Elections 2010 Kikwete aahidi kupandisha hadhi hospitali

ICHONDI

JF-Expert Member
Dec 3, 2008
600
134
na Tamali Vullu, Mbulu

MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete, amesema serikali yake ijayo itazipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini ziwe za rufaa, ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
Kikwete alitoa ahadi hiyo jana wilayani Mbulu, alipokuwa akizungumza na wananchi katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika Tarafa ya Haydom ambapo alisema lengo la kufanya hivyo ni kuboresha huduma za afya hapa nchini.

Alizitaja hospitali zitakazopandishwa hadhi ni ile ya Haydom, Arusha Lutheran, St Gasper iliyopo Itigi, St Francis iliyopo Ifakara, mkoani Morogoro, Ndada iliyopo mkoani Mtwara, Hospitali ya Peramiho (Ruvuma) na Hospitali ya Irembula iliyopo mkoani Iringa.

Alisema kuwa baada ya hospitali hizo kupandishwa hadhi hivi karibuni, zitakuwa na uwezo wa kuhudumia wanachi wengi na kutoa mfano kuwa Hospitali ya Haydom ikipadishwa hadhi itaweza kuhudumia wakazi wa Singida na Shinyanga.

"Tutataka kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, ili iweze kushughulikia magonjwa makubwa yaliyoshindikana badala ya wanachi kwenda kutibiwa nje ya nchi. Hospitali hizi maalumu tutakazozipandisha hadhi na kuwa za rufaa, zitahudumia wagonjwa ya kawaida," alisema.

Aliongeza kuwa mbali na kuzipandisha hadhi hospitali hizo pia wataboresha mazingira ya kazi katika hospitali hizo, ili madaktari waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi.

Kikwete pia alipata fursa ya kuzungumza na wakazi wa Kata ya Muslur, ambapo walimueleza kuwa tatizo la kutokuwapo kwa hosteli zimechangia kwa kiasi kikubwa watoto wa kike kupata mimba na kumuomba awasaidie wajenge hosteli.

"Mheshimiwa hapa tuna tatizo la watoto wetu kupata mimba, kwani wanaishi kwenye magheto, tunaomba utusaidie tupate hosteli, ili tuwaokoe watoto wetu," alisema mkazi mmoja wa eneo hilo.

Kikwete alisema yupo tayari kuwasaidia katika ujenzi wa hosteli lakini ni lazima wakusanye nguvu na kuanza ujenzi wa hosteli hizo.

Hivi si alipokuwa Moshi alisema ataipandisha Mawenzi Hospital kuwa ya rufaa? so keshawapiga wananchi wa Moshi changa la macho? Halafu hili la mimba na hostel si alishasema watoto wa kike wanapata mimba kwa kuwa wana kiherehere, mbona alivyojibu swali hakusema hivyo this time? Kweli JK ni kiboko, sijui kwa nini atautafuta uraisi kwa kishindo namna hiyo jamani, i am so worried na Tanzania baada ya October 31st lol
 
na Tamali Vullu, Mbulu

MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete, amesema serikali yake ijayo itazipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini ziwe za rufaa, ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
Kikwete alitoa ahadi hiyo jana wilayani Mbulu, alipokuwa akizungumza na wananchi katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika Tarafa ya Haydom ambapo alisema lengo la kufanya hivyo ni kuboresha huduma za afya hapa nchini.

Alizitaja hospitali zitakazopandishwa hadhi ni ile ya Haydom, Arusha Lutheran, St Gasper iliyopo Itigi, St Francis iliyopo Ifakara, mkoani Morogoro, Ndada iliyopo mkoani Mtwara, Hospitali ya Peramiho (Ruvuma) na Hospitali ya Irembula iliyopo mkoani Iringa.

Alisema kuwa baada ya hospitali hizo kupandishwa hadhi hivi karibuni, zitakuwa na uwezo wa kuhudumia wanachi wengi na kutoa mfano kuwa Hospitali ya Haydom ikipadishwa hadhi itaweza kuhudumia wakazi wa Singida na Shinyanga.

“Tutataka kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, ili iweze kushughulikia magonjwa makubwa yaliyoshindikana badala ya wanachi kwenda kutibiwa nje ya nchi. Hospitali hizi maalumu tutakazozipandisha hadhi na kuwa za rufaa, zitahudumia wagonjwa ya kawaida,” alisema.

Aliongeza kuwa mbali na kuzipandisha hadhi hospitali hizo pia wataboresha mazingira ya kazi katika hospitali hizo, ili madaktari waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi.

Kikwete pia alipata fursa ya kuzungumza na wakazi wa Kata ya Muslur, ambapo walimueleza kuwa tatizo la kutokuwapo kwa hosteli zimechangia kwa kiasi kikubwa watoto wa kike kupata mimba na kumuomba awasaidie wajenge hosteli.

“Mheshimiwa hapa tuna tatizo la watoto wetu kupata mimba, kwani wanaishi kwenye magheto, tunaomba utusaidie tupate hosteli, ili tuwaokoe watoto wetu,” alisema mkazi mmoja wa eneo hilo.

Kikwete alisema yupo tayari kuwasaidia katika ujenzi wa hosteli lakini ni lazima wakusanye nguvu na kuanza ujenzi wa hosteli hizo.

Hivi si alipokuwa Moshi alisema ataipandisha Mawenzi Hospital kuwa ya rufaa? so keshawapiga wananchi wa Moshi changa la macho? Halafu hili la mimba na hostel si alishasema watoto wa kike wanapata mimba kwa kuwa wana kiherehere, mbona alivyojibu swali hakusema hivyo this time? Kweli JK ni kiboko, sijui kwa nini atautafuta uraisi kwa kishindo namna hiyo jamani, i am so worried na Tanzania baada ya October 31st lol

RED:
Mbona hospitali zote ni za makanisa? kwa nini srekali hii haijengi hospitali zake? ina kimbilia kudandia za mashirika ya kidini na taasisi zisizo za kiserekali?

BLUE:
Huyu jamaa anamtatizo HYDOM inaudumia watu wa Manyara, Dodoma,Shinyanga,Singida, Tanga, Tabora ata Kigoma kwani ni hospitali yenye huduma nzuri na inasifika kwa kuwa na madaktari bingwa wengi.

Kifupi srekali ijenge za kwake hiache huu mchezo wa kusema ina bandisha hadhi hili ndio walilolitrumia kuchakachu Elimu kwani vyuo vyote vya kati walivipandisha kuwa vyuo vikuu badala ya kujenga vyou vikuuu vipya!
 
Hospitali ya rufaa maana yake lazima iwe na madaktari bingwa.
Je, hospitali iko tayari kupandisha mishahara na marupurupu mengine kwa madaktari bingwa ili kuwashawishi kutoka katika mikoa/ maeneo yenye maslahi zaidi (Dar, Mwanza, Mbeya, Kilimanjaro (kwa kiasi flani))? Au wasaidizi wa madaktari yaani AMO watapandishwa hadhi kama ambavyo vyuo vya kati vimepandishwa hadhi na kuwa vyuo vikuu katika mkakati wake huu?

Huo ni uongo, serikali haijaweza mpaka sasa kuboresha hizo hospitali 2 za rufaa (Muhimbili na Mbeya) inazomiliki ndio iweze kuboresha hizi nyingine? Mpango wa kuboresha huduma katika hospitali zote alizotaja ni mpango wa mashirika yeneyewe yanayomiliki hospitali hizo, na si wa serikali kimsingi
 
Ukweli ni kwamba anyone can make tons of promises sijui za kujenga matreni sijui flyovers, vivuko etc ..hata ur truly naeza kuweka ahadi right this minute ya kumpa juisi ya apple kila mtu aliyepo online jf hivi sasa..swali la kujiuliza ambalo ni la msingi ni kwamba mechanism gani itatumika kufulfill hizo promises..

Ukweli ni kwamba kuchagua Kikwete ni kuchagua mwendelezo uleule aliouanza...maana wanasema si rahisi kupanda bange ukavuna mchicha..sera za CCM ni kukabidhi kila fursa ya kiuchumi mikononi mwa wageni, na miradi mikubwa mingi bado inafadhiliwa na mashirika ya kigeni na/au ya kimataifa kama misaada au mikopo. Hakuna mikakati yoyote ya maana ambapo serikali imeweka ambayo itakuja kuzalisha au ku-stimulate uchumi na kuwezesha hata the tiniest of the promises to be fullfilled..
 
Nilisoma kwenye gazeti la rai kwamba huyu jamaa huwa msahaulifu.
Nakumbuka alipokuwa Rukwa hivi karibuni alisema serikali yake inakusudia kuweka hospitali ya rufaa kila mkoa. Mbali na bajaji 400 atakazotoa kwa kila hospital kubebea wajawazito.
Leo tena zimebadilika na kuwa saba tu?
Mungu ibariki Tanzania.
 
kwani serikali haina hospitali zake, ikazipa uwezo wa kuwa ni hospitali za rufaa? au ndio uongo wenyewe huo? maana huwezi kuzifanya za rufaa etc bila makubaliano na wamiliki, rejea mikataba kati ya kanisa katoliki na serekali kipindi cha mwinyi, ambayo imewahi kuongelewa humu kwenye jf, na wengine waliipinga?
sasa JK ameisha sawazisha haya mambo? au ndio ghiliba halafu uchaguzi ukiisha ataanza kesema walutheri wamekataa/wakatoliki hivyo sera/mpangilio wa serikali unabadilika .... miaka mitano inaondoka hakuna cha hospitali wala barabara. kwanza hiyo barabara ya haydom, kwenda sindida au shinyanga ina pitika kipindi chote? labda kwa kanali wetu akiwa anaenda chukua pembe za ndovu na ma four wheel drive yake.
hivi uchumi wa mikoa yetu tuna shindwa kuwa na hospitali nzuri za serikali? mfano ikiwa mo wa singida ni tajiri na huo utajiri kaupatia "singida" je kwa kutumia hiyo kodi inayo patikana hapo na utajiri mwingine singida hawawezi kuwa hiyo hospitali? shinyanga na pamba , almasi na mang'ombe ukiachilia mbali mchelle, wana shindwa kuwa hospitali nzuri???????
 
hiyo si ahadi mpya na utekelezaji ulishaanza kwa msaada wa watu wa marekani
 
DSCN0601.JPG


Mawenzi Hospital - MOSHI

Ni mojawapo ya hospital chafu sana nchini Tanzania, majengo yake ni machakavu mno, wakati wa mvua hapaingiliki sababu ya matope.

JK ameahidi 1.6 bilioni kuifanya hospital ya rufaa ya mkoa wa Kilimanjaro, pia amesikia kuna mhisani ameanza kujenga jengo la ghorofa 4, anataka apelekewe taarifa ni nani huyo.
 
Huyu naye asituchanganye kwani alikuwa wapi miaka mitano aliyokuwa madarakani alikuwa hazioni hizi hospitali ni leo ndio anaona kwamba watanzania wanahitaji huduma bora za afya.. Acha kutufanya sisi watoto wadogo ccm mmeimba wimbo huu miaka nenda miaka rudi leo utafanya muujiza gani kama si kutaka kutufanya sisi wendawazimu
 
Back
Top Bottom