Habarindiyohiyo
JF-Expert Member
- Aug 11, 2008
- 263
- 13
na Mwandishi Wetu
MGOMBEA wa nafasi ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) NEC, Shyrose Bhanji, jana aliwatoa machozi wajumbe wa NEC, alipotoa maneno ya shukrani baada ya kushindwa kwenye kiti hicho.
Shyrose alipewa nafsi ya kutoa maneno ya shukrani na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete, ili kuwaeleza wajumbe wa NEC alivyopokea matokeo ya kushindwa kwake katika nafasi hiyo iliyochukuliwa na Meya wa Kinondoni, Salum Londa.
Shyrose alisema kushindwa kwake kwa tofauti ya kura moja kunaonyesha ni jinsi gani NEC inavyozidi kumsogeza karibu kushika uongozi.
Nimefurahi sana na nimepokea kwa mikono miwili matokeo haya ya tofauti ya kura moja, kwani nikilinganisha na chaguzi za nyuma nilizoshiriki nilikuwa naachwa mbali na wagombea walionishinda.
.lakini safari hii nimefurahi kwa sababu nimezidi kusogezwa karibu na uongozi, alisema Shyrose na kusababisha baadhi ya wajumbe waliompigania kwenye kinyanganyiro hicho kutokwa na machozi.
Wakati baadhi ya wajumbe wakifuta machozi, Rais Kkiwete alikuwa akitikisa kichwa na baadaye alikiri kuwa Shyrose alitoa maneno mazito.
Shyrose maneno yako ni mazito sana . tumeyasikia, tumekuelewa, hayo mengine tuachie tutayafanyia kazi,alisema Rais Kikwete.
Kwa upande wake, Londa aliwashukru wajumbe waliomchagua kwamba wameonyesha imani kubwa kwake na kwamba hatawaangusha.
Nafasi hiyo iliachwa wazi na Jack Mwambi, aliyeomba kujiuzulu baada ya Rais Kikwete kumteua kuwa Balozi wa Tanzania nchini Urusi.
Londa alimshinda Shyrose Banji katika raundi ya pili ya kinyanganyiro hicho kwa tofauti ya kura moja ambapo Londa alipata kura 80 na Shyrose 79.
Katika duru la kwanza, wagombea wa kiti hicho walikuwa watatu ambapo Londa alipata kura 62, Shyrose kura 60 na Peter Selukamba kura 42, ndipo ilipoamuliwa Londa na Shyrose waingie katika duru la pili na wapigiwe kura upya, hatimaye Londa kuibuka kidedea.
Katika kinyanganyiro hicho jumla ya waombaji 20 walijitokeza kuwania kiti hicho kilichokuwa na ushindani mkubwa hasa katika kampeni zilizofanyika juzi mjini hapa.
MGOMBEA wa nafasi ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) NEC, Shyrose Bhanji, jana aliwatoa machozi wajumbe wa NEC, alipotoa maneno ya shukrani baada ya kushindwa kwenye kiti hicho.
Shyrose alipewa nafsi ya kutoa maneno ya shukrani na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete, ili kuwaeleza wajumbe wa NEC alivyopokea matokeo ya kushindwa kwake katika nafasi hiyo iliyochukuliwa na Meya wa Kinondoni, Salum Londa.
Shyrose alisema kushindwa kwake kwa tofauti ya kura moja kunaonyesha ni jinsi gani NEC inavyozidi kumsogeza karibu kushika uongozi.
Nimefurahi sana na nimepokea kwa mikono miwili matokeo haya ya tofauti ya kura moja, kwani nikilinganisha na chaguzi za nyuma nilizoshiriki nilikuwa naachwa mbali na wagombea walionishinda.
.lakini safari hii nimefurahi kwa sababu nimezidi kusogezwa karibu na uongozi, alisema Shyrose na kusababisha baadhi ya wajumbe waliompigania kwenye kinyanganyiro hicho kutokwa na machozi.
Wakati baadhi ya wajumbe wakifuta machozi, Rais Kkiwete alikuwa akitikisa kichwa na baadaye alikiri kuwa Shyrose alitoa maneno mazito.
Shyrose maneno yako ni mazito sana . tumeyasikia, tumekuelewa, hayo mengine tuachie tutayafanyia kazi,alisema Rais Kikwete.
Kwa upande wake, Londa aliwashukru wajumbe waliomchagua kwamba wameonyesha imani kubwa kwake na kwamba hatawaangusha.
Nafasi hiyo iliachwa wazi na Jack Mwambi, aliyeomba kujiuzulu baada ya Rais Kikwete kumteua kuwa Balozi wa Tanzania nchini Urusi.
Londa alimshinda Shyrose Banji katika raundi ya pili ya kinyanganyiro hicho kwa tofauti ya kura moja ambapo Londa alipata kura 80 na Shyrose 79.
Katika duru la kwanza, wagombea wa kiti hicho walikuwa watatu ambapo Londa alipata kura 62, Shyrose kura 60 na Peter Selukamba kura 42, ndipo ilipoamuliwa Londa na Shyrose waingie katika duru la pili na wapigiwe kura upya, hatimaye Londa kuibuka kidedea.
Katika kinyanganyiro hicho jumla ya waombaji 20 walijitokeza kuwania kiti hicho kilichokuwa na ushindani mkubwa hasa katika kampeni zilizofanyika juzi mjini hapa.