Kikwete anawakwepa watanzania wa USA - tena!

Mwafrika wa Kike

JF-Expert Member
Jul 5, 2007
5,185
56
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete,

Inawezekana ni wewe au ni wasaidizi wako ila bado natafuta kujua hili maana linatia aibu. Kwa nini unawakwepa watanzania wanaoishi marekani?

Kwa nini unapenda private settings? Kwa nini unafanya mambo kwa ufichouficho mwingi? Kwa nini hautoi maelezo ya maamuzi yako?

Well, kuna mtu alisema hapa JF kuwa inaonekana ni wivu unasumbua baadhi ya memba hapa ambao wangetaka kuongea nawe. Wengi hapa sio wivu bali ni haja ya kupata nafasi ya kukusikia ukisema kitu kuhusu hali ya baadaye ya nchi yetu. Sio kila mtu anataka kukutolea kashfa (haziuwi) au maneno ya kejeli. Unaweza ukanikwepa mimi ila sio kila mtu mwingine aliyeko hapa USA

Stand up baba and face the muziki. Kama ulidhani uraisi ni kuwa mbali na watu umejidanganya. You never know, labda washauri ulio nao wengi ni vilaza. Wape vijana wako wanaotuma pesa nyingi nyumbani kuliko pesa inayolipwa na makampuni ya madini nafasi ya kuongea na prezidaa wa nchi yao (kumbuka hii ni ofisi) sio kitu chako binafsi.

Mheshimiwa rais, Tafadhali baba!
 
.... Wape vijana wako wanaotuma pesa nyingi nyumbani kuliko pesa inayolipwa na makampuni ya madini nafasi ya kuongea na prezidaa wa nchi yao (kumbuka hii ni ofisi) sio kitu chako binafsi.
Mheshimiwa rais, Tafadhali baba!

Ooouuch!! no you didn't ! girl... this is when people say you kicked him right there!!! it hurts!
Unaweza kumfanya mtu apaliwe hivi hivi...
 
Apart from kwenda ku-mingle na wabongo mi hata muda naye sina, najua kamba zake ataishia kuwayeyusha watu tu.
 
Anasubiri muunde 'Jumuia' kwanza ndio akutane nanyi. Hamuoni wenzenu wa Uingereza mambo yanavyowanyookea?
 
bravo mwk. umenena tumekusikia. labda this time around ataona aibu na kuamua kuongea na watu wake waliopo USA.
 
Anasubiri muunde 'Jumuia' kwanza ndio akutane nanyi. Hamuoni wenzenu wa Uingereza mambo yanavyowanyookea?

Hao wa kwa mama kipi kilichowanyookea!? Hayajawanyookea Watanzania waliopo Tanzania ambao waliahidiwa 'ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya' halafu na 'maisha bora kwa kila Mtanzania' ndio yatawanyookea walio UK!
 
Nimeishi marekani miaka mingi tu na ninatuma pesa nyumbani "zaidi ya makampuni ya madini" lakini lugha mbovu kama yako kwa niaba ya watanzania tulioko huku US sikubaliani nayo na haitufikishi popote. Kukaa kwetu marekani basi tena tunawaita wenzetu vilaza. Hivi wewe umeshaongoza nchi? Hivi Kikwete atukwepe kwa nini! Kwani anakija USA basi katufuata sisi tuliozamia huku hata nyumbani kurudi kwa mbinde. Wengine tumefiwa na baba zetu miaka nenda rudi hata kwenda kuhani tunashindwa, halafu kelele kibaooo!

Raisi Kikwete ni raisi wa watanzania karibu milioni 40 kwa hivyo sisi tulioko huku USA kwa nini Rais atupe preference, kwa vile tuko US ? Kwa nini tusifunge safari kwenda Ikulu Dar Es Salaam if we are serious. I will be the first one to join the bandwagon!

Watanzania tulioko Marekani tuko fragmented hatuna ushirikiano ila kelele nyiingi.Vigroup viingi, mikutanoni ni kutambiana na kuchekana, kila mmoja na interest zake. Mwacheni muungwana afanye kazi zake na kwa wale tuliotegemea kupewa madaraka kwa vile we feel we are capable, tukubali kuwa wamepewa wengine na ingawa ni vilaza based on our perception,hao ndio wanaoiongoza Tanzania na ni ukweli na utabakia hivyo.

Watanzania wajanja tuko wengi USA, kila mtu na mambo yake kila mmoja mjuaji, kila mmoja msomi, wenye majumba wapo, wenye kazi nzuri wapo, wenye green card, wanafunzi tupo, wenye pasipoti za Bush wapo,wenye makampuni wako; tunaondesha taxi tupo, wenye makanisa wapo, wenye-madeal na shughulizao wapo. Ilimradi tupo USA basi Kiwete lazima atupe special preference maanake tuko majuu bwana au vipi mshikaji?

MFUPA ULIOSHINDA FISI MPE MENOSUGU
 
Nimeishi marekani miaka mingi tu na ninatuma pesa nyumbani "zaidi ya makampuni ya madini" lakini lugha mbovu kama yako kwa niaba ya watanzania tulioko huku US sikubaliani nayo na haitufikishi popote. Kukaa kwetu marekani basi tena tunawaita wenzetu vilaza. Hivi wewe umeshaongoza nchi? Hivi Kikwete atukwepe kwa nini! Kwani anakija USA basi katufuata sisi tuliozamia huku hata nyumbani kurudi kwa mbinde. Wengine tumefiwa na baba zetu miaka nenda rudi hata kwenda kuhani tunashindwa, halafu kelele kibaooo!

Raisi Kikwete ni raisi wa watanzania karibu milioni 40 kwa hivyo sisi tulioko huku USA kwa nini Rais atupe preference, kwa vile tuko US ? Kwa nini tusifunge safari kwenda Ikulu Dar Es Salaam if we are serious. I will be the first one to join the bandwagon!

Watanzania tulioko Marekani tuko fragmented hatuna ushirikiano ila kelele nyiingi.Vigroup viingi, mikutanoni ni kutambiana na kuchekana, kila mmoja na interest zake. Mwacheni muungwana afanye kazi zake na kwa wale tuliotegemea kupewa madaraka kwa vile we feel we are capable, tukubali kuwa wamepewa wengine na ingawa ni vilaza based on our perception,hao ndio wanaoiongoza Tanzania na ni ukweli na utabakia hivyo.

Watanzania wajanja tuko wengi USA, kila mtu na mambo yake kila mmoja mjuaji, kila mmoja msomi, wenye majumba wapo, wenye kazi nzuri wapo, wenye green card, wanafunzi tupo, wenye pasipoti za Bush wapo,wenye makampuni wako; tunaondesha taxi tupo, wenye makanisa wapo, wenye-madeal na shughulizao wapo. Ilimradi tupo USA basi Kiwete lazima atupe special preference maanake tuko majuu bwana au vipi mshikaji?

MFUPA ULIOSHINDA FISI MPE MENOSUGU


Kweli upambe sawa na utumwa..mmeanza kuandika ata mambo ya aibu
 
Nimeishi marekani miaka mingi tu na ninatuma pesa nyumbani "zaidi ya makampuni ya madini" lakini lugha mbovu kama yako kwa niaba ya watanzania tulioko huku US sikubaliani nayo na haitufikishi popote. Kukaa kwetu marekani basi tena tunawaita wenzetu vilaza. Hivi wewe umeshaongoza nchi? Hivi Kikwete atukwepe kwa nini! Kwani anakija USA basi katufuata sisi tuliozamia huku hata nyumbani kurudi kwa mbinde. Wengine tumefiwa na baba zetu miaka nenda rudi hata kwenda kuhani tunashindwa, halafu kelele kibaooo!

Raisi Kikwete ni raisi wa watanzania karibu milioni 40 kwa hivyo sisi tulioko huku USA kwa nini Rais atupe preference, kwa vile tuko US ? Kwa nini tusifunge safari kwenda Ikulu Dar Es Salaam if we are serious. I will be the first one to join the bandwagon!

Watanzania tulioko Marekani tuko fragmented hatuna ushirikiano ila kelele nyiingi.Vigroup viingi, mikutanoni ni kutambiana na kuchekana, kila mmoja na interest zake. Mwacheni muungwana afanye kazi zake na kwa wale tuliotegemea kupewa madaraka kwa vile we feel we are capable, tukubali kuwa wamepewa wengine na ingawa ni vilaza based on our perception,hao ndio wanaoiongoza Tanzania na ni ukweli na utabakia hivyo.

Watanzania wajanja tuko wengi USA, kila mtu na mambo yake kila mmoja mjuaji, kila mmoja msomi, wenye majumba wapo, wenye kazi nzuri wapo, wenye green card, wanafunzi tupo, wenye pasipoti za Bush wapo,wenye makampuni wako; tunaondesha taxi tupo, wenye makanisa wapo, wenye-madeal na shughulizao wapo. Ilimradi tupo USA basi Kiwete lazima atupe special preference maanake tuko majuu bwana au vipi mshikaji?

MFUPA ULIOSHINDA FISI MPE MENOSUGU
ee bawna yaani wewe ni kama huu ujumbe umeandika mwenyewe basi naweza kusema kuwa ni mmoja kati ya watu wachache sana humu wenye uwezo mkubwa wa kiakili, samahani naomba nikuulize swali binafsi kama ni sawa hivi unasomea nini.... manake uwezo wako wa ufahamu umenishtua...kwani ni mara chache sana humu ninaweza soma vitu vilivyotulia kama ulivyoandika.. watu wengi humu kazi yao kulaumu lkni hawatoi suluhisho, wanasahau kwamba hakuna kitu rahisi kama kuangalia kitu na kutoa kasoro, lkni hawasemi ni nini wata/mefanya tofauti na serikali yetu kuboresha mambo kwa kifupi bado wengi wamebanwa ktk mzunguko wa kuzaliwa na kufa na hawajaweza kutoka nje ya hapo........
 
Meno sugu aliandika
Nimeishi marekani miaka mingi tu na ninatuma pesa nyumbani "zaidi ya makampuni ya madini" lakini lugha mbovu kama yako kwa niaba ya watanzania tulioko huku US sikubaliani nayo na haitufikishi popote. Kukaa kwetu marekani basi tena tunawaita wenzetu vilaza. Hivi wewe umeshaongoza nchi? Hivi Kikwete atukwepe kwa nini! Kwani anakija USA basi katufuata sisi tuliozamia huku hata nyumbani kurudi kwa mbinde. Wengine tumefiwa na baba zetu miaka nenda rudi hata kwenda kuhani tunashindwa, halafu kelele kibaooo!
Na wale waliopo Uk je! huwa anawafuata wao?
JF kaaazi kweli kweli
 
Kwa kweli, Menosugu, sikubaliana nawe! Rais ni lazima akutane na wananchi, kama ni hivyo ina maana akienda Lindi au Mtwara hakutani na wananchi wake? Akiwa USA ni lazima aonane nao unless ana sababu ya kutokutana nao. Sababu hiyo ya kuwa fragmented kama community siyo sababu! Nadhani ubalozini watakuwa na majinana contacts za baadhi ya watanzania, hasa wale prominent na wanaweza wakaitwa na wakaonana na President.
Lakini also ubalozi wa hapo Washington DC inafanya kazi gani? Maana suala la kufuatilia na kuwa na contacts za watanzania wanaoishi USA ni ya kwao!
 
Heshima mbele.
Nimeshindwa kuvumilia....kumbe tuliopo Bongo ni vilaza! Hakika ni fedheha ya hali ya juu. Siku hizi kuwa Mareakani tu ni ticketi ya akili nyingi, busara na utajiri?
Utumwa, Utumwa, Utumwa.
 
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete,

kukutolea kashfa (haziuwi) au maneno ya kejeli. Unaweza ukanikwepa mimi ila sio kila mtu mwingine aliyeko hapa USA

Stand up baba and face the muziki. Kama ulidhani uraisi ni kuwa mbali na watu umejidanganya. You never know, labda washauri ulio nao wengi ni vilaza. Wape vijana wako wanaotuma pesa nyingi nyumbani kuliko pesa inayolipwa na makampuni ya madini nafasi ya kuongea na prezidaa wa nchi yao (kumbuka hii ni ofisi) sio kitu chako binafsi.

Mheshimiwa rais, Tafadhali baba!

This is how young Africans Talk to their elders nowadays isn't it?.,
how modern kids yell to their fathers to beg for candies and chocolates and sweets.

Dare talk to the president like your houseboy?. where is an african manners.

What is this rigid american supeority over your elders, an insult to the president of the united republic of Tanzania.shame! shame!, shame!

This is the president whose hands lies destiny of millions of people, our own brothers ,sisters,moms and dads, and yet a single human being armed with rockets of illusion and misjudgement and lack of african manners to respect their elders tries to undermine.

With all your rights to speak miss young lady,it is not your right to yell blindly and undermine the President of the united Republic of Tanzania.

As you once used to apologize about your fantasies over the president, you better once again do it! you cant yell to Mr president like this girl!!.
 
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete,

Inawezekana ni wewe au ni wasaidizi wako ila bado natafuta kujua hili maana linatia aibu. Kwa nini unawakwepa watanzania wanaoishi marekani?

Kwa nini unapenda private settings? Kwa nini unafanya mambo kwa ufichouficho mwingi? Kwa nini hautoi maelezo ya maamuzi yako?

Well, kuna mtu alisema hapa JF kuwa inaonekana ni wivu unasumbua baadhi ya memba hapa ambao wangetaka kuongea nawe. Wengi hapa sio wivu bali ni haja ya kupata nafasi ya kukusikia ukisema kitu kuhusu hali ya baadaye ya nchi yetu. Sio kila mtu anataka kukutolea kashfa (haziuwi) au maneno ya kejeli. Unaweza ukanikwepa mimi ila sio kila mtu mwingine aliyeko hapa USA

Stand up baba and face the muziki. Kama ulidhani uraisi ni kuwa mbali na watu umejidanganya. You never know, labda washauri ulio nao wengi ni vilaza. Wape vijana wako wanaotuma pesa nyingi nyumbani kuliko pesa inayolipwa na makampuni ya madini nafasi ya kuongea na prezidaa wa nchi yao (kumbuka hii ni ofisi) sio kitu chako binafsi.

Mheshimiwa rais, Tafadhali baba!
Mwafrika wa Kike,its good tunapoona watanzania walioko marekani wanataka kuongea na RAIS wa JAMHURI HURU YA TANZANIA,lakini ni jaribu kusema kwa niaba ya Rais why hana muda huo.
1;Its just kupoteza muda kuongea na wananchi kama ww ambao wana mawazo ya kusadikika kama wewe.
2;Sisi wakulima huku vijijini tuna onana na Rais every time bcs nchi hii ni ya WAKULIMA sasa nyie wazamiaji hamjui sera za nchi u will just west time ya rais kujadiliana na nyie bcs Mawazo,Fikra na idea zenu zote ni za kusadikika.
3;Kama mnataka kumuona Rudini BONGO tuje tulime ARDHI ni kubwa sana huku Fedha mnazodai mnaleta hapa Nyumbani mbona hazina impact kwetu wananchi au JEANS na Tshirt,Nyie mnachangia kukua uchumi wa Marekani sasa i thout mngeli omba kuongea na GEORGE BUSH.na JK bcs yy anatufanyia kazi sisi watanzania na si watanzania wamarekani.
MWISHO HOJA MNAZOTAKA KUONGEA NA RAIS WEKENI HAPA TUTASAIDIA KUJIBU KAMA WANANCHI WA JAMHURI HII.
 
Heshima mbele.
Nimeshindwa kuvumilia....kumbe tuliopo Bongo ni vilaza! Hakika ni fedheha ya hali ya juu. Siku hizi kuwa Mareakani tu ni ticketi ya akili nyingi, busara na utajiri?
Utumwa, Utumwa, Utumwa.

Son of the Soil,
Wapi hayo maneno yameandikwa? Hizi si ndiyo hasira za mkizi...!! No spins, fullstop!

MwK ameandika "labda washauri ulionao wengi ni vilaza", sioni pahala alipo andika kuwa tuliopo Bongo ni vilaza...Hiyo fedheha jitwike wewe mwenyewe siyo wale tulioelewa kilicho andikwa. Ahsante.

SteveD.
 
This is how young Africans Talk to their elders nowadays isn't it?.,
how modern kids yell to their fathers to beg for candies and chocolates and sweets.

Dare talk to the president like your houseboy?. where is an african manners.

What is this rigid american supeority over your elders, an insult to the president of the united republic of Tanzania.shame! shame!, shame!

This is the president whose hands lies destiny of millions of people, our own brothers ,sisters,moms and dads, and yet a single human being armed with rockets of illusion and misjudgement and lack of african manners to respect their elders tries to undermine.

With all your rights to speak miss young lady,it is not your right to yell blindly and undermine the President of the united Republic of Tanzania.

As you once used to apologize about your fantasies over the president, you better once again do it! you cant yell to Mr president like this girl!!.

This is absolutely ridiculous!
The president is human NOT a demi god! He has been put in his position by Tanzanians who have voted for him! So if the voters want to yell at him it is their right!
Sasa unaanza kwenda off point Gamba! Kwanza you have a problem that it's a woman who wrote this maana you keep repeating 'girl' She's not a girl but a woman! RESPECT her! Sto being condescending!
Two, if she wants to throw a tantrum at her father, her president or her husband that is her right!
Leta hoja hapa siyo kuleta condescending remarks!
 
Acheni udikteta kwa kisingizio kuwa maadili ya Kiafrika yanakiukwa kama vile MwK alivyo uliza au kutoa hoja yake.

Ni kweli maadili yetu ni muhimu tuyathamini na kuyatekeleza. Lakini kile ambacho kimeongelewa na MwK sidhani kama kinakiuka haya, miye pia nisingeunga mkono kama hilo lingefanyika kwenye maandishi yake.

SteveD.
 
This is how young Africans Talk to their elders nowadays isn't it?.,
how modern kids yell to their fathers to beg for candies and chocolates and sweets.

Dare talk to the president like your houseboy?. where is an african manners.
!!.

Hizi "African manners" ndio zimetufikisha hapa tulipo. Kuna haja gani ya kuwa na manners kwa watu ambao hawajali kuhusu maisha ya wananchi wao?

Hizi manners za kiafrika ndio zinawafanya viongozi wetu wawe hivyo walivyo. Wanajua ya kwamba hata wakiboronga waafrika hawatawasema vibaya. Wanajiona Miungu watu.

Halafu una maana gani kusema kuwa anaongea kama anaongea na houseboy wake? Ina maana houseboy ndio mtu wa kutukanwa? Kama tusipoacha huu upuuzi wa kuwaona viongozi wetu kama Miungu watu, tutabaki hapa tulipo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom