Papa D
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 753
- 182
Baada ya wabunge wa Chadema kususia hotuba ya JK, mheshimiwa wetu alikosa diplomasia rahisi ambayo ingewaweka CHADEMA mtegoni!! Ningekuwa mimi ndo JK siku hiyo ya tukio ningeongea kama ifuatavyo:-
Ndugu zangu nimeshtushwa na baadhi ya wabunge kuondoka ukumbini kwani kuondoka kwao kumefanya wananchi wanaowawakilisha wasipate uwakilishi stahiki!! Mimi Kama Raisi wa Jamhuri ya TZ nisingependa kuona baadhi ya Raia wa nchi hii wakitengwa kwenye mijadala inayohusu masuala ya maisha yao kwa namna yeyote ile. Kwa kuwa Mimi ni Rais wa Watanzania wote nahitaji kutatua dukuduku la kila Mtanzania bila kujali Dini, itikadi, rangi wala kabila! Mh. Spika, kwa idhini yako ningependa waheshimiwa walioondoka wafikishiwe ujumbe kwamba, Napendekeza Wateue wawakilishi watatu hadi sita ili nikutane nao kwa ajili ya kufahamu kiini cha tatizo, tukizungumze, tupange mikakati ya kuboresha kisha kupata muafaka. Mh. Spika naamini unawafahamu walioondoka na uwakilishi wao.