Kikwete Akataa Balali Asiletwe!

jmushi1

Platinum Member
Nov 2, 2007
24,967
22,476
Balozi wa Marekani nchini, Bw. Mark Green amesema kuwa serikali ya nchi yake haijaombwa na Serikali ya Tanzania kumrudisha nchini aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dk. Daudi Balali.

Alisema kwa kiasi kikubwa, hatua kama hizo zitategemea maamuzi yatakayochukuliwa na Serikali ya Tanzania kuhusiana na jambo hilo.

Hata hivyo, alisema wao wako tayari kumsaidia Rais Jakaya Kikwete kushughulikia ombi litakalofanikisha utekelezaji wa azma hiyo kama ipo.

Bw. Green alikuwa akijibu maswali ya wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari ofisini kwake ambapo aliwaita kuzungumzia ujio wa Rais George Bush nchini mwezi ujao.

Alipoulizwa mahali alipo hivi sasa Dk. Balali huko Marekani, Balozi huyo alijibu kwamba hajui na kuongeza kwamba sheria za Marekani hazimruhusu kutangaza nyendo na mahali walipo watu wanaoishi Marekani.

Kuhusu uwezekano wa kurudishwa nchini fedha zinazodaiwa kuchotwa BoT endapo sehemu yake imehifadhiwa kwenye mabenki ya Marekani, alisema kwa kuzingatia sheria za nchini mwake, fedha kama hizo zitafuatiliwa na hata kama zilipitia katika mkondo wa benki za Marekani.

Alisema suala la kurudishwa kwa fedha (kama zipo), kama ilivyo katika kumrejesha Balali, kwa kiasi kikubwa pia litategemea maamuzi ya Serikali ya Tanzania.

Aidha, kuhusu habari zilizozagaa kuwa Dk. Balali alipatiwa uraia wa Marekani kwa njia ya Green Card, alisema kuwa mtu yeyote anayeomba viza maana yake siyo raia wa Marekani na kwamba Balali aliomba viza miaka miwili iliyopita kwa wadhifa aliokuwa nao kama Gavana wa BoT.

Alisema, juhudi za Rais Kikwete kuhusu mapambano dhidi ya Rushwa ni miongoni mwa mambo ambayo Rais Bush atayazungumzia akiwa nchini.

Tanzania ni miongoni mwa nchi tano za Afrika ambazo zitatembelewa na Rais George Bush wa Marekani mwezi ujao. Nchi zingine ni Rwanda, Benin, Ghana na Liberia.
  • SOURCE: Nipashe
 
Sasa mkuu this is a big twist .Hata waandishi wa habari wana nafuu . Maelezo yote nimesoma sijaona anapo husika JK na kumleta jamaa . Ama umekosea kuleta habari hapa ?Unaweza kuwa umechanganya habari hizi ?
 
Ni wazi kwamba Mh Rais amesikia vilio vya watanzania kuhusu kurejeshwa kwa Ex Governor Balali.

Ni wazi kwamba amekuwa akiziba masikio kuhusiana na vilio hivi vya wazalendo.

Wananchi walikuwa wakifikiri kuwa Kikwete hawezi kumrudisha Balali!

Leo hii kwa kudra za mwenyezi Mungu watanzania wamefunguliwa macho kwa kiasi fulani kuhusiana na kugoma huko kwa Rais kuwaeleza wananchi kuwa kwanini alimfukuzia Balali nje na sasa anagoma kumrudisha ili sheria ichukue mkondo wake!


Leo hii wananchi wamejulishwa kwa kupitia balozi wa Marekani nchini kwamba"KIKWETE PEKE YAKE NDIYO MWENYE UWEZO SI TU WA KUMRUDISHA BALALI BALI PIA HATA FEDHA ZILIZOWEKWA NJE YA NCHI"

Tunabaki kujiuliza...kwanini Kikwete amegoma kumrudisha Balali?

Je Kikwete atagoma kuzirudisha fedha zilizoko kwenye akaunti za nje?Ni budi tujiulize maswali haya.

Pongezi nyingi zimekuwa zikitolewa kwa Rais kuhusu uundaji wa bodi ya uchunguzi kupitia taarifa ambazo wananchi wataziwasilisha kwa wajumbe wa bodi hiyo.

Sitaki kuwa negative..ila kama kweli juhudi hizi hazina siasa..then hatua dhidi ya wale ambao tayari wamegundulika kuhusika zichukuliwe!

Wananchi watumie njia za amani kama vile maandamano ili kumshinikiza Mh Rais amlete swahiba wake Balali ili kulinda heshima yake mbele ya taifa si tu kwa kizazi hiki,bali historia itamlinda mbele ya kizazi kijacho kwa uzalendo atakaouonyesha!

Ni wazi kwamba uzalendo kwa Kikwete hivi sasa ni kama neno baya sana!Uzalendo ina maana kuwa radhi kuwatelekeza maswahiba wako kwa manufaa ya Taifa!

SWALI MOJA BADO LITABAKI KICHWANI MWA WAZALENDO WOTE.."JE KIKWETE NI MWENZAO?
 
BALALI, BALAI BALI BA. jamani balozi katoboa siri, hamuoni? Tangu saga la balali lianze na ana tuhuma nzito bado serikali haijaomba kibali cha kurudisha ili ajibu tuhuma? tunasema kiwete yumo, maana kama hayumo si angemwagiza mwema akamkurupue huko usa. Au anasubiri bwana kichaka aje ili aombe. Wahat they are doinhg ni delaying tactics ili mapesa yahmishiwe uswis ambako yatatulia na mwisho unasikia balali ni raia wa marekani. hivyo hawezi kuja. Someni btn lines.
 
Sasa mkuu this is a big twist .Hata waandishi wa habari wana nafuu . Maelezo yote nimesoma sijaona anapo husika JK na kumleta jamaa . Ama umekosea kuleta habari hapa ?Unaweza kuwa umechanganya habari hizi ?
Lunyungu wewe ni senior expert member..sasa hapa itabidi unionyeshe jinsi hicho cheo chako cha expertisim kinavyofanya kazi!
Swali la kwanza...

1)Serikali ni nani?Yani we ulitaka balozi akwambie kuwa"KIKWETE NDO KAGOMA"?

Anaposema serikali..ni kwasababu hataki kuwasingleout viongozi..tunajua serikali inajumuisha yeye rais mwenyewe,makamu wake na mawaziri wake..sasa nani mtopu hapo?

We hujui kuwa rais wa tanzania ana madaraka makubwa kuliko mtu yeyote yule?Na si tu ndani ya serikali,bali nchini kote!

Sina haja ya kuongeza swali la pili..naomba unijibu hili kwanza!
 
BALALI, BALAI BALI BA. jamani balozi katoboa siri, hamuoni? Tangu saga la balali lianze na ana tuhuma nzito bado serikali haijaomba kibali cha kurudisha ili ajibu tuhuma? tunasema kiwete yumo, maana kama hayumo si angemwagiza mwema akamkurupue huko usa. Au anasubiri bwana kichaka aje ili aombe. Wahat they are doinhg ni delaying tactics ili mapesa yahmishiwe uswis ambako yatatulia na mwisho unasikia balali ni raia wa marekani. hivyo hawezi kuja. Someni btn lines.
HANA HAJA YA KUMWAMBIA MWEMA..APIGE SIMU TU KWA BALOZI WA MAREKANI BONGO..NA BALALI ANALETWA HAPA!
 
Hizi SPIN zingine hatari kabisa, kwanini mumwekee JK mdomoni maneno ambayo hajayhasema?

Subiri hiyo miezi yake sita na akishindwa basi tumhukumu, vinginevyo heading kama hiyo ambayo haina ukweli wowote inaitwa SPINNING.
 
Hizi SPIN zingine hatari kabisa, kwanini mumwekee JK mdomoni maneno ambayo hajayhasema?

Subiri hiyo miezi yake sita na akishindwa basi tumhukumu, vinginevyo heading kama hiyo ambayo haina ukweli wowote inaitwa SPINNING.

...bob hakuna spin hapo,issue ni kwamba balali ni fisadi na mpaka leo hajafikishwa mahakamani,sasa unataka tufikirie nini hapo? si tunajua wamekataa tuu kumshughulia na hakuna kingine maana report iko wazi na 133bl zimepotea under his watch,kamata huyo Balali akaongee na majaji aseme pesa ziko wapi sio kutuundia tume nyingine
 
hizi spin zingine hatari kabisa, kwanini mumwekee jk mdomoni maneno ambayo hajayhasema?

Subiri hiyo miezi yake sita na akishindwa basi tumhukumu, vinginevyo heading kama hiyo ambayo haina ukweli wowote inaitwa spinning.
spinning?give me a break!kwanini asingesubiri hiyo miezi sita kabla ajasema balali ni mwizi?

Anasubiri nini ndani ya hiyo miezi sita ili kumhoji balali kuhusu tuhuma hizo?ama amefanya makosa kumfukuza balali kabla ya kufanya uchuinguzi?

Nani anaspin hapo?serikali yake ambayo marekani imesema hajakubaliana nao kumrudisha balali ama mimi ninayetoa hoja yenye nguvu?

Mtanzania wewe ni mzalendo kweli?ama jina tu?
 
Afadhali hata Koba uwaeleze..wamarekani wameulizwa..wakasema Rais wenu hajasema Tanzania inamhitaji Balali!sas nani ashikwe shati hapa zaidi ya kiongozi mkuu wa serikali ambaye ni Kikwete?Ama rais siyo serikali?wajibu hayo maswali na waache spinning
 
ingawa sijapenda kichwa cha habari lakini mantiki ndani yake ni dhahiri. Je, serikali ya Rais Kikwete inataka Balali arudi nyumbani. Arudi kufanya nini?

a. Hadi hivi sasa Balali ni mtu huru hajatuhumiwa kosa lolote lile.

b. Kuvuliwa visa yake ya Marekani hakuhusiani hata kidogo na kitendo chochote cha kihalifu.

c. Serikali ya TAnzania aidha inao ushahidi wa vitendo vya kihalifu vya Balali au hauna. Kama haina basi hakuna sababu ya kumtaka Balali arudi.

d. Kama serikali inaamini Balali ameshiriki kwa namna yoyote ile na ubadhirifu (kwenye tamko lake haisemi hivyo), basi wangekwisha kufikisha kesi mahakamani, mbona ya Rada wameifikisha mahakamani wakati Vithlani hayupo?

HIvyo, hadi hivi sasa serikali ya JK haijaonesha nia ya kutaka Balali arudi kwani hawajamtuhumu kitu chochote.
 
What the F.........k is this!

Sisi sio watoto, naona kuna members ambao wanatakiwa wachangie Darhotwire tu!

Moderators naomba hii spin iunganishwe na topic halisi
 
ingawa sijapenda kichwa cha habari lakini mantiki ndani yake ni dhahiri. Je, serikali ya Rais Kikwete inataka Balali arudi nyumbani. Arudi kufanya nini?

a. Hadi hivi sasa Balali ni mtu huru hajatuhumiwa kosa lolote lile.

b. Kuvuliwa visa yake ya Marekani hakuhusiani hata kidogo na kitendo chochote cha kihalifu.

c. Serikali ya TAnzania aidha inao ushahidi wa vitendo vya kihalifu vya Balali au hauna. Kama haina basi hakuna sababu ya kumtaka Balali arudi.

d. Kama serikali inaamini Balali ameshiriki kwa namna yoyote ile na ubadhirifu (kwenye tamko lake haisemi hivyo), basi wangekwisha kufikisha kesi mahakamani, mbona ya Rada wameifikisha mahakamani wakati Vithlani hayupo?

HIvyo, hadi hivi sasa serikali ya JK haijaonesha nia ya kutaka Balali arudi kwani hawajamtuhumu kitu chochote.
Labda mimi kuna mambo ambayo sielewi na kama waungwana mkinielewesha..basi sina nongwa!Kuvuliwa madaraka kwa Balali ni kwa sababu ipi?hiyo ni moja.

Mbili..kama uchunguzi umefanyika na kugundulika kwamba kuna watu wametumia madaraka na taaluma zao kwa nia mbaya..je uwajibikaji uko wapi?

Haya..wananchi wanatakiwa wakatoe ushaidi..kwanini Balali asitoe ushahidi?Hivi mtuhumiwa wa kwanza si ndio mwenye maelezo ya kutosha?

Mi naona wanabuy time tu!KAMA KWELI HAKUNA SPIN HAPO..KWANINI WATU WALIOANGUKA HAYO MASAINI KURUHUSU HIZO FEDHA ZITOLEWE HAWAHOJIWI?
 
What the F.........k is this!

Sisi sio watoto, naona kuna members ambao wanatakiwa wachangie Darhotwire tu!

Moderators naomba hii spin iunganishwe na topic halisi
I love politics..But above all i love my country!

There's no way i can explain that!Samahani..sidhani kama wewe ni mtoto!Ila swali lako ni muhimu sana!

Nafikiri Kikwete ndio anadhani sisi ni watoto!

Balozi wa Marekani amesema Kikwete hajaomba Balali arudishwe..Sasa kama wewe unafikiri Balali sio muhimu kwenye hili suala nyeti..then una lako jambo!Ila mimi nataka ukweli uwekwe bayana!
 
Sasa mkuu this is a big twist .Hata waandishi wa habari wana nafuu . Maelezo yote nimesoma sijaona anapo husika JK na kumleta jamaa . Ama umekosea kuleta habari hapa ?Unaweza kuwa umechanganya habari hizi ?

Lunyungu,

Siku nyingi nakufahamu kama ni mtu makini ingawa nyakati fulani kwa makusudi au kwa bahati mbaya inatoka nje ya mstari.

Posting yako hii inathibitisha upeo wako mkubwa ktk mijadala mipana hapa JF

Bravo mkuu keep it up...
 
What the F.........k is this!

Sisi sio watoto, naona kuna members ambao wanatakiwa wachangie Darhotwire tu!

Moderators naomba hii spin iunganishwe na topic halisi

FD,
Yaani we acha tu mtu anakurupuka tu wala hana haja ya kufiki mara 2 na ku sensationalize story ile watu wa bandwagon.. thanx God JF kuna vichwa visivyo buruzwa ovyo.
 
fd,
yaani we acha tu mtu anakurupuka tu wala hana haja ya kufiki mara 2 na ku sensationalize story ile watu wa bandwagon.. Thanx god jf kuna vichwa visivyo buruzwa ovyo.
nani anamburuza nani?mbona hakuna anyejibu maswali?ama kikwete na serikali yake wameshazigawa humu jf?tuelezane!

Sasa ni nani yuko responsble unapomention serikali?

Si ni rais mwenyewe?

Sasa kama marekani wanansema hawajaombwa na serikali kumrudisha balali..ni nani mwenye kichwa kinachoburuzwa ovyo?

I am positive sio mimi!wewe vipi?
 
NANI ANAMBURUZA NANI?MBONA HAKUNA ANYEJIBU MASWALI?AMA KIKWETE NA SERIKALI YAKE WAMESHAZIGAWA HUMU JF?TUELEZANE!SASA NI NANI YUKO RESPONSBLE UNAPOMENTION SERIKALI?SI NI RAIS MWENYEWE?SASA KAMA MAREKANI WANANSEMA HAWAJAOMBWA NA SERIKALI KUMRUDISHA BALALI..NI NANI MWENYE KICHWA KINACHOBURUZWA OVYO?I AM POSITIVE SIO MIMI!WEWE VIPI?

Keep dreaming kwa kuwa wewe una bei ya kununuliwa unadhani wote tupo hivyo? Kama upo positive endelea kuishi kwa matumaini Mungu atakusaidia kuugua sio kufa...
 
Hili swala la ufisadi katika benki kuu litaeleweka vizuri zaidi hapo tu Balali atakapozungumza aidha kwa vyombo ya habari au akijitetea mbele ya sheria.
 
Mushi unaweza kusema kwa uhakika kabisa "Kikwete Akataa Balali asiletwe"? Tumia maneno yako vizuri basi arawa! Otherwise unaonekana kama kituko hivi.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom