Kikosi cha intelijinsia chaingia rasmi Njombe kuongeza nguvu ya upelelezi wa mauaji

kilagalila

JF-Expert Member
Nov 8, 2018
320
154
1548953589611.jpeg


Kamishna wa operesheni na mafunzo ya jeshi la polisi nchini NSATO MARIJANI akiwa na wataalamu wengine wa intelijensia wamefika mkoani Njombe ili kuungana na jeshi la polisi mkoani humo katika kupambana na mauaji dhidi ya watoto wadogo.

kikosi hicho maalumu kimewasili mkoani Njombe Ikiwa ni siku moja imepita tangu naibu waziri wa mambo ya ndani ya nchi amuagize IGP SIMON SIRRO kutuma kikosi maalumu cha kiintelijensia kuongeza nguvu katika uchunguzi wa watekaji na wauaji wilayani Njombe.

Akizungumza katika mkutano wa dharura na wananchi katika kituo kikuu cha mabasi mkoani Njombe mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher Olesendeka wakati akitamburisha kikosi hicho kilichosheheni wataalamu mbalimbali kutoka vyombo mbalimbali vya ulinzi na usalama nchini amewataka wananchi kutoa ushirikiano ili kuwabaini wahusika wa maovu hayo huku akidai hakuna mtu atakae achwa salama kama amehusika na mauaji.

"Naamini kwa sasa zoezi la kuwapata wahusika wote itakamilika mapema na kazi hii itafanywa kwa namna ambayo mtaiona hasira ya serikali yenu kwa wendawazimu hawa,serikali ya dk.JOHN POMBE MAGUFULI haitakubali damu ya mtanzania aendelee kuumia hapa kwa kisingizio chochote mufilisi"Olesendeka aliwaambia wananchi

Katika mkutano huo pia Olesendeka amemuagiza kamanda wa polisi mkoa wa Njombe RPC Renatha Mzinga kumkamata mara moja aliyekuwa mratibu wa tiba mbadala na asilia mkoa wa Njombe ,baada ya kulalamikiwa na waganga wataalamu wa tiba asili na mbadala kuwa amekuwa chanzo cha kusababisha migogoro katika chama chao pamoja kufanya usajiri holela wa waganga hao.

Nae kamanda wa kikosi hicho maalumu Nsato Marijani ambaye ni Kamishna wa operesheni na mafunzo wa jeshi la polisi nchini alisema kuwa kikosi hicho kimekuja kwa kazi ya kuwasaka wahusika wa mauaji na kwamba kitawasaka popote walipo kwa hiari au shari.

"Naamini kabisa sisi sote tuliopo hapa tutashirikiana katika kufanya kazi na tukifanya kazi kwa ushirikianao haiwezekani mtu akajificha labda atajificha kwenu kwasababu mmoja wenu hataki kutoa taarifa,sasa mimi nitapata taarifa kwa hiari au kwa shari lakini nikipita huko kwa shari wapo wengine watu wema watakaoumia sasa ili wale wema wasiumie ni heli tukatoa taarifa mapema ili mimi nikashughulika na wale wabaya"alisema kamishna MARIJANI

Kwa upande wananchi wanapongeza serikali kwa kuchukua hatua za haraka za kukabiliana na vitendo hivyo vya ukatili dhidi ya watoto.

MC.AMIRI/MR.MTAANI
 
Wawakamate Mwakipande jr na huyo Mwandulami wa hapo Mtwango wawasaidie maana hao ndio waganga wakuu wa akina laki si pesa!
 
Kuna haja sasa serikali ikatengeneza sheria dhidi ya washikina na wachawi.watu hawa sio kabisa, wanasababisha matatizo makubwa kwenye jaimii, maradhi yasiyopona, na umasikini uliokithiri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kikosi kilichoshindwa kupata waliompiga risasi Lissu na kamera zikimulika, wataweza kuwapata wahusika huko Njombe kweli?
 
sasa muda huu wahusika si watakua wameshakimbia? polisi walichokifanya ni sawa na zile vita za zamani, jeshi linasonga kuelekea uwanja wa vita huku linapiga ngoma, vigelegele na makelele ya kutosha ili kumtisha adui.
 
Habari za asubuhi Wapendwa....

Juzi tu, niliandika uzi humu kumuomba IGP Saimoni Sirro kuwashughulikia kisawasawa Wauaji wa watoto. Sasa leo nimeona taarifa inayosema kuwa IGP Sirro ameunda Kikosi maalumu cha kuwasaka hao washenzi

Hivyo sina budi kukushukuru IGP, lakini kwa ujumla Serikali nzima ya Rais Magufuli, hakika kwa hili Serikali mmeonyesha usikivu wa hali ya juu na mnastahili pongezi.

WanaNjombe tunawashukuru sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani hata watuhumiwa hawajakamatwa wewe unashukuru?usije shangaa kuambiwa wahusika wanatoka nchi ya jirani
 
Mimi nilidhani chanzo cha hayo mauaji kimeshajulikana na sehemu ya wahusika waliohusika wamekamatwa! Kumbe umeamua umwage kwanza pongezi kwa mheshimiwa IGP kwa kuunda kikosi kazi! Ok umeeleweka.
 
Ikiwa siku moja imepita tangu naibu waziri wa mambo ya ndani ya nchi amuagize IGP Siro kutuma kikosi maalumu cha kiintelinsia kuongeza nguvu katika uchunguzi wa watekaji na wauaji wilayani Njombe , Hatimae hii jana kikosi hicho kimewasili mkoani Njombe kikiongozwa na Kamisha wa operesheni na mafunzo wa jeshi la polisi nchini Nsato Marijani.

Akizungumza katika mkutano wa dharura na wananchi katika kituo kikuu cha mabasi mkoani Njombe mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher Olesendeka wakati akitamburisha kikosi hicho kilichosheheni wataalamu mbalimbali kutoka vyombo mbalimbali vya ulinzi na usalama nchini amewataka wananchi kutoa ushirikiano ili kuwabaini wahusika wamaovu hayo huku akidai hakuna mtu atakae achwa salama kama amehusika na mauaji.

Katika mkutano huo pia Olesendeka amemuagiza kamanda wa polisi mkoa wa Njombe RPC Rennata Mzinga kumkamata mara moja aliyekuwa mratibu wa tiba mbadala na asilia mkoa wa Njombe Matias Gambishi ambaye pia ni afisa afya wa mkoa huo baada ya kulalamikiwa na waganga wataalamu wa tiba asili na mbadala kuwa amekuwa chanzo cha kusababisha migogoro katika chama chao pamoja kufanya usajiri holela wa waganga hao.

Nae kamanda wa kikosi hicho maalumu Nsato Marijani ambaye ni Kamisha wa operesheni na mafunzo wa jeshi la polisi nchini alisema kikosi hicho kimekuja kwa kazi ya kuwasaka wahusika wa mauaji na kwamba kitawasaka popote walipo kwa heri ama shari.

Kwa upande wananchi wanapongeza serikali kwa kuchukua hatua za haraka za kukabiliana na vitendo hivyo vya ukatili dhidi ya watoto.
 
Kuna mambo mengine hayastahili asante maana sio hisani ni haki yako.

Nyie ndio Umeme ukikatika na ukaja kurudi mnawapigia tanesco kushukuru kwa kuwarudishia japo kimsingi haukutakiwa kukatika.
 
Back
Top Bottom