Kikwete alijua na kuruhusu jengo la ubalozi Italy kununuliwa

Yo Yo

JF-Expert Member
May 31, 2008
11,217
1,702
Kesi inayoondelea mahakamani dhidi ya aliekuwa balozi wa Tanzania mjini Roma Prof Mahalu; leo katika utetezi wake kasema kuwa Raisi Kikwete by then waziri wa mambo ya nje alifahamu na kubariki ununuzi wa jengo la ubalozi wetu Italy ambalo lilipelekea aliyekuwa balozi wa wakati huo Prof Mahalu kushtakiwa kwa kuliingizia taifa hasara ya mamilioni ya Euro....

Prof mahalu katika utetezi wake kasema Kikwete alipokuwa waziri wa mambo nje mnamo mwaka 2001 alitembelea nchini Italy na kukagua mjengo huo.....na aliuliza iweje ununuzi wa jengo uwe na mikataba miwili akaambiwa ni kawaida kwa ununuzi wa majengo ya bei nafuu kama lile......
 
Suala si Kikwete kujua, kesi inayomkabili Prof.MAHALU ni ubadhilifu wa fedha uliofanywa ambao Kikwete wakati huo akiwa Waziri wa mambo ya nje inawezekana hakuujua.
 
Kesi inayoondelea mahakamai dhidi ya aliekuwa balozi wa tz mjini rome prof Mahalu...leo katika utetezi wake kasema kuwa raisi kikwete by then waziri wa mambo ya njealijua na akabariki ununuzi wa jengo la ubalozi wetu Italy ambalo lilipelekea aliekuwa balozi wa wakati huo Prof mahalu kushtakiwa kwa kuliingizia taifa hasara ya mamilioni ya Euro....

Prof mahalu katika utetezi wake kasema KIkwete alipokuwa waziri wa mambo nje mnamo mwaka 2001 alitembelea nchini Italy na kukagua mjengo huo.....na aliuliza iweje ununuzi wa jengo uwe na mikataba miwili akaambiwa ni kawaida kwa ununuzi wa majengo ya bei nafuu kama lile......

Unategemea kuwa yeye kama Waziri wa mambo ya nje asingejua kuwa kuna ununuzi wa jengo? au unataka kutuambia nini?
 
It's taking too long! Nothing that much big! Au kuna mengine nyuma yake?
 
Suala si Kikwete kujua, kesi inayomkabili Prof.MAHALU ni ubadhilifu wa fedha uliofanywa ambao Kikwete wakati huo akiwa Waziri wa mambo ya nje inawezekana hakuujua.
Kikwete alijua alikagua jengo na kuambiwa jengo lina mikataba miwili.....na kama aliona mkataba ina maana alijua hata hela govnt itakayolipa.....ina maana hata yeye alishiriki huu ubadhirifu.....
 
Bila hizo Pesa asingeweza Kuchaguliwa; sababu walihonga, walitengeneza khanga, T-Shirt, kofia, na sherehe kila Wilaya ili ashinde....

Tatizo ni Wabaya wa Mahalu aliyekuwa ikulu ndie aliyefungua hiyo kesi na huyo Jamaa yuko Ubalozini hajabadilishwa kazi, Anaelekea Mwaka wa 6 sasa bila hata kubadilisha station.
 
Unategemea kuwa yeye kama Waziri wa mambo ya nje asingejua kuwa kuna ununuzi wa jengo? au unataka kutuambia nini?
Tafadhali hebu chukua taimu kidogo usome kilichoandikwa na haya majibu yako, wapi na wapi! Kikwete alijua na alibariki kama alivyojua ya Richmond na kubariki. Alitembelea Italy kabla ya ununuzi wa jengo kama alivyotembelea Houston Texas, USA kabla ya mkataba wa Richmond.

Both LCM na HCF in these two equations is Jakaya Mrisho Kikwete! Lakini ili kumsetiri mkulu, scapegoats lazima wapatikane na wote hadi dakika hii wanaonesha dalili za kukataa kuwa mabangusilo.
 
Suala si Kikwete kujua, kesi inayomkabili Prof.MAHALU ni ubadhilifu wa fedha uliofanywa ambao Kikwete wakati huo akiwa Waziri wa mambo ya nje inawezekana hakuujua.

Kwani kuna lipi linalotolea kwenye uongozi wake akalijua?

Kwani hao akina magufuli wao wanajuaje uozo unaotokea kwenye vizara na kuufanyia kazi Kikwete asijue yatokeayo kwenye vizara yake? Wizara kaiongoza miaka 10 na bado uozo unatokea hajui!? Yaani kaenda katembelea jengo, kaoneshwa hati mbili tofauti za jengo moja nae anacheka cheka tu na kutoa go ahead jengo linunuliwe. Tena kuonesha kuwa alilijua hilo dili, alipoenda kutembelea hilo jengo na kuuliza inakuwaje lina hati mbili akajibiwa kuwa nyumba za bei poa Italy huwa zina hati 2 2, bila hata kufikiri nae akakubali tu akatoa go ahead nunua.


Mahakama inatakiwa kumwita mahakani aje atoe ushahidi bana.
 
Kikwete alijua alikagua jengo na kuambiwa jengo lina mikataba miwili.....na kama aliona mkataba ina maana alijua hata hela govnt itakayolipa.....ina maana hata yeye alishiriki huu ubadhirifu.....

This is too much, kila siku wana JF tunaokoteza okoteza tu mambo yanayomhusu Kikwete... don't we have other important issues than these as Great thinkers?
 
Jamani hii ishu kumuhusisha JK tutakuwa tunamuonea tu.
Angalieni uwezo wa upeo wake, hana critical mind, hata kama aliona mikataba 2, i am sure aliona ni kama makaratasi mengine tu.
Historia inaonyesha JK hakuwa mtu wa madili au mishemishe, yeye zake zilikuwa totoz.
Sasa ukichanganya hulka yake na uwezo wa upeo wake, kwa ili tunamuonea...
 
This is too much, kila siku wana JF tunaokoteza okoteza tu mambo yanayomhusu Kikwete... don't we have other important issues than these as Great thinkers?
True, this is too much. Kila siku Kengemumaji kazi yake ni kumtetea Kikwete...dont you see where our beloved country is headed to? Remember the buck stops with the President!
 
This is too much, kila siku wana JF tunaokoteza okoteza tu mambo yanayomhusu Kikwete... don't we have other important issues than these as Great thinkers?

baadh ya ishu zinazomhusu Jk ni important sana,kama hii ya mahalu
 
Kwani kuna lipi linalotolea kwenye uongozi wake akalijua?

Kwani hao akina magufuli wao wanajuaje uozo unaotokea kwenye vizara na kuufanyia kazi Kikwete asijue yatokeayo kwenye vizara yake? Wizara kaiongoza miaka 10 na bado uozo unatokea hajui!? Yaani kaenda katembelea jengo, kaoneshwa hati mbili tofauti za jengo moja nae anacheka cheka tu na kutoa go ahead jengo linunuliwe. Tena kuonesha kuwa alilijua hilo dili, alipoenda kutembelea hilo jengo na kuuliza inakuwaje lina hati mbili akajibiwa kuwa nyumba za bei poa Italy huwa zina hati 2 2, bila hata kufikiri nae akakubali tu akatoa go ahead nunua.


Mahakama inatakiwa kumwita mahakani aje atoe ushahidi bana.

Hivi ni nani aliyebaini kuwepo kwa wizi wa fedha katika ununuzi wa jengo hilo?
 
Kujua habari za ununuzi wa jengo hakuepushi mahalu kumdanganya waziri wa mambo ya nje (kikwete) by then. Labda angesema Kikwete alijua udanganyifu huo ndio tungehoji kuhusika kwa JK.
 
Mahalu ni mwizi aliyekubuhu anatumia mgongo wa kujuana na Mkapa na Kikwete kujinasua na kesi mahakamani. Kwani uwizi wote unaofanyika hapa nchi kikwete anajua kwa kuwa ni Rais wa nchi? nonsenses zingine hazilingani na hadhi ya uprofesa.
 
The guy is everywhere!!!!Sasa sheria itamuadhibu nani? Au ndio mambo ya mbuzi wa kafara??
 
jamani naomba kuuliza, mahalu amekula ngapi? maana tokea hii serikali ya kishkaji imeshika hatamu wanaopelekwa mahakamani niwa vijisent tu. halafu mimi hata sijui hivi mramba iliishaje? jairo? kagoda? deepgreen? kengemumaji na ritz wanaweza kuwa na majibu maana nadhani hata hela ya voucher ya moderm wanalipiwa na ikulu ya rangi za yanga.
 
Mbona kila tuhuma anatajwa? I cant get the picture of what will take place as from 2016
 
Jamani hii ishu kumuhusisha JK tutakuwa tunamuonea tu.
Angalieni uwezo wa upeo wake, hana critical mind, hata kama aliona mikataba 2, i am sure aliona ni kama makaratasi mengine tu.
Historia inaonyesha JK hakuwa mtu wa madili au mishemishe, yeye zake zilikuwa totoz.
Sasa ukichanganya hulka yake na uwezo wa upeo wake, kwa ili tunamuonea...


Kikwete ni mtaalam wa hati za majengo na mikataba? wizi ni fani tusidanganyike kwamba mwizi anafanya mambo ili akamatwe. Mahalu hakuwa mjinga kiasi cha kufanya Jk ajue kama hakuhusika na deal hiyo.
 
Kujua habari za ununuzi wa jengo hakuepushi mahalu kumdanganya waziri wa mambo ya nje (kikwete) by then. Labda angesema Kikwete alijua udanganyifu huo ndio tungehoji kuhusika kwa JK.

Duh, MAMA POROJO, je kudanganywa kwenyewe ni kama hii hapa chini? Yaani alidanganywa akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na hadi leo anadanganywa akiwa Raisi - je hagutuki? Bila shaka hapa anayelaumiwa ni mzungu wa watu, LOL...

ru76er.jpg

 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom