Kipenseli
JF-Expert Member
- Feb 9, 2020
- 800
- 1,050
- Thread starter
- #61
Nimekuelewa SanaKijana wa kisasa anatakiwa awe na yafuatayo.
1 Timotheo 4:12
"Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi."
Hapa (1Tim4:12) Mt.Paulo anatufundisha vijana Tuwe KIELELEZO katika USEMI (Kijana unapaswa kuwa na kauli njema, yenye kuvutia na Kumpendeza Mungu.. sio mijitusi, mala kuwa na kauli za kishetani, sio kusema Uongo, mara kauli za kuusifia uzinzi na ulevi hapana, Kauli yako kijana iwe Safi kwa Lugha ya staha), Lakini pia Kijana anatakiwa awe KIELELEZO katika MWENENDO (Mtindo wa maisha ya kijana kwanza Uwe wenye Kumpendeza Mungu, na kisha umvutie mwanadamu, uwe Mwema, Mpole, Mwenye Kiasi, Mpenda Haki n.k sio Mzinzi, Mlevi, Mchawi, Mgomvi, n.k), Lakini pia awe mwenye UPENDO (kwa watu wote), IMANI (Mungu pekee ndiye chanzo cha uhai na mafanikio ya haki, Mtafute Sana Mungu na Uyashike Maagizo yake), Mwisho kijana awe na USAFI (Kijana lazima awe safi Rohoni, Mwilini na Kwenye Fikra zake - Pureness)
Mengine yote ni ubatili.