Kiingereza bado ni tatizo kubwa shule za sekondari

MANYORI Jr

JF-Expert Member
Mar 25, 2012
462
343
Ikiwa imepita siku moja tangu kutangazwa kwa matokeo ya mtihani wa taifa wa kidato cha nne uliofanyika mwaka 2019, moja ya masomo yaliyopelekea matokeo mabovu ni English Language.

Somo la lugha ya Kiingereza linalea takribani masomo 7 na lenyewe likijilea katika yale masomo 9 ya msingi kwa shule za sekondari.

Hii inadhihirika pale "you no, this were, ok or yes" zinapowapelekea wadogo zetu kushindwa kueleza mawazo yao katika maswali kutoka kwenye masomo yale 7 na Kiingereza kama somo la 8.

Serikali, kwa nafasi yake, inaweza kukabiliana na changamoto ya ufaulu sekondari kwa kuajiri rasimali watu (walimu) wa somo la lugha ya Kiingereza kwa kuwa hata uhalisia watu hawa ni adimu na hawatoshelezi mahitaji.

Zaidi ya hili somo la lugha ya Kiingereza ndilo changamoto mama katika changamoto zinazoukabili mfumo wetu wa elimu hasa sekondari na hata ngazi za juu.

Ni dhahiri kuwa panahitajika hatua madhubuti ili kuinusuru elimu ya taifa letu.

Kama watoto watakaa 'kambi' bila lugha ya Kiingereza, hii ni sawa na mganga bila tunguli.
 
Hata wakiajiriwa, walimu wenyewe hawakijui kiingereza ipasavyo(wengi wao). Ukitaka kuthibitisha hili, nenda shule(hasa za serikali), ukibahatika kukutana na mwalimu anayefundisha kiingereza, ongea naye, usikie grammar na tense zinavyovurugwa.

Usidhani tatizo litaishia kwenye kuongea tu, kwenye kuandika ni kasheshe pia.

Note:
Nazungumzia kizazi cha walimu kuanzia mwaka 2006 mpaka leo.
 
Tatizo jingine ni exposure, wawe wakali kuhakikisha katika mazingira ya shule wanafunzi wawasiliane kwa kiingereza pekee. zipo adhabu za kutosha kwa wale watakaokutwa wakiongea kiswahili, wazitumie hizo.
Walimu wenyewe kuongea kitasha(kiingereza) ni tabu, ndiyo wasisitize wanafunzi waongee? Labda kwa shule za private, ila serikalini, ni shule chache sana zinazoweza kufanya hilo.
 
Tatizo jingine ni exposure, wawe wakali kuhakikisha katika mazingira ya shule wanafunzi wawasiliane kwa kiingereza pekee. zipo adhabu za kutosha kwa wale watakaokutwa wakiongea kiswahili, wazitumie hizo.
adhabu bila lengo lenye utaratibu maalumu unaweza kuwa "negative rainforcement" .
Cha msingi wapelekwe vijana waliosomea kufundisha Lugha ya Kiingereza kama lugha ya kimataifa na mawasiliano ya dunia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata wakiajiriwa, walimu wenyewe hawakijui kiingereza ipasavyo(wengi wao). Ukitaka kuthibitisha hili, nenda shule(hasa za serikali), ukibahatika kukutana na mwalimu anayefundisha kiingereza, ongea naye, usikie grammar na tense zinavyovurugwa.

Usidhani tatizo litaishia kwenye kuongea tu, kwenye kuandika ni kasheshe pia.

Note:
Nazungumzia kizazi cha walimu kuanzia mwaka 2006 mpaka leo.

Wewe ni MUONGO!
Unakutana na walimu wa 'St.Magumashi tu hao wa kutoa rushwa wapewe course work.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
utaongeaje wakati Sheria na kanuni za kukiongea hujui, sana sana utaishia kuchekwa tuu na wanafunzi wenzako
Kama wote wanajifunza sidhani atakuwepo wa kumcheka mwenzake, bila kuwa na watu ambao mtawasiliana mara kwa mara ni ngumu ku master hicho kiingereza, shuleni fully kiswahili, nyumbani kiswahili, mitaani kiswahili halafu utarajie kuongea kiingereza kwa ufasaha, sahau.. ni wachache sana wanaoweza katika mazingira ya namna hiyo na bado wanakuwa siyo wazuri sana, wanakuwa wanatafuta tafuta maneno na hawana misamiati ya kutosha kutumia katika mazingira tofauti tofauti.
 
Tatizo sio walimu ndugu yangu. Hicho kizazi cha waalimu kuanzia 2016 ukumbuke unajumuisha na private schools ambao wanafanya vizuri sana.
Waalimu hao hao wakirudi government schools uwezo wao utapungua na unaweza kushangaa imekuwaje.

Tatizo ninalo liona mimi ni moja ambalo ni mfumo wa kusimamia kikamilifu matumizi ya lugha ya kiingereza katika government schools ni mbovu tena Sana. Hawako strict na hilo. English speaking programs hazipo na kama zipo ni zimamoto especially shule za kata.
Hakuna usimamizi,mambo yako kimazoeazoea tu.
Wenzetu wa private wako makini kwa kila kitu.
No English no service. Mwanafunzi yeyote atakayejiunga na private schools atake asitake atajua tu kiingereza maana mfumo utamshape hivyo vingenevyo atachemka na kuacha shule.

Hata wakiajiriwa, walimu wenyewe hawakijui kiingereza ipasavyo(wengi wao). Ukitaka kuthibitisha hili, nenda shule(hasa za serikali), ukibahatika kukutana na mwalimu anayefundisha kiingereza, ongea naye, usikie grammar na tense zinavyovurugwa.

Usidhani tatizo litaishia kwenye kuongea tu, kwenye kuandika ni kasheshe pia.

Note:
Nazungumzia kizazi cha walimu kuanzia mwaka 2006 mpaka leo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe ni MUONGO!
Unakutana na walimu wa 'St.Magumashi tu hao wa kutoa rushwa wapewe course work.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahahaha, ningekuwa sijabahatika kufundisha kwenye shule za serikali na za private na kuyaona hayo niliyoyaandika, ningekubali kupewa sifa ya shetani(uongo).

Fanya research ya niliyoyaandika, au anzisha research institute utembee kwenye shule angalau 100 za serikali(uwe vizuri kwenye ung'eng'e) ili uweze kujua kiingereza cha hao walimu kipoje.

Narudia tena, siyo walimu wote wa kiingereza wana shida ya kiingereza, bali wengi wao wako ovyo.

Ajabu zaidi, usishangae, mwalimu wa kiingereza anaongea kiswahili asilimia kubwa ya muda aliopo darasani.
 
Tatizo sio walimu ndugu yangu. Hicho kizazi cha waalimu kuanzia 2016 ukumbuke unajumuisha na private schools ambao wanafanya vizuri sana.
Waalimu hao hao wakirudi government schools uwezo wao utapungua na unaweza kushangaa imekuwaje.


Sent using Jamii Forums mobile app
Kwani Nimesema walimu wote ndiyo wenye shida?

Mind you, private zinafanya interview ya kuchagua walimu bora, serikalini zamani walimu wanajaza nafasi wakiwa vyuoni, na kwa sasa, wanajaza particulars zao kwenye mfumo wa OTEAS, no interview at all. Sasa, anayefanya interview ya kuchagua walimu, na anayeajiri pasipo hata interview(somba somba) nani ana probability ya kupata walimu bora?

Hapo hapo, walimu wote walifaulu vizuri tu, usisahau, kuna kufaulu kwa kukariri na kwa kuelewa.

Ndiyo maana ningepewa nafasi ya kushauri, ningeshauri kiwepo kitengo cha kuajiri walimu kwa kupitia interviews.
 
Pana uhaba na upungufu wa walimu wa Somo la Lugha ya Kiingereza

Sent using Jamii Forums mobile app
Sijakataa kama kuna uhaba au hakuna. Concern yangu ni, wasiajiriwe watu wa kujaza nafasi(kisa walisoma na kufaulu kiingereza), bali waajiriwe walimu competent.

Mwalimu ovyo hutoa matokeo ya ovyo.

Nikiwa darasa la saba(shule za kayumba), alikuja mwalimu ambaye huyo ndiyo chanzo cha Mimi kujua na kukipenda kiingereza. Imagine, tangu darasa la saba nili-master tense na grammar, njoo wanafunzi leo, kamata pepa la mwanafunzi wa form four uone hizo sentensi zilivyopangiliwa.

Walimu wa sekondari, wangekuwa kama huyo mwalimu, nina uhakika ngeri ingekuwa inapanda sana kwa wanafunzi.

Usisahau, kufeli kwa mwanafunzi, ni matokeo ya kufeli kwa mwalimu.

Na pia
The primary cause of learner's failure, is inflexibility of teachers.
 
Back
Top Bottom