Kikwete aandamwa Marekani

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,006
Kikwete aandamwa Marekani

na Mwandishi Wetu
Tanzania Daima

USWAHIBA ambao Rais Jakaya Kikwete aliujenga na Watanzania wanaoshi nje ya nchi, sasa unaelekea kuanza kuyeyuka.
Hali hii imejitokeza hivi karibuni, baada ya Rais aliyeko katika ziara ya Marekani, kudaiwa kuondoka bila kuonana nao, kwa kile kinachodaiwa kwamba, kabla ya mkutano uliotarajiwa baina yao, walimpelekea maswali magumu na yasiyo ya kidiplomasia.

Habari ambazo Tanzania Daima Jumapili imezipata, zimeeleza kuwa Rais Kikwete ambaye tangu alipoingia madarakani, alijenga tabia ya kukutana na Watanzania walio nje ya nchi kila alipofanya ziara zake ughaibuni, safari hii amedaiwa kukataa kukutana na Watanzania wanaoishi nchini Marekani.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka mtandao wa Jambo, Rais Kikwete anadaiwa kukwepa kukutana na Watanzania wa huko ambao walikuwa wakitaka kupata ufanunuzi kutoka kwake kuhusu mwenendo wa mambo ulivyo hivi sasa katika serikali anayoiongoza.

Kikubwa kinachoelezwa katika taarifa hiyo ambacho Watanzania walikuwa wakitaka kumuuliza Rais Kikwete ni kuhusu utaratibu uliotumika kumsimamisha kuhudhuria shughuli za Bunge, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto.

Jambo jingine ambalo Watanzania hao walipanga kumuuliza rais ni ukweli kuhusu kusainiwa kwa mkataba wa Buzwagi nje ya nchi, na kama kweli una masilahi kwa taifa, kwa kurejea ahadi yake aliyoitoa ya kupitia upya mikataba ya madini ili kuifanya kuwa na manufaa kwa nchi.

Mbali na Watanzania hao kutaka kukutana na Rais Kikwete kwa lengo la kufanya naye mazungumzo, lakini bila mafanikio, waandishi wa habari nao walimsaka kwa mahojiano, na maswali yao yanadaiwa kulandana na yale ya Watanzania.

Taarifa zinaeleza kuwa waandishi wa habari wa Shirika la Utangazaji la Sauti ya Amerika (VOA) walimtumia Rais Kikwete maswali ya kutaka ufafanuzi kuhusu kusimamishwa kwa Zitto kuhudhuria shughuli za Bunge pamoja na kashfa ya mkataba wa Buzwagi.

Zinaeleza kuwa Mwandishi wa Habari wa Rais ambaye awali aliwataka waandishi hao kuwasilisha maswali yao kwanza kabla ya kukutana naye, aliwajibu waandishi hao kuwa rais hawezi kuzungumzia masuala hayo.

Taarifa hiyo inaeleza zaidi kwamba Mwandishi wa Rais aliwajibu waandishi hao waliokuwa wakimvizia Rais Kikwete kwa ajili ya kuzungumza nao kuwa maswali yao hayana (diplomatic tone), yaani hayako katika mpangilio wa kidiplomasia, hivyo rais hawezi kuyazungumzia.

Kinachodaiwa kumtatiza Rais Kikwete katika maswali hayo ambayo mwandishi wake aliomba ayapate kwanza na kumpelekea kabla ya kukutana na waandishi kuyajibu, ni kuwamo yale yaliyokuwa yakihoji uhalali wa kusimamishwa Zitto na utata wa mkataba wa Buzwagi.

“Si sahihi kumtaja Zitto mbele ya rais, kwa hiyo hakuna mahojiano na wewe ndugu mwandishi,” inasomeka sehemu ya taarifa hiyo.

Hii ni mara ya pili kwa Rais Kikwete kudaiwa kuwakimbia Watanzania wanaoishi nje ya nchi, wanaoonekana kutaka kumuuliza maswali ambayo majibu yake ni magumu.

Mara ya kwanza ilikuwa London, Uingereza mapema mwaka huu, ambapo inadaiwa Rais Kikwete aliwaacha solemba Watanzania wanaoishi nchini humo kwa kushindwa kujibu maswali katika mkutano nao, na kudaiwa kwamba ilielezwa anakwenda kwenye mkutano muhimu na Waziri wa Masuala ya Afrika.

Kinyume chake, katika muda ulioelezwa kuwa atakuwa katika mkutano na waziri huyo wa Uingereza, alionekana akishuhudia mechi ya Ligi Kuu ya England iliyoihusisha Tottenham Hotspur ‘Spurs’ na Newcastle United.

Lakini katika majibu juu ya tuhuma hizo, mapema mwaka huu ilielezwa kwamba, Kikwete hakukataa kujibu maswali, bali muda haukumruhusu kujibu kutokana na msafara wake kuchelewa kuingia mkutanoni.

Suala la Buzwagi lililoibuliwa na Zitto baada ya kuhoji sababu za serikali kusaini mkataba nje ya nchi, tena hotelini huko London ilhali rais alizuia kusainiwa kwa mikataba ya madini hadi hapo itakapotazamwa na kupitiwa upya, limekuwa gumzo kwa sasa.

Kama lilivyo suala la Zitto, kutajwa kwa vigogo wanaotuhumiwa kwa ufisadi hivi karibuni, pia ni jambo zito katika siasa za Tanzania kwa sasa.
 
Nafikiri katika Ziara zote za Nje,Ziara hii ya Mkuu wa Kaya huku USA ilikuwa ngumu na asiyoweza kuisahau!,.Masuala ya kutowajibika vyema kwa serikali yake na Watendaji wake,limekuwa jambo lililozungumzwa kila mahali.Hata Jay-Z (Music Mogul) amelalamika kwa muungwana kuwa ameshindwa kujenga visima vingi Tanzania kwa sababu hawakujiandaa kwa shughuli hiyo,wakati walipewa Taarifa miezi 6 kabla.

Kuna Taarifa kuwa Mkuu atarudi tena USA Mwishoni mwa mwaka huu, baada ya Mkutano wa Commonwealth - Kampala na ziara fupi ya Mashariki ya mbali.Kwa maneno ya Wasaidizi wake kipindi hicho atapata muda wa kuzungumza na Watanzania na baadhi ya vyombo vya Habari.

Rais amepata maswali magumu kutoka kwa watu wa World Bank kuhusu Matumizi mabaya na Ufujaji wa Pesa huko BOT,Alikutana na watu hawa huko Washington Dc mwanzoni kabisa mwa ziara yake,Pia kwa wakati tofauti ameelezwa kuhusu Wafujaji/Mafisadi 11(yeye akiwa mmojawapo) waliotajwa kwenye Orodha ya Dr Slaa,ameulizwa kuhusu uhalali wa kutia saini mikataba ktk Hotel wakati sehemu husika ina Ubalozi wetu!.Pia amepokea maswali 18 kutoka kwa wanaosemwa Watanzania waishio Marekani!,kikubwa kuliko chote ni maswali hayo! ambayo mmoja wa watu wa karibu wa Rais amesema Mkuu hawezi kuyajibu akiwa Nje ya Nchi.

Pamoja na mambo mengine Waziri Wa Mambo ya Nje Mh. Benard Membe ndiye alikuwa msemaji Mkuu wa maswala mengi,kwani anaonekana anajua maswala mengi kwa undani kuliko wengi walioandamana na JK.Amezungumza na kuutetea uhusiano wa Tanzania na Iran,Uhusiano mkubwa wa Tanzania na Palestine,na Nchi za kiafrika zinavyoitazama China ktk Maendeleo yao.Pia amezungumza suala la Uraia wa Nchi mbili (Dual Citizenship).

Mheshimiwa anarudi nyumbani,kwa Uhakika tutegemee mambo makubwa kutokea huko,ama Mabadiliko kwenye Cabinet yake ama watu kuombwa waachie ngazi kwa Hiari yao.Pressure imekuwa kubwa,na kwa kiwango kikubwa imeonekana mambo mengi ndani ya Serikali yanafanywa bila ya ufahamu wa Muungwana,ama kwa kuwaamini sana watendaji wake au kutokuwa na wepesi wa kufuatilia mambo ktk Serikali yake!,Muungwana ana credibility kubwa kwa masuala ya nje,kuliko ndani ambako mambo yanaonekana yanamshinda.

Kama wanavyosema waungwana humu stay tuned,nafikiri kuna Bomu Muungwana anakwenda kulilipua nyumbani!,inaweza kuwa mapema au baada ya Mfungo wa Ramadhan,lakini mabadiliko ni lazima!!!
 
Kuna Taarifa kuwa Mkuu atarudi tena USA Mwishoni mwa mwaka huu, baada ya Mkutano wa Commonwealth - Kampala na ziara fupi ya Mashariki ya mbali.Kwa maneno ya Wasaidizi wake kipindi hicho atapata muda wa kuzungumza na Watanzania na baadhi ya vyombo vya Habari.


Kama sikosei aliahidi katika zira zake kwamba safari za nje zitakwisha baada ya mwezi wa sita ambao umepita na alisema atakuwa nyumbani kushughulikia mambo ya pale. Sasa huu mfumuko wa safari hizi umetoka wapi? Au ameona raha ya hizi safari? Tanzania kwa umasikini wetu hatuwezi ku-afford safari namna hii kama anataka kufanya hivi basi aunganishe achukue na wizara ya mambo ya nje iwe ni jukumu lake na tubanie zile tunazompa Membe.
 
Nafikiri katika Ziara zote za Nje,Ziara hii ya Mkuu wa Kaya huku USA ilikuwa ngumu na asiyoweza kuisahau!,.Masuala ya kutowajibika vyema kwa serikali yake na Watendaji wake,limekuwa jambo lililozungumzwa kila mahali.Hata Jay-Z (Music Mogul) amelalamika kwa muungwana kuwa ameshindwa kujenga visima vingi Tanzania kwa sababu hawakujiandaa kwa shughuli hiyo,wakati walipewa Taarifa miezi 6 kabla.

Kuna Taarifa kuwa Mkuu atarudi tena USA Mwishoni mwa mwaka huu, baada ya Mkutano wa Commonwealth - Kampala na ziara fupi ya Mashariki ya mbali.Kwa maneno ya Wasaidizi wake kipindi hicho atapata muda wa kuzungumza na Watanzania na baadhi ya vyombo vya Habari.

Rais amepata maswali magumu kutoka kwa watu wa World Bank kuhusu Matumizi mabaya na Ufujaji wa Pesa huko BOT,Alikutana na watu hawa huko Washington Dc mwanzoni kabisa mwa ziara yake,Pia kwa wakati tofauti ameelezwa kuhusu Wafujaji/Mafisadi 11(yeye akiwa mmojawapo) waliotajwa kwenye Orodha ya Dr Slaa,ameulizwa kuhusu uhalali wa kutia saini mikataba ktk Hotel wakati sehemu husika ina Ubalozi wetu!.Pia amepokea maswali 18 kutoka kwa wanaosemwa Watanzania waishio Marekani!,kikubwa kuliko chote ni maswali hayo! ambayo mmoja wa watu wa karibu wa Rais amesema Mkuu hawezi kuyajibu akiwa Nje ya Nchi.

Pamoja na mambo mengine Waziri Wa Mambo ya Nje Mh. Benard Membe ndiye alikuwa msemaji Mkuu wa maswala mengi,kwani anaonekana anajua maswala mengi kwa undani kuliko wengi walioandamana na JK.Amezungumza na kuutetea uhusiano wa Tanzania na Iran,Uhusiano mkubwa wa Tanzania na Palestine,na Nchi za kiafrika zinavyoitazama China ktk Maendeleo yao.Pia amezungumza suala la Uraia wa Nchi mbili (Dual Citizenship).

Mheshimiwa anarudi nyumbani,kwa Uhakika tutegemee mambo makubwa kutokea huko,ama Mabadiliko kwenye Cabinet yake ama watu kuombwa waachie ngazi kwa Hiari yao.Pressure imekuwa kubwa,na kwa kiwango kikubwa imeonekana mambo mengi ndani ya Serikali yanafanywa bila ya ufahamu wa Muungwana,ama kwa kuwaamini sana watendaji wake au kutokuwa na wepesi wa kufuatilia mambo ktk Serikali yake!,Muungwana ana credibility kubwa kwa masuala ya nje,kuliko ndani ambako mambo yanaonekana yanamshinda.

Kama wanavyosema waungwana humu stay tuned,nafikiri kuna Bomu Muungwana anakwenda kulilipua nyumbani!,inaweza kuwa mapema au baada ya Mfungo wa Ramadhan,lakini mabadiliko ni lazima!!!

Nakubaliana na mawazo yako, lakini kumbuka mambo mengi ameyaridhi, na si haki kila jambo as if limefanyika ndani ya miaka hii miwili,,, kwa hiyo ngaungana na wewe kwamba yapo mengi yanahitaji majibu lakini... mengi yalikuwepo na yatakuwepo ndio maana hata Jaji Warioba anasema sio mapya, na kwa taarifa yako kuna jibu rahisi ya kila hayo maswali na lo,,,"Tutachunguza"!
 
Kama wanavyosema waungwana humu stay tuned,nafikiri kuna Bomu Muungwana anakwenda kulilipua nyumbani!,inaweza kuwa mapema au baada ya Mfungo wa Ramadhan,lakini mabadiliko ni lazima!!!

Kwa kweli nilimuona kwenye futari, kwa mtu yoyote aliyemuona kwenye hii ziara, ukweli ni kwamba yuko very tense, na nimeona wale waliokaribu naye wako katika wasi wasi mkubwa, I mean I could not help a jinsi hewa ilivyokuwa ngumu sana kuipumua arround him, anyway ninakubaliana na mkuu Mwawado,

kuwa something is up!
 
Kama hakujibu maswali ya Watanzania walio nje, kwa kiwango kikubwa zinajengeka hisia kuwa hakujiandaa kwa majibu ya issue nzito na topical zinazotokea nchini kwake...nini kikubwa kuliko haya mambo ambayo sasa yameleta mzozo na yanatishia kuivuruga serikali yake?
 
Marekani si Europe Watanzania wa hapa ni tough sana hakuna ujinga wala uongo. Kitu kingine watu wa hapa hawategemei serikali na hawana mpango wa kufanya kazi serikalini lakini wana uchungu sana na nchi.
 
Marekani si Europe Watanzania wa hapa ni tough sana hakuna ujinga wala uongo. Kitu kingine watu wa hapa hawategemei serikali na hawana mpango wa kufanya kazi serikalini lakini wana uchungu sana na nchi.

Wow .......................................hizi ni accusation au sijui niite nini? Anyway pengine wengine wajuzi zaidi.
 
Dua,
jamaa ana point na pengine zaidi ya hivyo............it's for you to find out!!!.
 
akirudi atacheka cheka alafu yataisha...kila wakati akiwa nje ameonesha determinations but akirudi ni business as usual...akiwa huko ameshawaagiza mawaziri wapite mikoani kutuliza mizuka ya wadanganyika ..what else do you guys expect after that..
 
..achana na Dua anasubiri post ya afisa tawala wilayani Bukoba vijijini
 
akirudi atacheka cheka alafu yataisha...kila wakati akiwa nje ameonesha determinations but akirudi ni business as usual...akiwa huko ameshawaagiza mawaziri wapite mikoani kutuliza mizuka ya wadanganyika ..what else do you guys expect after that..

Kutuliza mizuka this time kazi ipo!
Si umesikia visa vya kuzomewa viongozi kila kona alivosema Lissu?
Tusubilie vigele gele zaidi vya ziara hizi!

Ninacho sikitika ni kwamba wanazidi tafuna hela zetu unnecessarily
 
kweli kabisa Phillemon itakuwa siyo busara kuwaagiza hao mafisadi watembelee mikoani halafu akija awafute kazi, kitu ambacho hakiningii akilini.
 
jamani asingekubali hata kuja kwenye radio mbazo za kwetu maana hazisikiki sana... kwa hiyo inakuwa ni chini kwa chini tu
 
dua,alisema hatasafiri coz pesa ilikata hazina,
nw imerudi ndio maana wamepata na nguvu ya kuwaelezea wananchi masuala ya maisha bora!
nina breaking news hapa..naomba mwanakijiji unisaidie kuanzisha thread..natumia simu hapa,
mkurugenzi wa jiji la mwanza amesimamishwa kazi yeye pamoja na mtendaji mmoja wa jiji baada ya kutokea mkwaruzano baina yake na madaha baada ya mkurugenzi kumpa mkuu wa wilaya ripoti ya uongo..
more data ntazitoa asubuhi
 
JK Kaandamwa ? kivipi ? yaani yeye kutoonana na wabongo ndio kuandamwa ? but what do we expect kama source ya hii thread ni freemedia ? pengine hii habari imeandikwa na Mwana??jiji !
 
"Ikulu kuna biashara gani?" By JK Nyerere. Huyu jamaa alikuwa illusionist, alikuwa anaplan mambo akidhani kuendesha nchi katika karne ya 21 ni sawa na karne ya 18. Strategic plan alizoset zimeonyesha tangu mwanzo kufail, lakini aliendelea kutumia zimamoto system, kwamba pakiwaka hapa unazima then unagoja pengine, however things are getting more worse na moto is all over the place.

Kikwete still can flip things up, but this is if and only if he will use his power ya kuajili na kufukuza. First he need to clean all corrupted mambers of his cabinent. Unless other wise na hizi scandal kila siku investors will stay away due to high political distabilazation risk. Na hii inalikosesha taifa revenue.... the guy is in Big Trouble.
 
Kama hakujibu maswali ya Watanzania walio nje, kwa kiwango kikubwa zinajengeka hisia kuwa hakujiandaa kwa majibu ya issue nzito na topical zinazotokea nchini kwake...nini kikubwa kuliko haya mambo ambayo sasa yameleta mzozo na yanatishia kuivuruga serikali yake?

Alijua atavurunda maana maswali yangekuwa magumu na majibu ya kisanii yasingekubalika na hapo kuzidi kumshushia hadhi yake ambayo tayari imeshatetereka.
 
....next time mnapoamua kutoa 80% kama mliyompa JK hakikisheni mnaweka contract inayoeleweka,glad sikumpa kura yangu maana nilijua ni mswahili tuu na hawezi kubadilika
 
Back
Top Bottom