Kikosi Kazi: Tanzania ianze mchakato wa kupata Katiba Mpya baada ya Uchaguzi Mkuu 2025

Kikosi kazi cha kuratibu maoni ya wadau wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa kilichoundwa na Rais Samia Suluhu leo kinawasilisha taarifa ya yake na mapendezo kwa Rais Ikulu, Dar es Salaam.

Kikosi kazi chini ya mwenyekiti wake, Rewakaza Mkandala kimependekeza Tanzania ianze mchakato wa kupata katiba mpya baada ya uchaguzi mkuu 2025.
======

Rwekaza Mkandala: Mwisho mheshimiwa Rais ni suala la muda mrefu, mwaka 2011 Tanzania ilianza mchakato wa kutunga katiba mpya kwa kutunga sheria ya mabadiliko ya katiba namba 83 ya mwaka 2011.

Oktoba 2, 2014 Bunge maalum la katiba lilipiga kura kupitisha katiba inayopendekezwa ambayo ilipaswa kupigiwa kura ya maoni na wananchi ili kuithibitisha lakini mpaka sasa suala hilo halijafanyika.

Changamoto mheshimiwa Rais ni mbili
  1. Kuna wale ambao wanasema hakuna haja kuwa na katiba mpya kwani katiba ya sasa inaweza kufanyiwa marekebisho kukidhi mahitaji ya sasa na baadae.
  2. Mchakato wa kupata katiba pendekezwa haukuwa shirikishi vya kutosha kwasababu baadhi ya wajumbe wa bunge la katiba walisusia hivyo katiba hiyo kupitishwa na wajumbe waliobaki.
Pia kuna madai mchakato wa kupata katiba mpya haujakamilika, umesimama muda mrefu tangu mwaka 2014 hivyo unapaswa kukwamuliwa.

Pia kuna maoni katiba pendekezwa imeacha mambo ya msingi yaliyomo katika rasimu ya katiba pendekezwa.

Pia kuna suala la katiba mpya kwamba ni muhimu lakini halina haraka kwakuwa katiba ya sasa inafanya kazi vizuri.

Kuna wale wanaosema kuna mahitaji mengi ya wananchi ya maendeleo kuliko uhitaji wa katiba mpya hivyo ni vyema kutumia muda huu kujikita katika kuleta maendeleo ya wananchi.

Mwisho kuna wale wanaodai katiba mpya sio suluhisho ya kila changamoto zinazotukabili, zipo nchi zinazosemekana kuwa na katiba nzuri lakini bado kuna malalamiko kuhusu masuala kadhaa ikiwemo masuala ya uchaguzi.

Hapa suala la kufanyiwa kazi mheshimiwa Rais ni kupendekeza utaratibu wa mchakato wa kutiba mpya na muda wa kufanyiwa kazi.

Kikosi kazi kinapendekeza kwamba Tanzania ianze mchakato wa kupata katiba mpya mara baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. Mapendekezo ya namna mbalimbali ya kushughulika na suala la katiba mpya baada ya uchaguzi mkuu wa 2025

Pendekezo linatokana na sababu kuu nne
  1. Kuna haja ya kuanisha dira kuu ya maendeleo kwa miaka ijayo itakayotoa muelekeo kwa katiba mpya.
  2. Kukosekana kwa muda wa kutosha kuanza kutumia katiba mpya ndani ya kalenda ya uchaguzi wa 2025
  3. Kuna haja ya kutoa fursa kwa marekebisho ya sheria ya uchaguzi na sheria ya vyama vya siasa.
  4. Kuna haja ya kutoa fursa ya kutosha kufanyia kazi masuala ya muda wa kati ikiwa ni pamoja na kuanisha dira mpya ya maendeleo.
Hizi si ndiyo hoja za wana CCM na washabiki wao kwa miaka hii yote tokea 2014? Hata wangebadilisha kidogo lakini hivi zilivyo wamenakili na kuiita ripoti ya kikosi Kazi!

Ugumu Wa kupatikana Katiba mpya unakuwa upi? Nielewavyo Mimi kianzio ni rasimu ya Warioba,kuundwe timu ya wataalam huru,wapeleke mapendekezo kwa wananchi wapi pa kuboresha halafu liundwe Bunge Huru la Katiba ili tuandike Katiba mpya.Sifahamu kwa nini hawa wajumbe wameweza kuja na hayo mapendekezo kwa muda mfupi lakini tunashindwa hata kusogeza uchaguzi mbele kidogo kama kuna kukawia?

Hii maana yake kikosi Kazi kimetudharau sisi wananchi kuwa hatuwezi kukamilisha mchakato kabla ya 2025?
Je,hicho kikosi kilipewa hadidu za rejea zilizowaongoza hivyo?
 
Sasa hili swala linahaja ya kamati kweli,kamati zanyewe kama za kina manyele
 
Ubunge au nafasi yoyot ya juu ikinyimwa mshahara na marupurupu makubwa ya kutisha, watoaji rushwa watakosa pa kukimbilia /maslahi makubwa ndiyo yanayovuta rushwa za kifedha na hata kingono nadhani hapa cdm wananielewa vizuri sana.

-tukumbuke si wanasiasa wote wanadhamira ya kutumikia watanzania almost 80% ni kwa ajili ya maslahi yao na familia zao.
Wanasiasa wasio na uchungu kwa maslahi ya wananchi ni wale Wa chama chakavu,na hiyo asilimia siyo sahihi maana ni zaidi ya 99% yao wapo kimaslahi.Kukataa Katiba pia ni maslahi binafsi na inadhihirisha jinsi walivyokuwa wabinafsi.
 
Kamati hii ipo kuhakikisha Katiba mpya inacheleweshwa hadi baada ya uchaguzi mkuu 2025.

Lengo kuu likiwa kuhakikisha rais mwanamke mzanzibari anaendelea madarakani baada ya 2025.

Bila ya kujizatiti kweli kweli hapa tutagonga mwamba tu.

Umoja wetu ndiyo hivyo tena, mwingine yeyote kwa mtu ni mtuhumiwa wa usaliti isipokuwa yeye.

Kazi kweli kweli.

Cc: Babati
Hatari sn
 
I 'm not late on board.

Kwa hii kamati ya makada wa CCM niwape watanzania pole tena ni danganya toto part II inakwenda kutokea.

Kama nia ipo basi wangeanzia pale walipoishia.

I
 
Huu ni USHAMBA. Mi nasema hivi, mchakato uanze sasa, halafu kura ya wananchi ya kuipitisha ipigwe sambamba na upigaji kura wa uchaguzi mkuu wa 2025 ili raisi wa awamu ijayo aanze kuitumia kuanzia 2026. Ina maana Rais Samia mwenyewe awe wa Kwanza kui- practice! Inamaana uchaguzi mkuu wa 2025 uendeshwe chini ya katiba ya sasa pamoja na marekebisho hasa ya sheria ya uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu. Hakuna haja ya kuwafanya na hofu maana haiathiri utawala wa mitano tena ya Mama Samia, labda vyombo vya ulinzi na usalama viamue vinginevyo maana tume ya uchaguzi ni kugonga mihuri tu!
 
Waache kuchezea akili za Watanzania. Miaka 4 kabla ya uchaguzi eti haitoshi. Kama miaka haikutosha tangu kwenye Tume ya Waryoba (2014) mpaka leo, basi tusubiri wajukuu wetu waje watengeneze katiba ya nzuri ya nchi.
Kukosekana kwa muda wa kutosha kuanza kutumia katiba mpya ndani ya kalenda ya uchaguzi wa 2025
 
Wezi wa kura wanataka waendelee kuongoza nchi kwa kura za wizi. Yule mama akisikia neno Katiba anaweweseka!!
 
''mara baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025''

....Ni lini hasa ? Maana hata 2029 ni baada ya Uchaguzi mwaka 2025.
 
Back
Top Bottom