Kijana usije Dar es aalaam kabla hujahakikisha unakuja kufanya nini, huku watu wanaishi maisha ya umaskini uliokithiri.

Acha kutisha watu. Kila mtu ana baraka zake hata kwa hapo Dsm, tatizo umekariri kwamba Dsm ni shida tupu unasahau fursa nyingi za maisha zipo hapo Dsm pia.

Acha waje kila mtu atapambana kivyake.
Habari za asibuhi!
Napenda kuwaasa vijana wenzangu kuwa Dar es salaam si mahali pa kusaka maisha kichwa kichwa, kwamba utafute nauli tu na kusema unakuja dar kwa mjomba, Dada, kaka, rafiki n.k kutafuta maisha.
Huku wengi ni wapangaji, tena wamepanga kwenye mazingira hatarishi(machafu), wengi hugombania daladala, jioni mkitoka kazini hubanana kwenye magari kama ng'ombe wanapelekwa mnadani.
Wengi ni vibarua, watumwa wa Wahindi na Wachina. Wengi hulipwa 100,000- 150,000 tshs. Wengine laki na nusu -laki tatu, hao ndo huonekana wana unafuu.
Wengi hula Milo 2 tu kwa siku.
Msivutiwe na picha wanazopost fb, Dar nguo ni kama bure, wengi hununua sabufa, sofa siti 2 au 3 tu na TV hapo ndo anasema kayapatia.
Ni heri ukomae huko home, ujenge hata kibanda chako. Huku utageuzwa mtumwa, ndugu wengi wana roho mbaya, hii sijui inasababishwa na nini?
Kazi ambayo ni rahisi kuipata Dar ni ulinzi, kazi ambayo ni ya kinyonyaji na hatarishi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maisha ya dar ya ajabu ajabu sana
Unakuta mtu anashindia mihoga na kachumbari ilio wekwa pilipili nyingi hapo mchana kutwa anashindia maji ya kandoro
Halafu yuko mtaani anacheza dafti na kubeti
 
Miye mjomba wangu yangu aje mjini mpaka leo anakaa gheto, maisha yake ya ujanja ujanja tu miwani mikubwa kanyoa panki kuchomekea na kuvaa macheni shingoni na Pete tangu tupo darasa la kwanza mjomba maisha yake ya ujanja ujanja tu mpaka tunamaliza shule mjomba bado anamtegemea Dada yake mama yetu kiufupi simuelewagi uncle

Uncle kuoa ataki, kurudi shamba tanga ataki yani yeye usela tu kakomaa nao mjini

Dah! Ni Noma Sana Mkuu,, Yaani Wako Rais Wengi Tu Wenye Life La Hivo,, Kama Huwajui Unawezasema Bonge Latu Wa Maana,, Kumbe Chenga Tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Miye mjomba wangu yangu aje mjini mpaka leo anakaa gheto, maisha yake ya ujanja ujanja tu miwani mikubwa kanyoa panki kuchomekea na kuvaa macheni shingoni na Pete tangu tupo darasa la kwanza mjomba maisha yake ya ujanja ujanja tu mpaka tunamaliza shule mjomba bado anamtegemea Dada yake mama yetu kiufupi simuelewagi uncle

Uncle kuoa ataki, kurudi shamba tanga ataki yani yeye usela tu kakomaa nao mjini
Nimevuta picha jins mjomba wako alivo. Atakua anafanana na wale wenyeji wa manzese pale mda wote mapete vidoleni,machen shngon na bagharashia kichwani
 
Dar ni jiji la gharama, na mabahili wamejaa huko mazee! Mutu mpaka akukaribishe ujue amepigika.
 
Kuna mwimbo unaimba 'wacha kupiga mayowe weeee wacha wayaone wenyewe weee' Dar kuna jamii ya watu wengi inaishi maisha mabaya sana sio magumu ni mabaya ukianzia makazi hadi chakula wanachokila ambacho mwisho wa siku kinawaletea madhara makubwa ya kiafya
 
Dar es salaam in chid benz voice.
Waganga njaa tupo wengi kuliko waliotoboa na tunajipa matumaini usikimbie mjini ndio fursa zipo nnchini hapa na ukipata connection moja matata umetoboa.
 
35 Reactions
Reply
Back
Top Bottom