Kikao gani kiliamua Nyerere awe 'Baba wa Taifa'?

Kikao kilifanyika nyumbani kwako, mbele ya baba yako na mama yako....baada ya kukubaliana wakakutuma wewe
kuutangazia umma pale barazani kwenu kwa kutumia vuvuzela kama zile za kwenye world cup SA. Je, unalingine?

duh! Hii kali
 
Bornvilla,
My apology is advanced if this fresh news will hurt you the most!
attachment.php
attachment.php

 
Kila mtu ana mazuri na mabaya yake..lakini watz kutokana na uvivu wa kufikiri tumekaribia kumfanay huyu jamaa kama Mungu mtu vile, kitu ambacho ni dhambi hata Kwa Muumba, kila kitu nyerere ..yaani mpaka inaboa..moja wapo ya mabaya yake and this is very personal.

Huyu jamaa alikua anaogopa wasomi wenzake wa kipindi hicho akikuona una elimu sana lazima akupoteze usije mzidi..mfano..mwaka 1961, mzee wangu alirudi nyumbani tokea marekani akiwa na masters ya mathematics.

Lakini ajabu yake akapelekwa mkwawa kufundisha hesabu...wakaona aibu wakampeleka University of dar e s salaam...akaona huu ujinga akajiondoa na utumishi wa serikali..this guy alikua na roho mbaya sana kwa upande mwingine..sana sana kwa challengers wake.
 
Nimepitia comment nyingi lakini naona wengi wamejikita katika matusi na kejeli.Inanishawishi kusema sasa JF great thinkers ni wachache sana!

Wengi wanapenda kuchangia mada wasizojua lakini wanataka tu waonekane wamecomment. Tujadili hoja kuhusu ubaba wa taifa wa nyerere kama Great thinkers.

Ni kweli kila mmoja anamtazamo wake lakini hebu tutumie akili na busara katika kulijadili hili badala ya matusi na kejeli.
 
Surely, hakuna kikao chochote kilichokaa kuamua Nyerere awe baba wa taifa. But surely, kuna kikao kilichokaa kuamua na kupanga Nyerere auwawe.
 
Kuna wakati mbunge mmoja simkumbuki jina alisema"kwakuwa Nyerere anaingia kwenye mchakato wa utakatifu basi heshima ya ubaba wa taifa apewe mh.Mkapa!" akaongeza "kwakuwa utawala wa Mkapa ulikuwa mzuri basi napendekeza bunge liridhie tubadili katiba ili mkapa agombee tena ili aweze kutawala kwa miaka 10 mingine?".

To put the record in perspective kanisa Katoliki haliko kwenye Mchakato wa kumfanya Nyerere MTAKATIFU. Kanisa Katoliki liko kwenye mchakato wa kumtanganza Nyerere MWENYE KHERI.

Huo uzushi muwe mnauacha huko MISIKITINI, Sio kuuleta hapa JF, jukwaa huru la GTs
 
Nimepitia comment nyingi lakini naona wengi wamejikita katika matusi na kejeli.Inanishawishi kusema sasa JF great thinkers ni wachache sana! Wengi wanapenda kuchangia mada wasizojua lakini wanataka tu waonekane wamecomment. Tujadili hoja kuhusu ubaba wa taifa wa nyerere kama Great thinkers. Ni kweli kila mmoja anamtazamo wake lakini hebu tutumie akili na busara katika kulijadili hili badala ya matusi na kejeli.
Sema tu haukupata jibu ulilolitarajia. Vinginevyo ipotezee tu. Hakuna sheria au kanuni inayokulazimisha kumwita hivo lakini pia hutakiwi kutukataza baadhi yetu kumtambua na kumwita kwa hadhi na heshima hiyo.
 
Nakubaliana na mtoa hoja hii ni nzuri sana, kuna ukweli ndani yake. Binafsi napendekeza Nyerere anyang'anywe ubaba wa Taifa ili nafasi hiyo apewe Jakaya Kikwete. Halmashauri kuu ya ccm ipitishe azimio hilo na kuitangaza kupitia gazeti na radio uhuru, then Serikali itangaze kupitia gazeti la Daily news. Hii ni kwa sababu miaka zaidi ya 7 ya kikwete ni bora kuliko miaka 23 ya Nyerere - Imeleta maisha bora kwa kila mtz, wafanyakazi, wakulima na wafugaji ni raha tupu. Nyerere alishindwa kabisa. Rekodi hii ya Kikwete hata Chadema wakishinda nadhani hawataifikia. Hongera Mleta mada.
 
Hivi ni nani hasa mama wa taifa hili? Kama baba yupo (Gender balance).
Tukipata "UHURU" mpya toka kwa "mkoloni" wa sasa( CCM), na kiongozi wa kudai uhuru huo akawa ni mwanamke, bila shaka yoyote huyu atakuwa mama wa taifa hili jipya.
 
Suala zuri sana hili.

Binafsi jana nimeingia Tanzania hususan Dar es salaam nikiwa safarini kesho Insh'Allah naelekea Mwanza na Al'khamis nitakuwa Bukoba kuhudhuria harusi ya mwanangu mlezi huko kamachumu hapo l'jumaa.

Nimepata bahati asubuhi hii kupita afisi mbili za Serikali na kuona Picha kubwa ya Nyerere imeandikwa Baba wa taifa. Na nimepita hotel ya Al Basha )lebenese Hotel maeneo karibu na extelecomms posta nikaona picha ya Nyerere imeandikwa baba wa taifa.

Kwa kuwa picha hizo zimewekwa hata kwenye Afisi za Serikali naona pasi na shaka itakuwa imewekwa kwenye KATIBA yenu.

Tunaelewa kuwa Tz ni nchi inayoendeshwa na kufuata Rules of Law. Na kila kitu kitakuwa kimewekwa kwenye KATIBA. Labda naomba waTz mtujuze kuwa JE IPO KWENYE KATIBA na hivyo kuwa Sharia kuwa lazima kuwe na Picha ya Rais wa JMTz (hili lipo kwenye sharia) na pembeni yake ya baba wa Taifa?

Tunaomba ufafanuzi kwa wenye ujuzi wa sharia za Muungano.
 
Suala zuri sana hili.

Binafsi jana nimeingia Tanzania hususan Dar es salaam nikiwa safarini kesho Insh'Allah naelekea Mwanza na Al'khamis nitakuwa Bukoba kuhudhuria harusi ya mwanangu mlezi huko kamachumu hapo l'jumaa.

Nimepata bahati asubuhi hii kupita afisi mbili za Serikali na kuona Picha kubwa ya Nyerere imeandikwa Baba wa taifa. Na nimepita hotel ya Al Basha )lebenese Hotel maeneo karibu na extelecomms posta nikaona picha ya Nyerere imeandikwa baba wa taifa...
Hili nalo liingizwe kwenye KATIBA! Siasa za kujifunzia ukubwani hizi Barubaru. Hata Biblia na Quran hazina yote ambayo Mungu angependa yawemo! Uislam, Ukatoliki, Ulutheri,..., navyo havijatajwa kwenye katiba. Ulipita salama pale JNIA? Mwenzako Mohamed kwa Uislam wake alipekuliwa na kudhalilishwa pale mwaka 2006!
 
Nakubaliana na mtoa hoja hii ni nzuri sana, kuna ukweli ndani yake. Binafsi napendekeza Nyerere anyang'anywe ubaba wa Taifa ili nafasi hiyo apewe Jakaya Kikwete. Halmashauri kuu ya ccm ipitishe azimio hilo na kuitangaza kupitia gazeti na radio uhuru, then Serikali itangaze kupitia gazeti la Daily news. Hii ni kwa sababu miaka zaidi ya 7 ya kikwete ni bora kuliko miaka 23 ya Nyerere - Imeleta maisha bora kwa kila mtz, wafanyakazi, wakulima na wafugaji ni raha tupu. Nyerere alishindwa kabisa. Rekodi hii ya Kikwete hata Chadema wakishinda nadhani hawataifikia. Hongera Mleta mada.
hapa Ahali yangu nilitaka kukusaidia kidogo hususan kwa kukukumbusha itazame Tanzania kwa jicho la KIUCHUMI na sio KiSIASA.

Waarabu tuna usemi '' In order to build something strong, it helps to start with BEST and POSSIBLE material''. Kwa mantiki hiyo utaona Mkoloni alijenga Misingi imara sana ya Uchumi wa Tanganyika yenu na alihakikisha uchumi huo unasambaa kwa uwiano uliosawa kwa nchi nzima na kuhakikisha yale mahitaji muhimu kwa jamii yanapatikana tena kwa wakti.

Nyerere alihishimu sana SIASA na kudharau sana UCHUMI. Alijenga misingi ya UCHUMI kwa kutumia siasa na kuleta slogan yake , Ili tuendelee tunahitaji vitu vinne, watu, ardhi, siasa safi na Uongozi Bora. Sasa jiulizeni Tz mmekosa nini hapo mpaka leo mnazidi kuwa nchi masikini duniani?

Kumbukeni Nyerere ndio muasisi mkubwa wa Ulanguzi, yaani watu kujilimbikizia mali kitu ambacho leo hii kimekuwa na kinaitwa UFISADI. Wakti wa mkoloni hakukuwa na ulanguzi wa aina yoyote.

Kwa kifupi Tanzania hususan Tanganyika imejengwa kwa misingi mibovu sana yaani watu wanajipenda binafsi na hakuna uzalendo wa kulipenda Taifa lenu. Kwa aina yoyote ile kila atakaye kaa madarakani lazima ajilimbikizie mali pamoja na viongozi wengine atakao wachagua.

Kinachotkiwa kukifanya ku kuuwa siasa za Nyerere na kuweka sharia kali sna kuwaadhibu wezi wa mali za umma ikiwa pamoja na kujenga utamaduni kwa wananchi wa Tz kuipenda nchi yao.

Kwa maneno mengine tunaweza sema , ASILAUMIWE DOBI KWANI KANIKI NDIO RANGI YAKE''

 
Tujuavyo hapakuwa na kikao ila ni heshima tu apatiwayo mtu ambaye alikuwa mpiganaji katika uanzilishi wa tukio fulani-kwa mfano Uhuru wa Tanganyika.ndo maana akatunzwa BABA...Mbona hili lipo hata kwa wenzetu huko nje mfano
1.Mahtma Ghandi- Baba wa Taifa wa India (alikuwa ni muunganishi wa watu wa India katika kuleta Uhuru.....)
Unaweza ongezea wengine uwajuao....
 
To put the record in perspective kanisa Katoliki haliko kwenye Mchakato wa kumfanya Nyerere MTAKATIFU. Kanisa Katoliki liko kwenye mchakato wa kumtanganza Nyerere MWENYE KHERI.

Huo uzushi muwe mnauacha huko MISIKITINI, Sio kuuleta hapa JF, jukwaa huru la GTs
Mkuu kwani Msikitini kunakuwaga na uzushi? Si mahala patakatifu?
 
hapa Ahali yangu nilitaka kukusaidia kidogo hususan kwa kukukumbusha itazame Tanzania kwa jicho la KIUCHUMI na sio KiSIASA.

Waarabu tuna usemi '' In order to build something strong, it helps to start with BEST and POSSIBLE material''. Kwa mantiki hiyo utaona Mkoloni alijenga Misingi imara sana ya Uchumi wa Tanganyika yenu na alihakikisha uchumi huo unasambaa kwa uwiano uliosawa kwa nchi nzima na kuhakikisha yale mahitaji muhimu kwa jamii yanapatikana tena kwa wakti.

Nyerere alihishimu sana SIASA na kudharau sana UCHUMI. Alijenga misingi ya UCHUMI kwa kutumia siasa na kuleta slogan yake , Ili tuendelee tunahitaji vitu vinne, watu, ardhi, siasa safi na Uongozi Bora. Sasa jiulizeni Tz mmekosa nini hapo mpaka leo mnazidi kuwa nchi masikini duniani?

Kumbukeni Nyerere ndio muasisi mkubwa wa Ulanguzi, yaani watu kujilimbikizia mali kitu ambacho leo hii kimekuwa na kinaitwa UFISADI. Wakti wa mkoloni hakukuwa na ulanguzi wa aina yoyote.

Kwa kifupi Tanzania hususan Tanganyika imejengwa kwa misingi mibovu sana yaani watu wanajipenda binafsi na hakuna uzalendo wa kulipenda Taifa lenu. Kwa aina yoyote ile kila atakaye kaa madarakani lazima ajilimbikizie mali pamoja na viongozi wengine atakao wachagua.

Kinachotkiwa kukifanya ku kuuwa siasa za Nyerere na kuweka sharia kali sna kuwaadhibu wezi wa mali za umma ikiwa pamoja na kujenga utamaduni kwa wananchi wa Tz kuipenda nchi yao.

Kwa maneno mengine tunaweza sema , ASILAUMIWE DOBI KWANI KANIKI NDIO RANGI YAKE''

Ulipoteremka pale JNIA haukumkumbuka Mwalimu? Uliposoma pale UDSM haukumkumbuka Mwalimu? Unapowatembelea ndugu zako Waarabu hadi huko Bukoba vijijini kabisa haumkumbuki Mwalimu? Amani yote hii inayokuzunguka haikukumbushi Mwalimu? Usione vyaelea. Vinakuwa vimeundwa kwa misingi fulani hivi.
 
Mkuu kwani Msikitini kunakuwaga na uzushi? Si mahala patakatifu?

Mimi kwa masikio yangu nimewahi kupita ktk msikiti mmoja, nikasikia Sheikh akisema kwamba, Nyerere alikuwa muuaji mkubwa na alikuwa adui wa Waislamu. Pia Nyerere aliwapendelea WAKATOLIKI katika Elimu na Mdaraka serikalini. Kwa kutambua mission hiyo ndiyo maana leo KANISA KATOLIKI liko kwenye mchakato wa kumfanya Nyerere MTAKATIFU.

Ukiniambia sehemu wanayoongea UZUSHI huo ni PATAKATIFU, basi neno Takatifu lina maana nyingine tofauti kabisa na maana ambayo kila moja wetu anaifahamu.
 
hapa Ahali yangu nilitaka kukusaidia kidogo hususan kwa kukukumbusha itazame Tanzania kwa jicho la KIUCHUMI na sio KiSIASA.
Uchumi ni siasa pia.

Waarabu tuna usemi '' In order to build something strong, it helps to start with BEST and POSSIBLE material''.
Mkuu na wewe mfumo Kristo umekuathiri? Ulipaswa uandike hivi...

Kwa mantiki hiyo utaona Mkoloni alijenga Misingi imara sana ya Uchumi wa Tanganyika yenu na alihakikisha uchumi huo unasambaa kwa uwiano uliosawa kwa nchi nzima na kuhakikisha yale mahitaji muhimu kwa jamii yanapatikana tena kwa wakti.
Mkoloni yupi? Mwarabu, Mwingereza au Mjerumani?

Nyerere alihishimu sana SIASA na kudharau sana UCHUMI. Alijenga misingi ya UCHUMI kwa kutumia siasa na kuleta slogan yake , Ili tuendelee tunahitaji vitu vinne, watu, ardhi, siasa safi na Uongozi Bora. Sasa jiulizeni Tz mmekosa nini hapo mpaka leo mnazidi kuwa nchi masikini duniani?
Siasa ni Kilimo, Siasa ya Ujamaa na kujitegemea nk. Lkini Sheikh Barubaru kumbuka hayo yalikuwa ni mahitaji ya wakati ule. Hata kina Ustaadh Almarhum Kawawa, Ustaadh Ally Mwinyi, Ustaadh Almarhum Abdulrahman Babu, Ustaadh Almarhum Kigoma Malima, walielewa na wakakubaliana na dhana ya Mwenye Heri Nyerere kuwa SIASA NDIO UCHUMI wenyewe. Hata sasa principle haijabadilika. Ni siasa inayotawala ulimwengu, ni siasa inayoleta vita kwenye baadhi ya maeneo ulimwenguni na ni siasa hiyo hiyo inayoleta ustawi kwenye baadhi ya nchi ulimwenguni. Siasa mbaya, uchumi mbaya, na siasa safi Uchumi safi..

Kumbukeni Nyerere ndio muasisi mkubwa wa Ulanguzi, yaani watu kujilimbikizia mali kitu ambacho leo hii kimekuwa na kinaitwa UFISADI. Wakti wa mkoloni hakukuwa na ulanguzi wa aina yoyote.
Huu sasa ni utovu wa nidhamu. Nadhani hapa umesukumwa na utashi wako binafsi bila ya kuwa na facts. Kwa maoni yangu Mlanguzi namba moja nchini ni Alhaji Almarhum Kighoma malima aliyeiba fedha za watanzania maskini akazificha ughaibuni ili aanzishe chama ambacho baadae kingetuletea akina Boko Haram nchini

Kwa kifupi Tanzania hususan Tanganyika imejengwa kwa misingi mibovu sana yaani watu wanajipenda binafsi na hakuna uzalendo wa kulipenda Taifa lenu. Kwa aina yoyote ile kila atakaye kaa madarakani lazima ajilimbikizie mali pamoja na viongozi wengine atakao wachagua.
Haya ni maoni yako. Nayaheshimu ingawa kwa yeyote mwenye akili atayaweka kwenye kapu la maoni ya kipuuzi.

Kinachotkiwa kukifanya ku kuuwa siasa za Nyerere na kuweka sharia kali sna kuwaadhibu wezi wa mali za umma ikiwa pamoja na kujenga utamaduni kwa wananchi wa Tz kuipenda nchi yao.

Kwa maneno mengine tunaweza sema , ASILAUMIWE DOBI KWANI KANIKI NDIO RANGI YAKE''


Nakutakia safari nyema ya Mwanza - Bukoba
 
Hili nalo liingizwe kwenye KATIBA! Siasa za kujifunzia ukubwani hizi Barubaru. Hata Biblia na Quran hazina yote ambayo Mungu angependa yawemo! Uislam, Ukatoliki, Ulutheri,..., navyo havijatajwa kwenye katiba. Ulipita salama pale JNIA? Mwenzako Mohamed kwa Uislam wake alipekuliwa na kudhalilishwa pale mwaka 2006!

WildCard.

Ahali yangu nipo Dar na nitafirahi sana kama tutaonana pale Al Bashar restaurant (Lebanese Hotel) karibu na Helitage Hotel , Posta tupate Chai jioni baada al asr.

Vile vile kumbuka nimeishi na kuondoka vizuri sana Tz. Nikija siku zote napokewa na maswahiba zangu wakubwa sana Serikalini na mara zote napata fursa za kuonana na viongozi wenu wakubwa kubadilishana mawazo. Nakumbuka ni mara moja tu ndio nilisimamishwa pale Airport na kwa bahati yule mtu aliyenisimamisha alikuwa ni member wa JF. alinitaka kunisabahi na kujuliana hali.

lakin vile vile kama utasoma KATIBA yenu imebainisha wazi kuhusu kuweka picha ya Rais wenu katika Afisi na shughuli zote za Serikali na mamlaka zake. Kama utasoma Katiba yenu Kuhusu Rais wenu na Mamlaka yake katika sharia Namba 15 Ibara 9 ya mwaka 1984. Imebainisha
 
Back
Top Bottom