Kikwete anunuliwa na wamarekani?

Mwafrika wa Kike

JF-Expert Member
Jul 5, 2007
5,185
56
Vyanzo vyangu vya hapa USA vimethibitisha uvumi ambao kwa muda umekuwa unaendela Tanzania kuwa serikali ya marekani ina mpango wa kujenga kituo cha kijeshi cha kudumu (permanent base) nchini Tanzania.

Ingawa serikali ya Tanzania imekuwa inajaribu kuficha hizi habari kwa visingizio kuwa mambo ya kijeshi hayajadiliwi kwa vile yanahusu usalama wa taifa, nimeamua kuwaambia wanajeshi kuwa hili suala la kuwa na base ya wamarekani Tanzania ni kubwa na hivyo ni vyema wakaruhusu watanzania wakalijadili.

Siku za karibuni Kikwete amekuwa na vikao vya wazi na vya siri na wamarekani ambao wanatafuta nchi katika pwani na pembe ya afrika ili wajenge kambi ya kijeshi ya kudumu kama ile waliyo nayo kule KATARI (sijui namna ya kutamka hii nchi kwa kiswahili) kule mashariki ya kati.

Wazo la kuweka kambi Ethiopia limeonekana gumu kutokana na hali ya usalama, chaguo la pili la marekani lilikuwa Kenya ambayo hali ya ukabila inatishia usalama wa Kenya. Wamarekani wameamua kuchagua Tanzania ambao so far wanaona kama nchi yenye amani na utulivu.

Habari zinasema kuwa kimsingi Kikwete amekubali (nani angekataa pesa kibao wamarekani walizotoa) na Marekani imelipa pesa indirect kwa kuahidi kutoa mabilioni ya pesa za msaada. Yes, hizi pesa walizoahidi juzi za kuisaidia Tz zitaishia mfukoni mwa wachache na zitakazobaki zitasaidia kujenga base.

MY TAKE.

1. Mimi naunga mkono suala la wamarekani kuwa na base ya Tanzania maana ikiwepo au isiwepo sioni faida au hasara yoyote ukichukulia kuwa Kikwete na wenzake wanauza nchi kila siku.

2. Ni vizuri Kikwete aendeleze mchezo wa kula pande zote mbili za wa-Irani na wamarekani.

3. Kikwete awaambie ukweli wa-Tanzania wa kile kinachoendelea.

4. IMF na Benki ya dunia wakome kusifia Tanzania kuwa inaendelea wakati wakijua ni uongo ila wanatimiza moja ya masharti ya Tz kukubali ku-host base ya marekani.

5. Kikwete atimize ahadi yake kabla Raila hajashinda uchaguzi wa Kenya maana Raila naye amekubaliana na wamarekani katika hili.



Thanks!
 
Hiyo ya kuja tena nimeshaisikia. Si anakuja desemba or some' like that..
I just hope your well placed snitches are right on this...
 
2. Ni vizuri Kikwete aendeleze mchezo wa kula pande zote mbili za wa-Irani na wamarekani.

....ndio dawa ya kudeal na hawa mafia kwa hili JK is my hero,who cares anyway mkiwakatalia Kenya atawakaribisha kwa mikono miwili,waje tuu labda wanaweza hata kutupatia patia vijisenti kidogo kidogo vya umeme na barabara!
 
Vyanzo vyangu vya hapa USA vimethibitisha uvumi ambao kwa muda umekuwa unaendela Tanzania kuwa serikali ya marekani ina mpango wa kujenga kituo cha kijeshi cha kudumu (permanent base) nchini Tanzania.

Ingawa serikali ya Tanzania imekuwa inajaribu kuficha hizi habari kwa visingizio kuwa mambo ya kijeshi hayajadiliwi kwa vile yanahusu usalama wa taifa, nimeamua kuwaambia wanajeshi kuwa hili suala la kuwa na base ya wamarekani Tanzania ni kubwa na hivyo ni vyema wakaruhusu watanzania wakalijadili.

Siku za karibuni Kikwete amekuwa na vikao vya wazi na vya siri na wamarekani ambao wanatafuta nchi katika pwani na pembe ya afrika ili wajenge kambi ya kijeshi ya kudumu kama ile waliyo nayo kule KATARI (sijui namna ya kutamka hii nchi kwa kiswahili) kule mashariki ya kati.

Wazo la kuweka kambi Ethiopia limeonekana gumu kutokana na hali ya usalama, chaguo la pili la marekani lilikuwa Kenya ambayo hali ya ukabila inatishia usalama wa Kenya. Wamarekani wameamua kuchagua Tanzania ambao so far wanaona kama nchi yenye amani na utulivu.

Habari zinasema kuwa kimsingi Kikwete amekubali (nani angekataa pesa kibao wamarekani walizotoa) na Marekani imelipa pesa indirect kwa kuahidi kutoa mabilioni ya pesa za msaada. Yes, hizi pesa walizoahidi juzi za kuisaidia Tz zitaishia mfukoni mwa wachache na zitakazobaki zitasaidia kujenga base.

MY TAKE.

1. Mimi naunga mkono suala la wamarekani kuwa na base ya Tanzania maana ikiwepo au isiwepo sioni faida au hasara yoyote ukichukulia kuwa Kikwete na wenzake wanauza nchi kila siku.

2. Ni vizuri Kikwete aendeleze mchezo wa kula pande zote mbili za wa-Irani na wamarekani.

3. Kikwete awaambie ukweli wa-Tanzania wa kile kinachoendelea.

4. IMF na Benki ya dunia wakome kusifia Tanzania kuwa inaendelea wakati wakijua ni uongo ila wanatimiza moja ya masharti ya Tz kukubali ku-host base ya marekani.

5. Kikwete atimize ahadi yake kabla Raila hajashinda uchaguzi wa Kenya maana Raila naye amekubaliana na wamarekani katika hili.



Thanks!

Wewe mtoto wewe,

Haya mambo ndio nimekuwa nakuonya hapa. Wakati mwingine unafanya jambo unadhani kuwa ni sifa kumbe ni hatari kwa nchi. Mambo ya kijeshi yanaongelewa jeshini na ni ya usalama wa nchi. Hii habari inaweza kuwa ni ya kweli lakini sio vyema kuitoa wazi namna hii.

Wewe kwa nini hujiulizi kuwa kwa nini vyombo vya nyumbani bado haviongelei hii habari ya kambi ya kijeshi. Mambo mengine sana tunakaa kimya ila inabidi ifike wakati tuyakatae. Hutakiwi kabisa kuongelea mambo ya kijeshi hapa hadharani.

Utoto tu ndio unakusumbua!
 
Wewe mtoto wewe,

Haya mambo ndio nimekuwa nakuonya hapa. Wakati mwingine unafanya jambo unadhani kuwa ni sifa kumbe ni hatari kwa nchi. Mambo ya kijeshi yanaongelewa jeshini na ni ya usalama wa nchi. Hii habari inaweza kuwa ni ya kweli lakini sio vyema kuitoa wazi namna hii.

Wewe kwa nini hujiulizi kuwa kwa nini vyombo vya nyumbani bado haviongelei hii habari ya kambi ya kijeshi. Mambo mengine sana tunakaa kimya ila inabidi ifike wakati tuyakatae. Hutakiwi kabisa kuongelea mambo ya kijeshi hapa hadharani.

Utoto tu ndio unakusumbua!


...kwa mawazo ya kufilisika kama haya unahukumiwa mara moja adhabu ya mijeledi ishirini mbele ya umati.
 
Wewe mtoto wewe,

Haya mambo ndio nimekuwa nakuonya hapa. Wakati mwingine unafanya jambo unadhani kuwa ni sifa kumbe ni hatari kwa nchi. Mambo ya kijeshi yanaongelewa jeshini na ni ya usalama wa nchi. Hii habari inaweza kuwa ni ya kweli lakini sio vyema kuitoa wazi namna hii.

Wewe kwa nini hujiulizi kuwa kwa nini vyombo vya nyumbani bado haviongelei hii habari ya kambi ya kijeshi. Mambo mengine sana tunakaa kimya ila inabidi ifike wakati tuyakatae. Hutakiwi kabisa kuongelea mambo ya kijeshi hapa hadharani.

Utoto tu ndio unakusumbua!
Heshima mbele mkuu,
Lakini uliyosema sikubaliani nayo hata chembe.We are not KIDS.Take it home with you.
 
....ndio dawa ya kudeal na hawa mafia kwa hili JK is my hero,who cares anyway mkiwakatalia Kenya atawakaribisha kwa mikono miwili,waje tuu labda wanaweza hata kutupatia patia vijisenti kidogo kidogo vya umeme na barabara!

Acha mawazo ya kitumwa wewe...
 
Wewe kwa nini hujiulizi kuwa kwa nini vyombo vya nyumbani bado haviongelei hii habari ya kambi ya kijeshi. Mambo mengine sana tunakaa kimya ila inabidi ifike wakati tuyakatae. Hutakiwi kabisa kuongelea mambo ya kijeshi hapa hadharani.

haya yote yanawahusu watanzania hakuna kuyaficha siku Osama ameamua kutungua wamarekani nasi tutakuwemo maana tuko nao!!

hakuna kuficha ili kila mwananchi ajiandae mwenye kuhama ahame

Believe me Tanzania inaandaliwa kuwa uwanja wa mapambano. Tukatae hili!
Muamerika siku zote plan yake ni kupigana vita nje ya nchi yake hivyo WaTZ mjiandae kutolewa kafara kama hili litafanyika
Utoto tu ndio unakusumbua
Huo si utoto kama anatuhabarisha mambo yajayo kinyemela. nchi yetu inakuwa mahantaki ya vita

Tusikubali hili tutalaumiwa na vizazi vijavyo kama tunavyolaumi sisi nile treaty. Ubabe wa Marekani uko mbioni kuisha someni nyakati msifikiri tutapata kinga hakuna ni zamu ya taifa lingine sasa kuinuka someni nyakati

walianza wayahudi, harafu Rumi, Hitla, Muingereza, Marekani na sasa laja lingine. Someni nyakati!!!!
 
Acha mawazo ya kitumwa wewe...

....sio utumwa hapo mkuu labda uniite kibaraka wa marekani nitakubali,si unajua washatuzuga na zile dollar milioni 700 za millenium,bora hii deal ni bora kuliko zote za IPTL,Buzwagi,M Net etc,hebu mkuu niambie hasara ya kuwa na base ya hawa jamaa ni nini kwa nchi njaa kama yetu labda naweza kubadili mawazo.
 
Wewe kwa nini hujiulizi kuwa kwa nini vyombo vya nyumbani bado haviongelei hii habari ya kambi ya kijeshi. Mambo mengine sana tunakaa kimya ila inabidi ifike wakati tuyakatae. Hutakiwi kabisa kuongelea mambo ya kijeshi hapa hadharani.

Utoto tu ndio unakusumbua!

Magazeti ya nyumbani yatapata wapi taarifa kama JF isipoanzisha... ebu kata usingizi kumekucha saa hizi!
 
Masaka,
Dunia ya leo mkuu hakuna siri tena, maadamu tumeukubali utandawazi. ndiyo maana kuna maeneo yamekatazwa kupigwa picha, lakini picha zinapigwa jiulize why? Usipotoa wewe habari kwa kudhania ni mambo ya usalama wa Taifa au ya Kijeshi sijui, wengine wanaitoa pasipo hofu.

By the way hiyo Base itakuwa haionekani kwa macho? kwa hiyo tuendelee kufichwa? Masaka naomba unijibu
 
hebu wanaojua haya mambo ya hizi base za kijeshi yana operate vipi,na hasara na faida zake ni nini kwa nchi kama yetu,wengine hapa tumeangalia pesa tuu labda hatujui,huyo masaka bado anishi 47' mwacheni.
 
Is this a rumor, whisper, hearsay, or a matter of fact...?

hata kama ni ukweli lakini mzee nyani naona watu wanaangalia nje nje, kwani marekani ndo kwanza wanaanza kujenga base yao tanzania ?

kwanza kujengwa kwa base tanzania haitotugarimu chochote
itaongeza usalama na kuepusha ugaidi kwa kiasi fulani
misaada itaongezeka
huduma zitaongezeka mfano:mafuriko, njaa n.k (kumbukeni tz ilitumia mabilioni ya mapesa wakati wa njaa kiasi nusu tu tuanze kutumia reserve ya taifa)
hivyo naamini kabisa kwamba hata kama wakijenga, hawajengi bure kuna faida zake zitaambatana !
 
watu humu mawazo yao ovyo kweli kuanzia huyo mwanzilishi wa hii thread, nashangaa tena sana watu wanapoona ubaya wa kitu fulani na kukashifu tu bila ya uzuri wake kuonyeshwa !

tukiendelea hivyo tutajiweka katika wakati mgumu sana maana ukweli utabainika na uwongo utajitenga !
 
hebu wanaojua haya mambo ya hizi base za kijeshi yana operate vipi,na hasara na faida zake ni nini kwa nchi kama yetu,wengine hapa tumeangalia pesa tuu labda hatujui,huyo masaka bado anishi 47' mwacheni.
hasara ya kwanza.
mmarekani akiweka base basi ujue na osama hana muda ataleta base yake ndani ya manzese. kitachofuatia ni tanzania kugeuka iraq. be well prepared.
 
watu humu mawazo yao ovyo kweli kuanzia huyo mwanzilishi wa hii thread, nashangaa tena sana watu wanapoona ubaya wa kitu fulani na kukashifu tu bila ya uzuri wake kuonyeshwa !

tukiendelea hivyo tutajiweka katika wakati mgumu sana maana ukweli utabainika na uwongo utajitenga !

Shida ya kuwa na kituo cha kijeshi cha Wamarekani Tanzania ni kwamba sisi wenyewe tutakuwa ni lengo la magaidi kwa mara ya pili. Mnamo mwaka 1998, magaidi walilipua ubalozi wao hapa Dar, na pia kule Nairobi. Ina maana sasa kama wamarekani wanajenga kituo chao cha kijeshi Tanzania basi hata "Vulnerability" yetu kwa matukio ya ugaidi itaongezeka. Angalia mifano ya Saudi Arabia, Indonesia na nchi nyingine zenye vituo vya namna hiyo.
Tushishabikie mambo mengine ambayo yatatufanya tusiwe huru. Nisingependa kusikia siku moja kuwa Mtanzania kapelekwa Guantanamo kwenda kuteswa bila kufunguliwa mashtaka, kisa? Wamarekani wamemtuhumu kwa ugaidi na upelelezi!
Siku hizi hakuna siri tena, kila kitu kinawekwa wazi. Mnadhani hicho kituo watajenga angani? Si kitakuwa ardhini? Sasa kama ni ardhini ina maana kuna ardhi itachukuliwa, tutarudi kule kule kwa akina Bulyanhulu, Buzwagi nk.
Napinga kuwa na kituo hiki Tanzania.
 
Back
Top Bottom