Mohamedi Mtoi
R I P
- Dec 11, 2010
- 3,321
- 6,328
Ndugu zangu.
Kijana Amiri Mtoi ambaye ni mtoto wa kaka yetu Mtoi Kolowa Daffa (mtoto wa baba yetu mkubwa) amezikwa leo majira ya saa 5 kijijini kwetu Mkuzi wilayani Lushoto.
Marehemu Amiri ni miongoni mwa wahanga wa tukio la bomu kule Arusha, amesafirishwa usiku kuamkia leo na amezikwa mapema asubuhi kufuatia imani ya dini yetu lakini pia ili kutoa fursa ya watu walio sindikiza mwili kutoka Arusha waianze safari yao mapema.
Amiri Mtoi amekatishwa masomo angali darasa la tatu, amiri hakuwahi kufikiri wala kuzadhani kuwa atakufa akiwa na tundu la risasi kwenye mwili wake, nimeangalia picha zake nimeumia sana, ametangulia mbele ya haki, walio rusha risasi nao watamfuata, Mwenyezi Mungu atawalipa, sio kwa dua mbaya za familia, lakini kwa mapenzi yake yeye (Mungu).
Watu wa Arusha kwa wingi na umoja wao wameonyesha ushirikiano wa kutosha.
Kwa niaba ya wana ukoo wa Mtoi tunawashukuru sana!
Tumuombee Amiri apumzike kwa amani baada ya kukatishwa uhai wake na watu wasio kuwa na huruma na wenye kujiona wao pekee ndio wenye mamlaka ya kuitawala Tanzania na kuamua nani aishi na nani atangulie mbele za Mungu.
Itoshe kusema.
Inauma sana, hasira zangu dhidi ya ccm hazita koma na wamefungua ukurasa mpya wa mapambano dhidi yao, sisi ni maskini na wanyonge hatuwezi kumiliki bunduki wala bastola zenye risasi lakini tunaweza kuuwa kwa kutumia sanduku la kura. Nitayaongoza mapambano
"All those that fight when oppressed incur no guilt, but Allah shall punish the
oppressor." Come the day.
Inna Lillahi wa inna ilaihi raji'un
Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums.
Kijana Amiri Mtoi ambaye ni mtoto wa kaka yetu Mtoi Kolowa Daffa (mtoto wa baba yetu mkubwa) amezikwa leo majira ya saa 5 kijijini kwetu Mkuzi wilayani Lushoto.
Marehemu Amiri ni miongoni mwa wahanga wa tukio la bomu kule Arusha, amesafirishwa usiku kuamkia leo na amezikwa mapema asubuhi kufuatia imani ya dini yetu lakini pia ili kutoa fursa ya watu walio sindikiza mwili kutoka Arusha waianze safari yao mapema.
Amiri Mtoi amekatishwa masomo angali darasa la tatu, amiri hakuwahi kufikiri wala kuzadhani kuwa atakufa akiwa na tundu la risasi kwenye mwili wake, nimeangalia picha zake nimeumia sana, ametangulia mbele ya haki, walio rusha risasi nao watamfuata, Mwenyezi Mungu atawalipa, sio kwa dua mbaya za familia, lakini kwa mapenzi yake yeye (Mungu).
Watu wa Arusha kwa wingi na umoja wao wameonyesha ushirikiano wa kutosha.
Kwa niaba ya wana ukoo wa Mtoi tunawashukuru sana!
Tumuombee Amiri apumzike kwa amani baada ya kukatishwa uhai wake na watu wasio kuwa na huruma na wenye kujiona wao pekee ndio wenye mamlaka ya kuitawala Tanzania na kuamua nani aishi na nani atangulie mbele za Mungu.
Itoshe kusema.
Inauma sana, hasira zangu dhidi ya ccm hazita koma na wamefungua ukurasa mpya wa mapambano dhidi yao, sisi ni maskini na wanyonge hatuwezi kumiliki bunduki wala bastola zenye risasi lakini tunaweza kuuwa kwa kutumia sanduku la kura. Nitayaongoza mapambano
"All those that fight when oppressed incur no guilt, but Allah shall punish the
oppressor." Come the day.
Inna Lillahi wa inna ilaihi raji'un
Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums.