King Octavian
JF-Expert Member
- Oct 1, 2011
- 403
- 349
Hili tukio limetokea huko mkoani Rukwa, manispaa ya Sumbawanga, stori inaanza hivi.
Inadaiwa kuwa kijana huyo ambae ni kitinda mimba katika familia ya marehemu, mzee aliyefahamika kama Mzee Kifwema, kijana huyo inasemekana alikuwa ana mgogoro na baba yake huyo akidai kugawiwa mali ambao ni ng'ombe, lakini baba yake alimkatalia, ndipo kijana huyo akawa akimlalamikia mzazi wake huyo hasa kwa madai kuwa kwa sababu gani hataki kumgawa ili hali baba huyo kawagawia ndugu wa kijana huyo ambao ni dada zake walioolewa ili wauze wapate pesa wawalipie watoto wao ada ya shule.
Jambo hilo lilimkasirisha kijana huyo ndipo, siku ya jumapili ya tarehe 25.05.2014 majira ya asubuhi, mzee Kifwema akiwa anaenda zake Kanisani, kijana wake akamvizia barabarani huku ameshika Machette.
Akamzuia baba yake na kukazuka majibizano, namnukuu kutokana na mashuhuda walivyoeleza "" utanipa ng'ombe haunipi?" mzee kajibu "sikupi" ,ndipo kijana kamkata mzee na panga mara tatu tu kichwani na kumfumua ubongo, mzee kakata roho pale pale.
Wananchi wakamvamia kijana na kumpa kipigo hatari sana, hivi tunavyoongea yupo Hospital ya Manispaa amelazwa kutokana na kipigo hicho, na mzazi wake huyo marehemu amezikwa siku ya Jana tarehe 27.
Je? ni lazima mzazi wako akupe mali baada ya kukuleta duniani? kama anazo? au ni ubidamu wake tu kukuwezesha?
Inadaiwa kuwa kijana huyo ambae ni kitinda mimba katika familia ya marehemu, mzee aliyefahamika kama Mzee Kifwema, kijana huyo inasemekana alikuwa ana mgogoro na baba yake huyo akidai kugawiwa mali ambao ni ng'ombe, lakini baba yake alimkatalia, ndipo kijana huyo akawa akimlalamikia mzazi wake huyo hasa kwa madai kuwa kwa sababu gani hataki kumgawa ili hali baba huyo kawagawia ndugu wa kijana huyo ambao ni dada zake walioolewa ili wauze wapate pesa wawalipie watoto wao ada ya shule.
Jambo hilo lilimkasirisha kijana huyo ndipo, siku ya jumapili ya tarehe 25.05.2014 majira ya asubuhi, mzee Kifwema akiwa anaenda zake Kanisani, kijana wake akamvizia barabarani huku ameshika Machette.
Akamzuia baba yake na kukazuka majibizano, namnukuu kutokana na mashuhuda walivyoeleza "" utanipa ng'ombe haunipi?" mzee kajibu "sikupi" ,ndipo kijana kamkata mzee na panga mara tatu tu kichwani na kumfumua ubongo, mzee kakata roho pale pale.
Wananchi wakamvamia kijana na kumpa kipigo hatari sana, hivi tunavyoongea yupo Hospital ya Manispaa amelazwa kutokana na kipigo hicho, na mzazi wake huyo marehemu amezikwa siku ya Jana tarehe 27.
Je? ni lazima mzazi wako akupe mali baada ya kukuleta duniani? kama anazo? au ni ubidamu wake tu kukuwezesha?