Kikwete alivyoondoka Monduli chuo cha Jeshi kwa misukosuko

WOS,

Kama umeelewa somo, tunaambiwa kwamba JK alitoroka kwenye kikao baada ya Mkuu SAYORE kugawa barua(ya FITNA)) kwenye kikao akiacha wazitazame, na yeye (sayore)kutoka nje.

JK alitambua ambacho kingefuatia... hivyo aliamua kutoroka KWA KUPITA NJIA ZAKUJIFICHA!(hapo ndio kwenye ishu)..
Asingeweza kufuata barabara, maana alijua angeshikwa, kama wewe umeshawahi kufika Monduli, utaijua ile barabara ya kutoka Monduli kikosini hadi kuikamata barabara kuu ilivyonyooka, na hivyo asingewahi kuimaliza angeshikwa fasta, na option ya kupanda gari ndio usiongelee, maana asingeenda mbali, lakini pia magari ya kule yote yalikuwa ni ya kijeshi(hasa kwa enzi zile).

Chakufanya ilikuwa ni kukatiza kwa njia za porini...Zipo njia nyingi san kutoka Monduli kwenda mjini Arusha bila kufuata barabara!
Na tunaposema porini, si lazima iwe MSITU....NI NJIA YOYOTE ISIYOKUWA OFFICIAL, hivyo usitafute msitu hapo.
LAKINI UKUMBUKE PIA JK alikuwa Mwanajeshi, hivyo ujue alikuwa amehitimu masomo ya kijeshi kama MM(Mbinu za Medani etc), ambapo KUTEMBEA PORINI NI ISHU KAMA CHAI TU, na sehemu kubwa ya mafunzo inafanyikia huko...Hivyo hakuna sababu ya njia ZOZOTE kukutana, kama unavyotaka wewe iwe, wajeshi hawahitaji njia nyoofu!

Hivyo sioni uzito wa hoja yako ya kushangaa jiografia ya Arusha na kutembea Porini.

Unachekesha mno halafu una hoja sana. hufai!
 
Kwa nini hakumjulisha bosi wake Meja Jenerali Natepe? Kwa madai yako kuwa Msuguri pia alihusika mbona hakumshitaki naye kwa Nyerere?
.

Unachoshangaza zaidi ni kwamba, ukipeleka tuhuma za uhalifu kwa IGP anatakiwa kukurudisha kuanzia ngazi za chini ndio protocol au itifaki sio kweli. Mimi ninavyojua IGP atapokea na kuagiza ngazi ya chini kumpa taarifa sahihi juu ya jambo hilo na mara nyingine sio lazima kuwaeleza ngazi za chini chanzo cha taarifa yake ili kumlinda mtoa taarifa. Kwa hiyo, kwa mtoa taarifa yeyote kuruka ngazi za uongozi kunategemea sana jinsi yeye Kikwete alivyokuwa anamwamini Natepe na Msuguri katika suala hilo.
 
Kipindi hicho mkuu wa chuo alikuwa Gideon Sayore, Kikwete alikuwa ni mmoja wakufunzi wa siasa chuoni hapo.

Sasa ilikuwa hivi,
Mzee Sayore alikuwa anafuga ng'ombewengi pamoja kufanya shughuli za kilimo kwawingi wakati huohuo akiwa mkuu wa chuo cha kijeshi Monduli.

Hivyo basi baada ya kuona ng'ombe wanatoa maziwamengi mno na mazao yametapakaa mashambani,. akaamua kuwa awe analiuzia jeshi mazao kama vile maharage na mahindi pamoja na maziwa na nyama kutoka kwenye mifugo yake.......na pesa anachukua yeye mwenye mazo.

Aliendelea kufanya hivyokwa kipindi kirefu tu.. ikiwa ni kama sehemu yake ya maisha....

Sasa bwana ,,kumbe Kikwette (JK) ilikuwa inamuuma sana sana, yaani mno! sasa haieleweki kama ilikuwa kweli ni kwa uzalendo ua wivu tu....akaandika barua kwa raisi kipindi hicho JK Nyerere.

Katika barua hiyo akaandika lawama nyiingi mno na majungu mengi sana dhidi ya Sayore, akimwita bepari, bwenyenye, mnyonyaji n.k huku akisema hafai kuwa mkuu wachuo hicho kwakuwa navunja miiko ya uongozi na mambo mengine meengi (si mnamjua JK anavyojua kupiga fitna!)...

Basi bwana, akamalizia mwisho kwakujiandika jina lake na sahihi yake huku akijiita mzalendo kamili barua ikapostiwa ikiwa imeadresiwa kwa rais wa nchi wakati huo!......

Mwalimu, aliipata barua ile aliifungua akaisomaaaa kisha akapiga hesabu zake....sijui aliwaza nini mzee yule, akaihifadhi ile barua ikaa sana ofini kwake bila kuchukua uamuzi wowote.

Siku moja alipokuja mkuu wa majeshi wakati huo "General Mtukula" (David Musuguli) ofisini kwa Mwalimu eaisi kipindi hicho, mwalimu akampa ile barua kutoka kwa Kikwete "akisema hayo ni maMbo yenu kayamalizeni hukohuko".

Basi bwana ile barua Mkuu wa majeshi alikaa nayo muda hivi kwenye makabrasha yakee...., sasa siku mija alikuja Mkuu wa chuo cha kijeshi Monduli(Sayore) Dar es salaam kufanya shughuli za kikazi akaenda hadi ofisini kwa Mkuu wa majeshi.

Baada ya shughuli kwisha na Sayore akiwa anajiandaa kwenda Monduli Mkuu wa majeshi alimwita, akampa ile barua ya Kikwete aliyomwandikia rais!!....

Sayore akaisoomaaa we akashangaa mno!! na akafura kwa hasira yule mmasai...., akuliza mwalimu kasemaje? Akaambiwa mwalimu kasema yamalizeni wenyewe!!.... Akasema naam, na akaondoka na ile barua hadi Monduli...

Alipofika tu yule mmasai aliitisha kikao cha wakufunzi wote na wakuu wengine pale chuoni, wakati wanajikusanya kwenda kwenye chumba cha mkutano yeye aliamua kwenda kutoa copy ile barua ya Kikwete, kopi nyingi idadi sawa na wajumbe wa mkutano ule....

Alipoingia mkutanoni akawaona wakuu na wakufunzi wote wameketi wakimsubiri wajue alicho waitia,.. akaanza kwa kuwauliza..jamani kama kuna mtu ana matatizo, au anaona kuna jambo haliendi sawa anyooshe mkono na saemekinacho mkereketa......watu wote wakawa kimya huku wengine wakisema hamna mkuu akiwemo Kikwette!!!

Basi bwana, tumalizie mkasa huu wa mkwere...

Sayore akaanza kuwagawia zile nakala (copies) za ile barua ya Kikwete kwenda kwa rais akawagawia wooote including Kikwete!!! Huku yule mmasasi Sayore akiwa amefura kwa hasira, macho mekunduuu! Akagonga ngumi juu ya meza kwa hasira na kusema someni hiyo barua!! kisha akatoka na kusema anakuja muda si mrefu...

Hapo Kikwete akajua kifo chake kimefika, akikumbuka macho ya yuile mmasai! akatetemeka macho yakamtoka lip! kwa woga!.. na wenzie wakamwanzishia zogo mle ndani......

Alichokifanya ni kuondoka haraka pale kikaoni wenzie wakajua bado yupo chuoni, kumbe safari ya Dar ikawa imeanza...!! Jamaa alitembea uchochoroni kwa muda mrefu sana huku akiogo kabisa kuingia barabara ya kuu...

Mashuhuda wanasema yule bwana akaja kupanda lift ya gari za vyama vya ushirika maeneo ya USA RIVER, hakukumbuka kubeba mzigo wowote!! Just imagine kutoka Monduli hadi hapo jamaa aliteseka sana... lakini yeye hakujali, cha muhimu ilikuwa kusalimisha maisha yake......

Basi huo ndiyo ukawa mwisho wa JK Monduli,........... hukurudi akaja Dar na kupangiwa kazi nyingine na chama... lakini alikuwa anamlaani sana Nyerere eti kwanini alimfanyia vile!!

Hicho ndicho chanzo cha JK kumchukia mwalimu na kugoma katakata kumwita baba wa taifa hadi leo! Yeye humwita mzee Nyrere tu au mwalimu baasi...na mara chache akiwa nje ya nchi humwita 'Father of our Nation', lakini ni pale anapotaka kupigiwa makofi kwa nukuu za Mwalimu....

**Ndugu zangu hiki ni kisa cha ukweli kwa 100%, inawezekana uandishi wangu ukawa na upungufu, lakini niemekipata kutoka watu mbalimbali waliowahi kuwa karibu sana na mkasa huu...

...kumbe umbea kaanza muda!
 
Hoja yangu hapa ni kuwa......Kwa mfano hata hivi sasa namba ya simu ya Rais kikwete iko wazi kwa wananchi wote na watumishi wote wa umma na serikali kama watafikia kutaka kumpa taarifa yeyote. Leo tukiona Rais kikwete anapokea taarifa isionekane kama kuna mtu hakufuata itifaki au kamshitaki mwingine bali ni jambo la kawaida katika utendaji kazi wenye lengo la kupunguza urasimu kwa kupunguza kufuaata chain of command kwa kila jambo. Hoja hapo isiwe kwa nini kikwete alimpatia nyerere taarifa hiyo bali ukweli wa taarifa hiyo ndio jambo la msingi.
 
Kwa nini hakumjulisha bosi wake Meja Jenerali Natepe? Kwa madai yako kuwa Msuguri pia alihusika mbona hakumshitaki naye kwa Nyerere?

Hoja yangu hapa ni kuwa......Kwa mfano hata hivi sasa namba ya simu ya Rais kikwete iko wazi kwa wananchi wote na watumishi wote wa umma na serikali kama watafikia kutaka kumpa taarifa yeyote. Leo tukiona Rais kikwete anapokea taarifa isionekane kama kuna mtu hakufuata itifaki au kamshitaki mwingine bali ni jambo la kawaida katika utendaji kazi wenye lengo la kupunguza urasimu kwa kupunguza kufuaata chain of command kwa kila jambo. Hoja hapo isiwe kwa nini kikwete alimpatia nyerere taarifa hiyo bali ukweli wa taarifa hiyo ndio jambo la msingi.
 
.

Unachoshangaza zaidi ni kwamba, ukipeleka tuhuma za uhalifu kwa IGP anatakiwa kukurudisha kuanzia ngazi za chini ndio protocol au itifaki sio kweli. Mimi ninavyojua IGP atapokea na kuagiza ngazi ya chini kumpa taarifa sahihi juu ya jambo hilo na mara nyingine sio lazima kuwaeleza ngazi za chini chanzo cha taarifa yake ili kumlinda mtoa taarifa. Kwa hiyo, kwa mtoa taarifa yeyote kuruka ngazi za uongozi kunategemea sana jinsi yeye Kikwete alivyokuwa anamwamini Natepe na Msuguri katika suala hilo.

Unachoshangaza wewe ni kutoelewa kuwa JK alikuwa mtumishi wa CCM wakati huo na sio Jeshi pamoja na kuwa na cheo cha kijeshi.Yeye pengine alimwandikia Nyerere kama Mwenyekiti na sio Rais,naye akamtupia Musuguri kama mwenyekiti wa mkoa wa 'Majeshi' na si kama CDF?(Wewe umechanganya na IGP). CCM hata leo mwanachama wa kawaida hawezi kulianzisha jambo ataambiwa pitia kwenye vikao kwanza. Sasa kipindi hicho cha mid 1980s kulikuwaje? Labda ulikuwa hujazaliwa au hujakuwa. Jikumbushe Kolimba ndugu yangu...ndiyo CCM hiyo!
 
Unachoshangaza wewe ni kutoelewa kuwa JK alikuwa mtumishi wa CCM wakati huo na sio Jeshi pamoja na kuwa na cheo cha kijeshi.Yeye pengine alimwandikia Nyerere kama Mwenyekiti na sio Rais,naye akamtupia Musuguri kama mwenyekiti wa mkoa wa 'Majeshi' na si kama CDF?(Wewe umechanganya na IGP). CCM hata leo mwanachama wa kawaida hawezi kulianzisha jambo ataambiwa pitia kwenye vikao kwanza. Sasa kipindi hicho cha mid 1980s kulikuwaje? Labda ulikuwa hujazaliwa au hujakuwa. Jikumbushe Kolimba ndugu yangu...ndiyo CCM hiyo!
.

Soma vizuri taarifa ya kwanza 'post' iliyoleta mjadala huu hapa inasema wakati huo Msuguri alikuwa mkuu wa majeshi( CDF). Ni yupi mkweli wewe au aliyeleta thread hapa. Wewe unaonekana hata nyumbani kwako ni mrasimu, mtoto akileta mashitaka kwako utamrusha kupeleka kwanza kwa kaka yake, kisha kwa mama yake ndipo akuletee wewe, taarifa za nchi kupinduliwa utaendelea kufuata protocal 'chain of commnd'. Rudi tena kwenye somo la management.....Ndugu acha kukariri mambo ya itifaki. kama umekuja hapa kututoa nje ya mada basi kazi unayo.
 
.

Soma vizuri taarifa ya post iliyoleta mjadala huu inasema wakati huo Msuguri alikuwa mkuu wa majeshi( CDF). Ni yupi mkweli wewe au aliyeleta thread hapa.

Sasa mimi kwani nimekataa kuwa Musuguri hakuwa CDF au wewe hujui historia. Chini ya chama kimoja majeshi yote yalichukuliwa kama 'mkoa' wa 21 wa CCM na kuwa na uongozi wake kama mikoa mingine CDF alikuwa Mwenyekiti wa mkoa na Natepe alikuwa katibu wa mkoa....na nilikuwepo sijasimuliwa
 
Mkwere ni mzee wa fitina kweli kweli, na Rizwani amerithi fitina za babake, kumbuka yaliyomkuta Masauni, ama kweli like father like son.

MIMI NAKUMBUKA YALIYOMKUTA KIFUKWE.......ETI WATU WANAOSHINDA BAKURUTU HAWANA NAFASI YANGA....PIA NAKUMBUKA SANA UFIRAUNI ALIOUFANYA BIG-BOSS KWA KUDANGANYA KUWA BASHE SI RAIA ili apate tu kumng'oa kwenye kura za maoni.
 
fotokop machine zilikuwepo tokea muda mrefu sana tu ndugu, tena kwa watu kama jesh ambapo huwa wanapata vitu vya teknolojia mapema, hilo nwala si la kuuliza aisee

Hii hapa 1972 IBM copier

Xerox914Big.jpg
 
Ungeniaminisha haya majungu 2005, leo ni kupoteza mda bila tija.Wala sitaki kuamini maana nikiamini itachukua memory ktk nvram ya kichwa yangu bure.

Mkuu unaonyesha kichwa yako inamemory ndogo sana mpaka unakwenda kwa budget.
Naweza amini story kwa kuwa kuna mifano mingi ya Mkwere ambayo inaonyesha jamaa hakuanza fitna leo wala jana.
Yupo wapi Steven Mashishanga nenda kamuone morogoro mzee alivyochoka kwa kumsupport Sumaye wapi Philip Mangula katibu mkuu CCm kipindi cha mkapa hakumsupport JK sasa anaendesha baloon lililochoka Iringa, na wengi wa wanazuoni wanasema katika kosa alilofanya Mkwere CCM ni kumpiga chini Mangula mtu aliyeweza kudumisha nidhamu chamani.

Fuatilia stori ya Professa Mahalu na kesi yake ya ubadhirifu wa pesa kule ubalozini Italia na safari ya Kikwete Italy pindi Mahalu akiwa balozi na baada ya kikwete kurudi kesi ikashonwa ili kumkomoa Mahalu. so binafsi naweza amini kwani inaendana na visasi na fitna nyingi, ikumbukwe Kikwete alikuwa mkufunzi so maya be alidhani anaweza pandishwa cheo but hakufuata Military Chain of Command
 
Kwani yeye JK alijaribu kulima huo mchicha na kuiuzia kambi na akazuiwa? Au ndio uvivu wenyewe wa kikwere,jembe halishikiki?

Kwi kwi kwi. Duh! Sasa na yeye angelima na kuliuzia jeshi matembele si angekuwa anashindana na wakubwa wake jeshini? Mgongano wa kimaslahi.

Kweli kwenye jamii forum kuna watoto, wafitini, mabinafsi na mabeberu ya kisasa. Yaani mtu alikua anapinga utumwa nyie mnasema mfitini? kama mnachuki binafsi msilete humu, siasa haina urafuki wala undugu kwa sasa mnaweka chuki against JK but kumbuka atakuja Mbowe au Slaa vizuri tu siku akimess up wote mtamchukia binafsi and this is what is happening in Libya.

Tuwe makini sana na tunapotoa comments zetu na tusilete story za vijiweni humu JF. Nikukumbushe tu kuwa JK alimaliza mafunzo yake vyema kabisa (alihitimu). Pia kumbuka kwa kipindi kile shimbo hakuwa Monduli fuatilia vizuri historia ya shimbo, na unapomuita Pimbi maana yake unajiita mwenyewe pimbi mdogo. Kimbuka wakati ule ilikua ukitoka nnje ya kambi ukiacha walinzi wa kambi kulikua na wanyama wakali kama simba na chui katika pori linalozunguka kambi hiyo hata leo kuna ushahidi wa kutosha kuhusu hilo.

Ndugu zangu lets be firm on useful issues and not on gossip na majungu na fitna zisizokuwa na maana kwetu.

Ndugu mtoa hoja,
Kama umesoma vema hoja za hapa, kuna watetezi wa JK na wale wanaounga mkono madongo kwa JK kwa ushahidi wa kimazingira. Please read carefully kabla hujatoa hitimisho la namna hiyo!
Mie sitetei ubaya, ila ukitaka kujua JK ni mtu wa namna gani, jaribu kifikiri kwa akili ya kawaida kabisa (ukichanganya na ya wenzako) kile alichokishabikia kuhusu uraia wa Hussein Bashe. Kama baba mwenye nyumba (Mwenyekiti wa Chama) hakutakiwa kumhukumu Bashe bila kungoja ushahidi wa kitaalamu kutoka kwa Idara ya Uhamiaji kuhusu uraia wa Bashe. Hata kama thread hiini ya uongo kuhusu JK, lakini ukiangalia namna alivyolishughulikia auala la Bashe basi iunaweza kuhitimisha kwamba majungu ni tabia yake.
Kama ushahidi huu wa kimazingira hautoshi, basi tuanze kujadili suala la Francis Kifukwe wa Yanga na majungu yaliyomzunguka.
 
Mkuu unaonyesha kichwa yako inamemory ndogo sana mpaka unakwenda kwa budget.
Naweza amini story kwa kuwa kuna mifano mingi ya Mkwere ambayo inaonyesha jamaa hakuanza fitna leo wala jana.
Yupo wapi Steven Mashishanga nenda kamuone morogoro mzee alivyochoka kwa kumsupport Sumaye wapi Philip Mangula katibu mkuu CCm kipindi cha mkapa hakumsupport JK sasa anaendesha baloon lililochoka Iringa, na wengi wa wanazuoni wanasema katika kosa alilofanya Mkwere CCM ni kumpiga chini Mangula mtu aliyeweza kudumisha nidhamu chamani.

Fuatilia stori ya Professa Mahalu na kesi yake ya ubadhirifu wa pesa kule ubalozini Italia na safari ya Kikwete Italy pindi Mahalu akiwa balozi na baada ya kikwete kurudi kesi ikashonwa ili kumkomoa Mahalu. so binafsi naweza amini kwani inaendana na visasi na fitna nyingi, ikumbukwe Kikwete alikuwa mkufunzi so maya be alidhani anaweza pandishwa cheo but hakufuata Military Chain of Command

JF Ni burdani kwelikweli.

Ina maana kama wasingekuwepo watu wanaofitiniwa, walala hoi tungekuwa na mzigo mzito wa kuwabeba watu ili waendelee kuishi maisha laini.

Hapo kwenye bold natamani kama idadi ya wafitiniwa ingeongezeka maana kwa sasa hivi watu wengi mno wanaishi na kuvuna pale ambapo hawastahili, wanabebwa kwa vile wako kwenye vitabu vizuri vya wenye mamlaka.
 
Heshima kwenu wanajamvi,

Kwanza naomba nimpongeze mleta thread Mzizi wa Mbuyu.

Kuna baadhi ya matukio yanayoondoa uwezekano wa habari yenyewe kuwa kweli au labda muanzisha thread kashindwa kuniaminisha kutokana na mtiririko wa hoja na matukio.

[1] Lt Gen Gideon Sayore kuuza bidhaa alizozalisha mwenyewe kwenye chuo anachokiongoza ni ukiukwaji mkubwa wa taratibu na kanuni za manunuzi ambazo zilikuwepo wakati huo.Ebu fikiria mkuu wa chuo analeta chuoni maziwa yaliyotiwa maji afisa anayepokea ana cheo cha Captain ataweza kuhoji ubora wa maziwa ya mkuu wake wa kazi mwenye cheo cha Brigadia ?.

[2] Major Kikwete kuandika barua kwa Amiri jeshi mkuu ni utovu wa nidhamu wa hali ya juu.Kwanini hakuipeleka barua kwa mkuu wa utawala jeshini ?,au kwa mkuu wa majeshi ?.Alipaswa kufahamu kwamba Rais ambaye pia ni amiri jeshi mkuu hakupaswa kupelekewa issues ndogo kiasi hicho.

[3] Ni makosa makubwa mwanajeshi kutoroka jeshi.Sipendi kuamini Kikwete aliondoka Monduli kwa staili ya mleta mada anavyotaka kutuaminisha.Yawezekana kweli ulikuwepo mtafaruku wa kuchongeana lakini akili yangu inaniambia jambo hilo lilishughulikiwa kivingine kabisa na pengine ndiyo maana Kikwete aliteremshwa cheo hadi ukatibu wa wilaya [graduate wa wakati wake halikuwa jambo dogo].

[4] Mwl Nyerere kama ni kweli aliandikiwa barua na Major Kikwete akaamua kuiteremsha kwa mkuu wa majeshi General Musuguru pengine hakutaka ishughulikiwe namna ilivyoshughulikiwa,yamkini alitaka Gen Musuguru alichunguze suala lenyewe ili kubaini ukweli wenyewe.Gen Musuguru alikuwa na uwanja mkubwa wa kumshulikia mkosaji lakini kwa mshangao aliamua kumpa barua mkosaji badala ya kumchunguza mtuhumiwa.Sioni kosa la Mwl Nyerere alieamua kufuata itifaki ya kijeshi.
 
JF Ni burdani kwelikweli.

Ina maana kama wasingekuwepo watu wanaofitiniwa, walala hoi tungekuwa na mzigo mzito wa kuwabeba watu ili waendelee kuishi maisha laini.

Hapo kwenye bold natamani kama idadi ya wafitiniwa ingeongezeka maana kwa sasa hivi watu wengi mno wanaishi na kuvuna pale ambapo hawastahili, wanabebwa kwa vile wako kwenye vitabu vizuri vya wenye mamlaka.

Mzee Edgar Maokola-Majogo...kama sio kuwa karibu sana na Mkapa naye angeipata fresh...yeye ndie aliyekabidhiwa JK baada ya kutoka Monduli kule Lindi...akampeleka Nachingwea (Farm 17 kwa mnaokumbuka JKT) badala ya kukaa town...alimchukia vilivyo
 
Back
Top Bottom