Kijichi, Dar: Maafisa feki wa TAKUKURU, wakishirikiana na Polisi wadaiwa kumbambikia Kesi ya Rushwa diwani

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,746
11,877
MADAI YA RUSHWA KWA DIWANI WA KIJICHI: MAAFISA WALIOHUSIKA SIO WA TAKUKURU

IMG_20200208_120732_112.jpg

Diwani wa Kijichi, Eliasa Kassim Mtarawanje

VIDEO:





Maafisa waliohusika katika video inayoonekana ikimhusisha Diwani wa Kijichi, Eliasa Kassim Mtarawanje (28) sio wa kutoka TAKUKURU. Baada ya kuwasiliana na mamlaka hiyo, imekiri kuwa na taarifa za tukio hilo lakini imesema maafisa wake hawajahusika katika tukio hilo.

Aidha, JamiiForums imefuatilia sakata hili na kubaini maafisa wawili wanaoonekana kwenye video hiyo ni kutoka Kituo cha Polisi Chang’ombe jijini Dar na askari waliohusika wametambulika kwa jina moja moja “Afande Jumanne” na “Afande Lugoma”.

KILICHOTOKEA
Chanzo chetu kimebaini kuwa chanzo ni mgogoro unaohusisha ardhi inayodaiwa kuwa ya Serikali ambapo mfanyabiashara mmoja wa eneo hilo, Shaaban Matimbwa almaarufu “Timbwa” anadaiwa kuhusika kwa kiasi kikubwa na imebainika watu wengine waliohusika katika tukio hili (wasiovaa sare) ni walinzi (mabaunsa) wa Timbwa.

Diwani Mtarawanje anadaiwa kupigwa na kuumizwa wakati wa tukio hilo kwa mujibu wa mashuhuda. Shuhuda wetu amemuona akiwa Hospitali ya Kijichi alikoenda kwa matibabu kufuatia majeraha kichwani na mdomoni ambapo jino lake limelegea

MGOGORO WA ARDHI
Inadaiwa kuna eneo ambalo Serikali imelitenga ajili ya ujenzi wa Stendi ya Mabasi ambapo taarifa zinaonyesha kuwa waliokuwa eneo hilo walishalipwa isipokuwa mtu mmoja aliyetambulika kwa jina moja “Mzee Mkumba” na Timbwa anadaiwa ‘kununua kesi’ ya eneo hili ili adai fidia ya takribani Sh. Milioni 700 toka serikalini. Eneo hilo ambalo inakadiriwa ni nusu ekari, linatambulika na Serikali ya Mtaa huo kuwa bado mmiliki wake (Mzee Mkumba) hajapewa fidia na kuwa suala hilo lipo hadi kwenye kumbukumbu za Halmashauri

Timbwa anadaiwa kujaribu ‘kuwaweka sawa’ watu wengi ili aweze kupata fedha hizo na tayari Diwani Mtarawanje aliripoti ofisi za TAKUKURU mnamo Februari 4, 2020 juu ya kinachoendelea kabla ya kuwekewa ‘tego’ tarehe 6 Februari 2020 (tukio linaloonekana kwenye video)

JamiiForums ilipomtafuta diwani huyo, alikiri kushawishiwa na Timbwa achukue kiasi cha fedha lakini akakataa na amesema ndiyo sababu alipoombwa na mwananchi huyo wa eneo lake (Timbwa) waonane, aliamua kwenda na Mwenyekiti wa CCM wa eneo lake ili yasiwepo mazingira ya rushwa. Simu ya Timbwa ilikuwa ikiita bila kupokelewa.

Diwani huyo ambaye alipatikana baada ya uchaguzi mdogo 2017 ni diwani wa 3 kuongoza kata hiyo tangu uchaguzi Mkuu wa 2015, ameiambia JamiiForums kuwa yeye anaviachia vyombo vya dola vifanye kazi lakini akaonyesha kusikitishwa na alivyotendewa na askari walioshiriki katika tukio hilo.
 
Diwani amepigwa akiwa wapi? Kituo cha polisi? Na kama aliumizwa amefungua kesi? Je ni kweli alichukua pesa? Je polisi wanaruhusiwa kukamata mchukua rushwa?
 
Waache wamalizane fisiem na rushwa ni sawana mgonjwa na uji mie ni jirani kabisa na eneo husika ila sikuwa nalifahamu hilo swala
 
Timbwa mmiliki wa Giraffe paleni Sudan temeke.

Ila jamaa anapenda kweli kununua kesi za ardhi
Atakuja kupata anachostahili.

Michael Wambura wa TFF alikua mmoja wa watu wanaopenda kesi sana,kitu kidogo tu kakimbilia mahakamani wakaona huyu asituchoshe kapigwa kesi ya utakatishaji fasta tu kakaa ndani karibu mwaka mzima,ametoka na kutakiwa kulipa Tsh.100mil.

Kamuulizeni sasa hivi kama kiherehere cha kupenda makesi kesi bado anacho,akiona mahakama anaipita kwa mbaali bila kugeuka.

dodge
 
Ila huyu dogo diwani naye anapenda kujiingiza katika ishu kama hizi. Anapenda sifa na kuonesha kuwa ana mamlaka kwa kila jambo. Anahusika sana kujenga mazingira ya kula rushwa na ubaguzi wa kisiasa kwa kuzuia maeneo au shughuli za kibiashara. Hicho kilichompata ni matokeo ya tabia zake za kujifanya yeye ndo kila kitu kwa wananchi wa Kijichi.
 
Ila huyu dogo diwani naye anapenda kujiingiza katika ishu kama hizi. Anapenda sifa na kuonesha kuwa ana mamlaka kwa kila jambo. Anahusika sana kujenga mazingira ya kula rushwa na ubaguzi wa kisiasa kwa kuzuia maeneo au shughuli za kibiashara. Hicho kilichompata ni matokeo ya tabia zake za kujifanya yeye ndo kila kitu kwa wananchi wa Kijichi.
Mbona unamhukumu kabla ushahidi haujakamilika. Kwa mujibu mtoa habari alikuwa anamtetea mpiga kura wake asidhulumiwe ndipo zengwe likaanza.
 
Atakuja kupata anachostahili.

Michael Wambura wa TFF alikua mmoja wa watu wanaopenda kesi sana,kitu kidogo tu kakimbilia mahakamani wakaona huyu asituchoshe kapigwa kesi ya utakatishaji fasta tu kakaa ndani karibu mwaka mzima,ametoka na kutakiwa kulipa Tsh.100mil.

Kamuulizeni sasa hivi kama kiherehere cha kupenda makesi kesi bado anacho,akiona mahakama anaipita kwa mbaali bila kugeuka.

dodge
Kabisa mkuu.

Anapenda kununua nyumba,ardhi zinahusiana na kesi bwana Timbww
 
Mbona unamhukumu kabla ushahidi haujakamilika. Kwa mujibu mtoa habari alikuwa anamtetea mpiga kura wake asidhulumiwe ndipo zengwe likaanza.
Sijamhukumu bali nimemuelezea kutokana na ninavyomfahamu. Lakini kwanini mtoa mada anatetea diwani hana makosa kabla ya vyombo husika hawaja-rule out kama amehusika kweli au la kama anavyosema mwenyewe diwani kuwa anawaachia vyombo husika wafanye kazi yao (kubainisha ukweli)?
 
Sijamhukumu bali nimemuelezea kutokana na ninavyomfahamu. Lakini kwanini mtoa mada anatetea diwani hana makosa kabla ya vyombo husika hawaja-rule out kama amehusika kweli au la kama anavyosema mwenyewe diwani kuwa anawaachia vyombo husika wafanye kazi yao (kubainisha ukweli)?
Wote tusubili vyombo vya dola vifanye kazi.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom