Kijue kisiwa cha Ukerewe kwa undani. Kisiwa cha kifahari kilichopo pembezoni mwa jiji la Mwanza

Kisiwa hiki kinapatikana ndani ya Ziwa Viktoria nje kidogo ya jiji la Mwanza ambacho kwa ujumla wake kinaundwa na visiwa vidogo dogo vipatavyo 38 huku kisiwa kikubwa kikiwa ni kisiwa cha Ukara huku vingine vikiwa havikaliwi na watu.


Visiwa 38 havikaliwi na watu???--- kwanini wasiuze hiyo ardhi kwa watu binafsi kwa ajili ya kuwekeza???
 
Hapo kwenye nauli ya Basi,,mabasi yanapita wapi kuingia nansio,au Yana muundo wa hovercraft?

Pili,kisiwani Cha Kome kilichoungua juzi nacho kipo ukerewe au bukoba?
Kisiwa cha kome kipo Buchosa, unapita sengerema hadi Nyakalilo unapata zako kivuko cha Mv kome safi kabisa
 
Kwanza nashukuru kwa swali zuri ulilouliza na hili swali limekuwa likiulizwa mara kwa mara

Kwanza nakushukuru kwa swali zuri na hili swali limekuwa likiulizwa mara kwa mara na sisi kama wanaukerewe bila kuchoka tumekuwa tukilijibu na tutaendelea kulijibu mpaka pale watu watakapopata uelewa wa kutosha kuhusiana na uvumi huu.

Imani za kishirikina kiujumla ni imani potofu ambazo zinatakiwa kupingwa si tu ukerewe peke yake bali na jamii zote za kitanzania kwa sababu ni miongoni mwa mambo yanayokwamisha maendeleo katika jamii.

Katika wilaya ya Ukerewe,Ni kweli nakiri wazi kwamba hizo imani zilikuwepo lakini baada ya muingiliano wa watu kutoka makabila tofauti tofauti, imani hizo zimepungua kwa asilimia kubwa kama siyo kutokomea kabisa. Nikuhakikishie tu kwamba kwa sasa hali ni shwari, watu wako bize zaidi kuchapa kazi kwa lengo la kujiletea maendeleo. kwahiyo ukisikia mtu bado anaishutumu hii wilaya kwa imani za kishirikina ujue anatumia historia ya zamani ya miaka mingi iliyopita(ambayo haipo kwa sasa) kuchafua sifa na taswira nzima ya uzuri wa kisiwa hiki.
Bado imani zipo hasa kule pande za Rubya na Lukara

Zinaweza kuwa zimepungua sana ila hazijaisha. Bado watu hawawezi kuua chatu maeneo ya Rubya hata akiingia ndani

Bado watu wanaamini kwenye kutumiana mamba.

Labda utufafanulie, ni kwanini kila anayeua chatu huko Rubya lazima apate madhara? Nilikuwa huko juzi juzi mwezi Machi, hizo Imani bado zipo
 
Ila mleta uzi ame generalise Sana,,hasa fursa,,je nijitaka kununua samaki wa biashara nakuja Hapo nansio?,
Dagaa je?.
Hebu nenda kiundani ili wawekezaji tuje kisiwani kuwekeza
Siyo simple kihivyo. Ngoja tusubiri jibu ila samaki nansio! Labda wa mboga tu
 
Hahaa aya mkaruka chilimo karibhu ,, anye ndi bwiro kumulambo
Daah huyu bhana kanikumbusha sana sana home hongera hongera sana mleta maada leo nimejisikia amani na furaha kusoma uzi wa nyumbani thanks mr
 
Visiwa 38 havikaliwi na watu???--- kwanini wasiuze hiyo ardhi kwa watu binafsi kwa ajili ya kuwekeza???
Sidhani kama kaandika hivyo. Vipo ambavyo havikaliwi na watu ila vipo vinavyokaliwa na watu. Uwekezaji wa visiwani umeangalia sana uvuvi. Hivyo katika uwekezaji kuna sifa ya kisiwa lasivyo unaweza pata hasara kati ya maandalizi ya uwekezaji ukilinganisha na uzalishaji
 
Nimevutiwa sana na haya maelezo.
Nimesoma maelezo yote hapo inaonekana wazi kabisa Ukerewe ni wilaya na kisiwa chenye fursa zote za kiuchumi na kijamii huenda toka tunapata uhuru.

Sasa inakuwaje mpaka leo hii bado maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya wakazi wa Ukerewe yapo chini sana?
Yaani ukizungumzia Umaskini, Ujinga au Ushirikina katika kanda ya Ziwa, huwezi kukwepa kuitaja Ukerewe.

Pia ni kwanini wenyeji asili wa Ukerewe waliokuja mjini na kusoma au kufanikiwa kimaisha huwa wengi wao kamwe hawarudi tena Ukerewe kuishi, kujenga na kuendeleza miji na vijiji vyao vya asili?
Ninavyojua mimi wakala, wajita na wakelewe ni watu wenye kushabihana tabia na tamaduni kwa mujibu wa makabila yao.
Sasa kinachowarudisha nyuma kimaendeleo ni ile kasumba ya "wivu na chuki" dhidi ya waliofanikiwa, kasumba hiyo wamekuwa wakifanyiana sana wao kwa wao; yaani ndugu wa wanafamilia hataki nduguye afanikiwe kimaisha (hususani maendeleo ya kielimu).
Si ajabu Mwanafunzi aliyemaliza kidato cha sita na kufanikiwa kwenda chuo akarogwa na mmojawapo wa wanaukoo. Ndiyo sababu wanafunzi wengi wakifaulu aidha kwenda kidato cha tano au kwenda chuo, huwa hawarudi vijijini kwao kipindi cha likizo.
Naliongea hili, kwa kuwa nilishashuhudia Mwanafunzi (kabila mjita) wa chuo cha Mzumbe tawi la Mbeya alifariki ktk mazingira ya kutatanisha mda mfupi baada ya kujiunga ktk chuo hicho.
 
Salaam kwenu wote wana jamvi

Haya ni mambo machache kuhusu wilaya/kisiwa cha Ukerewe.

Maelezo mafupi
UKEREWE ni moja wapo ya wilaya zinazounda mkoa wa Mwanza. Pia ni miongoni mwa wilaya za mwanzo mwanzo (kongwe) kuanzishwa nchini Tanzania. Wilaya ya Ukerewe ina ukubwa wa kilometa za eneo zipatazo 530.

Idadi ya watu

Wilaya ya ukerewe ina jumla ya wakazi wapatao 345,147. Kata 25, tarafa 4 na vijiji 76.

Ukerewe ni kisiwa
Mbali na kuwa wilaya, Ukerewe ni kisiwa. Ndicho kisiwa kinachoongoza kwa ukubwa barani Afrika na kisiwa cha tano kwa ukubwa duniani. Pia Ukerewe ndicho kisiwa pekee kisichokuwa ndani ya bahari kwa ukanda mzima wa Afrika.

Kisiwa hiki kinapatikana kusini mashariki mwa Ziwa Viktoria nje kidogo ya jiji la Mwanza ambacho kwa ujumla wake kinaundwa na visiwa vidogo dogo vipatavyo 38 huku kisiwa kikubwa kikiwa ni kisiwa cha Ukara huku vingine vikiwa havikaliwi na watu.

Makabila yanayopatikana
Wilaya ya Ukerewe inakaliwa na watu wa makabila mbali mbali kutoka kila pembe ya nchi na nje ya nchi. Lakini makabila makuu ni matatu ambayo ni Wakerewe(wenyeji), Wajita na Wakara. Mbali na kuzungumza lugha tofauti, haya makabila wanasikilizana kwa ukaribu kabisa. Pia Kikerewe kinarandana na kihaya kutokana na ufanano wa baadhi ya maneno.

Hali ya hewa na vivutio vya asili vinavyopatikana
Ukerewe ni wilaya iliyobarikiwa kuwa na hali ya hewa safi ya wastani na uoto wa asili pia ni kitovu cha utalii wa ndani. Miongoni mwa vivutio vya utalii vinavyopatikana ni pamoja na mapango ya Handebezyo, jiwe linalocheza "dancing stone" la Nyaburebeka.

Mbali na vivutio hivyo uwapo ukerewe utapata fursa ya kulitazama ghorofa la kwanza kumilikiwa na mtu mweusi. Vile vile utapata fursa ya kutembelea na kuitazama shule kongwe ya Kagunguri ambapo profesa wa kwanza nchini Tanzania alipata kusomea hapo pamoja na viongozi mbali mbali waliowahi kushika nyadhifa mbali mbali za juu serikalini kama vile Pius Msekwa na wengineo.

Mji mkuu
Mji mkuu wa ukerewe ni NANSIO (Kiswahili) au NANSYO (Kilugha). Ni mji mzuri wenye mandhari ya kupendeza na unaokua kwa kasi sana. Hali ya kimaisha katika mji huu ni ya kawaida sana kwa mtu yeyote mwenye kipato ama mtafutaji kuweza kuishi na kuendesha maisha yake.

Shughuli za kiuchumi
Shughuli kubwa ya kiuchumi inayotegemewa ni uvuvi japo kilimo na ufugaji vinafanyika lakini kwa kiwango kidogo sana. Pia ni kisiwa kizuri kwa kufanyia shughuri za biashara, usafirishaji na utalii wa ndani.

Huduma ya elimu
suala la elimu wilayani Ukerewe limepewa kipaumbele. Katika jitihada za kutokomeza adui 'ujinga' wilayani Ukerewe kuna jumla ya shule za msingi 125 na shule za sekondari 25.

Huduma za afya
wilaya inatambua umuhimu wa afya bora kama nguzo muhimu katika kuchochea suala la maendeleo ya mtu binafsi, familia na Taifa kwa ujumla katika kuleta maisha bora na kupunguza umaskini. Kwa kulitambua hilo, wilaya imejenga jumla ya vituo ya afya 4, zahanati 28( sawa na uwiano wa zahanati moja kwa kila kata) na hospitali moja ya wilaya kwa lengo la kutoa huduma za afya kwa wananchi.

Huduma zingine za kijamii
Huduma zote za kijamii kama vile usafiri, maji na umeme vinapatikana. Pia uwepo wa benki mbili na mawakala mbali mbali wa kifedha na huduma za simu waliotapakaa kila sehemu umerahisisha upatikanaji wa huduma za kifedha uwapo kisiwani ukerewe.

Gharama za usafiri
Gharama za usafiri kutoka mwanza kufika ukerewe zinatofautiana kutokana na chombo cha usafiri ulichotumia. Mchanganuo wa gharama za usafiri ni kama ifuatavyo,
kivuko cha Nyehunge
nauli ni Tsh 6,000/= ( kawaida) na Tsh 7,000/=( seat za juu)
Umbali wa safari: masaa 3

Kivuko cha serikali(Mv clarias na butiama)
nauli ni Tsh 6,000/=
Umbali wa safari: masaa 2 na nusu

Kivuko cha serikali(Mv ilemela)
nauli ni Tsh 2,000/= Hiki kivuko kipo pembezoni kidogo mwa mji kinafanya safari zake kati ya ukerewe na kayenze kupitia kisiwa cha bezi.

Kivuko cha Mv Rafiki(fast boat)
nauli ni Tsh 10,000/= (kawaida) na Tsh 15,000/= (seat za juu)
Umbali wa safari: Saa moja na nusu

Nauli za mabasi ni Tsh 10,000/=
Umbali wa safari: masaa 8-9


Hitimisho
Haya ni machache kati ya mengi yanayopatikana katika kisiwa hiki adhimu kabisa. Wenyeji wa hiki kisiwa ni watu wakarimu na wapenda wageni hivyo msisite kukitembelea na kujionea mengi yanayopatikana kwenye hiki kisiwa cha Ukerewe kilichopo pembezoni mwa jiji la Mwanza.

Viambatanisho

View attachment 1461593
Monarch beach resort
View attachment 1461599
Nansio tower

View attachment 1461601
Nansio port

View attachment 1461602
Some landscape

View attachment 1461605
Mwiboma-hamuyebe

View attachment 1461606
Mv Rafiki( fast boat)

View attachment 1461612
Jiwe linalocheza(dancing stone)

View attachment 1461613
Handebezyo

View attachment 1461614
Mapango ya handebezyo

View attachment 1461615
Mv ilemela( ukerewe to kayenze-mwanza via bezi island)

View attachment 1461616
Nyehunge ferry

View attachment 1461617
Mv clarias

View attachment 1461619
Mv Butiama( kuanza kazi karibuni)

View attachment 1461621
Lake Victoria view

View attachment 1461623
Shughuli za uvuvi(fishing activities) zikiendelea

View attachment 1461624
Kitoweo cha samaki aina ya sato

View attachment 1461625
Kitoweo cha samaki aina ya sangara

View attachment 1461627
Monarch beach

Karibu Nansio, karibu kisiwa cha Ukerewe
Lazima siku moja nifike ukerewe my best destination
 
Back
Top Bottom