Kikwete anapumzika Serengeti kwa kazi gani aliyowafanyia watz?

dihihaka na kejeri zingine ni za kiwendawazimu wakati Jk anakwenda kupumzika kwani alikuwa anajua kitakachofuata nyuma yake.
 
jk ni rais wetu naye ni binadamu..kisheria watu hawatakiwi kujenga mabondeni

Ndio kisheria watu hawatakiwi kujenga mabondeni lakini waliotakiwa kusimamia sheria hizo kikamilifu tangu awali ni serikali, I blame the government for 100%. Labda tujiulize kitu kimoja kwani bonde la jangwani na kwingine hamna watendaji wa kata/vitongoji? ni dhahiri wapo kwasababu tumewasikia juzi, hawa ni viongozi wa kiserikali je, kama kukaa maeneo yale ni makosa na serikali wanajua hilo kwanini hawa watu wakateuliwa kuwakilisha/kuongoza maeneo yale? swali la pili, kama serikali haitambui rasmi makazi yao waliwezaje kuwekewa umeme na shirika la serikali tanesco. swali la tatu, kwanini serikali iliweka vituo vya kupiga kura kama walikuwa hawapatambui kama makazi rasmi?

The bottomline serikali ndiyo ya kulaumiwa kwa kuwa ina sera mbovu za makazi na inaziendeleza pamoja na kuwa na kiongozi wa makazi ambaye ni profesa lakini ni bure kabisa hata mwanangu aisha anamshinda akili huyo profesa.
 
Nadhani tatizo si magnitude ya kazi bali uwezo wake kukabiliana na hiyo kazi.
Jasusi, kutokuwa na uwezo wa kukabiliana na kazi; Kwa nature ya kazi ya urais ilivyo, basi obvious the problem is its magnitude...
Uwezo wake ukiwa chini ya kazi ya aliyokabidhiwa, basi ni wazi kazi immemzidia...

This is how i arrived to the conclusion...
 
12_11_g3w0ke.jpg
Rais Jakaya Kikwete akiwasalimia wananchi waliokuwa upande wa pili wa mto Msimbazi katika eneo la Jangwani, Dar es Salaam wakati alipofanya ziara ya kukagua athari za mafuriko yaliyosababishwa na mvua zilizonyesha kwa siku mbili mfululizo jijini humo. (Picha na Ikulu)
Huyu Jamaa kila sehemu ni kupunga mikono, hata kwenye misiba anapunga mkono. Vasco Da Gama amezoea safari yeye hajui wapi pakupunga mkono au kwenye majanga, akili yake mawazo yake, yeye anawaza safari tu. sehemu yoyote yeye akienda basi mtaagwa hata kwenye matatizo atatoa mkono wa kukuageni :lol: Oooh Vasco is Comedian wa Watanzania. Niaibu kuwa na Kiongozi kama Kikwete. Just waste of time in our country 5yrs without President in Tanzania 2010-15 longway to go
 
"....kazi ya u-Rais,ni mzigo! Watu wakilala na njaa,ni mzigo wako! Shida zao ni zako....!" - Mwl Nyerere.
Leo hii,viongozi wetu,wanalitambua hilo?
 
Huyo ndiye rahisi bwana.****** lazma atanue huku bagamoyo hamna pa kupumzika
 
Ni jambo la ajabu na la kusikitika rais wetu kuacha wananchi wakihaha na maafa ya mafuriko na kwenda kupumzika serengeti,si pinda wala kikwete waliojitokeza mapema kuwapa watz wenzetu moyo,badala yake leo ndo wanatangaza kuwa rais kakatiza mapumziko au alikimbia mafuriko? Barabara za dar,madaraja infrastructure za umeme zimeharibika,wananchi hawana makazi kwa sababu ya athari za mafuriko,hatuna viongozi wanaojali wananchi,na kuwa nao wakati wa matatizo makubwa kama kipindi hiki,mkuu wa mkoa,wakuu wa wilaya ndo wanahangaika huku huku!

Yaani wewe hujui kwamba zile siku 100 zi karibu kutimia-lazima kujificha!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Ndg zangu huyu ni kibaraka wa magharibi ndo mana upumzka pasi kfanya kaz.Kwan anaombe Wananchi 2angamie wote ardhi amkabidhi Bush.Wapi Kambarage? Nchi inauzwa baba!!!?
 
President-Kikwete-of-Tanzania.jpg

Jamaa anainjoi eeh?
Pole na kazi nzito wastahili mapumziko!
Ah

Ah extremely irritating....

Nadhani tunaoiharibu Tanzania ni sisi Tunaodhani kutukana na kashfa ndio uwe mfumo wa Maisha yetu watanzania.

Ziko njia za Busara hata kama humpendi Mtu au hukubaliani nae unaweza kujenga hoja na kumface kwa challenge lakini napata shida kuamini pengine wengi wetu humu tunauelewa mdogo na labda hii ndio iwe style ya Maisha yetu hata Ikitokea siku anaingia madarakani Yule tunamtaka na kumuona yeye ni malaika na Mkombozi kwa mtazamo wako HALAFU wale wasiomsapoti wamrundikie lawama na kashfa Kama JK..


Hapa sio Kama namtetea ila nadhani huwa tunapitikiza kwani lazima tujifunze kuona LOGIC then tunaitumia hiyo kujadili na kukandia nikisoma sipati kitu Zaidi ya kujiona nami ni miongoni kwa watu wanaoangamiza Taifa kwa my own fingertips just for brainwashing and planting a bad seed ambayo ikistawi Nina wasiwasi hata sisi tunaochangia tukidhani tunauchungu na nchi siku za usoni tunaweza kupata nafasi ya kutawala tutakua tunatawala kizazi mdomoni wamejaa lawama, matusi na vinywa visivyo na Staha wala heshima.


Siomini Kama wote tunaochangia humu ni watu tusiokua na dreams that always kept us wishing for good..

Anyway Tuwe na Busara na tutambue Siku Yule tunamtaka akitawala nae atatukanwa ila Je nani analijenga hili au nani anashabikia na kupandikiza ustaarabu huu.


Nadhani sio sahihi sna ingawaje ukiwa na mtazamo km wangu utaambulia matusi ila si sahihi sana kiongozi wetu wa nchi kumtukana na kumkashifu ktk hali ya kawaida hata kijana mwenzangu usie na madaraka kwa nidhamu ya kawaida siwezi kujuvunjia heshima
 
Nimegundua kwa nini JK alikuwa na gadhabu alivyoenda kuwaona wahanga wa mafuriko pale mchikichini, Kumbe alikatishwa kula bata zake serengeti.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom