Kijana aliyenusurika kifo kwa manyanyaso ya ndugu, atoa shukrani kwa kutolewa gizani

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
Anord Patrick Kalinga (21) mkazi Mlevelwa, Kata ya Mdabulo, Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa ambae ni miongoni mwa vijana 100 kutoka kwenye familia duni walioibuliwa na Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi na mradi wa Youth Agency Mufindi (YAM) amepongeza mradi huo kwa kumuona.

Anord alisema akiwa mdogo alipitia mazingira hatari na hata wakati mwingine alinusurika kifo kutokana na kazi ngumu za mateso alizokuwa akipewa na ndugu zake.
Anord Patrick Kalinga (1).jpg

Akitoa shuhuda zake Alhamisi Machi 10, 2022 katika warsha ya Afya ya Akili katika Ukumbi wa Yatima Igoda, Wilaya ya Mufindi alisema kuwa kwa upande wake alikuwa amekata tamaa ya maisha hasa kutokana na mazingira magumu aliyopitia.

Hivyo, kupitia mradi huo wa YAM anaamini atasimama tena na kupambana kuwa na maisha bora kwani kwa muda wa mafunzo aliyopata kuna mambo mengi na mazuri amejifunza ambayo kwake ni kama mtaji.

"Kutokana na changamoto za maisha niliyopitia leo nimenifunza mambo mengi ya kunifanya kusonga mbele kimaisha na sasa sijuti tena kuwa kijana kutoka mazingira magumu ila naitumia fursa hii niliyofikiwa kusonga mbele," alisema Anord.

Malengo yake ni kwenda chuo cha ufundi wa magari na udereva ili kupitia kazi hiyo aweze kusimama kiuchumi.

Alisema mbali ya kuwa na maisha duni ila amekuwa nguzo ya familia kwa kutafuta fedha za kusaidia kuendesha familia yake na kupitia elimu ya ufundi atakayoipata ataweza kuondoa hofu ya kiuchumi inayomkabili kwa sasa.
Anord Patrick Kalinga (2).jpg

Mkufunzi wa mafunzo hayo, Dr Heriel Mfangano aliwataka washiriki wa mafunzo hayo kuitumia elimu hiyo kama plani B ya kuendelea na ndoto zao za kumiliki uchumi wao.

Alisema elimu ya ujasiriamali ni nguzo sahihi kwa vijana hao kuja kukuza uchumi wao na kuondokana na hali ya kujitenga, kuona hawana uwezo wa kufanya shughuli za kiuchumi.

Halmashauri ya Mufindi chini ya mradi wa FCWC na YAM kupitia ufadhili wa Finland utatelekelezwa kwenye kata za Luhunga, Ihanu na Mdabulo ni mradi wa miaka minne ulioanza mwaka jana na utekelezaji wake utakaonufaisha vijana na watoto wanaotoka katika familia duni zaidi ya vijana 770 katika vijiji 16.

Source: Matukio Daima Blog
 
Bwana weee!! mapitio yako kwa kila mutu hasa waafrica!!! narudia tena hii hasa waafrica!! na kwingine wapo pia!!....wengine hatukujua tutakuwa wataalamu wa Ikulu za USA lkn Mungu alifungua njia vibaya sana!!

hata km uko juu kimaisha lkn kuna baadhi ya watu ndg bado tu wanakuponda, hawafurahiii!! wanatakakuua na kurengesha wapenzi wenye ukimwi!! ndg wabaya sana hasa maskini huko vijijini usipeleke watoto wako huko umaskinini!!...

kisa eti ulipita kwake unaenda shule ukala ugali wake na utumbo wa ng'ombe! basi atatangazia watu eti alikusaidia mweee!...ukavuka kimaisha!!...kuponapona kufa wengi binadamu wako ivo!! Nyerere alipona KUFA mara 17!

Idd amini alipona kufa mara 30!!! Yasser arafat mama weee!! mara 150...mara ya mwisho alianguka na ndegekwa tego la jangwani haswaaa!! akapotolea kwenye dhoruba ya vumbi!! alipatikana baada ya siku saba!! Reagan wa USA pamoja na ubabe wake woooote aliponea chupuchupu kufa kwa risasi mfululizo zikajaa mwilini mwake!

usitutishe na kifo chako hicho cha madafu.........mie nimeponea chupuchupu kufa mara kibao!!......kwanza kiuchawi!! na mara nyingi tit for tat! na wengine kuja na ukimwi kabisaaa!! eti waniambukize na mie nife Loo!!ool! Binadamu??? lkn nilisonga mbaya...

sasa weye usitulilie lilie humu! eti una mapito, ulipona pona kufa kivipi??? ndo maana huna wachangijai wengi!! Maskini mnajionea hruma sana wakt watu mapito yetu utaona weyey cha mtoto tu!

watu wameponea kufa wakivuka Border kutafuta maisha!! wengine walitoswa baharini waka salimiana na Mamba!! Mandela utasemaje sasa?? Nkwame nkrumah!Dedan kimath!! Martin ruther king nk! acha vistori vya ki hivi;

komaaa mtoto wa kiume muweke Mungu mbele!
 
Anord Patrick Kalinga (21) mkazi Mlevelwa, Kata ya Mdabulo, Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa ambae ni miongoni mwa vijana 100 kutoka kwenye familia duni walioibuliwa na Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi na mradi wa Youth Agency Mufindi (YAM) amepongeza mradi huo kwa kumuona.

Anord alisema akiwa mdogo alipitia mazingira hatari na hata wakati mwingine alinusurika kifo kutokana na kazi ngumu za mateso alizokuwa akipewa na ndugu zake.
View attachment 2146507
Akitoa shuhuda zake Alhamisi Machi 10, 2022 katika warsha ya Afya ya Akili katika Ukumbi wa Yatima Igoda, Wilaya ya Mufindi alisema kuwa kwa upande wake alikuwa amekata tamaa ya maisha hasa kutokana na mazingira magumu aliyopitia.

Hivyo, kupitia mradi huo wa YAM anaamini atasimama tena na kupambana kuwa na maisha bora kwani kwa muda wa mafunzo aliyopata kuna mambo mengi na mazuri amejifunza ambayo kwake ni kama mtaji.

"Kutokana na changamoto za maisha niliyopitia leo nimenifunza mambo mengi ya kunifanya kusonga mbele kimaisha na sasa sijuti tena kuwa kijana kutoka mazingira magumu ila naitumia fursa hii niliyofikiwa kusonga mbele," alisema Anord.

Malengo yake ni kwenda chuo cha ufundi wa magari na udereva ili kupitia kazi hiyo aweze kusimama kiuchumi.

Alisema mbali ya kuwa na maisha duni ila amekuwa nguzo ya familia kwa kutafuta fedha za kusaidia kuendesha familia yake na kupitia elimu ya ufundi atakayoipata ataweza kuondoa hofu ya kiuchumi inayomkabili kwa sasa.
View attachment 2146506
Mkufunzi wa mafunzo hayo, Dr Heriel Mfangano aliwataka washiriki wa mafunzo hayo kuitumia elimu hiyo kama plani B ya kuendelea na ndoto zao za kumiliki uchumi wao.

Alisema elimu ya ujasiriamali ni nguzo sahihi kwa vijana hao kuja kukuza uchumi wao na kuondokana na hali ya kujitenga, kuona hawana uwezo wa kufanya shughuli za kiuchumi.

Halmashauri ya Mufindi chini ya mradi wa FCWC na YAM kupitia ufadhili wa Finland utatelekelezwa kwenye kata za Luhunga, Ihanu na Mdabulo ni mradi wa miaka minne ulioanza mwaka jana na utekelezaji wake utakaonufaisha vijana na watoto wanaotoka katika familia duni zaidi ya vijana 770 katika vijiji 16.

Source: Matukio Daima Blog
To be frank, wakazi na hasa vijana wa Mufindi hususan kata za Luhunga, Mdabulo na Ihanu wanahitaji ardhi tu na maarifa ya matumizi sahihi na bora ya ardhi husika ili kujikwamua kiuchumi. Msemo wa Wachina 'Usinipe samaki kama kitoeo, nipatie ndoano na unifundishe namna ya kuvua samaki' unahusika.
 
Back
Top Bottom