IsangulaKG
JF-Expert Member
- Oct 14, 2010
- 706
- 386
Nikiwa katika majukumu yangu ya ujenzi wa Taifa,nikapitia katika kijiwe fulani cha walalahoi. Baada ya kuwasabahi, waungwana ambao awali walionyesha kustushwa na ujio wangu, wakaitikia salamu kama ilivyo ada kwa watanzania. Baada ya kujiaminisha kuwa uwepo wangu mahali pale ni wa kheri si shari, wakaendelea na maongezi yao.
"Nakwambia Serikali yetu imeoza sana, Kitengo cha chanjo za mifugo kimetengeneza maelfu ya chanjo feki...jambo la ajabu ni kwamba virutubisho chanjo viliagizwa kutoka kubwa kumbe vilikuwa vimekaribia muda wa ku-expire" alisema mmoja wa wasemaji aliyeonekana mwongeaji sana.
"Japo la ajabu ni kwamba virutubisho vilipokelewa kuanzia bandarini mpaka TBS wakavipitisha...hivi kweli hawakujua kuwa muda wake umekaribia kuisha au ni miradi ya wakubwa? alihoji mwingine.
"Pengine wataalamu wetu ni feki, ina maana hawakufanya majaribio kabla hawajaanza massive production?" akarukia mwingine
"Yaani nchi hii bwana, virutubisho feki, wataalamu feki, TBS feki...mabilioni ya fedha yamepotea na hakuna aliyewajibishwa" akasema mwingine aliyeonekana kuwa na uchungu sana na kodi anayokatwa kwenye mshahara wake
Kwa ufupi ni kwamba majaribio yalifanyika, virutubisho vikaagizwa Cuba lakini inasemekana vilikuwa vimeisha muda wake au havikuwa na contents sahihi, vikapokelewa na kupitishwa bandarini na wataalamu wa TBS na kitengo cha chanjo kikatengene maelfu ya chanjo ambazo hazifanyi kazi. Haijajulikana kama chanjo hizo zilishaingizwa sokoni na kama zilikuwa 'dead' au 'live' . Kwani kama zilikuwa 'live' zaweza kusababisha madhara makubwa sana kwa mifugo.
Hata hivyo, kwa kuwa mimi si mwandishi wa habari na si mtalaamu wa investigative journalism, sikwenda mbele kufuatilia habari hii katika idara ya mifugo, kitengo cha chanjo za mifugo.
"Nakwambia Serikali yetu imeoza sana, Kitengo cha chanjo za mifugo kimetengeneza maelfu ya chanjo feki...jambo la ajabu ni kwamba virutubisho chanjo viliagizwa kutoka kubwa kumbe vilikuwa vimekaribia muda wa ku-expire" alisema mmoja wa wasemaji aliyeonekana mwongeaji sana.
"Japo la ajabu ni kwamba virutubisho vilipokelewa kuanzia bandarini mpaka TBS wakavipitisha...hivi kweli hawakujua kuwa muda wake umekaribia kuisha au ni miradi ya wakubwa? alihoji mwingine.
"Pengine wataalamu wetu ni feki, ina maana hawakufanya majaribio kabla hawajaanza massive production?" akarukia mwingine
"Yaani nchi hii bwana, virutubisho feki, wataalamu feki, TBS feki...mabilioni ya fedha yamepotea na hakuna aliyewajibishwa" akasema mwingine aliyeonekana kuwa na uchungu sana na kodi anayokatwa kwenye mshahara wake
Kwa ufupi ni kwamba majaribio yalifanyika, virutubisho vikaagizwa Cuba lakini inasemekana vilikuwa vimeisha muda wake au havikuwa na contents sahihi, vikapokelewa na kupitishwa bandarini na wataalamu wa TBS na kitengo cha chanjo kikatengene maelfu ya chanjo ambazo hazifanyi kazi. Haijajulikana kama chanjo hizo zilishaingizwa sokoni na kama zilikuwa 'dead' au 'live' . Kwani kama zilikuwa 'live' zaweza kusababisha madhara makubwa sana kwa mifugo.
Hata hivyo, kwa kuwa mimi si mwandishi wa habari na si mtalaamu wa investigative journalism, sikwenda mbele kufuatilia habari hii katika idara ya mifugo, kitengo cha chanjo za mifugo.