka uwe na dollar,na kuruhusu watu wajichotee hela BOT jinsi wanavyo taka,kwanza aliisha tuhumiwa na bunge kuwa aliishi kifisadi.
Alikuwa na mamlaka gani yakuruhusu watu wachote Hela BoT
 
Hii miamala ya kifedha kwenye simu imekua msaada mkuvwa sana.
Nikweli kabisa mkuu, upo zako Kakonko huko unamtumia Bi mkubwa aliye Namanyele buku ten.....maisha yanasonga mbele.....au umekwama sehemu unahitaji msaada mshikaji anakuboost unasaidika....maisha yanaenda
 
Back
Top Bottom