Kijana miaka 38 amempenda mwanamke wa miaka 44 leta maoni ya busara



Mimi inaniumiza japo sikumwambia maana kama mwanamke ana miaka 44 je wataweza kuzaa hata mtoto mmoja wa kuwaunganisha? Ila nilimwambia anipe wiki moja kuanzia jana nitampa ushauri anaoutaka barabara. Ninajua JF ni kisima cha mawazo, kuna weledi wa mambo hapa. Ninawaomba sana changia mada hii kwa ukweli na busara maana ni kitu cha ukweli si cha kufikirika ili nipate mawazo yako nipate kumshauri kijana ipasavyo. Asante sana na karibu kwa maoni na ushauri. Mimi Zogwale.

Maadamu wanaelewana hilo ndo jambo la msingi, ndugu yako tayari ana mtoto so siyo lazima wazae na huyo mwanamke, mtoto ni majaaliwa toka kwa Mwenyezi Mungu huenda akaoa hata mwanamke ambaye hajafika menopause na asipate mtoto vile vile (God forbid).
 
oa tu, kuzaa majaliwa, siku hizi kuna mbinu nyingi za kumfanya mwanake aendelee kufeel-tena kinatural siyo mambo ya kizungu, oa tu, we unafikiri atajisikiaje huyo mama ukimdelete mhh sio fresh mradi anampenda basi, ndoa ni kuheshimiana, kujaliana, kusikilizana ndo mambo yote mradi kusiwe na udikteta baina yao, i hope mambo yataenda muruaa, all the best kwa nduguyo... tusikose kualikana
 
As longer unayarudi mavitu poa tu .uwe na pesa maana Kama huna utaitwa gold digger
 
Haswaaa!
Kujadili umri katika mahusiano kuna tija tu kama kuna mwenye umri mdogo sana.

Ukishavuka miaka 35 basi ule ujana wa kufanya watu wakutetee unapotea. Hii ni kwa wote wanawake na wanaume.

35+ na bado mtu yuko single, ina maana analijua analolifanya katika maisha yake.Kama ni kupitia mahusiano basi mhusika atakua ameshapitia vya kutosha na kuelewa karibu kila kitu. Hamna kipya kikubwa sana cha kujifunza.Kwa mantiki hiyo, mwanaume 38 na mwanamke kwenye 40s ni hiari yao na hakuna la ajabu. Waachwe wajiamulie maisha yao.
Asante sana mkuu. Hata mimi kwa mbali jana nilimwambia kuwa umeshavuka 35 sasa unataka nikuambie kitu gani? Hakuwa na jibu la maana sana. Nafikiri anataka tu nimuunge mkono kwa kumpa pro and cons na atakapoleta issue mbele ya wazee nimpe sapoti. Yeye kijana tayari ana mtoto wa miaka 6 ba mwanamke ana mtoto wa miaka 12.
 
NIngependa kujua kama huyo mama yeye alishawahi kuolewa,ana mtoto au hajawahi kuolewa na hana mtoto.kama alikwisha kwa nn aliachana na mume wake wa kwanza na kama hajawahi kwa nn mpaka anatimiza 44? ni mambo ya msingi kuyaangalia ayo nayo.
Asante mkuu wabukoba. Kijana ana mtoto wa miaka 6 alizaa na mwanamke ila hawakufunga ndoa na alishamchukua wiku nyingi yuko na wazazi wa kijana. Mwanamke naye ana mtoto wa miaka 12 alizaa ila hawakufunga ndoa na jamaa kwa sababu anazosema huyo kijana kuwa ni kosa la yule bwana maana inasemekana alishaoa wanawake kama wanne na walishaachana. kwa hiyo anaona huyu mama ni fiti kwake na hata tatizo.
 
oa tu, kuzaa majaliwa, siku hizi kuna mbinu nyingi za kumfanya mwanake aendelee kufeel-tena kinatural siyo mambo ya kizungu, oa tu, we unafikiri atajisikiaje huyo mama ukimdelete mhh sio fresh mradi anampenda basi, ndoa ni kuheshimiana, kujaliana, kusikilizana ndo mambo yote mradi kusiwe na udikteta baina yao, i hope mambo yataenda muruaa, all the best kwa nduguyo... tusikose kualikana

Asante sana mkuu mama dunia, ujumbe umefika na nitakusanya yote yaliyosemwa hapa pamoja na yangu nitampa live. Atachekecha maana above 35 ni mtu mzima mno.
 
Kama ulikuwa unalisikia limbwata ndio hilo amelishwa ndugu yako. 38 kwa 44 wapi na wapi? tuache kudanganyana hapa, wanawake wamejaa kibao huyo anapaswa kuoa mwanamke wa miaka 30 mpaka 35 mwisho. ushauri mwingine ni porojo tu hapa.
 
Zogwale, hapo ni heshima tu itawale umri haumati wamependana waacheni miaka nne tu,hy kaka nae pungu hy ilikuwa iwe siri yake binafc c kutangaza. Hayo tu.tupe kadi
Asante kwa ushauri mkuu Iwako. Ila sasa kwa umri wa miaka 6 wamepishana mwanamke si ataonekana pia. Jua wanawake wanaonesha umri zaidi kuliko wanaume. Anyway, ushari nimepoke na wengine wataendelea kunipatia ushauri na nitamweleza baada ya hizo siku saba nilizomwahidi. Mengine ataamua mwenyewe tu maana wote soon watakuwa 40s tu.
 
Kwa kweli hiyo ni very sensitive issue hasa kwa desturi zetu..Kwa wazungu sometimes huwa inakuwa kawaida..Cha msingi ni wao wenyewe kama wana amani moyoni.Mimi nilishawahi kuvunja mahusiano kama hayo kwa kuwa nilikuwa najihisi(nilijikataa mwenyewe) kuhusiana na hii issue ya age..Sikuwa na amani japo kijana alikuwa yupo ok...
Labda muulize kama huyo nduguyo ana amani..Hiyo itamsaidia badae kuhimili vishindo kwa kuwa lazima watakumbana na opposition kutoka kwa ndugu na marafiki.. Japo baadae itakuwa jambo la kawaida
Pia katika suala hili inategemea sana muonekano/mwili wa huyo mwanamke...wengine huwa hawazeeki na wanaonekana wasichana tu.. Hii pia itawasaidia kuongeza ujasiri wao....

Wao kama wao kijana anasema wana amani na wanapendana. Anayetaka kupata ok ni mwanamke maana naye naona kidogo anasita kama wewe ulivyosita. Hataki mambo ya kunyanyapaliwa umri. Ila tu kwa ninavyomfahamu huyu kijana wetu ni mtu ametulia sana maana hata kisa cha kumuacha mwanamke aliyezaa naye ni tabia ambazo hata sisi wenyewe tuliona hawatakuwa na maisha. Kijana alisikitishwa sana na tabia zile kiasi kwamba alisema hataki kuoa tena hadi hapo atakapoamua na atatunza mtoto wake. Na kweli alimchukua mtoto akiwa mdogo na amemlea mwenyewe akishirikiana na mama yake mzazi. Ni kijana mtulivu kwa hakika. Hata aliponiambia anataka kuoa nilishtuka kidogo maana alishaona kama wanawake wana usumbufu kiasi. Nikawa namtia sana moyo kuwa si wote na siku moja utampata wa kukufaa. Huenda ndiyo huyu, tuombe uzima na nitawapa matokeo yake.
 
Mh, kwa kweli hapo pagumu kutoa ushauri, ila kwa vile umri hawajapishana sana wanaweza kuoana mradi wapendane tu, ila mwanamke anakaribia menopause sa sijui huwa inakuwaje mwanamke anapofikia iyo kitu na kama mjuavyo ng'ombe hazeeki maini (hasa ng'ombe dume), teh teh
 
Kama ulikuwa unalisikia limbwata ndio hilo amelishwa ndugu yako. 38 kwa 44 wapi na wapi? tuache kudanganyana hapa, wanawake wamejaa kibao huyo anapaswa kuoa mwanamke wa miaka 30 mpaka 35 mwisho. ushauri mwingine ni porojo tu hapa.
Asante kwa mtizamo wako mkuu. Hapo kwenye red panahusika. Ni kwamba huyu mwanamke wala halazimishi kuolewa na huyu ndugu yangu. Kijana alisema wazi kuwa huyu mwanamke alikataa kabisa kuolewa na underage japo upendo upo. Na kwa hili alimtaka kijana aje kwanza kwa ndugu awaeleze ili apate ridhaa na kijana anasema kabisa kama majibu yatakuwa too negative na akimwambia mwanamke hatakubali kuolewa. Kijana yuko tayari, amempenda kweli. Jua si kila mwanamke anatumia tunguli kuwapata wanaume. Kuna wanawake wametulia sana pia. Kwa historia ya huyu mama ni kwamba alishapata mchumba awali na katika mahusiano wakazaa ila baadaye mwanaume yule akawa si muoaji kivile. Mwishowe alimwacha akalea mtoto wake wa miaka 12 sasa. Yule mwanaume ameshaoa wanawake 4 na wameshaondoka. Mwanamke huyu alitulia tu na hakutaka kuolewa tena zaidi ya kumlea mtoto na kumsomesha. Naona hawa wana historia sawa, na inaweza kuwafanya waishi ndoa njema. Ngoja tuone wengine nao wanasema nini.
 
Mh, kwa kweli hapo pagumu kutoa ushauri, ila kwa vile umri hawajapishana sana wanaweza kuoana mradi wapendane tu, ila mwanamke anakaribia menopause sa sijui huwa inakuwaje mwanamke anapofikia iyo kitu na kama mjuavyo ng'ombe hazeeki maini (hasa ng'ombe dume), teh teh
Kwa nini mnapenda kudanganyana? kuna faida gani ya kuoa mwanamke ambaye miaka mitatu mpaka mitano atakuwa anaogopa hata kumtambulisha kwamba ni mke wake?
 
Mh, kwa kweli hapo pagumu kutoa ushauri, ila kwa vile umri hawajapishana sana wanaweza kuoana mradi wapendane tu, ila mwanamke anakaribia menopause sa sijui huwa inakuwaje mwanamke anapofikia iyo kitu na kama mjuavyo ng'ombe hazeeki maini (hasa ng'ombe dume), teh teh

Huwa hapo nami ni kizungu mkuti ila ninafikiri kwa suala hilo liko kwa jinsi mtu anautunza mwili wake na afya pia. Kuna wanawake 50+ lakini kwa suala la tendo la ndoa humpati, anakugalagaza hadi unakoma ubishi. Wengine under 30s even 20s but ni hovyo kabisa kitandani, tena ni wachovu haswa. Sasa hapo mtihani upo. Wajuzi changieni hili la menopouse.
 
Asante kwa mtizamo wako mkuu. Hapo kwenye red panahusika. Ni kwamba huyu mwanamke wala halazimishi kuolewa na huyu ndugu yangu. Kijana alisema wazi kuwa huyu mwanamke alikataa kabisa kuolewa na underage japo upendo upo. Na kwa hili alimtaka kijana aje kwanza kwa ndugu awaeleze ili apate ridhaa na kijana anasema kabisa kama majibu yatakuwa too negative na akimwambia mwanamke hatakubali kuolewa. Kijana yuko tayari, amempenda kweli. Jua si kila mwanamke anatumia tunguli kuwapata wanaume. Kuna wanawake wametulia sana pia. Kwa historia ya huyu mama ni kwamba alishapata mchumba awali na katika mahusiano wakazaa ila baadaye mwanaume yule akawa si muoaji kivile. Mwishowe alimwacha akalea mtoto wake wa miaka 12 sasa. Yule mwanaume ameshaoa wanawake 4 na wameshaondoka. Mwanamke huyu alitulia tu na hakutaka kuolewa tena zaidi ya kumlea mtoto na kumsomesha. Naona hawa wana historia sawa, na inaweza kuwafanya waishi ndoa njema. Ngoja tuone wengine nao wanasema nini.
Hizi ni excuse ambazo ni total non sense, wapo wanaume wenye umri wa miaka 47 mpaka 50 ambao nao wana same status kama yeye na wanahitaji wenza mungu atampatia wake, hapo ni kulazimisha mambo hakuna kitu cha namna hiyo tuache kudanganyana.
 
Ni vigumu kujua sababu na mambo ambayo yamemvutia kaka yako kwa huyo mkongwe wa miaka 44, pia ukichunguza hata kaka yako ana umri mkubwa na gap iliyo kati yao ni miaka sita tu ambayo sioni kama ina tatizo. Usikute huyo mwanamke naye ana mtoto wake au watoto wake na akifanikiwa kuolewa na kaka yako basi wataunganisha familia na watoto wao pamoja so issue ya kuzaa si muhimu la umuhimu ni furaha zao tuu.

Muache kaka yako apate furaha na aenjoy maisha yake yaliyobaki.
 
Huwa hapo nami ni kizungu mkuti ila ninafikiri kwa suala hilo liko kwa jinsi mtu anautunza mwili wake na afya pia. Kuna wanawake 50+ lakini kwa suala la tendo la ndoa humpati, anakugalagaza hadi unakoma ubishi. Wengine under 30s even 20s but ni hovyo kabisa kitandani, tena ni wachovu haswa. Sasa hapo mtihani upo. Wajuzi changieni hili la menopouse.
Aisee wewe jamaa elewa mke si kwa ajili ya kumgalagaza tu, mke ni zaidi ya ngono, na kuna watu wanaowana na hawahitaji watoto. pamoja na sifa zote mke ni lazima muendane mnapokwenda sehemu na siyo yeye anaamkiwa na wewe unaambiwa mambo vipi!
 
Kwa nini mnapenda kudanganyana? kuna faida gani ya kuoa mwanamke ambaye miaka mitatu mpaka mitano atakuwa anaogopa hata kumtambulisha kwamba ni mke wake?

Sasa mkuu mtu keshapenda, na mie na wewe hatujua kapenda nini kwa uyu mzee mwenzie!Ila mkuu wapo wamama ambao wako aged lakini wanalipa kuliko hata vijana wenu hao wadogo!My bro kaoa mwanamke mtu mzima kama yeye ila ukiwaona huwezi jua yule mama ni mtu mzima! Sio wanawake wote aged wako vibaya
 
Sasa mkuu mtu keshapenda, na mie na wewe hatujua kapenda nini kwa uyu mzee mwenzie!Ila mkuu wapo wamama ambao wako aged lakini wanalipa kuliko hata vijana wenu hao wadogo!My bro kaoa mwanamke mtu mzima kama yeye ila ukiwaona huwezi jua yule mama ni mtu mzima! Sio wanawake wote aged wako vibaya
Tuache kudanganyana huyu unayemuona hapa haonekani mzee si kwa sababu ni Mmarekani bali kwa sababu ni Millionaire, pesa yake ndio inamfanya aendelee kuonekana wamo na alifanyiwa surgery ya hips.

45921-OprahWinfrey3.jpg
 
Back
Top Bottom