Kikongwe alia na DC Arumeru kukataa Amri ya Mahakama, amwomba Rais Magufuli kuingilia kati

Jembe Jembe

JF-Expert Member
Jun 9, 2016
749
1,797
Kikongwe mwenye umri wa Miaka 94,Ndesinio Ndewario Nko Mkazi wa Kijiji cha Nkoaranga,Wilayani Arumeru ,Mkoani Arusha,amemwomba rais John Magufuli kumsaidia kupata eneo lake baada ya kushinda kesi mahakamani lakini uongozi wa wilaya umeshindwa kutekeleza amri ya Mahakama.

Akiongea kwa uchungu na vyombo vya habari ,Ndesinio alisema kuwa alishitakiana na mtoto wake aitwaye Emmanuel Nko ambaye aliuza kinyemela eneo hilo lenye ukubwa wa ekari moja lililopo eneo la Kiwawa wilayani humo.

Alisema katika kesi mbalimbali zilizounguruma kuanzia baraza la Ardhi la Kata,baraza la wilaya, Mahakama kuu na Mahakama ya Rufaa alishinda na Mahakama hizo kumtambua yeye kama mmiliki halali wa eneo husika.

Kikongwe huyo alieleza kuwa kijana wake huyo aliuza eneo hilo kinyemela mwaka 2012 kwa Ester Palangyo (Mama chai Jana) mkazi wa Maji ya chai wilayani humo bila kuishirikisha familia wakati akijua si Mali yake nani kinyume cha sheria.

Baada ya kumalizika kwa kesi hiyo ,Mahakama ya rufaa ilitoa maelekezo kesi hiyo irejeshwe baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya ambao walitekeleza amri ya mahakama ya rufani kwa kukabidhi eneo kwa mdai.

Baraza hilo la Ardhi na Nyumba la wilaya la Arusha lilimwandikia barua Mkuu wa wilaya ya Arumeru yenye kumbukumbu namba DLHT/MISC.APP.NO.48 ya mwaka 2013 kuitambulisha kampuni ya udalali ya REGIZ COMPANY LTD kwa ajili ya utekelezaji wa Amri ya baraza katika shauri namba 48/2013 ya mdai Ndesinio Ndewario dhidi ya mdaiwa Immanuel Ndewario Nko.

Alisema kuwa Kampuni ya udalali ya Regiz kupitia barua yake yenye kumbukumbu namba RGZ/AR/48/2020 ilitekeleza hukumu ya shauri hilo namba 48/2013 ikiwa ni pamoja na kuondoa nyumba zilizokuwa zimejengwa na kumkabidhi mdai mbele ya watendaji wa ofisi ya kata ya Imbaseni.

Bibi huyo alidai kwamba julai 23,2020 alipokea barua kutoka kwa Mkuu wa wilaya ya Arumeru,Jerry Muro yenye kumbukumbu namba DC/ARUM/W.10/1XL/62 ya kusitisha kufika katika eneo hilo jambo ambalo amedai ni ukiukwaji wa amri ya Mahakama na kumtaka rais John Magufuli kuingilia kati na msaidia kupata eneo lake kwani ofisi ya Mkuu wa wilaya inajinufaisha kupitia mgogoro huo uliokuwa umemalizwa na Mahakama.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro akiongelea suala hilo ofisini kwake alisema kuwa ni kweli ofisi yake imesitisha utekelezaji wa Amri hiyo ya mahakama baada ya kuwepo kwa viashiria ya uvunjifu wa amani.

Akiongelea suala hilo alisema kuwa hawezi kutekeleza amri ya sasa inayotoka baraza la Ardhi wakati kuna amri nyingine ya nyuma ya Mahakama kuu juu ya shauri hilo ambayo ulitolewa na ilikuwa haijatekelezwa.

"Hapa lazima muelewe kwamba kuna amri mbili zilizotolewa na mimi naanza kutekeleza amri ya Mahakama ndio maana nimesitisha kwanza amri ya sasa ya baraza la Ardhi na Nyumba la wilaya "alisema Murro

Kabla ya kusitisha kwa Amri hiyo Mkuu huyo wa wilaya aliwahi kusaini hati ya utekelezaji wa Amri ya Baraza Kupitia barua ya kampuni ya udalali ya REGIZ yenye kumbukumbu namba RGZ/MB/AR/48/2020 iliyosaimiwa Mei 19 ,Mwaka huu 2020.

Ends.....

IMG-20200807-WA0004.jpg
IMG-20200807-WA0003.jpg
 
Daaah aridhi hizi lakini inawezekana ni malezi aliyo mlelea kijana wake

Yote kwa yote nimependa bandiko la bia hapo ukutani
 
Sasa hiyo amri iliyotangulia ni ipi?

Kwani hukumu za mahakama huwa zinatolewa kiholela hadi zinaleta mkanganyiko?

Hawa viongozi wetu wanafanya kazi zao vizuri, lakini kuna mambo wanakuja kujisahau hadi wanaharibu mpaka sifa zao.

Huyo kikongwe aende kwa Rc kwanza, ili asiposaidiwa sasa apaze sauti yake huko juu, waone moto utakavyowawakia.
 
Naona Jerry Muro analeta mambo ya siasa kwenye sheria. Sijui sheria inasemaje, lakini nijuavyo kama mahakama imetoa amri, basi yeye kama DC hana mamlaka ya kuingilia mahakama.

Juzi nilisikia watoto wa huyo Bibi walewekwa ndani kwa amri ya DC. Tetesi zilizopo ni kuwa Muro ana maslahi katika kesi hiyo, kitu ambacho kimemfanya mkuu wa kituo cha polisi na hakimu aliye toa hukumu kutokuwa na mhusiano mazuri na huyo DC.

NB:
Naona mwisho wa Muro kwa DC meru umekaribia
 
Kisheria Mkuu wa Wilaya Mhe. Muro anapaswa kutekeleza amri hii ya mahakama ambayo ndiyo latest.

Anaposema kuna amri nyingine ya mahakama ni wazi kuna mashaka kwenye maamuzi ya mkuu wa Wilaya.

Akitenguliwa kwa kujitia hamnazo asijekujilaumu
 
*UFAFANUZI*
Kuna picha inazungushwa kwenye Magroup ikimuonyesha bibi Ndesinio Ndewario Nnko anaomba msaada kwa Mhe Rais Magufuli kumsaidia akabidhiwe eneo lake baada ya kushinda kesi na Uongozi wa wilaya kugoma

*UFAFANUZI KUTOKA OFISI YA MKUU WA WILAYA ARUMERU*

1. Kwanza tunataka ieleweke hakuna Amri ya Mahakamani ilishafika ofisi ya Mkuu wa wilaya Arumeru kutoka mahakamani ikashindwa kutekelezeka HAKUNA AMRI KAMA HIYO na hakuna maombi ya Bibi Nnko ofisini kwetu

2. Ofisi ya mkuu wa wilaya inatumbua kuna mgogoro kati ya bibi Nnko na familia yake wakiwemo watoto wanaopambana mahakamani kuhusu Ardhi hiyo na kwa taarifa zilizopo baina yao kila upande una Mashauri mahakamani ambayo baadhi yameamuliwa katika njia tofauti na pande zote zina Mashauri mahakamani uku kila upande ukisema umeshinda, jambo ambalo limetusababisha hata sisi ofisi yetu ishindwe kujua inasimama wapi

3. Mwandihi wa Ngilisho Tv alifika ofisi yetu na akapewa ufafanuzi wa kutosha kuhusu mgogoro huu badala yake amekwenda kuandika habari ya upande mmoja kwa malengo ya kupotosha na kuleta taharuki katika jamii, huyu atachukulia hatua kwa mujibu wa sheria na jambo hili liko kwenye vyombo vya usalama kwa hatua zaidi dhidi ya upotoshaji huu mkubwa

*Hitimisho*
Sisi tunajua huu ni mwaka wa uchaguzi na yako mengi yatasemwa kwa lengo la kutaka kuichafua serikali, Tunaomba wananchi mpuuze habari za Ngilisho Tv zinazolenga kuleta uvunjifu na kuchochea vurugu miongoni mwa jamii, ofisi ya Mkuu wa wilaya Arumeru inaendelea kutatua kero za migogoro ya ardhi kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu na sio kwa mujibu wa Blog ambayo ofisi inachunguza usajili wake TCRA.

*Imetolewa na ofisi ya mkuu wa wilaya Arumeru *
09/08/2020
 
Naona Jerry Muro analeta mambo ya siasa kwenye sheria. Sijui sheria inasemaje, lakini nijuavyo kama mahakama imetoa amri, basi yeye kama DC hana mamlaka ya kuingilia mahakama.

Juzi nilisikia watoto wa huyo Bibi walewekwa ndani kwa amri ya DC. Tetesi zilizopo ni kuwa Muro ana maslahi katika kesi hiyo, kitu ambacho kimemfanya mkuu wa kituo cha polisi na hakimu aliye toa hukumu kutokuwa na mhusiano mazuri na huyo DC.

NB:
Naona mwisho wa Muro kwa DC meru umekaribia
Huyo jeni si alikua anasuluhisha mgogoro wa familia ya msuya,huku tv uchwara zikiwa mubashara
 
Back
Top Bottom