BASIASI
JF-Expert Member
- Sep 20, 2010
- 9,735
- 5,003
udiwani sasa anavaa nguo rasmi
na Ahmed Makongo, Bunda
MGOMBEA udiwani wa kata ya Balili, kwa tiketi ya CCM, Edda Motte, ambaye hivi karibuni mgombea urais kwa tiketi ya cham hicho, Jakaya Kikwete, alimtambulisha kwamba ni mwanamke kutokana na tabia ya kuvaa nguo za kike, sasa amebadilika na amekuwa akiomba kura akiwa amevaa nguo za kiume.
Baadhi ya viongozi waandamizi wa chama hicho wilayani hapa, ambao hawakupenda majina yao yaandikwe, wamedokeza kuwa mgombea huyo sasa anavaa nguo hizo tofauti na awali na kwamba hali hiyo imetokana na uongozi wa CCM pamoja na wafuasi wake kumshawishi afanye hivyo.
Wakati wa ziara yake wilayani Bunda, Rais Kikwete wakati anatambulisha wagombea udiwani, alimtambulisha mgombea huyo kama mwanamke baada ya kumuona amevaa nguo za kike kwa kujifunga kitenge.
Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi katika mikutano yote ya kampeni ya mgombea huyo, umegundua kuwa siku hizi ameacha kujifunga kitenge na anavaa traki suti. Wakati huo huo, mgombea huyo amewaomba wananchi wa kata hiyo kumchagua ili aweze kuwaletea maendeleo.
na Ahmed Makongo, Bunda
Baadhi ya viongozi waandamizi wa chama hicho wilayani hapa, ambao hawakupenda majina yao yaandikwe, wamedokeza kuwa mgombea huyo sasa anavaa nguo hizo tofauti na awali na kwamba hali hiyo imetokana na uongozi wa CCM pamoja na wafuasi wake kumshawishi afanye hivyo.
Wakati wa ziara yake wilayani Bunda, Rais Kikwete wakati anatambulisha wagombea udiwani, alimtambulisha mgombea huyo kama mwanamke baada ya kumuona amevaa nguo za kike kwa kujifunga kitenge.
Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi katika mikutano yote ya kampeni ya mgombea huyo, umegundua kuwa siku hizi ameacha kujifunga kitenge na anavaa traki suti. Wakati huo huo, mgombea huyo amewaomba wananchi wa kata hiyo kumchagua ili aweze kuwaletea maendeleo.