Abel Ndundulu
JF-Expert Member
- Sep 17, 2015
- 845
- 383
Hakika kilichofanyika Zanzibar na Tanganyika ni "Mapinduzi" ya Maamuzi sahihi ya Wananchi..Naam,Maamuzi mujarab ya Watanzania yamepinduliwa tena kwa kile kinachotafsiriwa kuwa ni demokrasia ilihali ni ubakwaji mkubwa wa HAKI kwa kupiga mikwara vyombo vya habari,kuvamia Kituo cha Haki za Binadamu,Kuwapora Wapinzani vifaa vya kukusanya takwimu na kukataa Maamuzi sahihi ya Wananchi katika sanduku la kura!!!Dhambi hii haitoishia hapa,tumepanda mbegu hatari ya kutufarakanisha,yumkini isiwe leo..Ila siku itakapofika ukimya huu wa Walioporwa haki utageuka kuwa uchungu mkubwa sana ambao haujawahi kutokea!!!..Najaribu kutafakari kwa sauti!!!