R.B
JF-Expert Member
- May 10, 2012
- 6,296
- 2,571
WANANCHI wa Kijiji cha Nganjoni Wilaya ya Moshi vijijini mkoani Kilimanjaro, wanalazimika kutembea umbali wa kilometa 35 kutafuta huduma ya afya. Wananchi hao wamekuwa wakitembea hadi katika Hospitali ya Kilema, iliyopo Marangu kutafuta huduma hiyo, kutokana na zahanati iliyopo kijijini hapa kutokuwa na dawa.
Mwenyekiti wa kijiji hicho, Salehe Zuberi alisema licha ya kuwapo kwa zahanati yenye daktari na wauguzi watatu iliyojengwa na wafadhili, lakini hakuna huduma yoyote.
Alisema wananchi wa kijiji hicho ambao ni zaidi ya 5,000 wanalazimika kutembea umbali mrefu na wengine kubebwa na machela, huku wajawazito wakijifungulia njiani kutokana na eneo hilo kuwa mbali na kituo cha afya.
Alisema kijiji hicho kinakabiliwa na changamoto mbalimbali na kuiomba Serikali kuangalia uwezekano wa kuwasaidia wananchi wa kijiji hicho kupata huduma za afya katika zahanati hiyo.
Alisema iwapo Serikali italeta huduma muhimu katika hospitali hiyo, kwa kiasi kikubwa itapunguza idadi ya vifo vya akina mama wajawazito na watoto katika kijiji hicho.
Kwa kweli hii hospitali uwepo wake tulifikiri tumepata msaada, lakini ni kinyume na matarajio ya wananchi wetu jambo ambalo linafanya wananchi kukosa imani na Serikali yao, alisema.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirikika la Kuwezesha Wanawake Kiuchumi mkoani Kilimanjaro (WEECE), Valeria Mrema, alisema matatizo mengi yanayokabili kijiji hicho yanatokana na wananchi kutoshirikishwa katika miradi ya maendeleo.
Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Ibrahimu Msengi ambaye alitembelea zahanati hiyo aliwaagiza watendaji wa kijiji hicho kuhakikisha wanakutana na wananchi, ili kutoa taarifa ya mapato na matumizi.
Mwenyekiti wa kijiji hicho, Salehe Zuberi alisema licha ya kuwapo kwa zahanati yenye daktari na wauguzi watatu iliyojengwa na wafadhili, lakini hakuna huduma yoyote.
Alisema wananchi wa kijiji hicho ambao ni zaidi ya 5,000 wanalazimika kutembea umbali mrefu na wengine kubebwa na machela, huku wajawazito wakijifungulia njiani kutokana na eneo hilo kuwa mbali na kituo cha afya.
Alisema kijiji hicho kinakabiliwa na changamoto mbalimbali na kuiomba Serikali kuangalia uwezekano wa kuwasaidia wananchi wa kijiji hicho kupata huduma za afya katika zahanati hiyo.
Alisema iwapo Serikali italeta huduma muhimu katika hospitali hiyo, kwa kiasi kikubwa itapunguza idadi ya vifo vya akina mama wajawazito na watoto katika kijiji hicho.
Kwa kweli hii hospitali uwepo wake tulifikiri tumepata msaada, lakini ni kinyume na matarajio ya wananchi wetu jambo ambalo linafanya wananchi kukosa imani na Serikali yao, alisema.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirikika la Kuwezesha Wanawake Kiuchumi mkoani Kilimanjaro (WEECE), Valeria Mrema, alisema matatizo mengi yanayokabili kijiji hicho yanatokana na wananchi kutoshirikishwa katika miradi ya maendeleo.
Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Ibrahimu Msengi ambaye alitembelea zahanati hiyo aliwaagiza watendaji wa kijiji hicho kuhakikisha wanakutana na wananchi, ili kutoa taarifa ya mapato na matumizi.