Kijana unayeanza maisha usinunue pikipiki kama usafiri wako, utaondoka mapema

SISIS

JF-Expert Member
Jan 14, 2019
10,671
2,028
Leo nimetoka kumzika rafiki yangu kipenzi, alifariki juzi kwa ajali ya pikipiki ametoka kuinunua juzi tu hapo ni kama usafiri wa kuanzia katika safari yake ya maisha maana ndivyo alivyosema kipindi anaplan za kuinunua, huyu ni mtu wangu wa karibu wa 9 namzika mean marafiki wa karibu, bado ndugu 4 niliowazika ndani ya miaka 3 tu kwa ajali za pikipiki.

Kifo kipo popote ila pikipiki zinamaliza watu sana, yaani ni heri ukajenge au ujichange ukanunue gari lakini sio pikipiki, kwa nchi yetu hii unaweza ukawa ni dereva mzuri wa pikipiki ila ukashangaa unakuja kuuliwa na madereva wa magari makubwa hata madogo wasiofuata sheria.

Ni ushauri wangu tu.
 
Bonge la ushauri sana sijui hii jamiii ingekuelewaa. Mimi hakuna chombo cha usafiri hakini vutii kama toyo ni bora niingie gharama za uber..

ikitokea napanda huwa nasali Sana maana ajali nilizozishudia na kusikia huwa zinanitia hofu nimepoteza ndugu na marafiki na vijana kama Mimi wengi sana kisa hili pepo bodaboda.
 
Mkuu umeongea point. Mimi mwenyewe niliplan kununua gari, nilipoanza kuendesha la rafiki yangu nikaponea ajali ya semi trela, haki ya Mungu.

Niligeuza mawazo faster nikaachana na mpango wa gari hiyo pesa nikajengea nyumba kwasababu niliona kama nanunua kaburi la kuzikiwa mapema, kweli kijana tuna changamoto katika kununua chombo cha usafiri tungali bado wadogo.

Hadi leo ni miaka karibu 12 sina hamu wala sitamani kuendesha gari. Bora nikodishe tax na siku nikinunua gari nitaendeshwa tu. Mungu atupiganie.
 
Dah, hii ina ka ukweli, mwaka 2018 nimempoteza rafiki yangu anaitwa Erick, jamaa alikua alimaliza IFM pale akaanza harakati za maisha, alikua hard worker kweli kweli maana alikua anafanya kazi mbili ndani ya masaa 24 kupumzika ni Jumapili tu.

Ndani ya mwaka alikua yupo kwenye aina fulani ya maisha ya kati, maana alikua anamiliki baiskeli kwa ajili ya misele ya mjini na aliapa hataki kabisa chombo cha Moto cha kuitwa pikipiki lakini mafanikio ya kati yakampelekea abadili mawazo.

Akanunua bonge la pikipiki, yale manene manene yani miguu haikanyagi wala kufika chini, ndio akawa anafanyia misele ya mjini. Bhana bhana weeee from nowhere akapata wazo aende Morogoro, huko ndio home kwa wazazi wake. Dah ndio ukawa mwisho wa uhai wake maana lile pikipiki lilimchana mabandama yote, lenyewe hata mchubuko halikupata.
 
Mwaka wa 5 huu ndIo usafiri naoutegemea...

WP_20150601_11_23_09_Pro.jpg
 
Back
Top Bottom