Kikwete akubali kuhusika na wizi na benki kuu

Mwafrika wa Kike

JF-Expert Member
Jul 5, 2007
5,185
56
Nimesoma hiyo story ya magazetini kuhusu maelezo ya balozi wa marekani kuwa serikali ya Kikwete haijawasiliana na serikali ya Marekani kuhusu suala la Balali kurejeshwa nyumbani. Nimesoma pia ile story ya wizara ya mambo ya nje wakijikoroga kuwa wao sio wanaotakiwa kumtaka Balali arudi nyumbani bali ni wizara ya fedha ndiyo inatakiwa kufanya hivi (what a moronic excuse!).

Haya yote yanadhihirisha wazi kuwa serikali ya Kikwete haina mpango wa kumtaka Balali arudi nyumbani kusimamia kesi ya wizi wa pesa za BoT unaomkabili (kulingana na maelezo ya serikali). Wakati serikali ya Kikwete imetoa miezi sita kwa waliohusika na wizi huu kukimbia nchi na kuficha mali zao (huku pia wakisubiria kuona kama Balali atakufa) oooopsss kuipa bodi ya BoT kufanya uchunguzi wa wizi wa BoT, hotuba ya waziri Meghji bungeni kuhusu wizi huu inaonyesha kuwa mengi sana yanataka kufichwa hapa ili kuwafunika wahusika wakuu wa wizi huu - Mkapa, Mramba, Mgonja, Rostam Aziz, na sasa mkuu wa kaya mwenyewe Kikwete.

Inabidi sasa Kikwete akubali kuhusika na wizi huu wa BoT na ajiengue kabisa katika kuendesha uchunguzi huku akiruhusu tume huru ya bunge ifanye uchunguzi wa kila kilichotokea huko BoT na uchunguzi huu urudishwe kwa miaka kumi nyuma kwa kuanza na madai ya Mrema yalifanyiwa uchunguzi na kina Oyombe (mb-Rorya) na wengine.

Inabidi sasa Kikwete akubali kuhusika na wizi huu moja kwa moja na akubali kuwa ushindi wake wa "kishindo" dhidi ya wapinzani wake ndani ya ccm na ule mkuu ni flawed na inabidi taratibu zifanyike za kuwa na uchaguzi mwingine wa haki.

Inabidi sasa Kikwete akubali kuhusika na wizi huu na pia aombe msamaha kwa wapinzani wake wa ndani ya ccm kina Malecela, Sumaye, Salim Ahmed Salim na wengine wote aliotumia pesa za wizi na vyombo vya habari vichafu vya mkoloni na mwizi Rostam Aziz kuwachafua ili ashinde kwa "kishindo"

Raisi Kikwete, chagua kufanya kitu chema mapema kabla jehanam haijashushwa juu yako kutoka kwa vilio vya wazazi na ndugu wanaopoteza watoto wao na mama zao kwa kukosa madawa huku wewe ukitumia mabilioni kusafiri na kufanya personal shoping zako kwa pesa za wizi
!
 
Tangu lini JAMBAZI akampeleka mahakamani JAMBAZI mwenzake ambaye wameshirikiana nae kuiba. Hiyo Haiyumkiniki kabisa. Kikwete ni FISADI unategemea ataenda kumkamata FISADI mwenzake Balali au kuwachukulia hatua hao wengine wanaotanua hapo Bongo.
 
Nimesoma hiyo story ya magazetini kuhusu maelezo ya balozi wa marekani kuwa serikali ya Kikwete haijawasiliana na serikali ya Marekani kuhusu suala la Balali kurejeshwa nyumbani. Nimesoma pia ile story ya wizara ya mambo ya nje wakijikoroga kuwa wao sio wanaotakiwa kumtaka Balali arudi nyumbani bali ni wizara ya fedha ndiyo inatakiwa kufanya hivi (what a moronic excuse!).

Haya yote yanadhihirisha wazi kuwa serikali ya Kikwete haina mpango wa kumtaka Balali arudi nyumbani kusimamia kesi ya wizi wa pesa za BoT unaomkabili (kulingana na maelezo ya serikali). Wakati serikali ya Kikwete imetoa miezi sita kwa waliohusika na wizi huu kukimbia nchi na kuficha mali zao (huku pia wakisubiria kuona kama Balali atakufa) oooopsss kuipa bodi ya BoT kufanya uchunguzi wa wizi wa BoT, hotuba ya waziri Meghji bungeni kuhusu wizi huu inaonyesha kuwa mengi sana yanataka kufichwa hapa ili kuwafunika wahusika wakuu wa wizi huu - Mkapa, Mramba, Mgonja, Rostam Aziz, na sasa mkuu wa kaya mwenyewe Kikwete.

Inabidi sasa Kikwete akubali kuhusika na wizi huu wa BoT na ajiengue kabisa katika kuendesha uchunguzi huku akiruhusu tume huru ya bunge ifanye uchunguzi wa kila kilichotokea huko BoT na uchunguzi huu urudishwe kwa miaka kumi nyuma kwa kuanza na madai ya Mrema yalifanyiwa uchunguzi na kina Oyombe (mb-Rorya) na wengine.

Inabidi sasa Kikwete akubali kuhusika na wizi huu moja kwa moja na akubali kuwa ushindi wake wa "kishindo" dhidi ya wapinzani wake ndani ya ccm na ule mkuu ni flawed na inabidi taratibu zifanyike za kuwa na uchaguzi mwingine wa haki.

Inabidi sasa Kikwete akubali kuhusika na wizi huu na pia aombe msamaha kwa wapinzani wake wa ndani ya ccm kina Malecela, Sumaye, Salim Ahmed Salim na wengine wote aliotumia pesa za wizi na vyombo vya habari vichafu vya mkoloni na mwizi Rostam Aziz kuwachafua ili ashinde kwa "kishindo"

Raisi Kikwete, chagua kufanya kitu chema mapema kabla jehanam haijashushwa juu yako kutoka kwa vilio vya wazazi na ndugu wanaopoteza watoto wao na mama zao kwa kukosa madawa huku wewe ukitumia mabilioni kusafiri na kufanya personal shoping zako kwa pesa za wizi
!


M/kike
natanguliza heshima, nimependa sana ulivyoandika hii article hivi magazeti ya home hayawezi chapisha kitu kama hii kwa public consumption ingesaidia wanainchi kuona wanavyochezewa shere mchana kweupe na changa la macho juu....
 
Tangu lini JAMBAZI akampeleka mahakamani JAMBAZI mwenzake ambaye wameshirikiana nae kuiba. Hiyo Haiyumkiniki kabisa. Kikwete ni FISADI unategemea ataenda kumkamata FISADI mwenzake Balali au kuwachukulia hatua hao wengine wanaotanua hapo Bongo.[/QUOTE/]
HILI NI TATIZOLA KUWA NA HARAKA KULIKO WEPESI,TUME ZIMEUNDWA WAMEPEWA MIEZI SITA MNATAKA KUJUA KWA NINI HAJAKAMATWA.WATU HAWKATWI BILA TARATIBU NDUGU YANGU NI LAZIMA SHERIA ZIFUATE MKONDO WAKE.WAPENI MUDA MAWAZO YA UDIKTETA HAYANA NAFASI
 
HILI NI TATIZOLA KUWA NA HARAKA KULIKO WEPESI,TUME ZIMEUNDWA WAMEPEWA MIEZI SITA MNATAKA KUJUA KWA NINI HAJAKAMATWA.WATU HAWKATWI BILA TARATIBU NDUGU YANGU NI LAZIMA SHERIA ZIFUATE MKONDO WAKE.WAPENI MUDA MAWAZO YA UDIKTETA HAYANA NAFASI
Watanzania wameshasubiri vya kutosha na hakuna chochote kinachofanyika na hii sio tu suala la ujambazi uliofanyika BOT, ni mambo mengi sana yanayohusuyo mustabali wa nchi yetu, haya mambo ya kuunda tume ya kwanza kuchunguza kitu fulani halafu inaundwa tume nyingine kuchunguza majibu ya tume ya kwanza tumeshachoshwa nayo, halafu mwisho watakuja na tume ya tatu kuchunguza majibu ya tume ya kwanza na ya pili, gimme a break.
 
Mwafrika Jike you have pressed it really hard. Hebu wacha nichukue mhindi wangu wa kuchoma kwanza then nirudi hapa cafe .
 
Mwafrika Jike you have pressed it really hard. Hebu wacha nichukue mhindi wangu wa kuchoma kwanza then nirudi hapa cafe .

Kwi kwi kwi!!!! Mwafrike wa Kike ni Ruto wetu JF. Anapiligilia misumari kweli kweli.

Itabidi nimwingize kwenye kampeni yangu 2010, ninaamini sitaibiwa kura.

Kwenye hili JK amechemsha au anachemsha mno, inaweza kumtokea puani. Wacha
wengine tusubiri hiyo miezi sita ila dalili sio nzuri kabisa.

Kitu cha kwanza inabidi atoe hiyo report, tusome wenyewe maana tuna uwezo wa kuielewa. Kuna madudu mengi sana ambayo tunadanganywa.
 
Mtanzania
Mimi nasema JK anajipalia mkaa kila mara . Moto huu ni mkali na kwa mwendo huu wa umasikini kukua kwa kasi basi hakuna wa kusahau . Miezi sita si mingi lakini leo wamepitisha sheria za kuchunguza kabla ya kukamata mtu . Mchezp huu baada ya kusainiwa na kuwa ni sheria basi CCM watachezo na hiki kipendele hadi mshangae.
 
Kwi kwi kwi!!!! Mwafrike wa Kike ni Ruto wetu JF. Anapiligilia misumari kweli kweli.

Itabidi nimwingize kwenye kampeni yangu 2010, ninaamini sitaibiwa kura.

Kwenye hili JK amechemsha au anachemsha mno, inaweza kumtokea puani. Wacha
wengine tusubiri hiyo miezi sita ila dalili sio nzuri kabisa.

Kitu cha kwanza inabidi atoe hiyo report, tusome wenyewe maana tuna uwezo wa kuielewa. Kuna madudu mengi sana ambayo tunadanganywa.

Kwi kwi kwi

Mtanzania, mimi nikiwa Ruto sijui nani atakuwa Odinga sasa.
Hii report ndiyo inasubiriwa tu hapa, mengine yote ni usanii
 
madudu kibao mpaka vichwa vinatuuma Watanzania.

Balali aliomba kustaafu, akakataliwa, anafukuzwa kazi ohh no uteuzi umetenguliwa akiwa hayupo (Lakini bado ni mtumishi wa serikali). Hawasemi yuko mji gani, anaumwa nini, atarudi lini haya yote hawayajui wakati hospital bill wanamlipia, tiketi walimkatia, hotel walimlipia huko kudai kwamba hawajui aliko kunaleta utata, baya zaidi ni pale Serikali ya Joji Kichaka inaposema iko tayari kutusaidia kumrudisha Balali na mapesa yaliyoibiwa lakini mpaka mkuu wetu aka Brother Vasco Da gama aseme. Anangoja nini kutumia nafasi hiyo kuomba Balali na mapesa yetu yarudishwe? Kuna kitu gani kinafichwa hapa?. Watanzania walio wengi ambao ndiyo waliokupa Ofisi ama waliokuajili kazi wanamtaka Balali arudi na wewe kama mkuu wa kaya ukisema tu kwa balozi wa america "Yes tuleteeni Balali", bila shaka atakuwa hapa Bongo in two days time from today. Sasa mkuu wetu wa kaya unaogopa nini ama unataka wapiga kura wako wakuelewe vipi?.

Ripoti ya uchunguzi wa ufisadi huo ndani ya chombo chetu nyeti cha fedha katika nchi kwanini isiwekwe wazi ama bayana ili kila mwenye uwezo wa kuisoma na aisome?. Kuna madudu gani ndani ya ripoti hiyo mpaka uifanye siri?. BOT ni mali ya watanzania na yale mapesa yaliyochotwa ni mali ya watanzania, na ile kampuni iliyopewa kazi ya uchunguzi imelipwa pesa za watanzania, sasa kwanini tusipewe ripoti yetu hadharani?. Naona kabisa machafuko yanakuja ndani ya Tanzania katika awamu hii ya uongozi. Damu na roho za wananchi wa Tanzania ziko mikononi mwako mkuu wa kaya, sisi ni sawa na wasomali, warwanda ama wakenya sisi siyo malaika hivyo maudhi na dhuluma bila shaka vimefika kikomo, wananchi wataingia mitaani na kuanza kuchinjana.
 
This whole thing is a fairy tale.....

Mjomba angalia waungwana wasikushikie bango kuwa unaundermine effort za watu. Dah nimecheka sana.

Hii issue ya BOT naona for now imekwenda half time tusubiri hao mabwana waliopewa 6 months watupe upande wao wa kazi. other than than tusitegemee kipya labda spin tuu.
 
"
Inabidi sasa Kikwete akubali kuhusika na wizi huu na pia aombe msamaha kwa wapinzani wake wa ndani ya ccm kina Malecela, Sumaye, Salim Ahmed Salim na wengine wote aliotumia pesa za wizi na vyombo vya habari vichafu vya mkoloni na mwizi Rostam Aziz kuwachafua ili ashinde kwa "kishindo
.

Nafikiri ni Salim Ahmed Salim pekee maybe hakuwepo waliochota pesa zetu walala hoi....kama mnakumbuka wakati wa kampeni pesa zilikuwa zikimwagwa kama mchanga from all campaign camps except Salim's camp.
 
JK anafanya mchezo na walalahoi? wale vijana wasio na sehemu za kufanyia biashara zao,kukosa ajira na matibabu duni yanayo sababisha vifo vya ndugu zao wakielimika na kuelewa nini serikali inawafanyika katika rasilimali zao patakuwa hapatoshi hapa.
JK aache kutupeleka pabaya,atimize wajibu wake kwa uadilifu mkubwa bila kujali kuwatoa kafara washirika wake hapo ndio atkapojenga heshima yake na kuiepusha nchi na hatari ya watu kujichukulia sheria mikononi mwao.
Kuvamiwa kwa mashamba ya Balali ni ishara tosha ya yatakayojiri siku za usoni.
 
HILI NI TATIZOLA KUWA NA HARAKA KULIKO WEPESI,TUME ZIMEUNDWA WAMEPEWA MIEZI SITA MNATAKA KUJUA KWA NINI HAJAKAMATWA.WATU HAWKATWI BILA TARATIBU NDUGU YANGU NI LAZIMA SHERIA ZIFUATE MKONDO WAKE.WAPENI MUDA MAWAZO YA UDIKTETA HAYANA NAFASI[/QUOTE]


Hivi, kama ninaweza kumpongeza M/Kike au M/Kjj kwa jumbe makini wanazotoa, Je, haki hiyo ninayopia kumsiriba mtu anayeleta pumba humu jamvini?

Kama jibu ni ndiyo, basi niseme: nasikia kut.p..ka kila nikisoma replies za Fisadi Mtoto. Nashauri kwamba hata kama kuna uhuru wa kutoa maoni, basi hapa JF watu kama huyu Mtoto wapewe uhuru wa kusoma na kusikiliza maoni mpaka hapo watakapokuwa wamekuwa. Hiyo ndiyo itakuwa haki na stahili yao.

Pili, jina huashiria matendo. Na mtazamo wetu wana JF lazima uendane na utambulisho wetu. Mwl aliwahi kusema "Kiongozi ukisema unaichukia rushwa, tukikuangalia wewe na matendo yako yatudhihirishie maneno yako" Huwezi kuruhusu kukaa na Mwanajeshi mpinzani katika kombania na ukampa haki na stahili zote sawa na za wale watiifu. Yamkini atawapotosha watiifu au itasaliti. Imekuwa tabia yetu ya damu Wadanganyika kila mara kutafuta fimbo baada ya kuumwa na nyoka au kukinga baada ya mvua kukatika. (Rejea tukio la Mushi). Hebu JK tujifunze mara moja maana tayari tulikwisha umwa na nyoka. Tungeyafanyia kazi ya JJ Mnyika Habari na historia ingekuwa Ushindi kwetu.

Hatujachelewa, maadamu JF bado iko mahali pake pa enzi, Moderator naomba kuwasilisha. Mpe limited access Fisadi Mtoto. Mwachie uwezo wa kusoma na kusikiliza audio au kuangalia video hapa JF.

Naomba kupingwa na kuungwa mkono!
 
Tume zimeundwa na kampuni ya kufanya uchunguzi ikapewa kazi,tukaambiwa kilichotokea na wahusika wakatajwa moja kwa moja,unahitaji ushahidi gani na busara zipi kuendelea kusubiri uchunguzi wa tume? Sheria zetu zinasemaje? Ukiwa mtuhumiwa unastahili kukaa chini ya polisi mpaka pale itakaPOTHITIKA UKUSHUSIKA JAPO NI SHERIA YA KIKOLONI BUT IT WORK TO ALL PEOPLE AND NOT ONLY FOR MINORITY? FISADI MTOTO SIKUBALIANI NA WEWE
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom