Balantanda
JF-Expert Member
- Jul 13, 2008
- 12,476
- 4,754
Na Sadick Mtulya
MWANASIASA kijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Katibu wa chama hicho, wilayani Tarime mkoani Mara, Livingstone Lusinde amesema mwanasiasa mkongwe nchini, John Malecela (75) ni mwenye siasa za chuki na pia amemsihi asigombee tena ubunge katika jimbo hilo.
Lusinde alisema kauli ambazo Malecela aliitoa jana, inaashiria kwamba anazeeka vibaya na atamaliza vibaya.
Lusinde ambaye ametoka kijiji cha Mvumi ambako Malecela pia anatoka, alimtuhumu Malecela kwamba ni mbinafsi na kwamba siku zote maneno na ahadi anazotoa si za kweli.
Lusinde alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam mbele ya waandishi wa habari wakati akitangaza nia yake ya kugombea ubunge kupitia CCM katika jimbo hilo.
Kutokana na uchovu wa kushindwa kushawishi na siasa za chuki alizokuwa nazo mzee Malecela, uchu wa madaraka usiokuwa na kikomo pamoja na kugeuzwa na watu kumi kama taasisi ya Deci, amesababisha maendeleo duni katika Jimbo la Mtera mkoani Dodoma.
"Pia pamoja na kuwa amewahi kuwa msaidizi wa DC, Mkuu wa Mkoa, Balozi kwenye Umoja wa Mataifa na Uingereza, Waziri wa Kilimo, Mambo ya Nchi za Nje, Waziri Mkuu na Makamu wa kwanza wa Rais, Makamu Mwenyekiti wa CCM bara na Mbunge wa Jimbo la Mtera tangu lilipoanzishwa, amekuwa ni mbinafsi na kwamba siku zote maneno na ahadi anazotoa si za kweli,"alisema Lusinde.
Lusinde alifafanua kwamba ameamua kutoa kauli hiyo, kwa kuwa Malecela alikiuka makubaliano waliyoafikiana mwaka 2005 kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu kwamba mwaka huu Malecela, angeachiwa kugombea jimbo hilo.
"Pamoja na Malecela kunilea kisiasa, miaka mitano iliyopita aliniahidi kwamba hatogombea mwaka 2010 katika Jimbo la Mtera, na sio tu kugombea Mzee Malecela alifika mbali zaidi kwa kunibariki kwamba nitakuwa mbunge wa Mtera ninayemfuata yeye.
"Lakini amebadilika na kwenda kinyume na maneno pamoja na ahadi zake. Tayari ametangaza nia yake ya kugombea tena katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu," alisema
Lusinde ambaye pia amewahi kuwa katibu wa CCM Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma alisema katika mwaka 2005, ilipofika wakati wa mchakato wa kuteuliwa na CCM kwa ajili ya kugombea Ubunge, Malecela alimuomba ajiondoe katika kinyanganyiro hicho na akakubali kutokana makubaliano maalumu waliyowekeana mbele ya mashahidi.
"Keneth Salali ni mmoja wa mashahidi walikuwepo wakati mzee Malecela aliponiomba nijiondoe katika kinyanganyiro cha kuteuliwa na chama na aliniahidi kuwa mwaka 2010 hatogombea tena.
"Namsihi Mzee Malecela aache mara moja mpango wake wa kugombea ubunge Jimbo la Mtera,"alisema Lusinde
Hata hivyo, Lusinde hakuwa tayari kuyataja majina ya watu ambao anadai kuwa wamemgeuza Malecela kama taasisi ya Deci kwa kupanda na kumvuna.
Lakini alisema watu hao ni wanachama wa CCM na mmoja wao aliwahi kuwa mlinzi wa Malecela kabla hajaumia.
"Hawa watu kumi waliomgeuza Malecela kama DECI wapo kwa maslahi yao binafsi na muda ukifika kila mmoja nitawataja," alisema.
Gazeti hili lilipomtafuta Malecela, liliambiwa kuwa yupo nchini Uingereza kwa kushughuli za kichama.
Source: Gazeti la Mwananchi
My Take:
Naona kazi imeanza sasa Mtera,huyu kijana(Lusinde) ni mwanasiasa machachari hasa,nakumbuka mwaka 2005 alimuumiza kichwa sana mzee Malecela kiasi kwamba wakafikia makubaliano kwamba asubiri mwaka huu wa 2010,kijana alikubali hasa baada ya kupewa kazi ya kuwa Katibu msaidiz wa CCM wa wilaya ya Kongwa-Dodoma(Ikumbukwe kwamba kabla ya hapo alikuwa ni mwanachama wa NLD na mwaka huo wa 2005 alitaka kugombea kwa tiketi ya NLD na alikuwa tishio kiasi kwamba mzee Malecela hakuwa na la kufanya zaidi ya kumuomba ajitoe na pia kumshawishi ajiunge na CCM kisha akapewa nafasi hiyo ya Katibu msaidizi wa CCM(W).
Binafsi Lusinde ni mtu wangu wa karibu sana na ni mwanasiasa mzuri hasa(CCM wanamtumia sana kwenye kampeni zao),wakati wa uchaguzi mdogo wa jimbo la Tunduru Lusinde alitumika ipasavyo katika kampeni kiasi cha kupelekea mgombea wa CCM ndugu Mtutula kushinda,baada ya hapo Lusinde alipandishwa cheo na kuwa Katibu wa CCM wa wilaya ya Tunduru,kisha baadaye akahamishiwa Tarime aliko sasa...Kijana ana kipaji hasa kwenye siasa za kuongea/kujieleza...Mzee Malecela inabidi ajizatiti hasa kama kweli kaamua kugombea maana Lusinde anawezambwaga(endapo hakutatokea mizengwe ndani ya CCM
Pia kuna jamaa mwingine anaitwa Laurent Hoya(mmiliki wa mabasi ya Mshikamano na mabucha ya kisasa ya Mshikamano),huyu naye anakubalika sana Mtera na Mvumi,naye nasikia ana mpango wa kugombea ubunge wa Mtera na juzjuzi tu hapa kapewa Ukamanda wa vijana wilaya ya Chamwino...Kazi ipo Mtera mwaka huu,tusubiri na tuone
MWANASIASA kijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Katibu wa chama hicho, wilayani Tarime mkoani Mara, Livingstone Lusinde amesema mwanasiasa mkongwe nchini, John Malecela (75) ni mwenye siasa za chuki na pia amemsihi asigombee tena ubunge katika jimbo hilo.
Lusinde alisema kauli ambazo Malecela aliitoa jana, inaashiria kwamba anazeeka vibaya na atamaliza vibaya.
Lusinde ambaye ametoka kijiji cha Mvumi ambako Malecela pia anatoka, alimtuhumu Malecela kwamba ni mbinafsi na kwamba siku zote maneno na ahadi anazotoa si za kweli.
Lusinde alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam mbele ya waandishi wa habari wakati akitangaza nia yake ya kugombea ubunge kupitia CCM katika jimbo hilo.
Kutokana na uchovu wa kushindwa kushawishi na siasa za chuki alizokuwa nazo mzee Malecela, uchu wa madaraka usiokuwa na kikomo pamoja na kugeuzwa na watu kumi kama taasisi ya Deci, amesababisha maendeleo duni katika Jimbo la Mtera mkoani Dodoma.
"Pia pamoja na kuwa amewahi kuwa msaidizi wa DC, Mkuu wa Mkoa, Balozi kwenye Umoja wa Mataifa na Uingereza, Waziri wa Kilimo, Mambo ya Nchi za Nje, Waziri Mkuu na Makamu wa kwanza wa Rais, Makamu Mwenyekiti wa CCM bara na Mbunge wa Jimbo la Mtera tangu lilipoanzishwa, amekuwa ni mbinafsi na kwamba siku zote maneno na ahadi anazotoa si za kweli,"alisema Lusinde.
Lusinde alifafanua kwamba ameamua kutoa kauli hiyo, kwa kuwa Malecela alikiuka makubaliano waliyoafikiana mwaka 2005 kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu kwamba mwaka huu Malecela, angeachiwa kugombea jimbo hilo.
"Pamoja na Malecela kunilea kisiasa, miaka mitano iliyopita aliniahidi kwamba hatogombea mwaka 2010 katika Jimbo la Mtera, na sio tu kugombea Mzee Malecela alifika mbali zaidi kwa kunibariki kwamba nitakuwa mbunge wa Mtera ninayemfuata yeye.
"Lakini amebadilika na kwenda kinyume na maneno pamoja na ahadi zake. Tayari ametangaza nia yake ya kugombea tena katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu," alisema
Lusinde ambaye pia amewahi kuwa katibu wa CCM Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma alisema katika mwaka 2005, ilipofika wakati wa mchakato wa kuteuliwa na CCM kwa ajili ya kugombea Ubunge, Malecela alimuomba ajiondoe katika kinyanganyiro hicho na akakubali kutokana makubaliano maalumu waliyowekeana mbele ya mashahidi.
"Keneth Salali ni mmoja wa mashahidi walikuwepo wakati mzee Malecela aliponiomba nijiondoe katika kinyanganyiro cha kuteuliwa na chama na aliniahidi kuwa mwaka 2010 hatogombea tena.
"Namsihi Mzee Malecela aache mara moja mpango wake wa kugombea ubunge Jimbo la Mtera,"alisema Lusinde
Hata hivyo, Lusinde hakuwa tayari kuyataja majina ya watu ambao anadai kuwa wamemgeuza Malecela kama taasisi ya Deci kwa kupanda na kumvuna.
Lakini alisema watu hao ni wanachama wa CCM na mmoja wao aliwahi kuwa mlinzi wa Malecela kabla hajaumia.
"Hawa watu kumi waliomgeuza Malecela kama DECI wapo kwa maslahi yao binafsi na muda ukifika kila mmoja nitawataja," alisema.
Gazeti hili lilipomtafuta Malecela, liliambiwa kuwa yupo nchini Uingereza kwa kushughuli za kichama.
Source: Gazeti la Mwananchi
My Take:
Naona kazi imeanza sasa Mtera,huyu kijana(Lusinde) ni mwanasiasa machachari hasa,nakumbuka mwaka 2005 alimuumiza kichwa sana mzee Malecela kiasi kwamba wakafikia makubaliano kwamba asubiri mwaka huu wa 2010,kijana alikubali hasa baada ya kupewa kazi ya kuwa Katibu msaidiz wa CCM wa wilaya ya Kongwa-Dodoma(Ikumbukwe kwamba kabla ya hapo alikuwa ni mwanachama wa NLD na mwaka huo wa 2005 alitaka kugombea kwa tiketi ya NLD na alikuwa tishio kiasi kwamba mzee Malecela hakuwa na la kufanya zaidi ya kumuomba ajitoe na pia kumshawishi ajiunge na CCM kisha akapewa nafasi hiyo ya Katibu msaidizi wa CCM(W).
Binafsi Lusinde ni mtu wangu wa karibu sana na ni mwanasiasa mzuri hasa(CCM wanamtumia sana kwenye kampeni zao),wakati wa uchaguzi mdogo wa jimbo la Tunduru Lusinde alitumika ipasavyo katika kampeni kiasi cha kupelekea mgombea wa CCM ndugu Mtutula kushinda,baada ya hapo Lusinde alipandishwa cheo na kuwa Katibu wa CCM wa wilaya ya Tunduru,kisha baadaye akahamishiwa Tarime aliko sasa...Kijana ana kipaji hasa kwenye siasa za kuongea/kujieleza...Mzee Malecela inabidi ajizatiti hasa kama kweli kaamua kugombea maana Lusinde anawezambwaga(endapo hakutatokea mizengwe ndani ya CCM
Pia kuna jamaa mwingine anaitwa Laurent Hoya(mmiliki wa mabasi ya Mshikamano na mabucha ya kisasa ya Mshikamano),huyu naye anakubalika sana Mtera na Mvumi,naye nasikia ana mpango wa kugombea ubunge wa Mtera na juzjuzi tu hapa kapewa Ukamanda wa vijana wilaya ya Chamwino...Kazi ipo Mtera mwaka huu,tusubiri na tuone