Kijiswali kuhusu Zika: Kipimo kitapimaje kusikokuwa na ugonjwa?

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
NIMR walisema kuwa imebainika, kiutafiti, kuwa virusi vya ugonjwa hatari wa Zika vipo nchini Tanzania. Utafiti ukasema kuwa asilimia zaidi ya kumi ya waliotafitiwa wamebainika kuwa na vimelea vya Zika.

Lakini, Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu alikanusha haraka yenye baraka kuwa utafiti huo haujathibitisha kuwepo kwa Zika nchini. Waziri Ummy akasema, na kuwatoa hofu watanzania, kuwa Tanzania haina Zika. Akasema kuwa utafiti huo ulifanyika kwa kipimo cha Zika.

Sasa, inawezekanaje kutafiti kuhusu kipimo cha Zika mahali pasipo na Zika? Inawezekanaje kutafiti ulaji wa matunda kusipo na matunda? Mniwie radhi kwa kuchelewa kukauliza kaswali haka kwakuwa nilikuwa 'bize'.

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
NIMR walisema kuwa imebainika, kiutafiti, kuwa virusi vya ugonjwa hatari wa Zika vipo nchini Tanzania. Utafiti ukasema kuwa asilimia zaidi ya kumi ya waliotafitiwa wamebainika kuwa na vimelea vya Zika.

Lakini, Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu alikanusha haraka yenye baraka kuwa utafiti huo haujathibitisha kuwepo kwa Zika nchini. Waziri Ummy akasema, na kuwatoa hofu watanzania, kuwa Tanzania haina Zika. Akasema kuwa utafiti huo ulifanyika kwa kipimo cha Zika.

Sasa, inawezekanaje kutafiti kuhusu kipimo cha Zika mahali pasipo na Zika? Inawezekanaje kutafiti ulaji wa matunda kusipo na matunda? Mniwie radhi kwa kuchelewa kukauliza kaswali haka kwakuwa nilikuwa 'bize'.

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Hampendi kuambiwa ukweli Mjomba,naona hata kesho nikikwambia Bintiyo anaolewa utakasirika na kunitupa Keko kisa hukutaka kulisikia hilo,kwani unataka kuambiwa kuwa bado bintiyo ni mdogo.
 
Mshua anataka atoke na clean sheet.tuje kusema wakati wake hakukuwa na magonjwa.
 
Mahali pa wataalamu bora kuwaachia wataalam,tatizo letu kila kitu siasa.Huyu Waziri Ummy sijui kwanini anakanusha tena sijui anatumia kigezo zaidi ya siasa za kubwabwaja tu.
 
NIMR walisema kuwa imebainika, kiutafiti, kuwa virusi vya ugonjwa hatari wa Zika vipo nchini Tanzania. Utafiti ukasema kuwa asilimia zaidi ya kumi ya waliotafitiwa wamebainika kuwa na vimelea vya Zika.

Lakini, Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu alikanusha haraka yenye baraka kuwa utafiti huo haujathibitisha kuwepo kwa Zika nchini. Waziri Ummy akasema, na kuwatoa hofu watanzania, kuwa Tanzania haina Zika. Akasema kuwa utafiti huo ulifanyika kwa kipimo cha Zika.

Sasa, inawezekanaje kutafiti kuhusu kipimo cha Zika mahali pasipo na Zika? Inawezekanaje kutafiti ulaji wa matunda kusipo na matunda? Mniwie radhi kwa kuchelewa kukauliza kaswali haka kwakuwa nilikuwa 'bize'.

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
NIMRI hawakusema kuna Zika nchini bali kumegundulika kuwepo kwa vimelea/virusi vya zika. Nidhamu ya woga na unafiki wa mawaziri wetu ndio kimemgharimu Dr, Mwere kazi yake.
 
Kwa wataalumu waliosomea utafiti na kada zinazohusu utafiti hatujamuelewa ummy... Labda kama angekuwa na reference ya tafiti yake kuonesha tz hakuna zika tungemuelewa....
 
Otherwise huwezi kuja with single word bila kufanya utafiti na kusema hakuna zika
 
Dawa na kinga za malaria zipo dunia nzima unless utake kutuambia kua huu, ugonjwa upo kila mahali penye ugonjwa husika!
 
Namimi nasema HAKUNA ZIKA. (Hata kama ni hivyo) Ebo!! Mnataka nitumbuliwe na mimi?
 
Dawa na kinga za malaria zipo dunia nzima unless utake kutuambia kua huu, ugonjwa upo kila mahali penye ugonjwa husika!

Ukitoka na malaria yako bongo ukaenda nchi za ulaya (mfano Ujerumani/Austria/ nk) huwezi pata tiba kwenye hospitali yoyote hata iwe kubwa namna gani kwani hawana vipimo vya malaria! Ili kupima lazima uende hospitali maalumu zinashughulikia magonjwa ya tropikali (tropical diseases)!
 
Ukitoka na malaria yako bongo ukaenda nchi za ulaya (mfano Ujerumani/Austria/ nk) huwezi pata tiba kwenye hospitali yoyote hata iwe kubwa namna gani kwani hawana vipimo vya malaria! Ili kupima lazima uende hospitali maalumu zinashughulikia magonjwa ya tropikali (tropical diseases)!
Hizo hospitali maalum zinakua zipo nchi gani?
 
Umeuliza swali ambalo ni matokeo ya FIKRA PEVU.,unaenda kukijaribu kipimo kama kinafanya kazi husika sehemu isiyohusika?
 
Tuelewane kwanza kuhusu "Zika". Hili neno chanzo chake ni msitu wa Zika ulioko Uganda na ni kutoka huko ambako virus anayesababisha aina fulani ya homa alikoanzia. Homa hii inayoitwa "homa ya Zika" ina dalili kama homa zingine lakini kama mwanamke mjamzito ataipata basi inaweza kumfikia mtoto aliye tumboni na hatimaye kuzaliwa na umbile la kichwa lisilo la kawaida kama ambavyo naamini wengi picha tumeziona.
Ugonjwa huu pia unaweza kuambukizwa kwa kujamiiana.
Ni muhimu basi kuelewa neno na matumizi yake na kwa sababu hiyo kutokana na nini mtu anaongelea basi anapaswa kusema aidha "virusi vya Zika" au "homa/ugonjwa wa Zika".
Ukisema tu "Zika" unazungumzia msitu ulioko Uganda.
Sasa utafiti unafanyika sehemu fulani baada ya kuona dalili au fununu za jambo fulani na kwa hiyo wataalamu na watafiti wanakwenda pale ili kuthibitisha uwepo wa hilo jambo au kutokuwepo kwake. Matokeo ya utafiti ndiyo yatasema kiwango cha kuwepo kwa hilo jambo kama lipo lakini pia yatapendekeza hatua zaidi sahihi za kuchukua.
 
Marekani inafanya utafiti wa Malaria lakini sijawahi kusikia kuna mgonjwa wa malaria huko. Pia kipindi cha Ebola walifanya utafiti kabla mgonjwa wa kwanza kutambulika aliingia na ebola marekani.
 
Back
Top Bottom