Kijana afanya utani wa kutaka kumuua Rais Magufuli, aambuliwa kifungo cha miaka 2 jela

Soma maelezo vzr ujigundue ulivyo mjinga,kama mshtakiwa amekiri kosa unadhan kuna nn tena hpo kilichobaki.
 
Wahenga walinena:-, maneno yanaumba......na lisemwalo lipo kama halipo......
 
Katenda kosa tarehe 26/nov Leo tarehe 4/12 na hukumu tayari imeshatoka!!! Pongezi kubwa kwa Mahakama kwa kuendesha kesi ushaidi kukamilika na kutoa hukumu ndani ya wiki moja toka mshtakiwa kutenda kosa.Mahakama nyingine nchini kote ziige mfano huu maana kuna ndg, rafiki, jamaa zetu wengi sana wapo mahabusu bila kujua hatma ya mashtaka yao.
Wako mahabusu kwa ajili ya ile kauli ya, "Si kweli" huku ukiwa umenyosha ka mkono. Ukisomewa mashtaka, ukakili, mahakama inao uwezo wa kukuhukumu siku hiyohiyo.
 
Kwa hiyo alimaanisha kumuua rais au ukweli unaoufahamu wewe ni upi?

Vyovyote iwavyo point yangu ni kuwa watu wausome utawala uliopo na kujua waende nao vipi.

Utawala wowote ule hakuna wakati ni sawa kutishia kuua Rais

Hakuna cha kusoma alama za nyakati...

Au wewe unaona kuna nyakati au tawala ambazo ni sawa kutishia kumuua Rais?
 
Mnaotetea hebu igeuzeni picha iwe kwenu,
Anatokea mtu mmoja anadai "nitamuua baba yako ngoja nijipange, au nitakuua hesabu siku tu, au nitamuua huyu mtoto wako simpendi kabisa" n.k n.k,

Je utachukulia poa tu kua anatania?
Huyo amepata alichostahili iwe fundisho kwa wengine wenye mawazo ya kuua ua, kama mtu humpendi hata kumuona ni aidha uondoke sehemu alipo au kufa wewe.
 
Sijaona kosa hapo la kumfanya mtu afungwe jela miaka miwili, huyu mkuu wa malaika atakuja kulipa haya yote wanayofanyiwa wanyonge, nasema tena sijaona kosa, Askari polisi mmoja kule mkoani mara alimuua kijana mmoja raia ambaye hakuwa na silaha yeyote na mwisho wa siku akafutiwa kesi iliyokuwa inamkabiri, Askari polisi aliyefyatua risasi ya moto akaua Akwilina amefutiwa kesi, huyu kijana wa watu anafanya utani kusema kusema ataua jiwe anafungwa, huyu ungeweza kumpa kazi ya kufanya kwenye ofisi za umma kama karipio (na ina tija) na si kumfunga, hapo rais anafurahi sana.
 
unajuaje alikuwa anafanya masihara?

usifuatishe vichwa vya habari vya magazeti uozo yetu haya

masihara ni utetezi wake kizimbani, ambao mahakama imeukataa...
Hivi mtu anaweza kuua rais kweli ?, huyu rais nae ni janga la taifa.
 
Back
Top Bottom