Kikwete aanguka ghafla Jangwani...! (CLOSED)

Status
Not open for further replies.
Kuanguka sio yeye tu kumbuka Dr Slaa aliaguka majuzi bafuni Mwanza na kuvunjika mkono,ile ni ajali kama ajali nyingine
usichanganye mchanga na sukari! Slaa ameteleza yaani mabafu ya ma-guset na mahoteli yetu tiles hazina viwango! JK kadondoka kwa afya mbovu! tuseme ukweli
 
..maelezo yatakuwa Raisi alikuwa amezidiwa na swaumu.

..nadhani hii ni calculated move kutafuta kura za huruma za Waislamu.

..nashauri Slaa,Lipumba,..na wagombea wote wa Uraisi wajibwage kwenye majukwaa na kusingizia swaumu.
 
Naomba mambumbumbu wa amani muache kuchochea chuki na hulka ya dharau katika nchi hii iliyojengwa kwa misingi ya heshima na upendo. Ndio maana Dr. Slaa alipodondoka na kuteguka mkono hakuna aliyesema RIP. Badala yake watu wote tulimuombea apone haraka aendelee na kazi za ujenzi wa Taifa. Muwe wastaarabu.
Tofautisha kuanguka kwa Slaa na Kikwete, huwezi kusema kuanguka kwa Kikwete ni bahati mbaya mara ngapi anashauriwa apumuzike hataki, tatizo la JK ni ugonjwa ambao unafichwa tofauti na kuanguka kwa Slaa huwezi kusema kuteleza kwa Slaa kulisababishwa na ugonjwa.

Afterall huwezi kutegemea kila siku Slaa ateleze bafuni na kuvunjika mkono lakini hii ya JK ya kuanguka unaweza ukapredict kutokana na record ya afya yake.
 
hakuanguka jumla mabodyguard wake walimuwahi kabla hajafika chini. Mbona hata Dr Slaa alianguka bafuni huko mwanza hadi kuvunjika mkono. wote wameanguka tofauti mmoja kaanguka bafuni mwingine jukwaani. hii ni bahati mbaya inaweza ikamtokea mtu yoyoye wakati wowote.

Bahati mbaya mara ya tatu? i cant buy it!! hii haijawahi kutokea ata mara moja kwa maraisi watatu waliopita!!
 
good question....

na bila shaka katika group ya waliokuwa jangwani kuna wengi tu wana saumu why yeye tu????

kuhusu ikiwa wanafunga kinafiki au wanakula kwa siri sidhani...bali nadhani kuna unafiki kwa kikwete kusingizia saumu kila anapoanguka..

saumu saumu......good scapegoat eehh!!!!!


Rais ana majukumu mengi huwezi kumfananisha na mfunga saumu yoyote mahali popote.

Ni sawa na kuuliza mbona binadamu wote tunaumwa na mbu lakini hatugui kwa pamoja.Unaweza kuumwa na mbu kumi na mwingine akaumwa na mbu wawili tu lakini wa mbu kumi asiugue malaria yule wa wawili akaugua.
 
Kuyumba si kuanguka. atakuwa kamili tu baada ya muda mfupi. wadau haifai kuandika hovyo

Welcome, leo JF itapata wageni wengi sana, Invisible vipi sever yetu iko imara.

Luiza Gama

Junior Member
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png

Join Date Sat Aug 2010
Posts 1
Thanks : 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power 0
 
Pole JK; ila hii ni dalili mbaya sana; huenda inabidi tutafakari kama kweli watanzania wote tu salama na kama kuna wagonjwa wakatibiwe kwanza wakati huo wazima wakiendelea na kazi; na hili ni jambo la kawaida
 
Rais ana majukumu mengi huwezi kumfananisha na mfunga saumu yoyote mahali popote. Ni sawa na kuuliza mbona binadamu wote tunaumwa na mbu lakini hatugui kwa pamoja.Unaweza kuumwa na mbu kumi na mwingine akaumwa na mbu wawili tu lakini wa mbu kumi asiugue malaria yule wa wawili akaugua.

Au Nyerere, Mwinyi na Mkapa walikuwa wavivu katika utendaji wa majukumu yao?kwanini ni Kikwete tu ndiye anayezidiwa na uchovu na kuanguka mbele ya kadamnasi?

Ok..Ata Umaru YarAdua walikuwa wanasema ni mzima wa afya njema mpaka ilipofika point of no return.
 
mkuu hakuna mwenye kumtakia shari.......

swali ni kwanini ukweli hausemwi????????????!!!!!!!!!!

Ukweli upi? kama unaujua sema nasi tujue kwa vile hukubaliani na sababu zilizotolewa na viongozi wa CCM pale jangwani!!!!!!!!
 
Ajabu ni nini? nani hajawahi kuanguka? hata hivyo hakufika chini! Mambo mengi yanaweza kuwa yamechangia... swaumu, nk
Mimi naona ni bahati mbaya tu.
 
Tabia ya kutojua wapi kuwe na siasa wapi kuwe na ushauri wa kitaalamu kutamponza Jk. Jk anasahau kuwa mgomeba wa uraisi ni kubeba mizigo ya chama. Waliombebesha wengi wanataka aendelee kuibeba kwa faida yake na zaidi wao. Kama afya hairuhusu kwa nini asiwe mkweli akajipanga kulingana na uwezo wake kwa sasa? Nasubiri hotuba ya daktari wa raisi itakayotolewa. Tukicheza mpaka uchaguzi ufike tutapokea hotuba kibao za daktari wa rais

saluti mkuu...imeeleweka
 
Mkapa na u-obese wake wote ule sikuwahi kusikia kaangauka hata mara moja...labda awe alikuwa anaangukia ndani na habari hazitoki
 
yamkini ndani ya jamiiforums kuna washirikina wasio na utu kama Roza kusema Rest in peace (RIP) kwa Rais kabla hajafa hiyo ni dhambi huna dini?
Wewe unajua maana ya rest in peace si lazima kuambiwa mtu aliyekufa usichukulie mazoea yakawa ndiyo kweli.
 
Infact ni mara ya nne toka aanze rasmi mbio za urais. awali ilikuwa ni ile ya 2005, then zimewahi kutokea mbili hapa katika katika.

Ni vema sasa tuambie Rais wetu anaumwa nini? Ansbert Ngurumo aliwahi kuandika:

Rais wetu si dhaifu kama wananchi wake ambao wengi wanalalala au kushinda njaa; wanapata mlo mara moja moja (na wenyewe haujakamilika virutubisho); wanafanya kazi nzito na ngumu zinazokula nguvu ya mwili na akili; wana pato duni sana (chini ya shilingi 1000 kwa siku); wanakabiliwa na magonjwa hatari na hawana huduma ya matibabu inayoeleweka na inayoaminika; wanaishi katika mazingira hatari; wanakabiliwa na magonjwa sugu kwa miaka mingi; wanatembea kwa miguu au baiskeli, bajaji au wanasafiri kwa malori na mabasi mabovu; hata kwa wanaosafiri kwa ndege, wanatumia madaraja ya chini yanayochosha; wanalala kwa saa 2 au tatu kila siku; wanasumbuliwa na umaskini wa kutisha kiasi kwamba kila wanapolala hawana tumaini kama wataiona kesho.

Watanzania hawa hawazimii, hawaishiwi nguvu wala hawaanguki, aanguke rais mwenye afya isiyotetereka (kama tulivyoelezwa) na mwenye matunzo ya viwango vya juu?.."


Sasa iweje huyu? Kijua ndio hichi ni vyema Rais akate shauri sasa. kwani kwa hali yoyote, lazima mgombea binafsi ndo aongoze kampeni kwa nguvu zaidi..... na pengine wabunge waliopita bila kupingwa. ile confidence ya kusimama na kuikimbiza kura kwa hali ha hila lazima ipungue...

Ni faida kwa wengine walio katika mbio? historia itatuambia....
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom