Kikwete anapumzika Serengeti kwa kazi gani aliyowafanyia watz?

12_11_g3w0ke.jpg
Rais Jakaya Kikwete akiwasalimia wananchi waliokuwa upande wa pili wa mto Msimbazi katika eneo la Jangwani, Dar es Salaam wakati alipofanya ziara ya kukagua athari za mafuriko yaliyosababishwa na mvua zilizonyesha kwa siku mbili mfululizo jijini humo. (Picha na Ikulu)
hili daraja ndio wanaliamini sana ? au helkopta zile za uchaguzi kule igunga zitawahi kuja kumchukua
 
Nimefarijika sana baada ya kusikia Rais wangu
amerudi haraka kutoka likizo maridhawa huko
mbugani Serengeti (Mkoani Mara/Arusha).Ni
kweli hali tete ya mafuriko Dar ndiyo
imemrudisha Mhe. Rais hapa Dar baada ya
kuvumilia ndani ya siku mbili na masaa kadhaa
hatimaye kuona pengine Wananchi tutaanza kumuulizia yu wapi sasa katika kipindi hiki kigumu.

Taarifa za vyombo vya habari jana zilionyesha Mhe. Rais akiwasili Airport akitokea mbugani bila kupitia Ikulu, Mkulu alianza ziara kwa Helikopta kujionea hali halisi na hatimaye kushuka chini kwa Wahanga.Rais kweli ameguswa, agizo lake alilotoa la kuwatafutia maeneo salama Wahanga wa mafuriko NADHANI LITATEKELEZWA.

MAPUMZIKO YA RAIS
Hii haikuwa agenda kuu ya thread hii isipokuwa mafuriko ya Dar yamenisaidia kujua kumbe Marais wetu (Nyerere,Mwinyi,Mkapa na Sasa Kikwete) huwa wanapumzika Mbugani.Kumbe Serikali huwa ina Rest House ama Ikulu ndogo Mbugani hasa Serengeti!!!!(ni fikra tu) kama sivyo hiyo hotel ni mali ya nani?wale waliodharirisha wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge kipindi fulani huko mbugani? Hivi ni Serena Lodge (waliochukua iliyokuwa Shelaton,Royal Palm,Movenpick)?.

Bila shaka Rais anapenda kuwa karibu na hifadhi zetu kwani Nje ya Nchi Chrismas hainogi. Watanzania na Jf humu tumekuwa tukihoji na kuhesabu safari zake za nje na tayari takwimu zinaonyesha amevunja rekodi ya Marais Wenzake tangulizi. Likizo ya Mhe. Rais kuwa Ikulu si pazuri sana kwani pamezoeleka (miaka sita sasa).Msoga/bagamoyo/Chalinze mbali na kuwepo kasri binafsi ya Mhe. Rais pia si kuzuri na ni Bush mno.

Rais wetu huwa anapenda mbugani bana,ni kuzuri kwa kichwa chake kupumzika hasa katika kipindi hiki cha Sikukuu/mwisho wa Mwaka. Kikubwa zaidi tunatambua mchoko alionao baada ya maandalizi ya Sherehe za Miaka 50 ya Uhuru, sote tumeona Rais pamoja na kupenda kutembelea ndugu na jamaa zetu nje ya Nchi na baada ya kutoka Uganda aliamua kumtuma Pinda Kinshasa kuhudhuria Sherehe za kuapishwa Kijana wetu Kabila badala ya yeye kwenda. Ni kweli Mhe. Rais amechoka, anahitaji kupumzika.

MBUGANI
Sina kumbukumbu na Nyerere kama aliwahi kulala huko kwa mapumziko, Mwinyi nilisikia kipindi chake mifugo ndani ya hifadhi zetu iliuzwa (loliondo), Mkapa mara nyingi nilisikia akikimbilia Lushoto-Tanga kwa Mapumziko.

Najiuliza Mhe. anapokuwa likizoni Mbugani anatumia fedha yake binafsi ama kuna fungu limetengwa kwa ajili ya pumziko la Rais (marupurupu ya Likizo)?Bajeti hii ni kiasi gani (maake haijadiliwi bungeni zaidi ya kupitishwa tu)?kwa kuzingatia uhalisia (naamini hivyo) Serikali haina Ikulu ndogo Mbugani.Hapa namaanisha mapumziko ya Mhe. yanagharamikiwa kuanzia Accommodation,chakula na gharama nyinginezo hii ikihusisha wafuasi wake (ni dhahiri watakuwa wa kutosha) kwani yeye ni Taasisi si Kikwete kama Kikwete binafsi.

Mhe. anapokuwa mbugani kama likizo kazi kubwa ni kutazama Wanyama?kujisomea novel za Leadership theory? ama ni nafasi murua sasa ya kufikiria maisha yake binafsi kama vile miradi n.k?Hili mimi sijui ila ni maswali tu.

Nasikia huwa ni fursa ya yeye kukutana na Watu mbali mbali hasa wageni kutoka nje ya Nchi na kabla hajafika pale huwa watu fulani fulani wamekuwa on board kwa maana ya kujumuika na Rais ndani ya Mbuga na si wa kawaida kama Mafuru (aliepata kipato chake kidogo na kuamua kwenda kukimalizia huko).Hawa ni wafanya biashara haswaa (waasia,waarab na weupe wa magharibi).

Teeeeh....teeeeeh.Mbugani kuzuri bana, nadhani Rais wetu ni Mzalendo wa kweli huwa hatumii fursa ya mbugani (kuhujumu nchi) zaidi ya MAPUMZIKO tu.Bila shaka mapumziko yake mbugani mara kwa mara yamekuwa chachu ya kukuza utalii Nchini kwa maana ya kuweka mvuto kwa wageni maake Hotel anayolala Rais kila mtu angependa kulala na hasaa chumba chake .

Nadhani tumpe Mhe.Rais nafasi ya kurudi huko LIKIZONI, kwani mafuriko ya Dar yako ndani ya uwezo wa Mhe. Steven Wassira na Mkuu wa Mkoa Bw. Sadick Meck Sadick.Sote tumeshuhudia Pinda (Msimamizi Mkuu wa Kitengo cha Maafa) pamoja na wenzie Lukuvi na Mwanri hawajulikani waliko.

Nadhani Wassira ataweza hili.
 
Nimefarijika sana baada ya kusikia Rais wangu amerudi haraka kutoka likizo maridhawa huko Mbugani Serengeti (Mkoani Mara/Arusha).Ni kweli Hali tete ya mafuriko Dar ndiyo imemrudisha Mheshimiwa Rais hapa bongo baada ya kuvumilia zaidi ya siku mbili na masaa na kuona Wananchi tutaanza kuuliza yuko wapi mtu huyu.

mimi ningelikuwa ni JK ningeendelea kuchapa raha kwa sababu kipi ataweza ambacho miaka 6 iliyopita alishindwa kukitekeleza iwaje akitekeleze sasa??????????????????????

political gimmicks?
 
Hivi kweli JK hajawahi kujuta kugombea urais?

I just wonder...

Saidhani kama alitambua magnitude ya kazi aliyonayo kabla hajaiomba.
 
Nimefarijika sana baada ya kusikia Rais wangu
amerudi haraka kutoka likizo maridhawa huko
Mbugani Serengeti (Mkoani Mara/Arusha).Ni
kweli hali tete ya mafuriko Dar ndiyo
imemrudisha Mhe. Rais hapa bongo baada ya
kuvumilia ndani ya siku mbili na masaa kadhaa hatimaye kuona pengine Wananchi tutaanza kumuulizia yu wapi sasa katika kipindi hiki kigumu.

Taarifa za vyombo vya habari jana zilionyesha Mhe. Rais akiwasili Airport toka mbugani bila kupitia Ikulu, Mkulu alianza Ziara kwa Helikopta kujionea hali halisi na hatimaye kushuka chini kwa Wahanga.Rais kweli ameguswa na agizo lake la kuwatafutia maeneo salama Wahanga wa mafuriko NADHANI LITATEKELEZWA.

MAPUMZIKO YA RAIS
Hii haikuwa agenda kuu ya thread hii isipokuwa mafuriko ya Dar yamenisaidia kujua kumbe Marais wetu (Nyerere,Mwinyi,Mkapa na Sasa Kikwete) huwa wanapumzika Mbugani.Kumbe Serikali huwa ina Rest House ama Ikulu ndogo Mbugani hasa Serengeti!!!!(ni fikra tu) kama sivyo hiyo hotel ni mali ya nani?wale waliodharirisha wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge kipindi fulani huko mbugani? Hivi ni Serena Lodge (waliochukua iliyokuwa Shelaton,Royal Palm,Movenpick)?.

Bila shaka Rais anapenda kuwa karibu na hifadhi zetu kwani Nje ya Nchi Chrismas hainogi Watanzania na Jf humu tumekuwa tukihoji na kuhesabu safari zake za nje na tayari takwimu zinaonyesha amevunja rekodi ya Marais Wenzake tangulizi. Likizo ya Mhe. Rais kuwa Ikulu si pazuri sana kwani pamezoeleka (miaka sita sasa).Msoga/bagamoyo/Chalinze mbali na kuwepo kasri binafsi ya Mhe. Rais pia si kuzuri na ni Bush mno.

Rais wetu huwa anapenda mbugani bana,ni kuzuri kwa kichwa yake kupumzika hasa katika hiki cha Sikukuu. Kikubwa zaidi tunatambua mchoko alionao baada ya maandalizi ya Sherehe za Miaka 50 ya Uhuru, sotei tumeona Rais pamoja na kupenda kutembelea ndugu na jamaa zetu nje ya Nchi na baada ya kutoka Uganda aliamua kumtuma Pinda Kinshasa kuhudhuria Sherehe za kuapishwa Kijana wetu Kabila na si yeye kwenda. Ni kweli Mhe. Rais amechoka, anahitaji kupumzika.

MBUGANI
Sina kumbukumbu na Nyerere kama aliwahi kulala huko kwa mapumziko, Mwinyi nilisikia kipindi chake mifugo ndani ya hifadhi zetu iliuzwa (loliondo), Mkapa mara nyingi nilisikia akikimbilia Lushoto-Tanga kwa Mapumziko.

Najiuliza Mhe. anapokuwa likizoni Mbugani anatumia fedha yake binafsi ama kuna fungu limetengwa kwa ajili ya pumziko la Rais (marupu ya Likizo)?Bajeti hii ni kiasi gani (maake haijadiliwi bungeni zaidi ya kupitishwa tu)?kwa kuzingatia uhalisia (naamini hivyo) Serikali haina Ikulu ndogo Mbugani.Hapa namaanisha mapumziko ya Mhe. yanagharamikiwa kuanzia Accommodation,chakula na gharama nyinginezo hii ikihusisha wafuasi wake (ni dhahiri watakuwa wa kutosha) kwani yeye ni Taasisi si Kikwete kama Kikwete binafsi.

Mhe. anapokuwa mbugani kama likizo kazi kubwa ni kutazama Wanyama?kujisomea novel za Leadership theory? ama ni nafasi murua sasa ya kufikiria maisha yake binafsi kama vile miradi n.k?Hili mimi sijui ila ni maswali tu.

Nasikia huwa ni fursa ya yeye kukutana na Watu mbali mbali hasa wageni kutoka nje ya Nchi na kabla hajafika pale huwa watu fulani fulani wamekuwa on board kwa maana ya kujumuika na Rais ndani ya Mbuga na si wa kawaida kama Mafuru (aliepata kipato chake kidogo na kuamua kwenda kukimalizia huko).Hawa ni wafanya biashara haswaa (waasia,waarab na weupe wa magharibi).

Teeeeh....teeeeeh.Mbugani kuzuri bana, nadhani Rais wetu ni Mzalendo wa kweli huwa hatumii fursa ya mbugani (kuhujumu nchi) zaidi ya MAPUMZIKO tu.Bila shaka mapumziko yake mbugani mara kwa mara yamekuwa chachu ya kukuza utalii Nchini kwa maana ya kuweka mvuto kwa wageni maake Hotel anayolala Rais kila mtu angependa kulala na hasaa chumba chake .

Nadhani tumpe Mhe.Rais nafasi ya kurudi huko LIKIZONI, kwani mafuriko ya Dar yako ndani ya uwezo wa Mhe. Steven Wassira na Mkuu wa Mkoa Bw. Sadick Meck Sadick.Sote tumeshuhudia Pinda (Msimamizi Mkuu wa Kitengo cha Maafa) pamoja na wenzie Lukuvi na Mwanri hawajulikani waliko.

Nadhani Wassira ataweza hili.

mkuu nimeyakubali maandish yako. Ni kama jokes lkn ujumbe unafika vizuri mno. Big up kamanda
 
Hivi kweli JK hajawahi kujuta kugombea urais?

I just wonder...

Saidhani kama alitambua magnitude ya kazi aliyonayo kabla hajaiomba.

Nadhani tatizo si magnitude ya kazi bali uwezo wake kukabiliana na hiyo kazi.
 
Nimefarijika sana baada ya kusikia Rais wangu
amerudi haraka kutoka likizo maridhawa huko
mbugani Serengeti (Mkoani Mara/Arusha).Ni
kweli hali tete ya mafuriko Dar ndiyo
imemrudisha Mhe. Rais hapa Dar baada ya
kuvumilia ndani ya siku mbili na masaa kadhaa
hatimaye kuona pengine Wananchi tutaanza kumuulizia yu wapi sasa katika kipindi hiki kigumu.

Taarifa za vyombo vya habari jana zilionyesha Mhe. Rais akiwasili Airport akitokea mbugani bila kupitia Ikulu, Mkulu alianza ziara kwa Helikopta kujionea hali halisi na hatimaye kushuka chini kwa Wahanga.Rais kweli ameguswa, agizo lake alilotoa la kuwatafutia maeneo salama Wahanga wa mafuriko NADHANI LITATEKELEZWA.

MAPUMZIKO YA RAIS
Hii haikuwa agenda kuu ya thread hii isipokuwa mafuriko ya Dar yamenisaidia kujua kumbe Marais wetu (Nyerere,Mwinyi,Mkapa na Sasa Kikwete) huwa wanapumzika Mbugani.Kumbe Serikali huwa ina Rest House ama Ikulu ndogo Mbugani hasa Serengeti!!!!(ni fikra tu) kama sivyo hiyo hotel ni mali ya nani?wale waliodharirisha wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge kipindi fulani huko mbugani? Hivi ni Serena Lodge (waliochukua iliyokuwa Shelaton,Royal Palm,Movenpick)?.

Bila shaka Rais anapenda kuwa karibu na hifadhi zetu kwani Nje ya Nchi Chrismas hainogi. Watanzania na Jf humu tumekuwa tukihoji na kuhesabu safari zake za nje na tayari takwimu zinaonyesha amevunja rekodi ya Marais Wenzake tangulizi. Likizo ya Mhe. Rais kuwa Ikulu si pazuri sana kwani pamezoeleka (miaka sita sasa).Msoga/bagamoyo/Chalinze mbali na kuwepo kasri binafsi ya Mhe. Rais pia si kuzuri na ni Bush mno.

Rais wetu huwa anapenda mbugani bana,ni kuzuri kwa kichwa chake kupumzika hasa katika kipindi hiki cha Sikukuu/mwisho wa Mwaka. Kikubwa zaidi tunatambua mchoko alionao baada ya maandalizi ya Sherehe za Miaka 50 ya Uhuru, sote tumeona Rais pamoja na kupenda kutembelea ndugu na jamaa zetu nje ya Nchi na baada ya kutoka Uganda aliamua kumtuma Pinda Kinshasa kuhudhuria Sherehe za kuapishwa Kijana wetu Kabila badala ya yeye kwenda. Ni kweli Mhe. Rais amechoka, anahitaji kupumzika.

MBUGANI
Sina kumbukumbu na Nyerere kama aliwahi kulala huko kwa mapumziko, Mwinyi nilisikia kipindi chake mifugo ndani ya hifadhi zetu iliuzwa (loliondo), Mkapa mara nyingi nilisikia akikimbilia Lushoto-Tanga kwa Mapumziko.

Najiuliza Mhe. anapokuwa likizoni Mbugani anatumia fedha yake binafsi ama kuna fungu limetengwa kwa ajili ya pumziko la Rais (marupurupu ya Likizo)?Bajeti hii ni kiasi gani (maake haijadiliwi bungeni zaidi ya kupitishwa tu)?kwa kuzingatia uhalisia (naamini hivyo) Serikali haina Ikulu ndogo Mbugani.Hapa namaanisha mapumziko ya Mhe. yanagharamikiwa kuanzia Accommodation,chakula na gharama nyinginezo hii ikihusisha wafuasi wake (ni dhahiri watakuwa wa kutosha) kwani yeye ni Taasisi si Kikwete kama Kikwete binafsi.

Mhe. anapokuwa mbugani kama likizo kazi kubwa ni kutazama Wanyama?kujisomea novel za Leadership theory? ama ni nafasi murua sasa ya kufikiria maisha yake binafsi kama vile miradi n.k?Hili mimi sijui ila ni maswali tu.

Nasikia huwa ni fursa ya yeye kukutana na Watu mbali mbali hasa wageni kutoka nje ya Nchi na kabla hajafika pale huwa watu fulani fulani wamekuwa on board kwa maana ya kujumuika na Rais ndani ya Mbuga na si wa kawaida kama Mafuru (aliepata kipato chake kidogo na kuamua kwenda kukimalizia huko).Hawa ni wafanya biashara haswaa (waasia,waarab na weupe wa magharibi).

Teeeeh....teeeeeh.Mbugani kuzuri bana, nadhani Rais wetu ni Mzalendo wa kweli huwa hatumii fursa ya mbugani (kuhujumu nchi) zaidi ya MAPUMZIKO tu.Bila shaka mapumziko yake mbugani mara kwa mara yamekuwa chachu ya kukuza utalii Nchini kwa maana ya kuweka mvuto kwa wageni maake Hotel anayolala Rais kila mtu angependa kulala na hasaa chumba chake .

Nadhani tumpe Mhe.Rais nafasi ya kurudi huko LIKIZONI, kwani mafuriko ya Dar yako ndani ya uwezo wa Mhe. Steven Wassira na Mkuu wa Mkoa Bw. Sadick Meck Sadick.Sote tumeshuhudia Pinda (Msimamizi Mkuu wa Kitengo cha Maafa) pamoja na wenzie Lukuvi na Mwanri hawajulikani waliko.

Nadhani Wassira ataweza hili.

Waitu aina amatu na aulile!
 
Hivi kweli JK hajawahi kujuta kugombea urais?

I just wonder...

Saidhani kama alitambua magnitude ya kazi aliyonayo kabla hajaiomba.

you can say that again..................and again............
 
Atakuwa anakaa sangita grunet hotel ambayo mwaka huu imekuwa voted as the best hotel in the world..vyumba vya chini kabisa ni dola 1950 ambayo Kwa madafu ni appr. 3,217,500. Hebu pata picha tunavyochakachuliwa..wale walinzi woote, wapambe, akina salva etc. Si tupo tupo tu huku na njaa zetu na mishahara haijaingia.
 
HELLOW kwa wana jamvi sina shaka mko salama,niliweka mipango yangu ya kuwa mwishoni mwaka 2011 takuwa mmoja wa member hapa jamvini nashukuu sasa nimejiunga rasmi naomba nipokeeni.
 
ulitaka asipumzike mrais waastaafu kama George Bush, Clinton, Mkapa na mwinyi wanasafiri kikazi na kata mapumziko ndio ikawe Rais aliyopo madarakani?
 
kumbuka kuna fungu la safari, matibabu na mapumziko kwa Marais wote wastaafu na aliyoko madarakani. fungu hili lilipitishwa na bunge kwa kiasi cha fedha kwa mwaka. Hii haipo Tanzania tu duniani kote
 
tumekuwa tunahamasisha utalii wa ndani sasa kama Rais wetu haendi huko atamhamasisha nani? Tuwe fair au tunataka Mbowe na Dr Slaa tu ndio waende huko mbugani
 
na foleni anayotusababishiaga kila j'mosi na j'pili anapoenda msoga na kurudi,kwani sio likizo ile?
 
Jaribu kuwa mkweli, sio kweli kwamba walinzi wote, akina Salva wanalala hotel moja na Rais. Tupo hapa kusema ukweli sio kuongeza chumvi.


Atakuwa anakaa sangita grunet hotel ambayo mwaka huu imekuwa voted as the best hotel in the world..vyumba vya chini kabisa ni dola 1950 ambayo Kwa madafu ni appr. 3,217,500. Hebu pata picha tunavyochakachuliwa..wale walinzi woote, wapambe, akina salva etc. Si tupo tupo tu huku na njaa zetu na mishahara haijaingia.
 
Mkapa aliponunua ndege ya Rais tulipiga kelele sana leo hii Kikwete akinunua helkopta ya Rais ili kumzungusha kwa wananchi kukwepa foleni pia tunalalamika kwa matumizi mabaya ya kodi zetu. kati ya mvua na jua kipi bora? tunamchanganya Jk wengine tunasema mvua na wengine jua.


na foleni anayotusababishiaga kila j'mosi na j'pili anapoenda msoga na kurudi,kwani sio likizo ile?
 
Big up Jk kwa kuwatembelea waathirika na kuzungumza nao. Tunafarijika


Thursday, 22 December 2011 20:29
0digg
hameni-jk.jpg
Rais jakaya Kikwete(katika) Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mahusiano ya Jamii .Stephen Wasira(kushoto),Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadik,Meya wa Ilala jerry Slaa,waziri wa Tamisemi,George Mkuchika na Waziri wa ulinzi(kulia)Hussein Mwinyi wakiwa wameinamisha vichwa kuwakumbuka waliokufa kwenye mafuriko jana.Picha na Fidelis Felix​
WALIOKUFA WAFIKIA 30,MAELFU WAKOSA MAKAZI
Waandishi Wetu
RAIS Jakaya Kikwete ametoa tamko kwa wakazi wanaoishi mabondeni, kwa kuwataka wahamie kwenye maeneo mapya watakayopangiwa ili kuepuka madhara zaidi.Wakati Rais akitoa tamko hilo, takwimu zilizokusanywa na gazeti hili kutoka mamlaka mbalimbali tangu kuanza kwa mvua hizo mnamo Desemba 20, zinaonyesha waliokufa ni 30 lakini, Rais aliambiwa kuwa waliokufa ni watu 20.

Akizungumza jana katika shule ya msingi ya Mchikichini, Jijini Dar es Salaam alipokwenda kuwapa pole waathirika wa mafuriko yaliyotokana na mvua zilizonyesha kwa siku tatu, Rais Kikwete aliwataka watu kuhama mabondeni.

Shule ya Mchikichini ni miongoni mwa vituo vilivyotengwa kwa ajili ya kuwahifadhi waathirika wa mafuriko hayo.
Rais alisema: "Wakati Watanzania tunaomba usiku na mchana mvua iweze kunyesha ili mazao yaweze kustawi, wapo wenzetu ambao wanaomba jua liwake mwaka mzima."

Alisema wanaombea jua liwake mwaka mzima, ili mvua isinyeshe kwa sababu wamejenga nyumba zao mabondeni ambako hawaruhusiwi."Acheni kuishi kwa mashaka, ukiona wingu jeusi unaanza hofu, kila siku adui yako wewe ni mvua, tafadhali hamieni kwenye maeneo salama yatakayotengwa,"alisema Kikwete.

Mkuu huyo wa nchi aliongeza kwamba, katika maeneo mengine mafuriko yametokea kwa sababu watu wamejenga kwenye maeneo ya wazi na maeneo ya barabara.

"Maeneo hayo yakijengwa maji yanatafuta sehemu ya kupita, yakishindwa yanabomoa nyumba na miundombinu mingine," alisema Kikwete.Alisema yote hayo yanafanyika huku viongozi wakiwemo watendaji wa mitaa na kata, wakiwa wanaangalia.

"Watu wanajenga na kuziba barabara, wengine wanajenga kwenye viwanja vya wazi kuna madiwani, watendaji wa kata na watendaji wa serikali za mitaa lakini hawachukui hatua zozote," alisema Kikwete.

Rais Kikwete alisema hata kwenye maeneo hayo yanapotokea maafa, kazi ya uokoaji inakuwa ngumu kwa sababu maeneo yote yamejengwa nyumba.Alisema serikali itahakikisha waathirika wa mafuriko hayo wanapata huduma zote za kibinadamu zinazohitajika wakiwa katika vituo vua huduma.

Kabla ya kuzungumza na waathirika hao, Rais Kikwete alikagua maeneo ya jiji la Dar es Salaam yaliyokumbwa na mafuriko hayo kwa kutumia Helkopta.

RC Sadik

Kwa upande wake mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadik alimweleza Rais Kikwete kwamba ekari 2,000 za ardhi, zimetengwa katika wilaya ya Kinondoni kwa ajili waathirika wa mafuriko hayo.

Alisema katika eneo hilo vitapatikana viwanja 2,800, ambavyo vitagawiwa kwa watu hao waliopatwa na maafa.

"Mheshimiwa Rais wapo baadhi ya watu wanaoishi mabondeni waliowahi kupewa viwanja ili wahame lakini, hawakufanya hivyo na viwanja walivyopewa waliviuza," alisema Sadik.Alisema katika bonde la Msimbazi kila mwaka yamekuwa yakitokea maafa, ingawa hayakuwahi kutokea maafa makubwa kama ya sasa.

"Hatuwezi kuwa watu wa kusubiri maafa kila mwaka, ni lazima hatua sasa zichukuliwe ili wakazi wa mabondeni waweze kuhamia katika maeneo salama," alisema Sadik.

Alisema kwa kuwa shule za msingi zitafunguliwa katika kipindi cha wiki mbili zijazo, waathirika hao watahamishiwa kwenye eneo maalum litakalojengwa kwa mahema.Sadik akizungumzia misaada ya kibinadamu ambayo imeanza kutolewa, alisema wameanza kugawa vyakula na maji.

Alisema mablanketi 1,600 yameanza kutolewa na magodolo yataanza kugawiwa katika maeneo mbalimbali hivi karibuni huku huduma za afya zikiwekwa katika kila kambi.Kuhusu miundombinu iliyoharibika, Sadik alisema wahandisi wa mkoa wameanza kufanya tathimini kufahamu uharibufu na hatua kuchukua.

" Kuna madaraja kadhaa yamebomoka na barabara kuharibika, wahandisi wetu wanafanya tathimini ili tuweze kuchukua hatua za ujenzi," alisema Sadik.

Waliokufa wafikia 30
Wakati Rais akielezwa waliokufa ni 20 takwimu ambazo Mwananchi imezikusanya kutoka mamlaka tofauti zinaonyesha kuwa mvua hizo, zimesababisha vifo vya watu 30 na majeruhi 50.Takwimu hizo zilipatikana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Hospitali ya Amana, Hospitali ya Mwananyamala na Hospitali ya Temeke.

Hata hivyo, Sadik alimweleza Rais Kikwete kuwa waliokufa katika mafuriko hayo ni watu 20 na walioathirika ni 4,909.Hata hivyo, Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela alisema jana kuwa tangu mvua zilipoanza kunyesha, mkoa wake wa kipolisi wa Kinondoni, kuliripotiwa vifo 13, vikiwamo vitatu vya watu wa familia moja ya Abeid Mntangi, mkazi wa Kimara.

Alisema familia hiyo ilikumbwa na maafa hayo baada ya ukuta wa nyumba yao kuwaangukia, kwa kusukumwa na maji ya mvua.Kenyela alisema katika eneo la Kimara Baruti, ulikutwa mwili wa mtu mmoja mwanaume mwenye umri wa kati ya miaka 55 na 60, ukiwa umekwama kwenye mizizi.

"Maiti hiyo ilikutwa haina nguo na haijatambuliwa vilevile, eneo la Kawe mtu mmoja mwenye asili ya Kimasai miaka kati ya 40 hadi 45 mwili wake umekutwa mto Kawe nao pia uko Mwananyamala," alisema.Alisema eneo la Tabata Ami, mwili mwingine wa mwanaume mwenye umri kati ya 35 hadi 40 aliyekuwa amevaa fulana nyeupe na jinzi uliokotwa.

Katika eneo la Kigogo kwa Dua Said, Kamanda Kenyela alisema uliokotwa mwili wa mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 12 ukiwa pembeni ya mto Msimbazi.Kamanda Kenyela alisema mwili wa Khalid Ali (22) ambaye ni mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Mgulani, ulikutwa ukielewa kwenye Bonde la Mto Msimbazi.

Katika eneo la Magomeni Suna, mwili wa mtu aliyetambuliwa kuwa ni Mwinyi Makame (20) ulikutwa pembeni mwa bonde la Msimbazi.Kenyela alisema maiti za watu wanne ambazo bado hazijatambuliwa na miili mingine imehifadhiwa katika hospitali ya Mwananyamala.

Alisema katika eneo hilo la Magomeni Suna, pia ulikutwa mwili wa mtu aliyetambuliwa kwa jina moja la Athuman umri (22) ambaye ni fundi magari na mwili huo pia umepelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Hosipitalini Dar
Kwa upande wake Ofisa Uhusiano Msaidizi wa Hospiali ya Muhimbili, Jeza Waziri alisema katika hospitali hiyo kulipokelewa maiti 15 na majeruhi 11.Waziri alisema kati ya maiti hao, wanawake ni watatu na wanaume 12. Alisema majeruhi saba kati ya hao 11 bado wamelazwa na kuendelea na matibabu hospitalini hapo.

"Maiti zilizotambuliwa ni saba na ambazo hazikutambuliwa majina ni nane. Majeruhi wote walilazwa na kuruhusiwa,' alisema Waziri.Alitaja maiti waliotambuliwa kuwa ni Hidaya Amri (1) mkazi wa Jangwani, Hamisi Nyao (19) mkazi wa Vingunguti, Nyanda Kiangi (35)Mkazi wa Kigogo na mwingine aliyetambulika kwa jina la Bakari (10).

Wengine ni Nia Abrahamani (24) na Athumani (26) wote wakazi wa Magomeni."Kuanzia jana (juzi) hadi saa 7.10 mchana leo (jana), tumepokea maiti 15 ikiwamo maiti moja ambayo inakuja sasa hivi ninavyozungumza na wewe,"alisema Waziri.

Katika hospitali ya Amana ambayo ipo katika Manispaa ya Ilala, kulikuwa na kifo cha mtu mmoja na majeruhi 45.
Dk Mwaluka Shanny wa hospitali hiyo, alisema kumekuwa na ongezeko la majeruhi kutoka 10 katika siku ya kwanza mpaka 45 jana.

Dk Shanny alisema wengi wa majeruhi hao wanatoka katika maeneo ya Kigogo na kwamba baadhi yao walipata mshituko na wengine majeraha madogo.

"Mpaka leo (jana) saa 8:00 kamili mchana, tumepokea majeruhi 45, kati yao yupo mwanamke mmoja (60) ambaye hali yake ni mbaya kutokana na kupata mshituko wa moyo," alisema Dk Shaany.

Katika hospitali ya Temeke tangu mvua hizo zianze juzi, kuliripotiwa maiti moja na majeruhi wawili. Taarifa hizo zilitolewa jana na muuguzi wa zamu wa hospitali hiyo, Shamim Londo.

Kambi za wathirika
Baadhi wa waathirika katika kambi ya Shule ya Msingi Gilman Rutihinda iliyoko Kigogo, wamelalamika kwamba tangu wafike kambini hapo juzi hawajapewa huduma yoyote, hata chakula.

Wakati wenzao wa shule ya Mchikichini wakiwa wamenza kupata chakula, wao walisema hawajapata chakula wala maji licha ya viongozi kadhaa kuwatembelea.

"Viongozi wanakuja kutupa pole lakini sisi hatuhitaji pole ya mdomo tuna watoto wana njaa tangu jana hawakula chochote tunaomba msaada," alisema Mwasa Samwel.Waathirika wengine walimuunga mkono mwenzao na kuongeza kuwa licha ya kukosa chakula pia hawana mashuka, vyandarua na nguo.

"Tumekuja kama tulivyo, tunaomba msaada, hatuna chakula hatuna nguo wala fedha vyote vimechukuliwa na mafuriko," alisema Habiba Juma ambaye ana watoto wanne.

Wakati huohuo familia 15 zilizohifadhiwa katika Shule ya msingi Msimbazi baada ya nyumba zao kuzolewa na maji zimelalamikia kukosa misaada mbalimbali kikiwamo ya chakula.Fulugensi Kahima (37), mkazi wa Jangwani alisema msaada wa makazi waliopewa haitoshi na kwamba wanahitaji chakula hasa kwa watoto ambao ndio wamedhurika kwa kiasi kikubwa.

"Tumepewa hifadhi hapa lakini tangu tufike katika kituo hiki tumeishia kupewa juisi na maji lakini mpaka sasa hatujapata msaada wowote wa chakula zaidi ya kwenda kujitafutia wenyewe," alisema Kahima.

Mwananchi ilishuhudia sehemu hiyo waliopewa waathirika kwa ajili ya hifadhi ikiwa katika hali mbaya na hakuna vitu muhimu kama magodolo huku mikeka ikiwa ndio inatumika kama sehemu ya malazi.

Moja ya sehemu ambayo Mwananchi ilishuhudia ni katika chumba kimoja cha darasa, ambacho familia hizo zimehifadhiwa kukiwa na mchanganyiko wa wazazi na watoto.Familia hizo mbazo kwa sehemu kubwa zinatoka katika eneo la Jangwani walikutwa na mwananchi wakiwa katika maandalizi ya kwenda kufitajutia kipato.

Dk Slaa: Janga liwe funzo
Kwa upande wa Chadema, kimetoa pole kwa wananchi waliokumbwa na maafa katika jiji la Dar es Salaam, Mbeya na Dodoma na kuishauri serikali kujiandaa kuyakabili majanga makubwa.

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa alisema katika taarifa yake kuwa hawaridhishwi na hatua zilizochukuliwa na serikali kuwahudumia waathirika hao.

Alisema kutokana na wananchi kupoteza maisha, mali na miundombinu mingi kuharibika Chama wanaona kuwa hilo ni janga la kitaifa na kutaka serikali kuhakikisha inawahudumia kwa umakini wananchi wote walioathirika.

Dk Slaa alisema kutokana na hali hiyo, serikali inatakiwa kutunga sheria mpya ya ujenzi na kuweka viwango vya ujenzi vyenye hadhi ya kimataifa na hasa ujenzi wa kuta na majengo marefu na kuhakikisha ujenzi holela haujitokezi kwenye miji na majiji .

Alisema serikali inatakiwa kuhakikisha miji mikubwa inakuwa na mtandao wa mabomba ya maji ya dharura inawekwa ili kukabiliana na majanga ya moto na mafuriko yanapotokea.

Aliongeza kuwa serikali inatakiwa kujiandaa kukabiliana na magonjwa ya milipuko kama vile kuhara, kipindupindu na mengineyo ambayo yanaweza kujitokeza kutokana na janga hilo kuwa kubwa.

"Kitengo cha maafa kiwe na vifaa wakati wote kwa ajili ya uokozi, maeneo ambayo hali inakuwa tete pamoja na kutoa elimu jinsi kutumia vifaa, ili kuweza kujiokoa na sio kuacha hali iwe kama ilivyojitokeza jijini Dar es Salaam, waathirika waliposhindwa kutumia hata majaketi ya uokozi," alisema.

Alisema kutokana na janga hilo kugusa maisha ya watu wote, serikali kuwekeza nguvu nyingi zaidi kuwasaidia wanachi.

Dk Slaa alisema taifa limeonyesha dhahiri kuwa halijajiandaa kuyakabili majanga na kwamba hata vyombo vya ulinzi na usalama vimeonekana kutoandaliwa kimfumo na kinyenzo kukabiliana na majanga.

Alisema serikali inatakiwa kuondoa kudhaifu mkubwa uliooneshwa na Taifa, ili wanachi waendelee kuamini kile kilichopatikana baada ya miaka 50 .

Alisema kitengo cha maafa kinaonekana hakikuandaliwa vizuri kutokana na kushindwa kukabiliana na majukumu yanavyopaswa kufanywa wakati wa matatizo makubwa ya maafa.

Dk Slaa alisema iwapo chombo kilichopangwa kushidwa kufanya kazi yake serikali inatakiwa kukiangalia kwa makini ili kuweza kuhakikisha jamii inakuwa na imani pindi tatizo linapotokea.

Alisema matatizo kama hayo yanatokana mifumo mibovu ya kujulisha umma kuhusiana na majanga makubwa ndio sababu ya kuharibiwa kwa mali za wananchi na kwamba, serikali inatakiwa kuweka kipaumbele kuwajulisha wananchi ili kuweza kupunguza maafa.

Habari hii imeandaliwa na Raymond Kaminyoge, Keneth Goliama, Aidan Mhando, Pamela Chilongola na Ibrahim Yamola
 
Back
Top Bottom